MWANZA: Hotel ya Tai Five yapigwa mnada

MWANZA: Hotel ya Tai Five yapigwa mnada

binadam ni kujitambua inakua ngumu kwani ulivyo panda ndivyo utakavyo shuka .....
 
Watanyooka tu si walijifanya kusaidia kuiba kura
 
Unajidanganya,hakuna mkopo mzuri ni madogori tu hayo.
Kweli mkopo ni mzuri na ukijua kuutumia utatajirika. Ila biashara yako ikienda kombo utauchukuia mkopo. Hapo kesho mida ya saa 4 asubuhi kutakuwepo na mnada utakaohusisha uuzwaji wa Tai Five hotel iliyopo karibu na kona ya Bwiru Jijini Mwanza. Sijui huyu ndugu naye anaisoma namba maana siku hizi mikutano na semina za serikali hazifanyikii tena mahotelini; kawhiyo hali ya kibiashara hasa mahoteli makubwa ni mbaya.
 
Kwani hiyo hotel kuuzwa kuna shidah gani?
Atachukua mwingine ataajiri mambo yataendelea basi.
 
Hahah mbona umeshtuka mamdogo? Hapana ile haijauzwa ila imegeuzwa hostel ya wanachuo ila inapoelekea ni kuuzwa tu Mkuu
Hata hao wanafunzi watawapata wapi maana wengi hawana mikopo. Inasikitisha sana hali ilivo
 
Wacha waisome namba Eeeh waisome namba maandiko ni yale yale
 
Looh, na LANDMARK HOTEL ya Riverside nayo imepigwa mnada??? Sikuwa na taarifa hiyo, this is news!!! Nani kainunua??
landmark haijapigwa mnada bali mmiliki kaigeuza hostel ya wasomi wa udsm
 
Itafika mahali watu wataanza kujiuliza nikinunua na mimi nini itakuwa hatima yangu kwa hali hii ya uchumi tuliyonayo?
Unaweza kununua na kubadili matumizi. Kuna yule aligeuza hostel.
 
TAI5.gif
Hii ni Hotel Mwanza... Lodge Arusha na Dar
 
Hiyo hotel imejengwa juu ya makaburi ya kitangiri, usiku wateja wanakabwa na mashetani, labda atakayeinunua aifanye kanisa la walokole
 
Aisee nikajua namba zinasomwa Dar es salaam pekee, taratibu tutaanza kutofautisha udini, ukabila, ukanda, undugu, urafiki, ujamaa na ujirani kwenye masuala nyeti ya kitaifa. Pole sana kwa mmiliki.
 
Tanzania ndio Nchi pekee dunia ambayo watu wake hufarahi au kukejeli ....wafanya biashara wanavyo pata matatizo ya kibiashara ..na hata serikali pia huwa komoa watu wake .

Lkn serikali husahau kwamba wafanya biashara hao wanawao wa komoa ndio waajiri wa kubwa wa watu wake ambao yenyewe imeshindwa kuwa ajiri

Mfano mdogo tu serikal imepiga marufuku uva aji wa MOJOHO ya graduation kwa shule na collag .

Hebu tusubir laabda wana plan zilizo nzuri tutapa jibu muda sio mrefu
 
Sasa ndugu, sekta binafsi inapotetereka huyu mtu wa kawaida unayemsema anakuwa na hali gani? coz kuna mengi yanayofuata kukosekana ajira, kupungua mzunguko wa fedha nk. Tajiri hana shida atabadili namna ya uwekezaji na kuchagua utaomfaa yeye
Mkuu. Kuna concept moja kwenye uchumi inaitwa multiplier effect, naona watu wengi wanaoshabikia hizi biashara kuyumba hawaielewi. Sasa subiri maumivu yamfikie huyo "mtu wa kawaida" ndio watu wataanza kusaga meno. serikali ya jirani zetu kenya walijaribu hii kitu ya kunyanyapaa sekta binafsi. Ndani ya miezi michache uchumi wao ukaanza kuyumba..mapato ya kodi yakaanza kushuka. Uzuri rais kenyatta hua hachelewi kubadili gia akiona amekosea...akaruhusu tena serikali kutumia huduma binafsi..na ndio kilichowaokoa. Sasa sisi badala ya kujifunza kwa wenzetu...tunataka kurudia makosa yao. Ngoja tu sasa tuone...tuombeane uhai tu.
Yaani wewe acha tu kazi tunayo
 
Back
Top Bottom