Mwachieni Gire, nunueni mitambo ya Dowans!

Hapa simuelewi huyu Ngereja. Alisema hivyo ili kuonyesha kuwa kununua mitambo ya DOWANS ni jambo sahihi au?

Pia nimeshangaa sana kusikia Zito anaunga mkono jambo hili (soma Nipashe ya leo). Nadhani tunahitaji majibu zaidi toka kwa Zito ili tuweze kumuelewa vizuri. Kama Richmond/DOWANS ilisababisha serikali yote kuvunjika lakini leo tunataka kununua mitambo yao, basi kuna haja ya Bunge kufuta azimio lake, kuiomba radhi serikali kwa kuikosea adabu na hasa EL na mawaziri wengine walioachia ngazi. Baada ya hapo tuamue kuwalipa fidia wote walioguswa na huo uamuzi mbovu wa bunge ndo tukanunue hiyo mitambo. Kama ni mimi, ningekubali tukae gizani hata miaka 2 kuliko kuingia kwenye dili na kampuni ambayo ina utata.
 
Katika mahojiano aliyofanya Waziri wa nishati na madini mheshimiwa sana Ngereja na gazeti la Mwananchi (tolea la leo tarehe 27.02.2009) alipokuwa aking`aka kwa ujasiri kutetea uamuzi wa kununua mitambo mitumba ya Dowans aliamua kusema kwa ujasiri kuwataja mafisadi wengine bila kificho ambao wana tabia ya kukiuka sheria ya manunuzi kwa kununua mitumba na wamekuwa wakiachwa na srikali,bunge na mahakama bila kukemewa.

Mafisadi hao aliowataja bila kumeza maneno ni shirika la Ndege la Tanzania.Amewataja kuwa huwa wananunua ndege mitumba kinyume na sheria ya Manunuzi na hawapingwi.

Hongera mheshimiwa kututajia mafisadi wengine.Je kuna Waziri mwingine jasiri kama Waziri Ngeleja atutajie wengine wanaonunua mitumba kinyume na sheria ya manunuzi?

Mawaziri wengine igeni ujasiri wa Ngereja tunaomba tajaneni.Nadhani sasa vita ya ufisadi inaelekea kuzuri maana na mawaziri wameanza kuiunga mkono.Keep up Ngereja taja wengine.

Bunge mpira huo. ATCL walishanunua ndege mbovu kinyume cha sheria ya manunuzi na wapo wanaendelea kula kuku kwa mrija bila kubughudhiwa na bunge wala yeyote.Ngereja kawaletea mashtaka hayo mnanasemaje wabunge? Mwakyembe mtoto wa Kyela una la kuongea hapo? Au unayo mengi ya kuongelea Richmond tu yale ya ATCL unayakalia kimya?

Nadhani kama kuna wengine wanaowajua mahali popote walionunua vitu vibovu ambavyo ni mitumba ni vizuri kinyume cha sheria ni vizuri kuiga mfano wa Ngereja.Waanikwe na watajwe bila kumeza maneno.

Hii inasikitisha sana, anafanya kilekile na anajifanya anajua?
Mitambo ya Dowans inatofautiana nini na ndege walizonunua ATCL? Hili Haliingii kichwani kabisa.

Tanzania, Tanzania, nchi yangu nani atakae kuokoa?

Njimba
 
Wandugu mnabishana na MMJ nini? Wakati Serikali inasema hivi......

Mkuu heshima mbele,

Hii post yako ndo ilistahili kukaa kwenye post #1.

Lakini kama kawa ya JF, watu wanaanza weekend mapema, DHANA INAZAA DHANA, HALAFU INAZAA DHANA NYINGINE, HALAFU NYINGINE TENA...., HALAFU INAZAA MALUMBANO, HALAFU MALUMBANO WEEeee..halfu wengine wataingia na kuifanya kama chatroom,nakunza kuelezana jana nilivaa viatu vya buluu sijui nikaenda disco sijui nini, zengwe litaendelea weee, mpaka thread inaishia bila muafaka wowote na kufungwa na SILENCER baada ya watu kupewa ban baada ya kuanza kutukanana.

Kaazi kwelikweli..
 
Lakini Ngereja hapa sio kawataja ATCL wananunua ndege mitumba kwa nia ya kuonesha ama kutia nguvu kuwa nao wanaweza kununua mitambo ya Dowans ambayo ni mitumba. Sheria ya manunuzi inakataza kununua mitumba. Hivyo hastahili pongezi yoyote kwa kusema eti hata ATC hununua ndege mitumba.
 
Netanyahu unajua kila mtu lazima asingizie kitu fulani ndio kimenifanya nifanye hivi, lazima awepo wa kulaumiwa au ambaye amekufundisha. Kama akili zenyewe ndio hizo sawaa.
 
Mzee Mwanakijiji kwani hela zoote walizolipwa Dowans wakati walikuwa hawazalishi kama ilivyotakiwa si ndio yangukuwa malipo? Halafu tutaangalia na bei yenyewe ni Bora iwe wazii kabisaa, na kuna wataalamu wanajua mtambo mpyaa ni bei gani, maana bei isije ikawa kama ya kununua mtambo mpyaa wenye Waranty.
 
Well, kuna wakati inabidi tuseme tu kuliko kuzungushana kwenye huu utando wa buibui wa ufisadi. TUmekuwa kama kumbikumbi, na kama vipepeo tumenaswa na wao wanatuchezea tu.. kama paka aliyeshiba anavyomchezea chezea panya aliyechoka kukimbia!

Sasa naomba tulimalize hili la Richmond/Dowans:
b.) Mitambo ya Dowans hatimaye tutainunua kwa vile tunapaswa kuinunua kwani kutoinunua haiingii akilini wakati "ipo tu pale"! Mitambo hii haiendi kwa mtu yeyote binafsi na matatizo ya umeme yanayokuja mwezi wa nne itakuwa ni ushahidi kuwa ni "bora" tuinunue tu!. So why not buy them!?


Mwanakijiji naomba tubadili heading Isomeke tununue mitambo ya Richmond na wala sio Dowans ili watu tusikie uchungu wa fedha zetu nyingi tulizoibiwa na hawa jamaa kweli inauma lakini we acha tu wizi Mtupu!!!!!!
 
IO, nimetoa maoni yangu. Kama kuna kitu ambacho mtu hajakielewa au anataka nifafanue unauliza tu. Inashangaza hukuzingatia jibu lake kwangu ambalo ni hili:



Fuatilia majibu yake hadi nilipofikia kusema kwa vile ni mtu anayekwazwa na maneno yangu, basi dhamira yangu nitaendelea kuandika niwezevyo, kwa namna yangu na kwa staili yangu, mwenye kukwazika akwazike. Huo ndiyo msimamo. Sina lengo la kufurahisha kila mtu asomaye.



You can never have selective justice. Suala la Richmond ni kubwa mno lakini hakuna nia ya kweli ya kulishughulikia zaidi yakulifanya liendelee miaka nenda rudi. Mwaka huu atashtakiwa mmoja, miezi sita baadaye mwingine n.k Kwangu mimi huku ni kupoteza muda.

Hoja yangu ni kuwa hatuwezi kulizungumzia la Richmond na Dowans miaka nenda rudi. Yote uliyoyasema yanajulikana na wengine tumeyaandika sana huko nyuma. Tatizo serikali haina nia wala sababu ya kuhakikisha suala hili linafikia mwisho the same way hawana mpango wa kumaliza la Rada, JWTZ, Meremeta n.k

Ndiyo maana nimetoa hilo pendekezo la kwanza. Kwangu mimi ni bora hata kesi zote hizi zifutwe tu tuanze upya!! Kama kuibiwa tumeshaibiwa, vinginevyo tunachezeana mazingaombwe hadi qiyama. Tujifunze kumaliza masuala haya ya kitaifa aidha kwa kuyafuta au kuexpedite ile yafikie ukingoni.

that is the message katika ujumbe wangu.

Are you joking? yaani tuache tu huu uozo uliotokea? Kama tutaacha haya na kuyasamehe; i don't think we 'll call our nation a nation? Tutakuwa Taifa la wababaishaji; Mwakijiji ukiongelea pesa zilizopotea ni kias kama a billion USA Dollars; sasa eti tuache hizo; how can we know and plan our future if the present can not be defined!
 
Kuna WIZARA, TANESCO na PPRA. Kote huko kumejaa WATANZANIA wasomi wa fani karibu zote. Kwa nini tusiamini wanachokisema hawa? Badala yake tuamini WANASIASA wetu na VISASI vyao vya kinyang'anyiro cha MADARAKA visivyo na mwisho!
Utaifa kwanza siasa baadaye. Tulipoteza muda mwingi sana kuwatenga MAKABURU enzi hizo. Sasa hivi wako kila nyanja ya UCHUMI wa nchi yetu!
 
Kuna WIZARA, TANESCO na PPRA. Kote huko kumejaa WATANZANIA wasomi wa fani karibu zote. Kwa nini tusiamini wanachokisema hawa? Badala yake tuamini WANASIASA wetu na VISASI vyao vya kinyang'anyiro cha MADARAKA visivyo na mwisho!
Utaifa kwanza siasa baadaye. Tulipoteza muda mwingi sana kuwatenga MAKABURU enzi hizo. Sasa hivi wako kila nyanja ya UCHUMI wa nchi yetu!

Nakubaliana na wewe,

Kama kuna kitu kinachotakiwa kitiliwe maanani ili nchi isonge mbele ni kuwatumia wataalamu wetu. Ningependa tufike mahali ambapo kama vile bunge au mahakama vinapong'aka kuingiliwa kwa vyombo vyao vya utendaji, principle hiyohiyo itumike kuwalinda maamuzi ya wataalamu wetu.

Full stop!
 
Watanzania ni "wazoefu" vitu "USED". kuanzia kuoa/kuolewa mke/mme used, magari used, nyumba used, ndege used, mitambo ya Richmond used, vyeo na madaraka tunawapa viongozi ambao ni used,.....Chama kinacho tutawala ni kilekile used!
 
I learnt this earlier in my life tht "TWO WRONGS CAN NOT MAKE A RIGHT" and believe me it helps alot in judging issues constructively.
 
Watanzania ni "wazoefu" vitu "USED". kuanzia kuoa/kuolewa mke/mme used, magari used, nyumba used, ndege used, mitambo ya Richmond used, vyeo na madaraka tunawapa viongozi ambao ni used,.....Chama kinacho tutawala ni kilekile used!


Muzee,

Umeniacha hoi sana, haswa hapo kwenye red color nyekundu..teh teh.

Unajua hili suala la mitumba-mitumba, limenikumbusha sakata la vyombo vya usafiri hususan magari, Wizara husika inachimba biti kuwa watu wasilete magari yenye umri wa zaidi ya miaka 10, ukileta wanakupiga penati,wakati huohuo serikali hiyohiyo inanunua ndege mitumba! Yaani si vigumu kuona utaahira unaoendelea hapa bongo!
 
Naamini kabisa Mwanakijiji hayuko against wavunja sheria akina RA et al kuchukuliwa sheria. Ukweli ni kwamba kama wengine..amechoshwa na ubabaishaji wa viongozi wetu. Kifupi hakuna nia dhabiti kulimaliza hili swala..maana liko so clear that hata mahakama ya mwanzo wangelitolea uamuzi.

MKJJ anachokisema hapa ni kwamba katika saga yooote hii..WATANZANIA TUNARUSHIWA MCHANGA WA MACHO. Hakuna mwenye nia dhabiti ya kuwachukulia hatua hawa jamaa wa DOWNS au Richmond. Kifupi ni kwamba watu wanavuta mda kwa yale maneno tuliyoyazoea "upelelezi unaendelea" "ushahidi haujakamilika" just name it! na hili litaendelea mpaka mwisho...baada ya hapo..wanasheria wataanza kucheza na vifungu vya sheria kama statute of limitations! na wahusika watafutiwa kesi..as simple as that..na once again watanzania tutakuwa tumeambulia patupu na mafisadi watakuwa wameshinda...JK akiulizwa...atajibu "hayo maswala tuliwaachia wanasheria washughulike maana serikali yetu inaheshimu utawala wa sheria"..and the game will be over! Huhitaji kuwa mwanasheria kuligundua hili.

Jamani once again, nasema Tanzania yetu viongozi wetu ndo mafisadi. kisheria hawa Dowans na Richmond...kitendo cha kughushi tangu mwanzo kingewaondolea sifa ya kuwa mshirika wa serikali kwa namna yoyote ile. Infact serikali ingefuta any contractul relationship nao na kuwafungulia mashtaka ya kutaka kuiibia serikali (after all walishaiba)..na hili halihitaji mahakama ya Paris..hata ya Kisutu ingefanya hivyo. LAKINI UKWELI NI KWAMBA HAYA MAKAMPUNI YA KIZUSHI NI YA VIONGOZI WETU..NDO MAANA UNAONA SERIKALI INAWATETEA HAWA WEZI. KINACHOUMA NI KUONA KWAMBA HATA SISI WANANCHI TUNADANGANYWA NA TUMESHAKUBALI!

Anyway, msisahau kwamba next year ni uchaguzi..kwa hiyo serikali inatafuta pesa kwa njia yoyote ile!

Hivi kweli mnaamini mpaka leo kwamba TANESCO inashindwa ku-commission mitambo mipya mizuri hata kutoa GE au SIEMENS na kupewa guarantee (na wataalamu ) kuweka mitambo reliable ya umeme katika nchi yetu? mnadhani TANESCO haiwezi kufanya hivyo? Mpaka ikanunue mitambo iliyokwisha tumika na ambayo bado ina mgogoro? Kama siyo Project ya mafisadi ni nini? Yaani siku hizi watu wameshaamua kuyafanya matatizo ya wananchi kuwa miradi yao binafsi ya kujitafutia personal fortune. Siku hizi mvua imekuwa mradi wa umeme. Itdoesnt click..tutumie millions kununua mitambo mibovu wakati tungeweza kabisa kununua mitambo safi kutoka US au Germany..na tukapewa guarantee nzuri. Na kibaya zaidi..hiyo mitambo..itatumika few months..utaambiwa imeharibika..na kuitengeneza..itahitaji tena millions!

Hivi watanzania tutaamka lini? Sasa hivi mimi I am not worried with our leaders (najua viongozi wetu ni lost cause tayari), Iam rather getting worried with the capacity of thinking of we wananchi. Na shida zote hizi hatujifunzi? Duh! Honestly speaking, nachelea kuamini kwamba waafrika..MATATIZO YETU YAKO KWENYE DNA. SI BURE! MAANA HATA KUNGEKUWA NA MCHAWI..ASINGETUROGA WOTE KIASI HIKI!
 
Kuna WIZARA, TANESCO na PPRA. Kote huko kumejaa WATANZANIA wasomi wa fani karibu zote. Kwa nini tusiamini wanachokisema hawa? Badala yake tuamini WANASIASA wetu na VISASI vyao vya kinyang'anyiro cha MADARAKA visivyo na mwisho!
Utaifa kwanza siasa baadaye.

umesema kweli. safi sana.

lakini tatizo ni hili: wasomi wetu wengi wanakaa kujipendekeza kwa wanasiasa au wenye fweza au wenye madaraka. kwa hiyo hawakai wakafanya kazi zao kitaalamu. na mara nyingine hawawajibiki ipasavyo. kwamfano, tanesco kama wangekuwa wanafanya kazi zao ipasavyo miaka yote tangia ianzishwe tungekuwa na hali mbaya kiasi hiki katka suala zima la umeme?

na jingiine hili, wataalamu wetu unafikiri hawakuhusika katka mchakato mzima wa kuipa richmond kazi? walihusika sana.
halafu kingine, bosi na mtaalamu wa takukuru alipoliongelea suala la richmond alisema liko sawa. lakini leo wengi tunajua halikuwa sawa. sa vipi, bado huoni kuwa hawa wataalamu wanaingiliwa na wanene au wenye fweza au wanasiasa au hawawajibiki ipasavyo?

ni muhimu wataalamu wetu watuonyeshe kuwa wanafanya kazi kitaalamu na kuwa hawakubali kupindisha mambo ili tuwaamini siku zijazo.

wanasiasa wanaweza kuwa na visasi vyao lakini wakiongea kupinga au kuwa na wasiwasi katka hili wana make sense kiasi fulani katka akili ya kawaida.
 
umesema kweli. safi sana.

lakini tatizo ni hili: wasomi wetu wengi wanakaa kujipendekeza kwa wanasiasa au wenye fweza au wenye madaraka. kwa hiyo hawakai wakafanya kazi zao kitaalamu. na mara nyingine hawawajibiki ipasavyo. kwamfano, tanesco kama wangekuwa wanafanya kazi zao ipasavyo miaka yote tangia ianzishwe tungekuwa na hali mbaya kiasi hiki katka suala zima la umeme?

na jingiine hili, wataalamu wetu unafikiri hawakuhusika katka mchakato mzima wa kuipa richmond kazi? walihusika sana.
halafu kingine, bosi na mtaalamu wa takukuru alipoliongelea suala la richmond alisema liko sawa. lakini leo wengi tunajua halikuwa sawa. sa vipi, bado huoni kuwa hawa wataalamu wanaingiliwa na wanene au wenye fweza au wanasiasa au hawawajibiki ipasavyo?

ni muhimu wataalamu wetu watuonyeshe kuwa wanafanya kazi kitaalamu na kuwa hawakubali kupindisha mambo ili tuwaamini siku zijazo.

wanasiasa wanaweza kuwa na visasi vyao lakini wakiongea kupinga au kuwa na wasiwasi katka hili wana make sense kiasi fulani katka akili ya kawaida.

Isome tena taarifa ya kamati ya Bunge uone jinsi maoni na ushauri wa wataalamu wetu yalivyopuuzwa na hatimaye kuzua sakata lile la Richmond.
Tuwape nafasi wataalamu wetu na hasa kwa suala ambalo halina hata chembe ya siasa ndani yake.
 
Alipoulizwa sababu za kung'ang'ania kununua mitambo hiyo kinyume na Sheria ya Manunuzi ya Umme ambayo inazuia taasisi za serikali kununua mitumba, Ngeleja alihoji: "Mbona watu wanasema tununue mitambo ya IPTL.

"Ni kweli sheria ya PPRA inatakaza ununuzi wa vitu vilivyotumika, lakini yapo maeneo ambayo kutokana na mazingira halisi ya kisekta si lazima kinachonunuliwa kiwe kipya.

"Angalia, ATC leo hii inaweza kununua au kukodi ndege lakini si lazima iwe mpya. Tuangalie maeneo ya msingi, jambo kubwa ni watalaamu kuthibitisha ubora na uwezo wa kukidhi mahitaji ya nchi. Mitambo ile unaweza kuifunga leo hii katika toroli na kuipeleka mkoa wowote wenye uhaba wa umeme."


Hivi kwa nini huwa wananunua mashangingi mapya tu? Tungeliokoa sana pesa kwa kuchukua USED hata kama inakuwa miaka 2, bei huanguka sana.

Kama wanaweza KUVUNJA sheria na kununua mitambo mitumba, hivi kwa nini wanasema kununua mipya kutoka GE itachukua muda mrefu? Kwa nini wasifanye SHORT CUTkununua na within 2 weeks, dege la UKRAINE litue Kipawa na Generator yetu? Hivi hili nalo wanajifanya hawaoni?

Nafikiri kuna haja NGEREJA ajiwekee kamba shingoni kuwa kama mitambo ikishindwa kazi, hukumu gani apewe kwa kutuletea mitambo isiyo na warrant. Maana sidhani kama Dowans watatoa warrant.

NB: Wildcard, wake USED una maana yule Waziri FISADI Karamage aliyenyanganya mke wa Mongella siyo? Mgonja alimnyanganya Patrick Balisidya mke. Baba yake Mange alijiuwa, kisa ni kwamba GOGO lilimshika shanga mkewe!! Looo, USED WIFE!!! Fisadi kweli KUMBAKUMBA!!
 
Kununua mitambo iliyotumika kututapeli ni kuidhinisha utapeli huo,sijui masikini Zito kalishwa nini sasa anatetea mitambo ya kifisadi sasa chama chake kitaaminika vipi kama ameanza mapema hivi,Mungu endelea kutuonyesha wanafiki ili tutafute Viongozi wenye nia nzuri na Nchi hii.Mitambo hiyo ingetaifishwa na serikali kwani ilitumika kutapeli na si kuyanunua.Wapinzani wenye nia njema mpo?Zito naona anaelekea kubaya inabidi kutafakari nyendo zake.
 
Wanalumbana tu kuhusu Dowans ila mwisho wa siku lazima wanunue kina mamvi wachukue mgao wao wajindaekupenyeza fitna uchaguzi ujao mnabisha?ndio hivyo....
 
The Ministers who resigned in the Parliament because of Richmond saga must be cellebrating at this time.
 
Back
Top Bottom