Ni aibu kwa CHADEMA, Godbless Lema kuwa Mjumbe wa Kamati yake Kuu ya Taifa, nashauri avuliwe ujumbe haraka sana!

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,262
9,714
Ndugu zangu Watanzania,

Kamati kuu ya chama chochote kile ndio chombo Cha juu kabisa Cha kimaamuzi, ndio Taswira ya chama husika,Ndio Nembo ya chama,,Ndicho kitoacho muelekeo na misimamo yake, Ndio Nguzo ya chama,Ndio Tumaini la Chama,Ndio Ngome ya chama,Ndio moyo wa chama wenyewe, ndio kioo cha chama.

Hata ukitaka kukiteka chama chochote kile Basi wewe iteke na kuiweka mfukoni mwako kamati kuu ya chama na wajumbe wake, Ilevye kwanza kamati kuu tu utakuwa umekilevya chama chote mpaka mashinani, penyeza mkono wako na vidole vyako kamati kuu na utakuwa umekishika chama chote mateka na kubaki Unasikilizwa wewe tu kama mfalme hata Kama wewe siyo mjumbe wake kwa sababu kamati kuu ndio sauti ya chama na hivyo ukiishika na Kuiteka hii Basi wajumbe wote wataongea kwa niaba yako Kama makasuku tu,Hii ndio maana halisi ya siasa ni hesabu na ni sayansi.

Kwa mantiki hiyo wajumbe wa kamati kuu Taifa wanapaswa kuchaguliwa kwa umakini mkubwa Sana,Nidhamu kubwa Sana, weledi mkubwa Sana kwa kuwa hao ndio waanzisha na wasambaza Sera itikadi falsafa na ajenda za chama na ndio chama chenyewe na hata ukitaka kukivuruga na kukisambaratisha chama Basi wewe wavuruge na kuisambaratisha kamati kuu.

Wajumbe wake katika kuchaguliwa kwake wanapaswa kuwa Ni watu wenye busara hekima unyenyekevu upeo maarifa na wanaokijuwa chama na historia ya chama, watulivu wa akili,wenye vifua vya kiuongozi na siyo vifua vya kufungia vifungo vya mashati,wanaojuwa wazungumze Nini mbele ya kadamnasi na halaiki ya watu,wanaojuwa kuchambuaa na kuchagua maneno mbele za watu na wanaojiandaa kabla ya kuzungumza.

Nikimtizama na kumfuatilia Godbless Lema mjumbe wa kamati kuu ya Chadema nashindwa kuelewa alipitaje na kushinda kuwa Mjumbe wa kamati kuu,sielewi Ni vipi jina lake lilipitishwa ili agombee,sijuwi Ni busara ipi ilitumika kumpendekeza Lena,maana Ni mtu na kiongozi ambaye ingekuwa Ni CCM asingeweza kuwa hata mjumbe wa kamati ya CCM ngazi ya Tawi, maana Lema Ni mtu asiye Hekima Wala busara Hana adabu Wala staha,mdomo wake hauna chujio la kiuongozi,Hana breki Wala nati za kuufung mdomo wake pasipo stahiki kuzungumza,ujasiri wake upo katika ujinga na maneno ya kijinga na karaha mbele za watu wenye busara na hekima,Hana muunganiko mzuri wa ubongo wake na mdomo wake ndio sababu anaweza kuropoka chochote na lolote lile.

Huwezi ukapata chochote Wala maarifa yoyote kutoka kwa Lema ,usije ukathubuti ukamwambia Siri yoyote Ile Lema maana itakuwa Ni sawa na kutamka Jambo Hilo katika makutano ya watu njia panda,maana kesho Ni lazima ataropoka jukwaani au bar.

Leo Lema amerejea kutoka Canada na kuja Tanzania na kuanza kuwatukana watanzania,kuwadhalilisha watanzania, kuwakebehi watanzania,kuwatupia kila aina ya maneno ya kuudhi na kutia hasira, Hii Ni Baada ya kusahau namna vijana anaowatukana leo walivyompigania Arusha,walivyokesha viwanjani ili atolewe gerezani,walivyohatarisha maisha Yao, walivyo pigwa mabomu ya machozi na virungu kwa sababu yake,Amesahau michango alivyokuwa akichangiwa na akina mama wa vicoba bodaboda n.k walivyomsaidia kwa michango Yao ya Hali na Mali kumchangia, lakini leo anasema Ni maskini na wanalaana.

Hili Ni doa kwa chama chote Cha chadema, Ni dharau, Ni kauli ya chama chote Cha chadema kwa kuwa haijajitenga na kauli hii ya mjumbe wake wa kamati kuu.

Imeandikwa Amdhihakiye maskini humsuta muumba wake Na Amhurumiaye maskini humkopesha Mwenyezi MUNGU na atalipwa kwa Jambo Hilo jema, Dharau za Lema kwa watanzania Ni dhihaka kwa Mwenyezi Mungu, Ni dharau kwa muumba ambaye siku zote Tangu Enzi na Enzi Mwenyezi MUNGU amekuwa akiwatazama kwa jicho la huruma na upendo.

Lema na chadema yake watwambie Ni nchi gani isiyo na maskini? Ni Taifa lipi lisilo na maskini? Ni wapi huko? Au kwa kuwa yeye Ameukata na kushiba Kodi zetu kwa miaka yake ya ubunge ndio unamfanya aje atutukane watanzania? Ndio unamfanya ajione mwenye Heri? Mbarikiwa? Kupata Ni Majaliwa ya Mwenyezi MUNGU na anayetoa ridhiki Ni Mwenyezi MUNGU. Sasa kwanini aje kuwatukana watanzania kwa kuwa yeye kapata? Kwanini awaone watoto wa wenziye wanaojihangaikia mitaani kujitafutia ridhiki zao kwa njia Halali kuwa wamelaaniwa? Anajuwa mtoto wake maisha atakayo ishi huko siku za usoni? Anafikiri haa anaosema wamelaaniwa walipenda wawe hivyo? Kwamba Mungu kawalaani watu wake aliowaumbA kwa mfano wake?

Chadema inapaswa imuonye Lema na kumvua nafasi za uongozi alizonazo ndani ya chama kwa matendo yake na kauli zake za kifedhuli na kibuli kwa watanzania,maana nje na hapo itaonekana Ni msimamo wa chama dhidi ya watanzania waliowafikisha hapo walipo ambapo Sasa wamelewa na pesa walizo nazo.

Ni Bora jina Jema kuliko Mali nyingi,Njia ya mpumbavu imenyooka machoni pake pekee, Mali na fedha Ni vya kupita tu, mtu hukumbukwa kwa utu wake na siyo Mali alizo nazo maana hizo si kitu na hupukutika Kama Maua juani.

Msifadhaike mioyoni mwenu Watanzania kwa kauli hizi za ujeuri za chadema maana IPO CCM yenye uchungu na maisha yenu, yenye kujuwa shida na kero zenu, yenye kujuwa kuwa maisha ni hatua, yenye kuhangaika juu ya maisha yenu, yenye kukosa usingizi juu ya changamoto zenu, Tuiamini na kuiunga mkono ituvushe kwa kuwa imeonyesha uwezo wa kiuongozi katika kuwatumikia na kuwaleteeni maendeleo.

Tumuunge mkono Rais wetu mpendwa kipenzi Cha watanzania na Tumaini la watanzania katika kuwaletea maendeleo, Tuendelee kumwombea Afya njema na nguvu za Kuendelea kututumikia, Tuendelee kufunga na kuomba ili mwenyezi Mungu ampiganie na kumlinda Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani, Tumwamini na tumpe ushirikiano wetu wote.

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
 
Maoni yake yaheshimiwe
1678383683403.png
 
Back
Top Bottom