Muonekano mzuri wa Stendi mpya ya Mbezi umeharibiwa na Siasa zetu za kutafuta sifa kwa Wanyonge waliobatizwa Masikini

Wawepo tu muhim wapangwe vzr na wajengewe sehem nzur, wawe machinga wa kisasa
Mwanasiasa aliyewapa hiyo ruhusa angelisema hili la Kiakili kama ulilosema Wewe hapa ningemwelewa. ila Yeye kawaambiwa tena kwa kuwapa kabisa Jeuri na Kiburi kuwa waingie na kamwe wasibugudhiwe kwani hao ni Wapigakura wake na Masikini anaowapenda. Kuna Mtu naanza kuhisi nilivyokuwa nikimpenda huko nyuma sikutumia muda wangu mwingi Kumtathmini kwani naona anaharibu zaidi kuliko kutengeneza.
 
Punguza stress ndugu yangu!

Punguza chuki zako dhidi ya serikali na wananchi wanaoipenda au kuifurahia serikali yao.
Punguza hasira na wamachinga,mamalishe na wengine wanaopambana kupata tonge.

Pita nchi nzima,machinga na mama ntilie biashara zao wanafanya stendi ama pembezoni mwa barabara....ama mahali popote penye shughuli zinazofanya watu kupatikana kwa wingi...mfano viwandani na maeneo yanapopatika wanachuo au hata ndani ya fensi za baadhi ya shule za msingi na sekondari.

Ni upumbavu kutaka watu waruhusiwe kufanya shughuli hizo kwenye viwanja vya ndege au ikulu. Na pia,natiliashaka uelewa wako wa mambo. Jaribu kuwa na akili ya ziada kwenye kupambanua mambo.

ACHA HASIRA NA CHUKI.
 
Nimekuelewa
Swali langu linasema Airport hakuna abiria wa mikoani?

Tunapotoa huduma tunazingatia pia idadi ya wateja wanaopokea huduma hiyo

Kama unaona airport kuna abiria wanaohitaji huduma ya machinga au mama nitilie fuata taratibu ukatoe huduma... vinginevyo waache wenzio wajipatie riziki
 
WEWE NDIYO UNAKERA.UNATAKA WAZUNGU NDIYO WARUHUSIWE KUINGIA.HIYO NI MALI YA WAPIA KODI NA WANAHAKI YA KUITUMIA KUJIINGIZIA KIPATO ILI WAENDEELLEE KULIPA KODI.SI JABU WEWE HATA KODI HULIPI
 
Waende na airport pale, kwani si kuna wasafiri?
Kweli wanapiga vibanda vya mama ntilie, pale parking, wauze mitumba na 'kalcha' mbele na nyuma ya maviete.😂😂

Stendi yenyewe finyu sana kwa nafasi parking ya mabasi, pale asubuhi sijui inakuwaje?? Nafikiri wenye ofisi zao Shekilango na Ubungo kama Allys, BM, Kilimanjaro, ABC wataendelea kupakia abiria huko, kuepusha aibu ya basi kutokutosha hapo.

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Totally i agree with you
FB_IMG_1614492222333.jpg


Sent from my ACCESS55 Pro using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom