1. wanasema baadhi ya policy za manunuzi ya mitambo/products imepitwa na wakati!
2. na kwamba value of our money iwe ndio kigezo cha ku-overide standards zilizopo....dah
3. na kwamba eti hatuna option nyingine, bali ni kununua hiyo mitambo michakavu otherwise tuende gizani!
4. na kwamba mbona tunanunua mitambo ya IPTL ambayo ni ya zamani zaidi ya hii ya Dowans
5. na kwamba mtaalamu aliletwa kutathmini ili kuona kama mitambo michakavu ni value for our money or not......DAMN!
NB:
Hivi tulinunua/tulikodisha ile Ndege (sijui Boeing sijui AirBus) for value of our money.....kwa sababu pia tulitumia wataalamu kutathmini ile ndege Vs value of our money.....eehh
.......I mean mimi sio mhandisi, lakini i don't know what kind of a nation we are trying to build here........
Mkuu Ogah,
Labda kama huelewi maana ya value for money. Toka lini value for money ika overide standards zilizopo?
Mnaingiza siasa kwenye kila kitu na ndio matatizo ya Tanzania.
Value for money inaendana na quality, inaendana na return ambayo inaweza kupatikana kutokana na investment fulani.
Watanzania wengi sasa wamekuwa wafuata upepo. Eti Zitto katetea ununuzi wa mitambo tayari kasaliti Watanzania, kapewa pesa na mafisadi, nonesense!
Ningelikuwa mimi mhusika ningependekeza kununuliwa baada ya kuangalia sheria zilizopo na kisha ningekuwa tayari kuwajibika kama hasara ingetokea kutokana na ununuzi huo.
Kwenye hili suala watu mmegubikwa na chuki binafsi kuliko reasoning, sawa wengi hatumpendi Rostam, lakini je ndio tuathiri nchi nzima kwa ajili ya kumkomoa Rostam?
Hizi siasa za personalities ndio mwanzo wa matatizo makubwa kwa Afrika. Kama Rostam ana makosa, mpelekeni jela lakini sio kwamba hata jambo la maana kwasababu tu Rostam anahusika basi ni kupinga tu.
Leo hii wanasiasa eti wanajua wapi kwa kununua mitambo kwa bei rahisi. Ununuzi wa mitambo ni sehemu ndogo tu, matatizo makubwa yako kwenye operational cost.
Tutapoteza miezi kujadili jambo moja huku wananchi Tanzania hawana umeme na hakuna kinachofanyika.
Sawa endeleeni na siasa zenu za do nothing! Kama Tanesco wanapesa, sasa wanasubiri nini? Si wakanunue hiyo mitambo mipya na nchi iache kuhangaika na matatizo ya umeme?
Ni rahisi sana kwa mimi hapa Mtanzania nikiwa London kupiga siasa, kwasababu sipati hasara ambazo wananchi na wafanyabiashara walioko Tanzania wanapata shauri ya matatizo ya umeme.