BWANKU M BWANKU
JF-Expert Member
- Jan 12, 2019
- 328
- 414
Umoja wa Machifu Tanzania (UMT) kwa kushirikiana na Kituo cha Makumbusho cha Bujora Mwanza wameandaa tamasha kubwa la utamaduni lenye lengo la kurithisha utamaduni wetu kwa vizazi vyetu vya sasa litakalofanyika katika viwanja vya Redcross Kisesa Jijini Mwanza kuanzia leo Jumanne Septemba 07, 2021 mpaka kesho Septemba 08, 2021.
Mgeni rasmi kwenye tamasha hili ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan. Wote mnakaribishwa.
#Turithishe utamaduni wetu.
#Tudumishe utamaduni wetu.
#Amani na Umoja ni tunu zetu.
====
Tamasha la utamaduni laanza leo Mwanza
Mwanza. Tamasha la siku mbili la utamaduni wa mtanzania limeanza leo katika viwanja vya msalaba mwekundu vilivyopo karibu na makumbusho ya Bujora wilayani Magu mkoani Mwanza.
Mgeni rasmi katika tamasha hilo ni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan huku likihudhuriwa na viongozi wa kimila (Machifu) kutoka makabila 120 nchi nzima.
Akizungumza leo, Katibu wa tamasha hilo ambaye ni chifu wa wasukuma wa Mwanza, Aaron Mikomangwa amesema tamasha hilo linalenga kurithisha, kudumisha na kuendeleza mila na desturi za Mtanzania.
"Kuanzia leo watanzania watakaofika katika viwanja hivi watajifunza mila na tamaduni za makabila yao na mengine ikiwemo ngoma, mavazi, chakula na kushuhudia usimikaji wa viongozi mbalimbali wa kimila," amesema Mikomangwa.
Ameongeza kwamba katika tamasha hilo pia kutakuwa na mashindano ikiwemo mashindano ya kurusha mikuki, kusaga na kukoboa nafaka kwa kutumia vifaa vya asilia ikiwemo mawe, na ambapo watashuhudia jinsi ambavyo watu wa zamani walikuwa wakiwasha moto kwa kutumia miti na nyasi (Ulindi na ulimbombo).
Akizungumzia tamasha hilo Chifu kiongozi wa mkoa wa Mbeya Zulu Gama amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika tamasha hilo ili kujifunza mila na tamaduni za makabila mengine.
Mgeni rasmi kwenye tamasha hili ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan. Wote mnakaribishwa.
#Turithishe utamaduni wetu.
#Tudumishe utamaduni wetu.
#Amani na Umoja ni tunu zetu.
====
Tamasha la utamaduni laanza leo Mwanza
Mwanza. Tamasha la siku mbili la utamaduni wa mtanzania limeanza leo katika viwanja vya msalaba mwekundu vilivyopo karibu na makumbusho ya Bujora wilayani Magu mkoani Mwanza.
Mgeni rasmi katika tamasha hilo ni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan huku likihudhuriwa na viongozi wa kimila (Machifu) kutoka makabila 120 nchi nzima.
Akizungumza leo, Katibu wa tamasha hilo ambaye ni chifu wa wasukuma wa Mwanza, Aaron Mikomangwa amesema tamasha hilo linalenga kurithisha, kudumisha na kuendeleza mila na desturi za Mtanzania.
"Kuanzia leo watanzania watakaofika katika viwanja hivi watajifunza mila na tamaduni za makabila yao na mengine ikiwemo ngoma, mavazi, chakula na kushuhudia usimikaji wa viongozi mbalimbali wa kimila," amesema Mikomangwa.
Ameongeza kwamba katika tamasha hilo pia kutakuwa na mashindano ikiwemo mashindano ya kurusha mikuki, kusaga na kukoboa nafaka kwa kutumia vifaa vya asilia ikiwemo mawe, na ambapo watashuhudia jinsi ambavyo watu wa zamani walikuwa wakiwasha moto kwa kutumia miti na nyasi (Ulindi na ulimbombo).
Akizungumzia tamasha hilo Chifu kiongozi wa mkoa wa Mbeya Zulu Gama amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika tamasha hilo ili kujifunza mila na tamaduni za makabila mengine.