Mtwara: Simbachawene azuiwa njiani!

Mtwara: Simbachawene azuiwa njiani!

Mpaka muhongo atuombe radhi kwa dharau zake kwa watu wa kusini
 
nimesikia kuna magari yameshambuliwa wakidhaniwa ni msafara wa simbachawene, ila hakuwa yeye....ila angekuwa yeye cha moto wangekiona.....
 
Nilishasema tangu awali kabisa, katika hili, Mimi Manyerere Jackton, nawaunga mkono wana Mtwara. Wana hoja. Serikali inataka kupotisha. Si kwamba hawataki umeme usitoke Mtwara. Wanachotaka ni kuona mtambo unajengwa hapo hapo Mtwara, umeme unazaliwashwa, unaingizwa kwenye gridi ya taifa, na wao wanapata ajira. Hilo ni kosa? Hakika si kosa. Nawaunga mkono.
 
mbona kuna watu wanasema
lionchawene hajaenda mtwara baada ya kushauriwa na wanaccm
wenzake??:confused2::confused2:

hata kama hajaenda sawa! lakn huoni watu kupanga mawe njian wakimvizia waziri ni kitu ambacho sicha kawaida! Ccm kajipangen upya!
 
Haya sasa NAPE si ndo kwenu huko MTWARA mchukue na huyo LAMECK mpeleke proganda zenu Mtwara tuone kama nyie wanaume kweli kama hamjarudi Dar Magamba hayapo
 
hata kama hajaenda sawa! lakn huoni watu kupanga mawe njian wakimvizia waziri ni kitu ambacho sicha kawaida! Ccm kajipangen upya!

Ni kweli alienda na kama si FFU jamaa walikuwa wanafanya kitu mbaya leo. Katika hili Serikali ikubali kukaa na hawa jamaa vinginevyo huu moto unaweza ukasambaa kila kona na hali ikawa si hali.
 
Nilishasema tangu awali kabisa, katika hili, Mimi Manyerere Jackton, nawaunga mkono wana Mtwara. Wana hoja. Serikali inataka kupotisha. Si kwamba hawataki umeme usitoke Mtwara. Wanachotaka ni kuona mtambo unajengwa hapo hapo Mtwara, umeme unazaliwashwa, unaingizwa kwenye gridi ya taifa, na wao wanapata ajira. Hilo ni kosa? Hakika si kosa. Nawaunga mkono.

Nilifikiria kujenga kituo kingine kikubwa cha kufua umeme Mtwara na kuingiza umeme kwenye gridi ya taifa ni njia moja ya kulinda usalama wa taifa badala ya kuweka sehemu moja. Huu ni mtazamo wangu lakini inaonekana wenzetu ni wataalamu zaidi!
 
Nasikiasikia na Lindi napo wanataka kuliamsha kuanzia tarehe 20 ya mwezi huu, kwa kweli hawa jamaa wamekuwa exploited for quite some time now, dialogue is the best for mutual consent.
 
Thats good,let us teech them a lesson.
 
Hakuna ubishi kwamba dar ina viwanda vingi lakini wanamtwara nao tuwape haki yao ya kuanzisha viwanda kwa ajili ya kukuza uchumi na uzalisha wa bidha zitokanazo na gesi coz kama nimbolea mtwara ni mahali pake kwani itasaidia hata mikoa jirani kama ruvuma nayo kufaidika na mbolea kwa kupunguza ghalama za usafirishaji. Wanamtwara kaza uzi wala msikubali propaganda za serikali
 
Hata Congo machafuko yalisababishwa na rasilimali.. Hata sie tusipokua makini tutafika walipo Congo
 
...Ukiona Ncha ya Kas imekutana na Ncha ya Kus...basi ujue huo mshikamano ni kama wa sigma bond... hakuna wa kututenganisha tena Watanzania...
...Rasilimali za watanzania kwa manufaa ya watanzania...Salaam Aleykum/Milele Amina!
 
Nilifikiria kujenga kituo kingine kikubwa cha kufua umeme Mtwara na kuingiza umeme kwenye gridi ya taifa ni njia moja ya kulinda usalama wa taifa badala ya kuweka sehemu moja. Huu ni mtazamo wangu lakini inaonekana wenzetu ni wataalamu zaidi!
Wewew ni GENIUS MKUU,lakini usalama wa magamba ni kujnga kituo kingine karibu na Uwanja wa Ndege,maana kituo cha mabasi kipo!
 
Waache ma ccm wafunzwe adabu, wameacha kushughulikia matatizo ya wana Mtwara wamekazania eti CHADEMA ndo wanachochea, as if wana mtwara hawana akili zao.
 
Safari hii story nzuri nzuri zinatoka mtwara tu

Atom. Yani hio ndio stori nzuri nzuri! hivi kwanza una umri gani? je unajua madhara ya umwagaji damu nchi inapochafuka? wewe umekaa na laptop unakenua menu tu eti stori nzuri nzuri,mtapata mnachowatafutia watu wa Mtwara!
 
Last edited by a moderator:
Suala la Mtwara sio kama linavyopotoshwa na viongozi akiwemo JK na waziri wake wa Nishati. Kuna timu ya waandishi wa habari wameletwa leo asubuhi Mtwara na TPDC ,Jerry Muro yupo kwenye hiyo team. Navyosikia wameletwa kutengeneza documentary ili kupaka rangi kinachoendelea Mtwara. Wanataka waihadae dunia kama walivyofanikiwa kuaahadaa watz wachache waliyopo nje ya Mtwara.

Kwa kuwafahamisha kiuchache ni kwamba suala la GAS Mtwara halijaibuliwa na wana Mtwara. Hili suala limeibuliwa na baadhi ya Mawaziri waliovujisha siri za vikao vya siri vya Baraza la Mawaziri, ambapo wamechoshwa na uhuni wa Baba Riz wa kuvutia miradi kwa lazima Bagamoyo.

Baazi ya wazungu wanaofanya kazi kwenye GAS wameshaanza kuvujisha siri kwenye mataifa yao jinsi Mradi wa kujenga Plant ya kusafisha Gas Mtwara ulivyohamishwa kinyemela kupelekwa Mkoa wa Pwani. Baazi ya Wataalamu wa Gas (ngozi nyeupe) wamekiri wazi mradi huu hautakamilika kama serikali itaendelea na ubabe. Ikumbukwe wataalamu hawa wana uzoefu na maeneo kama Angola ,Ivory Cost , Nigeria ambapo pia wamefanya kazi kama hizi na madhara wameyaona pale serikali ilipokaidi matakwa ya wananchi.

Kwenye suala la Gas Mtwara ni Dhahiri hata watumishi wa Serikali Mtwara hawamuungi Mkono JK. Hivyo hujuma kwenye mradi atakapoulizimisha kufanyika kimabavu ipo wazi.

Kilichotokea jana kwa Mbatia ni ishara kuwa hili suala sio la kisiasa kama mwanzo walivyokuwa wanawahadaha Watanzania. Lingekuwa ni suala la kisiasa wangemsitiri Mbatia kwani chama chake kimeshiriki tokea mwanzo.

Suala la msingi ni Watanzania kuamka kwamba tunahitaji kuwa na majiji mengine zaidi ya Dar, yenye mipango ya kisasa kwa kila kitu.Mtwara ilikuwa ndio moja ya miji ya mifano Africa kwa mpango wa UN Habitat. Hilo limefichwa kwa makusudi kwa sababu ya Ubagamonism, Watanzania tunaonekana ni majuha kwamba mikoani hatana mchango kwa pato la taifa (asilimia 80 ya pato la taifa linatoka Dar) huu ni uvivu wa kufikiri na matusi kwa Wanzania. Watu wanatoa takwimu za kuwahadaha wananchi ili kuhalalisha ubadhilifu wa fedha za uma (Ufisadi).

Nawasilisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom