Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,898
- 942
📍 Jimbo la Ushetu: Wananchi wa Ukune, Ushetu Wampongeza Rais Samia Suluhu Hassan
🏥🚑🤰🏽🧑🏽🍼
▪️Wananchi wa Ukune,Ushetu Wampongeza Rais Samia Suluhu Hassan
▪️Mbunge wa Ushetu Mhe. Emmanuel Cherehani azidi kukonga nyoyo wananchi wa Ushetu
Wananchi wa Kata ya Ukune katika Halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga, wameishukuru Serikali pamoja na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia gari jipya la kubebea wagonjwa(Ambulance).
Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao mara baada ya kukabidhiwa gari hilo, Fabiani James na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wilaya ya Kahama Theresphora Saria wamesema gari hilo litasaidia kupunguza vifo vya wajawazito na watoto na kwamba awali walikuwa wanalazimika kutumia usafiri wa pikipiki kuwasafirisha wagonjwa kwenda kwenye hospitali wilayani Kahama
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ukune Dr. Elikana Lubango, amesema gari hilo litatumika kubeba wagonjwa wakati wote litakapohitajika.
Mbunge wa Jimbo la Ushetu Emmanuel Cherehani akisema Serikali imetoa magari hayo ukiwa ni mpango wa kuwaondolea Wananchi adha ya kuwasafirisha wagonjwa kwenda kupata matibabu kwenye Hospitali kubwa.
🏥🚑🤰🏽🧑🏽🍼
▪️Wananchi wa Ukune,Ushetu Wampongeza Rais Samia Suluhu Hassan
▪️Mbunge wa Ushetu Mhe. Emmanuel Cherehani azidi kukonga nyoyo wananchi wa Ushetu
Wananchi wa Kata ya Ukune katika Halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga, wameishukuru Serikali pamoja na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia gari jipya la kubebea wagonjwa(Ambulance).
Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao mara baada ya kukabidhiwa gari hilo, Fabiani James na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wilaya ya Kahama Theresphora Saria wamesema gari hilo litasaidia kupunguza vifo vya wajawazito na watoto na kwamba awali walikuwa wanalazimika kutumia usafiri wa pikipiki kuwasafirisha wagonjwa kwenda kwenye hospitali wilayani Kahama
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ukune Dr. Elikana Lubango, amesema gari hilo litatumika kubeba wagonjwa wakati wote litakapohitajika.
Mbunge wa Jimbo la Ushetu Emmanuel Cherehani akisema Serikali imetoa magari hayo ukiwa ni mpango wa kuwaondolea Wananchi adha ya kuwasafirisha wagonjwa kwenda kupata matibabu kwenye Hospitali kubwa.