Mungu ibariki Algeria kesho dhidi ya CCM

Mungu ibariki Algeria kesho dhidi ya CCM

inafurahisha hata mataifa tuliyodhani yana matatizo ya kisiasa na kikabila kama vile algeria na kenya kutumia yanayoendelea huko misri kuleta umoja wa kitaifa na kuwa kitu kimoja ila hali hiyo ni tofauti hapa kwetu ambapo tusio wana ccm tumetangaziwa wazi kwamba ile team ya CCM ambao kila mtu anajifunzia kunyoa haituhusu
kesho CCM hao wanaenda kukutana na mbweha the fox wa jangwani toka algeria,mara ya mwisho CCM hao wa lumumba walipigwa 7-0
Naomba nichukue nafasi kumuomba Mungu awabariki Algeria wapige goals 9-0 hapo kesho.Amen.
Akili ndogo umejiweka kwa Watu wenye akili kubwa mwishowe umekosa cha kupost
 
We are together with Taifa Star, kwenye shida na raha... God Bless Taifa Star, God Bless Tanzania... Taifa Star Make Country happy again.....
Ha ha ha ha ha ha
Mungu ameisha iacha CCM muda mrefu sana. Kule kwenye Jukwaa la sport jamaa alimuomba Mungu zidi ya Tanzania na Kenya. Alisema Mungu kama Taifa stars ni mali ya CCM basi wafungwe na Harambee stars. Uliona kilichojiri? Kenya wametoka nyuma mpaka wameshinda 3-2. Huyo Mungu unayemuabudu ameshaicha CCM muda mrefu.
Ww subiri kesho ccm stars itekeleze ilani ya CCM.
 
Usiwachukie hivyo Watz wenzako mkuu hao ni vijana wawakilishi wa hili taifa huko Afcon usiwatusi.
Hao wanamwakilisha Magufuli na Serikali ya awamu ya tano. Rejea Bashite alichosema "Timu itashinda kama vile CCM inavyoshinda kwenye chaguzi" Ulimsikia pia Samata kipindi anahojiwa?
Kuna mambo ya taifa na mambo ya chama. Ukishindwa kujua mipaka ya chama lazima uwagawe watu ndicho kinachotokea.
 
Labda yanayotokea ndio ambavyo sisiemu huwa inashinda, Goli la mkono
 
Kusema T'Stars ni ya Chama fulani,,, ni fikra binafsi na ushabiki fulani...

Kujitekenya - ukacheka, ni mambo ya kilimwengu (raha jipe mwenyewe)., lakini kujifinya - ukalia, jua una tatizo.

Ulimwengu wa Soka ni mchakato, T'Stars ni yetu. MUNGU ibariki Taifa Stars. MUNGU ibariki TANZANIA
 
Kusema T'Stars ni ya Chama fulani,,, ni fikra binafsi na ushabiki fulani...

Kujitekenya - ukacheka, ni mambo ya kilimwengu (raha jipe mwenyewe)., lakini kujifinya - ukalia, jua una tatizo.

Ulimwengu wa Soka ni mchakato, T'Stars ni yetu. MUNGU ibariki Taifa Stars. MUNGU ibariki TANZANIA
Utakua ccm wewe
 
Tatizo wanaccm wanashindwa kujua mipaka ya siasa. Wao kila kitu ni siasa. Wampeleke Jecha akafanye mambo. "Taifa Stars itashinda kama vile CCM inavyoshinda kwenye chaguzi".
Wao walidhani mpira ni siasa. Nitaishabikia Taifa Stars ile isiyokuwa na chama yaani ya watu wote. Hii naichukulia kama CCM Stars.
Jecha angeleta ukombozi kwa kweli 😂😅
 
Back
Top Bottom