Mtwara: Simbachawene azuiwa njiani!

Mtwara: Simbachawene azuiwa njiani!

Thats good,let us teech them a lesson.

Ranks, we usidanganye wenzako wakati we umekaa katika laptop tu! nyie Cdm mmeona m4c yenu imefeli ndo mnatumia karata ya wanamtwara! msisafirie nyota ya wenzenu mnawaponza wakina mama watoto na vikongwe kwa vurugu zenu!
 
Last edited by a moderator:
Thats good,let us teech them a lesson.

Ranks, we usidanganye wenzako wakati we umekaa katika laptop tu! nyie Cdm mmeona m4c yenu imefeli ndo mnatumia karata ya wanamtwara! msisafirie nyota ya wenzenu mnawaponza wakina mama watoto na vikongwe kwa vurugu zenu!
 
Last edited by a moderator:
walizoea kuwaita 'Chinga' eti mnajazana dar na kutembeza kiatu k1 mkononi ..ahaa,dharau sana aisee kwa wanamtwara
 
aisee usione watu wamenyamza kama makondooo, wakicharuka wanakuwa kama simba mwenye njaa kali.
 
Nilishasema tangu awali kabisa, katika hili, Mimi Manyerere Jackton, nawaunga mkono wana Mtwara. Wana hoja. Serikali inataka kupotisha. Si kwamba hawataki umeme usitoke Mtwara. Wanachotaka ni kuona mtambo unajengwa hapo hapo Mtwara, umeme unazaliwashwa, unaingizwa kwenye gridi ya taifa, na wao wanapata ajira. Hilo ni kosa? Hakika si kosa. Nawaunga mkono.

Kaka pia nawaunga mkono lakini hii hoja ni Dhaifu ukikaa na Ma-CCM wanaojua watakushinda kwa hoja hii kwani ki-Uchumi haitekelezeki, Ni gharama kubwa kuleta umeme wa kutosha kulisha Dar kutoka Mtwara kwani inahitaji Njia kubwa za Umeme zaidi ya Tatu, Kumbuka Njia moja ni 250 MW.
 
JK, bado pale mbeya kwenye ile nachorogesi ya paaaaaaale kwenye kamlima kaaaaale ka KYEJO. We thubiri, matter of time!
 
Ni kweli alienda na kama si FFU jamaa walikuwa wanafanya kitu mbaya leo. Katika hili Serikali ikubali kukaa na hawa jamaa vinginevyo huu moto unaweza ukasambaa kila kona na hali ikawa si hali.

Unamaanisha walitaka Kula KIBOGA.
 
Kwi ! Kwi ! Kwi ! Kwi ! Fisi chaweneee! Alama za nyakati hukuziona ? Hata kuuliza hutaki ? Hebu Muulize Mbatia , data zote anazo .
 
Suala la Mtwara sio kama linavyopotoshwa na viongozi akiwemo JK na waziri wake wa Nishati. Kuna timu ya waandishi wa habari wameletwa leo asubuhi Mtwara na TPDC ,Jerry Muro yupo kwenye hiyo team. Navyosikia wameletwa kutengeneza documentary ili kupaka rangi kinachoendelea Mtwara. Wanataka waihadae dunia kama walivyofanikiwa kuaahadaa watz wachache waliyopo nje ya Mtwara.

Kwa kuwafahamisha kiuchache ni kwamba suala la GAS Mtwara halijaibuliwa na wana Mtwara. Hili suala limeibuliwa na baadhi ya Mawaziri waliovujisha siri za vikao vya siri vya Baraza la Mawaziri, ambapo wamechoshwa na uhuni wa Baba Riz wa kuvutia miradi kwa lazima Bagamoyo.

Baazi ya wazungu wanaofanya kazi kwenye GAS wameshaanza kuvujisha siri kwenye mataifa yao jinsi Mradi wa kujenga Plant ya kusafisha Gas Mtwara ulivyohamishwa kinyemela kupelekwa Mkoa wa Pwani. Baazi ya Wataalamu wa Gas (ngozi nyeupe) wamekiri wazi mradi huu hautakamilika kama serikali itaendelea na ubabe. Ikumbukwe wataalamu hawa wana uzoefu na maeneo kama Angola ,Ivory Cost , Nigeria ambapo pia wamefanya kazi kama hizi na madhara wameyaona pale serikali ilipokaidi matakwa ya wananchi.

Kwenye suala la Gas Mtwara ni Dhahiri hata watumishi wa Serikali Mtwara hawamuungi Mkono JK. Hivyo hujuma kwenye mradi atakapoulizimisha kufanyika kimabavu ipo wazi.

Kilichotokea jana kwa Mbatia ni ishara kuwa hili suala sio la kisiasa kama mwanzo walivyokuwa wanawahadaha Watanzania. Lingekuwa ni suala la kisiasa wangemsitiri Mbatia kwani chama chake kimeshiriki tokea mwanzo.

Sulla la msingi ni Watanzania kuamka kwamba tunahitaji kuwa na majiji mengine zaidi ya Dar, yenye mipango ya kisasa kwa kila kitu.Mtwara ilikuwa ndio moja ya miji ya mifano Africa kwa mpango wa UN Habitat. Hilo limefichwa kwa makusudi kwa sababu ya Ubagamonism, Watanzania tunaonekana ni majuha kwamba mikoani hatana mchango kwa pato la taifa (asilimia 80 ya pato la taifa linatoka Dar) huu ni uvivu wa kufikiri na matusi kwa Wanzania. Watu wanatoa takwimu za kuwahadaha wananchi ili kuhalalisha ubadhilifu wa fedha za uma(Ufisadi).

Nawasilisha.

ninaweza kuamini ya 'watu weupe' uliyoyasema, hasa ukizingatia kuwa mradi wenyewe wa bomba unafanywa na Wachina ambao ni maadui wao wakubwa wa uchumi. Watu weupe wamekuwa wakionyesha kuchukizwa na uwekezaji Wachina wanaoufanya Afrika.

Hata hivyo kauli za Mawaziri kwa wana Mtwara kwenye suala hili la gesi zilikuwa za kukera. Vizuri kuomba radhi na kutafuta muafaka na hasa kubadilisha sera zetu za uchumi.
 
Safiiii safi sanaaa!!
Wanamtwara wembe ni huo huo, watanzanio wote tuliochoka na maisha magumu tunawaunga mkono.
 
Ntwara nsasa iko sawa sawa lazima nkieleweke kazeni uzi, gas izalishwe na kusafishwa mtwara si vinginevyo.
 
Kwangu mimi ninapoona Wa-Tz wanazidai haki zao kwa kuonesha kuchoshwa nafurahia sana. Hii itawafanya hawa wazandiki na sera zao za kujinufaisha zishindwa na kubwa zaidi wananchi wapange kuwapiga chini ili watupishe mbali kabisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom