Mtwara: Simbachawene azuiwa njiani!

Mtwara: Simbachawene azuiwa njiani!

Wana Mtwara endeleeni kutetea haki zenu kwa kuhitaji kufaidika kwa rasilimalim ya gesi. Kwanini wasizalishe umeme hukohuko na waingize kwenye gridi ya taifa. Gesi ya songosongo mbona hadi sasa haijashusha bei ya umeme.
 
kama mbwai mbwai ntwara komaeeni mwanzo mwisho.

BLACKTIGER,na wachaga komalieni mlima wenu wa Kilimakyaro, mapato yabaki K' njaro na wasukuma dhahabu zenu, wapemba mafuta yenu! uone mtafaidi nini watanzania! ACHENI UCHOCHEZI!
 
Last edited by a moderator:
Atom. Yani hio ndio stori nzuri nzuri! hivi kwanza una umri gani? je unajua madhara ya umwagaji damu nchi inapochafuka? wewe umekaa na laptop unakenua menu tu eti stori nzuri nzuri,mtapata mnachowatafutia watu wa Mtwara!
Kwa hiyo wewe unataka kutuambia hii kwako ni story mbaya? Yaani Mungu kaamua kujibu Maombi ya Wadanganyika kabla ya wakati,eti wewe unataka kumkosoa! Kajipange upya na Nape wako.Viongozi badala ya kuhangaika na matatizo yanayowasumbua Watanzania,wao wanahangaika na Dk Slaa na Chadema.waende kusini wakawaambie wana Mtwara na Lindi ni kwanini wao ni Masikini,na kwanini Serikali ya Ccm iliwatelekeza tangia uhuru hadi wa leo.,!
 
Last edited by a moderator:
Nikukaza buti wanamtwara yaan mwanzo mwisho mpaka Watubu ba'bakee!
 
Ranks, we usidanganye wenzako wakati we umekaa katika laptop tu! nyie Cdm mmeona m4c yenu imefeli ndo mnatumia karata ya wanamtwara! msisafirie nyota ya wenzenu mnawaponza wakina mama watoto na vikongwe kwa vurugu zenu!

Si kweli kuwa m4c imefeli. Nyie ni kwa vile mnaangalia mambo kwa mazoea ya kushughulikia matukio. In fact, kinachotokea Mtwara huwezi kukitenganisha na semina endelevu za elimu ya uraia kwa umma ambazo zimekuwa na zinaendelea kutolewa kupitia m4c chini ya uratibu wa Dkt W. Slaa na makamanda wenzake. Hayo ni matokeo ya semina endelevu (zingatia neno endelevu) - wadanganyika hawadangayiki tena.
 
''enyi viongozi mlioko madarakani kuweni na utu''hakuna sababu ya kutobadilika katika suala hili la gesi acheni kuwa wanafiki wa kutoa kauli ambazo zinalenga kuwachafua watu wa mtwara na kupenda saaaaaaana muonekane kuwa mna malengo mazuri na wananchi,nyie katika masuala ya rasilimali hakuna sehemu ambayo mnaweza mkaifanya kuwa reference point yenu,kwamfano sehemu zilizogundulika madini hakuna kitu cha pekee ambacho mnaweza kuwashawishi wananchi kwamba oneni kule wenzenu wamefaidika kwa moja,mbili tatu.......hivi kwanini mnanunua matatizo kiasi hiki??kwa muonekano wa nje mnaonesha huruma saaaana lakini nyie mtakua chanzo kikubwa cha machafuko katika nchi hii kwa sababu iweje watu wengi walilalamikie suala hilohilo??rais,mawaziri kumbukeni nani amewawezesha kuwa hapo mlipo hadi mnakuwa na viburi pamoja na majivuno,ni nani mnatakiwa kuwatumikia??mnajisikiaje kuwaona wananchi waliowachagua kwa kura nyingi mno wakidai vitu fulani na hamtaki kuwasikiliza??''kumbukeni kuwa mbegu hawatunzi katika kibuyu kimoja'' kwa lugha yetu ya kimwera tunasema ''mmbeju nngagoshea muntumba gumo'' kaeni mkijua kuwa kama kutatokea na machafuko kuhusu suala hili la gesi basi viongozi mlioko madarakani ndio mtakua chanzo kwa sababu maamuzi yenu hamtaki kuyatengua.......mnatakiwa kubadilisha maamuzi kwa kuwasikiliza wananchi wanataka nini kwa sababu sasa hivi walio wengi wanajua walau historia ya tanzania na ulimwengu kwa ujumla kwa sababu kila kukicha wanaelimika kwa namna moja au nyingine sio lazima kuingia darasani.
 
Ndugu zangu wa kusini hii ndo nafas yenu pekee ya kurudsha heshima, kama kuzaraulika the ifikie mwisho! Hakuna gesi kutoka mtwara, ful stop ... siasa zao wapeleke huko huko kwa wakwere!
 
Waziri Simbachawene amezuiwa njiani na wananchi hapa Mtwara kwa kuwekewa mawe njiani na FFU wanakuja hapa
mawazo ya viongozi wa ccm na serikali yake watasema hao ni chadema, na kama kweli ni chadema,ccm wajue sasa wamekwisha,mimi nilishasema kwamba mwaka 2015 ccm kitakuwa chama cha nne,nyuma ya nccr kwa maana ya CHADEMA,CUF na zhatatu NCCR
 
Kwa hiyo wewe unataka
kutuambia hii kwako ni story mbaya? Yaani Mungu kaamua kujibu Maombi ya
Wadanganyika kabla ya wakati,eti wewe unataka kumkosoa! Kajipange upya
na Nape wako.Viongozi badala ya kuhangaika na matatizo yanayowasumbua
Watanzania,wao wanahangaika na Dk Slaa na Chadema.waende kusini
wakawaambie wana Mtwara na Lindi ni kwanini wao ni Masikini,na kwanini
Serikali ya Ccm iliwatelekeza tangia uhuru hadi wa leo.,!

Sokoine, Wewe yaelekea hujui ulisemalo,serikali imewatelekeza vipi na kuliko mkoa upi na kwa vigezo gani! Toa data baada research sio kulishwa maneno na CDM na unakomaa na kutolea macho vitu bila data! weka facts zako hapa!
 
Last edited by a moderator:
BLACKTIGER,na wachaga komalieni mlima wenu wa Kilimakyaro, mapato yabaki K' njaro na wasukuma dhahabu zenu, wapemba mafuta yenu! uone mtafaidi nini watanzania! ACHENI UCHOCHEZI!
Huo mlima mboma upo huko kilimanjaro lakini unakufaidisha mpka wewe mpemba?wanamtwara wana haki ya kujua watafaidika vipi na rasilimali zao.Ningekuwepo kipindi kile dhahabu inagunduliwa geita walah mbona pangechimbika!wewe ndo mchochezi mkubwa tena utakuwa umetumwa.
 
Mkuu hayo siyo madai ya wana Mtwara, tafuta habari vizuri.

GWEN, hayo ndio madai yao ya msingi kama unakumbuka mabango yao siku ya maandamano! "GESI NI YA WAMAKOND" GESI HAITOKI MTWARA" n.k, vinginevyo wawe wameamua sasa iende Dar au wamefanyia amendment madai yao mkuu!
 
Last edited by a moderator:
Ndugu zangu wa kusini hii
ndo nafas yenu pekee ya kurudsha heshima, kama kuzaraulika the ifikie
mwisho! Hakuna gesi kutoka mtwara, ful stop ... siasa zao wapeleke huko
huko kwa wakwere!

munisijo,He hapo ndio umewashauri nini sasa! nenda na wewe huko Mtwara ukajiunge nao uandamane! we mbona uko uchagani kwenu unakula kiyoyozi cha mlima kilimakyaro! usichochee moto wa mwituni kuuzima na madhara kwa wengi wasio na hatia!
 
Last edited by a moderator:
Huo mlima mboma upo huko
kilimanjaro lakini unakufaidisha mpka wewe mpemba?wanamtwara wana haki
ya kujua watafaidika vipi na rasilimali zao.Ningekuwepo kipindi kile
dhahabu inagunduliwa geita walah mbona pangechimbika!wewe ndo mchochezi
mkubwa tena utakuwa umetumwa.

BLACKTIGER, kwani sasa hivi umekufa! si nenda mtwara sasa na wewe ili pakachimbike! au kwani dhahabu zimekwisha geita? mbona hujaenda utuletee picha za maandamano na updates! peleka ubaguzi wako huko Moshi!
 
Last edited by a moderator:
Haahaaa safari hii waliochukua ten percent lazima warudishe chenji yao

WE MTOTO UNAFIKILIA MBALI SANA, KWELI MAFISADI WASHALAMBA 10% NDO MAANA WANAKOMAA LZM ILETWE DAR, WKT HAKUNA JUSTIFICATION YA COST vs BENEFIT
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom