hili shairi ni zuri sana hususani kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari.. well done kaka mkubwa Ruta
Mkuu umetisha!Rutashubanyuma hoja hii ni tatizi,
Ni hoja tata vizazi hata vizazi,
Siyo hoja ya wajenzi wala wapagazi,
chanzo chake ni nyumbani, aina ya malezi,
Umelelewaje?
Kwani kwenu mko vipi, ni kipi cha thamani,
kwenu shujaa ni yupi, yule mnaye thamini
Nani kwenu ni kapi, asiyetakiwa nyumbani,
Kipi mnachothamini?
Kama nguo ndiyo mali, Elimu ni vuvuzela,
Basi hata wanawali, wamachinga watawala,
Watapenda suruali, elimu kwao jalala
Mnakuzwaje?
Uanaume ni sifa, si maumbile ya jalali
Uanaume si shufaa, au uwe jabali
Uanaume ni kufaa, jamii ikukubali,
Ni sifa ya uongozi.
Siyo kuvunja vitanda, au hodari kufanya,
Uanaume sawa sanda,hutunza si kutapanya,
Uanaume si kupinda, au tabia za panya
Uanaume utu wema
Mwanaume huwa kinga, kiongozi familia,
Hana sifa za kijinga, masuala hufuatilia,
Kama likizuka janga, hawezi kulia lia
Ni sifa ya Utume.
mwanaume ni nani?