Mwalimu Nyerere na ukabila

Dr Lizzy

Platinum Member
May 25, 2009
30,806
59,286
Habari zenu jamani?!

Naomba nianze kwa kusema ukweli kwamba mimi sikuwepo kipindi cha utawala wa Mwl na hata alipofariki nilikua mdogo sana hivyo sikuwahi kujua kwanini watu wengi walikua wanampenda sana huku bado kukiwa na mambo mengi hasi yanayosemwa juu yake.Nafurahi kwamba mwaka huu nimeweza kutumia muda wangu kiasi nikasoma vitabu kadhaa kumhusu...makusanyo ya hotuba zake pamoja na vitabu alivyoandika mwenyewe.Kutokana na niliyoyasoma niliridhika kwamba sifa zote anastahili...pia kukosolewa maana yeye kama mtu mwingine yeyote yule makosa hatuwezi tuyakwepa.

Katika vitu ambavyo Mwl alivisimamia haswa ni usawa.Hakutaka kabila moja lijione/jisikie liko juu ya jingine na kutengeneza matabaka.Sasa swali langu nnaloomba mnisaidie ni hili....ule msemo au sijui niyaite madai ya kwamba Mwl aliwahi kusema makabila fulani hayafai kupewa uongozi wa juu wa nchi ni wa kweli au ni propaganda za waliomchukia?!Nauliza hivi kwasababu niliyoyasoma juu yake hayaendani kabisa na madai haya...na wala haileti maana kusikia kwamba aliyepigania usawa ndie aliyekua wa kwanza kutengeneza matabaka lilipokuja swala la uongozi!!!

Naomba majibu kama yapo yawe na vielelezo na yasiwe maneno ya kusikika na kufikirika tu ili tusiojua tujifunze kitu.
Asanteni!
 
Wakati Ule Nchi Maendeleo yalikuwa ya Upande Mmoja na Siasa zetu ziliashiria wananchi kuendelea kimpango Mfano
Wachagga na Wahaya sisi tulikuwe tumepata Elimu na wakati wa Mkoloni tulishika Madaraka sasa kama Nyerere asinge fuatilia hiyo nchi ingekuwa inatawaliwa na makabila makubwa au makabila yaliyokuwa na Elimu
 
Wakati Ule Nchi Maendeleo yalikuwa ya Upande Mmoja na Siasa zetu ziliashiria wananchi kuendelea kimpango MfanoWachagga na Wahaya sisi tulikuwe tumepata Elimu na wakati wa Mkoloni tulishika Madaraka sasa kama Nyerere asinge fuatilia hiyo nchi ingekuwa inatawaliwa na makabila makubwa au makabila yaliyokuwa na Elimu
Kwani nchi inaongozwa na kabila au mtu?!
 
Ijumaa usiku inaonekana jukwaa la mapenzi kweli linakuwa limedoda watarudi wasubiri, tafsiri yangu tu usinijie juu.
 
Kwani nchi inaongozwa na kabila au mtu?!

Sio kuongozwa tu Madaraka Mbalimbali Nchini yangeegemea hayo Makabila na Usawa usingekuwepo Mfano Mzuri angalia Jirani zetu Kenya na Kabila la Kikikuyu wao walipendwa na wakoloni; wana Elimu zaidi ya wengine; Ardhi Zaidi ya Wengine; Mji bora zaidi ya wengine (NAIROBI) Wengi wana Madaraka na ni Mabwanyenye
 
Aliyataja makabila yanayokula ndizi kwa sana ambayo yalitafsiriwa kama Wachagga,Wahaya na Wanyakyusa ambao walikuwa juu kielimu na uwingi na alipendelea nafasi za juu(urais,makamu na waziri mkuu) ushikwe na makabila madogo ili makabila haya yasi-manopolize power.Hajatamkaa hadharani lakini aliwaambia watu wengi in private angependa iwe hivo.
 
Habari zenu jamani?!

Naomba nianze kwa kusema ukweli kwamba mimi sikuwepo kipindi cha utawala wa Mwl na hata alipofariki nilikua mdogo sana hivyo sikuwahi kujua kwanini watu wengi walikua wanampenda sana huku bado kukiwa na mambo mengi hasi yanayosemwa juu yake.Nafurahi kwamba mwaka huu nimeweza kutumia muda wangu kiasi nikasoma vitabu kadhaa kumhusu...makusanyo ya hotuba zake pamoja na vitabu alivyoandika mwenyewe.Kutokana na niliyoyasoma niliridhika kwamba sifa zote anastahili...pia kukosolewa maana yeye kama mtu mwingine yeyote yule makosa hatuwezi tuyakwepa.

Katika vitu ambavyo Mwl alivisimamia haswa ni usawa.Hakutaka kabila moja lijione/jisikie liko juu ya jingine na kutengeneza matabaka.Sasa swali langu nnaloomba mnisaidie ni hili....ule msemo au sijui niyaite madai ya kwamba Mwl aliwahi kusema makabila fulani hayafai kupewa uongozi wa juu wa nchi ni wa kweli au ni propaganda za waliomchukia?!Nauliza hivi kwasababu niliyoyasoma juu yake hayaendani kabisa na madai haya...na wala haileti maana kusikia kwamba aliyepigania usawa ndie aliyekua wa kwanza kutengeneza matabaka lilipokuja swala la uongozi!!!

Naomba majibu kama yapo yawe na vielelezo na yasiwe maneno ya kusikika na kufikirika tu ili tusiojua tujifunze kitu.
Asanteni!

Kwanza unakosea unaposema watu wengi walimpenda sana. Naomba kukufahamisha kuwa mimi nilikuwepo kabla, alipokuwepo, na baada yake. Nyerere hakupendwa na wengi kama unavyotakiwa kufikiria, Nyerere alilazimisha kupendwa, ukionesha kumpinga unapotezwa au unaswekwa ndani. Nyerere kisha koswa kupinduliwa mara nyingi tu kuliko Rais mwingine yoyote wa Tanzania.

Mengine hayo utajaza mwenyewe.
 
Kwanza unakosea unaposema watu wengi walimpenda sana. Naomba kukufahamisha kuwa mimi nilikuwepo kabla, alipokuwepo, na baada yake. Nyerere hakupendwa na wengi kama unavyotakiwa kufikiria, Nyerere alilazimisha kupendwa, ukionesha kumpinga unapotezwa au unaswekwa ndani. Nyerere kisha koswa kupinduliwa mara nyingi tu kuliko Rais mwingine yoyote wa Tanzania.

Mengine hayo utajaza mwenyewe.

Mkuu nami nilikuwepo na nipo hadi sasa. Pamoja na kuwasweka ndani watu lakini Nyerere alikuwa akipendwa na wengi. Huwezi kupendwa na kila mtu lazima wawepo wengine ambao hawakupendi lakini kwa ujumla ni kwamba alikuwa anapendwa. Kuhusu kukoswa koswa kupinduliwa ukilinganisha na Marais wengine utakuwa hutendi haki kwa kuwa kwenye miaka ya 90s Africa ilianza kunusa demokrasia ukilinganisha na miaka ya 60s na 70s ambapo demokrasia kwa Africa ilikuwa ndoto. Kipindi baada ya uhuru kwa nchi nyingi Africa kilitawaliwa na ubabe pamoja na udikteta kwa hiyo waroho wa Madaraka waliona hakuna njia nyingine ya kuchukua hatamu za uongozi zaidi ya kutumia mtutu wa bunduki. Miaka baada ya uhuru kulikuwa hakuna chaguzi za ushindani africa, vyama vingi vya siasa vilipigwa marufuku.

Kuhusu mada ni kwamba Nyerere hakuwa mkabila wa waziwazi lakini alikuwa na vimelea vya ukabila. Hakupenda Makabila kama Wachaga ambao wengi waliosomeshwa kupitia KNCU, Wahaya kupitia KCU pamoja na Wanyakyusa (ambao sijui walipata wapi bahati ya kusoma) waje kuchukua uongozi wa juu wa nchi kwa kuwa wangekuwa na solidarity na kupeana madaraka na kuyapuuza makabila mengine kama wakurya ambao elimu yao ilikuwa chini sana baada ya wakoloni kuwaona kuwa wanaweza tu kufungua bunduki na kupiga na wala siyo kufungua kurasa za vitabu.
 
Hongera sana Lizzy nilikuwa sifikirii kama na huku unakuwepo,hongera kwa mada yenye akili.BACK TO TOPIC,sikumbuki kuhusu hili kama alisema direct lakini wenye kumbukumbu watakujuza!
 
Yaani nyinyi watoto mliozaliwa baada ya nyerere kunga'tuka hamumjui vizuri huyo nyerere

alipoaapishwa urais,hotuba yake ya kwanza alisema

wale waliokosa upendeleo wakati wa mkoloni watapendelewa

lakini yaliyofuata ni maajabu

aliwafunga na kulivunja baraza la wazee la tanu

ambalo ndilo lilipigania uhuru na kumuwezesha yeye akubalike

akabadili historia

badala ya kusema chama cha taa kilibadilishwa kuwa tanu

yeye akasema nyerere aliunda tanu.....

Wachaga na wahaya kwa kuwa walikuwa na nguvu mfano vyama vya ushirika vya wachaga na wahaya

akavivunja huku

akiiimarisha vyama vya ushirika vya mikoa mingine

magazeti huru akapiga marufuku,ikabaki gazeti la uhuru na mzalendo

wahariri wenye mawazo huru mfano yule mama wa south afrika aliekuwa mhariri wa daily news

aliwatimua............

Vyama vya siasa marufuku........ikabaki tanu peke yake


akasema tuunganishe afrika mashariki umoja ni nguvu,wakati huo huo

jumuia ya waislamu ya afrika mashariki akaivunja,akawa undia waislamu bakwata....

Shule za wahindi waislamu nazo zikabebwa pamoja na shule za makanisa......

Akamuweka kawawa ndio mshauri wake mkuuu

na dini zikawekwa kando,ushirikina na watu wasio na dini kama

kingunge na wengine wakapewa kipaumbele.......

Na mengineyo...meeengi tu
 
Kila aliempinga alionja joto yajiwe

waulize kina bibi titi,kambona,edwin mtei na wengine weengi
 
Sio kuongozwa tu Madaraka Mbalimbali Nchini yangeegemea hayo Makabila na Usawa usingekuwepo Mfano Mzuri angalia Jirani zetu Kenya na Kabila la Kikikuyu wao walipendwa na wakoloni; wana Elimu zaidi ya wengine; Ardhi Zaidi ya Wengine; Mji bora zaidi ya wengine (NAIROBI) Wengi wana Madaraka na ni Mabwanyenye
Hayo ni mawazo yakufikirika tu...hamna mwenye uhakika kwamba kama hilo lingetokea nchi ingeenda kombo(zaidi ya ilivyo) au pengine tungekua mbali sana kimaendeleo!Kama kweli alijitahidi kuzuia/kushawishi mkabila haya yasipate uongozi wa juu ina maana kwamba alikua mbinafsi sana kwa kuinyima Tanzania nafasi ambayo ingeweza kutufikisha mbali!Swala la kupeana madaraka hata kama sio ndani ya makabila hata sasa hivi lipo...kama hili hakuliona inawezekana hakuweza kuona faida ya kuifanya Tanzania nchi yenye demokrasia ya kweli na sio danganya toto!!
 
Nyerere hajawahi kusema makabila fulani Tanzania hayastahili uongozi wa aina fulani. Umeona vyema kwani angefanya hivyo ingekuwa ni kwenda kinyume kabisa na yote aliyoyasimamia na kuyaamini. Hii ni mojawapo ya myths ambazo zimetengenezwa.
Hakusema kabisa au hakusema kwa uwazi?!
 
Kwanza unakosea unaposema watu wengi walimpenda sana. Naomba kukufahamisha kuwa mimi nilikuwepo kabla, alipokuwepo, na baada yake. Nyerere hakupendwa na wengi kama unavyotakiwa kufikiria, Nyerere alilazimisha kupendwa, ukionesha kumpinga unapotezwa au unaswekwa ndani. Nyerere kisha koswa kupinduliwa mara nyingi tu kuliko Rais mwingine yoyote wa Tanzania.Mengine hayo utajaza mwenyewe.
Asante kwa kunirekebisha ila bado naamini waliompenda wanazidi walio/wanaomchukua...au labda tuseme hawakumtambua sawasawa kiasi cha kuamini aliwatakia mema hivyo hawana malalamiko juu yake. Binafsi naamini alikua dikteta wa kichinichini..wale waliokua karibu yake tu ndo wanaojua ni kwa jinsi gani hakupenda upinzani!!
 
Asante kwa kunirekebisha ila bado naamini waliompenda wanazidi walio/wanaomchukua...au labda tuseme hawakumtambua sawasawa kiasi cha kuamini aliwatakia mema hivyo hawana malalamiko juu yake. Binafsi naamini alikua dikteta wa kichinichini..wale waliokua karibu yake tu ndo wanaojua ni kwa jinsi gani hakupenda upinzani!!

Ukweli ni kwamba Nyerere alikuwa dikteta kwa definition ya udikteta ya Ulaya Magharibi (by then). Ila kwa viwango vya Africa kwa wakati huo Nyerere alikuwa nafuu sana kulinganisha na viongozi wengine Madkiteta wa Africa ambao walikuwa wakiwaua wapinzani wao kwa maelfu. Nyerere alikuwa akiwanyima uhuru wapinzani wake kwa kuwapeleka huko vijijini na hawakutakiwa kufika mjini kujua nini kinaendelea. Mfano Kasanga Tumbo na Mzee Mapalala! Alikuwa Dikteta ila alikuwa si muuaji kama madikteta wengine wa Afrika wa enzi zake.
 
Kila aliempinga alionja joto yajiwewaulize kina bibi titi,kambona,edwin mtei na wengine weengi
Well kwa hayo uliyoyasema hapo juu nadhani mwl alichangia sana kutusimamisha sehemu moja tu kwenye mstari wa maendeleo!Kama angetoa uhuru kwa wote wenye mawazo mazuri kusikika hata kama yalipingana na yake tungekua tumeendelea sana kisiasa!
 
Ukweli ni kwamba Nyerere alikuwa dikteta kwa definition ya udikteta ya Ulaya Magharibi (by then). Ila kwa viwango vya Africa kwa wakati huo Nyerere alikuwa nafuu sana kulinganisha na viongozi wengine Madkiteta wa Africa ambao walikuwa wakiwaua wapinzani wao kwa maelfu. Nyerere alikuwa akiwanyima uhuru wapinzani wake kwa kuwapeleka huko vijijini na hawakutakiwa kufika mjini kujua nini kinaendelea. Mfano Kasanga Tumbo na Mzee Mapalala! Alikuwa Dikteta ila alikuwa si muuaji kama madikteta wengine wa Afrika wa enzi zake.
Basi hakua mshindani hata kidogo....inawezekana alikua anaogopa sana upinzani!
 
Well kwa hayo uliyoyasema hapo juu nadhani mwl alichangia sana kutusimamisha sehemu moja tu kwenye mstari wa maendeleo!Kama angetoa uhuru kwa wote wenye mawazo mazuri kusikika hata kama yalipingana na yake tungekua tumeendelea sana kisiasa!

kuna story ameandika edwin mtei
kwenye kitabu chake ukiisoma

na ukisikia uvumi kuwa alikuwa na matatizo ya kama ugonjwa hivi wa mentall hivi unaweza connect the dots

mfano nyerere alikuwa impulsive sana

analipuka lipuka mno....

kwenye kitabu mtei anasema aliwapeleka wazungu wa imf ikulu,
nyerere badala hata ya kuwasikilza na kukataa,akasusa kuonana nao.
wakati mwanzo alikubali waje ikulu.
yaani aibu tupu,mtei akamkuta nyerere yuko nje ya ikulu kanuna hataki hata kuongea...

na ukichanganya na jinsi zoezi la vijiji vya ujamaa lilivyopelekwa

yaani watu walihamishwa wakapelekwa kwenye mapori waanzishe hivyo vijiji wengine wakaliwa na simba

na ukiangalia mfano sera yake ya marufuku magari,ni baiskeli tu

unaweza ona
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom