Mwacheni Magufuli alishamaliza safari yake, endeleeni kushangilia mama yenu akiupiga mwingi.

Ni wajinga Fulani watakaoendelea kuamini kuwa makato yaliyoletwa na Mwigulu Nchemba Huku mama yenu alikuwa hajui ila alihujumiwa.
 
Jeuri ya namna hii huwa wanakuwa nayo Wanasiasa wa Tanzania tu. Sababu wanajua Wananchi wa Tanzania wanaowalipa mishahara na posho. hawana la kuwafanya.

Ni kauli iliyojaa dharau, kebehi, kiburi, ujivuni, ubazazi, ubaradhuli na ulaanatullah. Huyu amejikinai. Hawajali wananchi maskini wa Tanzania. Na watanzania sababu ni wapole sana nadhani hatuna la kufanya.
Anaupiga mwingi sana mwigulu.lipeni kodi nyie acheni kulialia
 
Huyu hapa

IMG-20210718-WA0139.jpg
 
Ana kitu inaitwa: academic arrogance. Anaamini yeye ana akili kuliko/kuwazidi wengine wote. Lakini ajue arrogance comes before the fall.
On records
2013 aliteuliwa kuwa naibu waziri wa fedha chini ya Saada Salum Nkuya hakuna alichofanikisha.

2015 JPM alimteua kuwa waziri wa Kilimo hakuna alichofnikisha mwisho mpaka anatoka mazao karibu yote yaliporomoka bei na pembejeo kupanda mara dufu.

2016 JPM alimteua Mwigulu kuwa waziri wa Mambo ya ndani kuanzia hapo likaibuka kundi la watu wasiojulikana, tukaokota maiti 9 akasema za wahamiaji haramu, watanzania wengi sana wakawa wanatekwa, kubwa kuliko yote Lissu was gunned down by unknown men, Mo akatekwa.

2019 akateuliwa kuwa waziri wa Fedha bajeti yake ya kwanza kila mtu analia mpaka rais mwenyewe

Apart from organisms what else Mwigulu has achieved ?
 
Ummy mwalimu mwenyewe kanjanja tu...juzi kwenye ajira za ualimu tamisemi amecheza prakatatumba za hovyoo sana...
 
Yaani mwigulu ni bonge la falla, kumbe ndiyo maana magufuli alikuwa anamchukia na ha mwamini hata kidogo, yaani kapata ka upenyo kadogo tuu anamdanganya na kumchonganisha mama wa watu.......!
Mama hana akili anachoweza n kula urojo tu
 
Hatufai. Ana Jeuri, Mdhalimu na Asiye na Utu. Ulisema unatajali haki na utu wa Wananchi. Anzia hapa kwa huyu Mwigulu tuondolee Balaah hili katika Uongozi huu.
 
Kiukweli Angekuwepo Mwendazake NSSF wangenyooka si kwa mateso wanayowapa wateja wake.
Wastahiki wanapata hekaheka mbele ya watoto waliowasomesha.Wanadharau,hawana hofu ya Mungu,huenda wametumwa na Boss wao.Mwendazake angeshasikia kilio hiki siku nyingi.Sidhani Kama nchi hii tutatoboa tena
 
Mamlaka ya uteuzi tuseme Sasa imetoshaaaaa

Tozo ya Mafuta juu
Tozo ya Fedha mitandaoni juu....
Maendeleo mwayapenda kodi hamtaki! Mtamkumbuka sana Magu, pamoja na maendeleo yote tuliyoyafikia, bei za vitu vinavyoliwa na wanyonge zilibaki chini! RIEP&P our great and true African hero Hon Dr JPM 🙏)!
 
Mwigulu ataendelea kula kuku kwa mrija mpaka rais aliyemteua aamue kumwondoa kwenye nafasi yake...
 
Nashauri mchakato wa katiba mpya uanze January 2026 (umalizike October 2028), lakini tume ya katiba mpya iundwe January 2022.

Tume huru ya uchaguzi ipatikane October 2023 (miaka miwili kabla ya uchaguzi mkuu wa October 2025).

Vyama vya siasa viruhusiwe kufanya mikutano ya hadhara ya kisiasa from January 2022.

Mada kuu ya katiba mpya iwe:

Katiba mpya iwe na a Bill of rights, itakayoheshimu basic human rights.

Muhimili wa Mahakama uwe huru.

Muhimili wa Bunge uwe huru.

Rais wa JMT asiwe na uwezo wa kulivunja Bunge la JMT.

Ikitokea kuna mvutano wowote ule usiotatulika baina ya Rais na Bunge, a national referendum ita amua nani kati yao aachie madaraka, na hakutakuwa na uchaguzi mpaka kipindi kijacho cha uchaguzi mkuu.

Kama Bunge litashindwa referendum, nchi itakuwa haina Bunge mpaka uchaguzi mkuu ujao. Kama Rais atashindwa referendum, Bunge litamchagua kaimu Rais atakae kaa mpaka uchaguzi mkuu ujao. Kaimu Rais huyo anaweza awe au asiwe Makamu wa Rais wa huyo Rais ambae ameshindwa referendum.

Principle hiyo hiyo ita apply kwa Rais wa SMZ na Baraza la wawakilishi.

Wananchi wa pande zote za Muungano watapiga referendum kama upande wao unataka Muungano au la. Na kama wanautaka Muungano, wanataka Muungano wa serikali ngapi, moja, mbili au tatu.

Wananchi wa upande husika wa Muungano, watapiga referendum kama wanataka serikali centralised (kama sasa) au serikali za mikoa (zinazoiga zile za counties za Kenya, ila kwa Tanzania zitakuwa kwa level ya mikoa na sio kwa level ya counties/districts) au serikali za majimbo kama kule Nigeria. Mimi nadhani, kwa Tanzania serikali itakayo faa ni serikali za mikoa, zinazoiga zile za counties za Kenya. Serikali za majimbo kama za Nigeria hazitafaa.

Je, Bunge la JMT litakuwa na two houses (house of representatives na Senate) au litakuwa na house moja (kama sasa hivi)?

Since uhuru wa Bunge utaongezeka, basi qualifications za wagombea ubunge zifanane kabisa na qualifications za wagombea urais. Isipokuwa tu, umri wa mgombea ubunge uwe miaka 21 au zaidi.

Since muhimili wa mahakama utakuwa huru, basi qualifications za mahakimu na majaji ziwe zina fanana kabisa na qualifications za wagombea urais isipokuwa tu, umri wa mahakimu na majaji uwe miaka 21 na kuendelea, na wawe na degree ya sheria (au degree ya somo lenye uhusiano na mambo ya sheria).

Tume hiyo mpya ya katiba inaweza ichukue au isichukue mapendekezo ya rasimu ya katiba ya tume ya Warioba.

Mwenyekiti wa tume mpya ya katiba anaweza kuwa Jaji Mary Longway.
 
Ebu tulia, kwani budget ni Dr. Mwigulu anapitisha, yeye anatoa proposals tu, Bunge ndio linapitisha budget, akiwemo mbunge wako, muulize mbunge wako, sbb zilizopelekea alikubali budget kuipitisha. Sio Mwigulu, umeelewa? Mwigulu ni mtoa hoja tu, waliokubaliana na hoja kupita waulize, mpigie mbunge wako
JF ya sasa kuna vilaza wengi sana...yaani wanafikiri Mwigulu anaweza kuamua peke yake....wakati mchakato wake ni mrefu na unawahusisha wabunge wote ,kamati ,baraza la mawaziri nk .Ingawa ni kweli Mwigulu ni kimeo
 
Back
Top Bottom