Mungu ibariki Algeria kesho dhidi ya CCM

Mungu ibariki Algeria kesho dhidi ya CCM

na wafungwe tu,hamna namna ila nahisi wakirudi huko AMUNIKE KIBARUA BASI
 
anawanunulia viatu na kuwasainia utadhani yeye ni Denzel washington na wendawazimu wakiongozwa na mbwana samatta wanachekacheka kama wagonjwa wa akili vilevile bado yupo huko maana kiwango cha aishi manula kinazidi kumkuna anaweza akamuongezea milion 10 nyingine you never know.
Mchukieni Mako...msiichukie Taifa Stars ... don't mix up things...
 
Wazee mnisamehe kwa kuuliza hili, mm nikisikia mwanasiasa yyt anazungumza nazima/naondoka au naziba masikio ila hili naomba nisikie kutoka kwenuu,
je alichosema mtoa mada ni serious kua kuna aliyesema stars ni ya ccm? na ni nanii huyo mbwa? maana nimesoma ila sikuona alieuliza hili, sidhan kama hawa fungus wamefikia mpk huku, km n kweli niambieni mapema kuna duka kabla halijafungwa nikanunue jez ya algeria, kenya na senegal nizivae zote, hii ya stars niliyopewa zawad naichoma sasa hv hata kabla hamjanijb,
km ni uongo mungu anawaonaa, mmenipandikiza chuki ya haraka sanaa na hakuna wa kuishushaa.
 
inafurahisha hata mataifa tuliyodhani yana matatizo ya kisiasa na kikabila kama vile algeria na kenya kutumia yanayoendelea huko misri kuleta umoja wa kitaifa na kuwa kitu kimoja ila hali hiyo ni tofauti hapa kwetu ambapo tusio wana ccm tumetangaziwa wazi kwamba ile team ya CCM ambao kila mtu anajifunzia kunyoa haituhusu
kesho CCM hao wanaenda kukutana na mbweha the fox wa jangwani toka algeria,mara ya mwisho CCM hao wa lumumba walipigwa 7-0
Naomba nichukue nafasi kumuomba Mungu awabariki Algeria wapige goals 9-0 hapo kesho.Amen.
Naunga mkono hoja!! wapigwe tu hao wawakilishi wa ccm
 
East Africa tz tunaropokwa sana,
Chuki dhidi ya Taifa Stars inareflect tabia zetu.
Kila la kheri Taifa Stars.
 
Naona kuna tatizo mahali flan. Iweje ameenda kiongozi kwenda kuwatia moyo nyiye mnaichukia timu yetu?? Mbona walienda wabunge wa vyama mbalimbali hamkuwazomea??
Jamani, tuache chuki binafsi tujiunge kwa pamoja kuiombe dua njema Taifa Stars yetu. Hivi tuseme; Kama mchawi wetu alifanya vyema halafu ghafla mkasikia kuwa Mbweha wa jangwa wameuogopa mwanga wa Nyota yetu halafu wakachapwa 1 - 0 tu mtalala wapi nyiye wenye roho ya korosho??
Nawaombea Taifa Stars nyota iwake wawalambe 1 - 0 hao mafisi wa jangwani. Sina chama ila ushindi wa Stars ni wetu sote ila kama ni kweli, warudishiwe ile chenji yao waliyoibiwa
Dua lako haliwezekani

Mtapigwa 7 mtungi na kikosi chenu cha ccm.

Haiwezekani mtu mwenye hips ....... mf
 
Hata kama ndani ya familia mmegombana sana, siyo vizuri kakaa kijiweni na kuanza kutangaza ugomvi wenu hadharani.
Mkiwa nje mnatakiwa muwe wamoja japo kwa ndani mligombana.
Hata kama ni kweli Stars ingekuwa ni ya CCM, still, kizalendo, Watz wote tungepaswa kuwapa sapoti Watz wenzetu, maana hata CCM nao ni Watz.
Kama huna mapenzi na Stars bora ubaki kimya ila usitangaze ubaya kwa majirani na mataifa mengine maana huko ni kujichora tu.
Kuna wabunge wanatuwakilisha Bunge la EAC, SADC, na Pan African Parliament, na baadhi yao ni wanaCCM, lakini bado tunawapa sapoti maana wanaiwakilisha nchi.
Sasa leo hii, iweje, mfano, kama Stars wangekuwa wanaCCM, tusiwape sapoti?
Kama huwasapoti, ni kwanini usikae kimya kuficha aibu na upumbavu wako?
Mwerevu hukaa kimya ila mpumbavu hunena hovyo na kudhihirisha upumbavu wake
 
Nimesoma 50% ya comments. Katika comments nilizosema nimegundua 98% ni againist CCM. Conclusion ni kuwa kumbe watu wanachuki kubwa sana dhidi ya CCM wamezitunza tu rohoni.
 
Back
Top Bottom