Salaam,Shalom!!
(Mithali 19:17)
Amhurumiaye maskini, humkopesha BWANA.
Mungu anachukia sana Umaskini, lakini anawapenda sana maskini,
Mungu ndiye hufukarisha, na ndiye hutajirisha!!
Maskini wa Leo ni tajiri kesho, maana Mungu ndiye huwapandisha maskini na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwashusha wenye viburi.
Mungu amekuwa akikemea sana kuwaonea maskini, hapendi waonewe Wala kuvunjiwa Heshima Yao, kuwachokoza maskini na wajane na yatima ni kugusa mboni ya jicho la Mungu.
Hivi unawezaje kumnyang'anya godoro pekee analolalia maskini baada ya kukopa pesa ya kununulia chakula Kwa ajili ya familia yake,Ujasiri huo umeutoa wapi, watoto wa maskini watajisikiaje kuona baba Yao ananyanganywa godoro pekee la kulalia?
Ujasiri wa kwenda kumpora kanga au kitenge alichojifunika Jirani Yako Kwa sababu ameshindwa kukulipa deni lako unautoa wapi?
Maskini amekuja kwako anakuomba umkopeshe unga Ili akampikie mgeni wake aliyefika usiku huo, unampa Kwa masharti ya kukulipa siku mbili zijazo, Kwa Bahati mbaya, anashindwa kutimiza AHADI yake, ujasiri wa kwenda nyumbani kwake na kuchukua sufuria pekee analotumia kupikia chakula umeutoa wapi?
Mungu Toka juu, anakuangalia, anakudai pesa kiasi Gani Kwa kutolipa ZAKA, mbona hajawahi kukudhalilisha?
Tangu Leo, jifunze kubariki maskini,
Ukimkopesha maskini na akashindwa kulipa, mpe Muda atakulipa atakapopata, kamwe usimdhalilishe. Mungu atakufungulia mlango wa kupata pesa bila kudhalilisha binadamu mwenzio.
Mungu na awabarikie wote wasaidiao binadamu wenziwe, hiyo ndiyo IBADA na DINI ya KWELI.
Aamen
(Mithali 19:17)
Amhurumiaye maskini, humkopesha BWANA.
Mungu anachukia sana Umaskini, lakini anawapenda sana maskini,
Mungu ndiye hufukarisha, na ndiye hutajirisha!!
Maskini wa Leo ni tajiri kesho, maana Mungu ndiye huwapandisha maskini na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwashusha wenye viburi.
Mungu amekuwa akikemea sana kuwaonea maskini, hapendi waonewe Wala kuvunjiwa Heshima Yao, kuwachokoza maskini na wajane na yatima ni kugusa mboni ya jicho la Mungu.
Hivi unawezaje kumnyang'anya godoro pekee analolalia maskini baada ya kukopa pesa ya kununulia chakula Kwa ajili ya familia yake,Ujasiri huo umeutoa wapi, watoto wa maskini watajisikiaje kuona baba Yao ananyanganywa godoro pekee la kulalia?
Ujasiri wa kwenda kumpora kanga au kitenge alichojifunika Jirani Yako Kwa sababu ameshindwa kukulipa deni lako unautoa wapi?
Maskini amekuja kwako anakuomba umkopeshe unga Ili akampikie mgeni wake aliyefika usiku huo, unampa Kwa masharti ya kukulipa siku mbili zijazo, Kwa Bahati mbaya, anashindwa kutimiza AHADI yake, ujasiri wa kwenda nyumbani kwake na kuchukua sufuria pekee analotumia kupikia chakula umeutoa wapi?
Mungu Toka juu, anakuangalia, anakudai pesa kiasi Gani Kwa kutolipa ZAKA, mbona hajawahi kukudhalilisha?
Tangu Leo, jifunze kubariki maskini,
Ukimkopesha maskini na akashindwa kulipa, mpe Muda atakulipa atakapopata, kamwe usimdhalilishe. Mungu atakufungulia mlango wa kupata pesa bila kudhalilisha binadamu mwenzio.
Mungu na awabarikie wote wasaidiao binadamu wenziwe, hiyo ndiyo IBADA na DINI ya KWELI.
Aamen