Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,305
- 33,763
Niweke sawa kauli ifuatayo 'makabila makubwa' a.k.a Wachaga, Wahaya n.k. Ukweli ni kuwa haya ni makabila mdogo. Mkoa wa Kilimanjaro wenye wachaga na wapare una watu milioni 2.5. Mkoa wa Kagera ni chini ya hapo. Wasukuma na wanyamwezi peke yao wakiamua kumchagua rais wa nchi hii atashinda katika sanduku la kura bila kuchakachua au kampeni. Haya ndiyo makabila makubwa.Wahaya na wachaga ni makabila yaliyopiga hatua si makabila makubwa.
Pili lazima tuangalie Nyerere aliichukua nchi katika hali gani. Wakati akiapishwa kulikuwa na wasomi wachache wakitoka makabila ya wahaya na wachaga. Hii ni kwasababu ya historia na mtazamo wa ukoloni na maendeleo ya vyama vya ushirika.
Baraza la mawaziiri wakati wa Nyerere lilikuwa na watu mchanganyiko na kuna wakati wengi walitoka mikoa ya Kagera na Kilimanjaro kwa vile walikidhi mahitaji ya wakati huo kiusomi. Nawakumbuka akina CD Msuya, Mzee Mtei, Elinawinga, Eliufoo, Peter Kisumo, Amir Jamal, Annur Kassam, Joseph Rwegasira n.k. Hata wakuu wa mikoa kama kina Dr Kleruu. Kwahiyo Nyerere kuna wakati alilazimika kuwatumia waliokuwa na uwezo na hii haina maana wao walipaswa kuwa marais! hell no! kuna nafasi moja tu ya rais at a time.
Si lazima msomi awe rais kwasababu usomi pekee si sifa ya uongozi. Watu waliomzunguka Tonny Blair ni wasomi waliobobea lakini Tonny ni Mwalimu wa kawaida tu. Kama usomi ndio sifa ya uongozi pekee basi tusingekuwa na rais Mwinyi. Kama usomi ndio sifa pekee basi Mugabe aliyebobea asingeipeleka Zimbw hapo ilipo. Lakini pia tungekuwa na marais wangapi ili tukidhi haja ya wasomi wa makabila husika?
Nyerere alitaifisha shule kwa nia njema ya kila mtoto apate kidogo. Nilipokuwa Musoma miaka ya 70 mji mzima ulikuwa na shule za Agakhan(Mkendo), Hindu Mandal(Iringo) na Catholic (Mwembeni), kama zisingetaifishwa kamji kale kangekuwa na shule mbili au tatu za serikali. Je wengine wangesoma wapi.? Nguvu ya kujenga shule kwa bajeti ya wakati huo na vipaumbele vya afya isingetosha kuelekeza katika maeneo yote kwa shule tu. Leo kuna maelfu ya wasomi waliokuwa wachunga mbuzi wamefaidika na mpango huo.
Je mpango huo ulikuwa wa haki na sahihi kwa kila mtu? tujadili faida na hasara na si kusema 'mbaya au mzuri tu bila hoja'
TV! Hili linanishagaza sana. Zanzibar ni moja ya nchi chache kuwa na TV tena coloured. Je kuwekeza katika TV kuliwasaidia Wazanzibar kinamna gani!
Kwanini tusiangalie Reli ya Uhuru, Reli ya Tanga-Dar ambazo ni infrastructure za maisha tulizoshindwa kuweka mabehewa tu? Kwanini tusingalie UFI, Urafiki, Mwatex, Mutex, Tanganyika Packers, Swala, Magunia, Moproco, Polyster, Tancut almas n.k vilivyotengeneza maelefu ya ajira na uchumi!
Dar miaka ya 70 na 80 kulikuwa na shift work kama nchi nyingine. Wanafunzi walipata part time na wapo waliofanya kazi mbili kwa siku. Je ilikuwa ni busara kwa Mwalimu kuomba misaada ya kujiimarisha kiviwanda au ni bora angeomba msaada wa kuwa na TV?
Mwalimu akiondoka 'Literacy level' ilikuwa 90-95% na UN ikasema Tz ni mfano, leo tumerudi nyuma na kufikia chini ya 70%, je ni lipi jema kuwekeza katika elimu na maendeleo au kuwaacha watoto wasiende shule wabaki wakiburudika na Joti? Mazingira ya wakati huu na vipaumbele ni tofauti na nyakati baada ya uhuru tusisahau.
Miaka ya 70 mtihani wa darasa la saba ulikuwa wa kitaifa. Kati ya watoto 600 robo tatu ilitoka K'njaro, Kagera na Mbeya.
Ndipo mpango wa nafasi kimikoa ukaanza. Ni kweli mikoa ya K'njaro, Kagera iliathirika sana, lakini ilikuwa ni changamoto nzuri kwani kwa kutumia elimu waliokwishaipata na kutambua umuhimu wake wakaanzisha shule za Private na hakika mwaka 2003 wilaya changa ya Mwanga ilikuwa na sekondari nyingi kuliko mkoa wa Lindi pamoja na 'affirmative action' Lindi iliyopata.
Alichofanya mwalimu ni '' positive affirmativa action' kama ya wabunge maalumu au shule za boarding kwa wamasai na wanyaturu ili kuinua jamii hizo ambazo hazikuwa tayari kiushindani. Tunaweza kulijadili pia kama affirmative action ina umuhimu kwa sasa.
Tusisahau changamoto alizopata mwalimu kama uhaba wa wasomi, kuvunjika EA, vita vya Kagera n.k. Ni ukweli usiopingika kuwa maendeleo yaliyopatikana miaka 23 ya mwalimu ni sawa au makubwa kuliko ya wamu zote tatu.
Kama maendeleo ni TV na kompyuta basi tumepiga hatua sana, lakini kama ni kuwekeza katika infrastructure, viwanda, elimu na afya basi tumerudi nyuma ya mwaka 1961.
Kama Nyerere alikuwa mkabila, Amir Jamal, Annur Kaasam, Leader sterling walikuwa wa kabila lipi dhidi ya kabila lipi? Viongozi hawa wamedumu madarakani katika nafasi nyeti karibu kipindi chote cha Mwalimu.
Tuangalie baraza la mawaziri toka aingie madarakani, makatibu wakuu, wakurugenzi n.k kabla ya kutoa hukumu isiyokuwa na vielelezo vinavyojitosheleza.
Ni ukweli pia kuwa mwalimu alikuwa na mapungufu yake na mimi nakubali kuwa kuua vyama vya ushirika au kutaifisha mashamba na kuyaacha mapori halikuwa wazo zuri ingawa kama mtawala huenda lilikuwa zuri kwake. Nafahamu alikuwa Mwanadamu na sote ni viumbe dhaifu tusio na utimilifu, tupime mazuri na mabaya yake kwa mizania na sio dhania.
Pili lazima tuangalie Nyerere aliichukua nchi katika hali gani. Wakati akiapishwa kulikuwa na wasomi wachache wakitoka makabila ya wahaya na wachaga. Hii ni kwasababu ya historia na mtazamo wa ukoloni na maendeleo ya vyama vya ushirika.
Baraza la mawaziiri wakati wa Nyerere lilikuwa na watu mchanganyiko na kuna wakati wengi walitoka mikoa ya Kagera na Kilimanjaro kwa vile walikidhi mahitaji ya wakati huo kiusomi. Nawakumbuka akina CD Msuya, Mzee Mtei, Elinawinga, Eliufoo, Peter Kisumo, Amir Jamal, Annur Kassam, Joseph Rwegasira n.k. Hata wakuu wa mikoa kama kina Dr Kleruu. Kwahiyo Nyerere kuna wakati alilazimika kuwatumia waliokuwa na uwezo na hii haina maana wao walipaswa kuwa marais! hell no! kuna nafasi moja tu ya rais at a time.
Si lazima msomi awe rais kwasababu usomi pekee si sifa ya uongozi. Watu waliomzunguka Tonny Blair ni wasomi waliobobea lakini Tonny ni Mwalimu wa kawaida tu. Kama usomi ndio sifa ya uongozi pekee basi tusingekuwa na rais Mwinyi. Kama usomi ndio sifa pekee basi Mugabe aliyebobea asingeipeleka Zimbw hapo ilipo. Lakini pia tungekuwa na marais wangapi ili tukidhi haja ya wasomi wa makabila husika?
Nyerere alitaifisha shule kwa nia njema ya kila mtoto apate kidogo. Nilipokuwa Musoma miaka ya 70 mji mzima ulikuwa na shule za Agakhan(Mkendo), Hindu Mandal(Iringo) na Catholic (Mwembeni), kama zisingetaifishwa kamji kale kangekuwa na shule mbili au tatu za serikali. Je wengine wangesoma wapi.? Nguvu ya kujenga shule kwa bajeti ya wakati huo na vipaumbele vya afya isingetosha kuelekeza katika maeneo yote kwa shule tu. Leo kuna maelfu ya wasomi waliokuwa wachunga mbuzi wamefaidika na mpango huo.
Je mpango huo ulikuwa wa haki na sahihi kwa kila mtu? tujadili faida na hasara na si kusema 'mbaya au mzuri tu bila hoja'
TV! Hili linanishagaza sana. Zanzibar ni moja ya nchi chache kuwa na TV tena coloured. Je kuwekeza katika TV kuliwasaidia Wazanzibar kinamna gani!
Kwanini tusiangalie Reli ya Uhuru, Reli ya Tanga-Dar ambazo ni infrastructure za maisha tulizoshindwa kuweka mabehewa tu? Kwanini tusingalie UFI, Urafiki, Mwatex, Mutex, Tanganyika Packers, Swala, Magunia, Moproco, Polyster, Tancut almas n.k vilivyotengeneza maelefu ya ajira na uchumi!
Dar miaka ya 70 na 80 kulikuwa na shift work kama nchi nyingine. Wanafunzi walipata part time na wapo waliofanya kazi mbili kwa siku. Je ilikuwa ni busara kwa Mwalimu kuomba misaada ya kujiimarisha kiviwanda au ni bora angeomba msaada wa kuwa na TV?
Mwalimu akiondoka 'Literacy level' ilikuwa 90-95% na UN ikasema Tz ni mfano, leo tumerudi nyuma na kufikia chini ya 70%, je ni lipi jema kuwekeza katika elimu na maendeleo au kuwaacha watoto wasiende shule wabaki wakiburudika na Joti? Mazingira ya wakati huu na vipaumbele ni tofauti na nyakati baada ya uhuru tusisahau.
Miaka ya 70 mtihani wa darasa la saba ulikuwa wa kitaifa. Kati ya watoto 600 robo tatu ilitoka K'njaro, Kagera na Mbeya.
Ndipo mpango wa nafasi kimikoa ukaanza. Ni kweli mikoa ya K'njaro, Kagera iliathirika sana, lakini ilikuwa ni changamoto nzuri kwani kwa kutumia elimu waliokwishaipata na kutambua umuhimu wake wakaanzisha shule za Private na hakika mwaka 2003 wilaya changa ya Mwanga ilikuwa na sekondari nyingi kuliko mkoa wa Lindi pamoja na 'affirmative action' Lindi iliyopata.
Alichofanya mwalimu ni '' positive affirmativa action' kama ya wabunge maalumu au shule za boarding kwa wamasai na wanyaturu ili kuinua jamii hizo ambazo hazikuwa tayari kiushindani. Tunaweza kulijadili pia kama affirmative action ina umuhimu kwa sasa.
Tusisahau changamoto alizopata mwalimu kama uhaba wa wasomi, kuvunjika EA, vita vya Kagera n.k. Ni ukweli usiopingika kuwa maendeleo yaliyopatikana miaka 23 ya mwalimu ni sawa au makubwa kuliko ya wamu zote tatu.
Kama maendeleo ni TV na kompyuta basi tumepiga hatua sana, lakini kama ni kuwekeza katika infrastructure, viwanda, elimu na afya basi tumerudi nyuma ya mwaka 1961.
Kama Nyerere alikuwa mkabila, Amir Jamal, Annur Kaasam, Leader sterling walikuwa wa kabila lipi dhidi ya kabila lipi? Viongozi hawa wamedumu madarakani katika nafasi nyeti karibu kipindi chote cha Mwalimu.
Tuangalie baraza la mawaziri toka aingie madarakani, makatibu wakuu, wakurugenzi n.k kabla ya kutoa hukumu isiyokuwa na vielelezo vinavyojitosheleza.
Ni ukweli pia kuwa mwalimu alikuwa na mapungufu yake na mimi nakubali kuwa kuua vyama vya ushirika au kutaifisha mashamba na kuyaacha mapori halikuwa wazo zuri ingawa kama mtawala huenda lilikuwa zuri kwake. Nafahamu alikuwa Mwanadamu na sote ni viumbe dhaifu tusio na utimilifu, tupime mazuri na mabaya yake kwa mizania na sio dhania.