Mtaji wa Milioni 5-10 (TZS): Biashara gani unaweza kufanya?

Wakuu kama kichwa cha habari hapo juu. Najua hapa kuna wajuzi wa aina mbalimbali. Nimeona nililete kwenu kwa msaada zaidi.
Kuna dogo anataka kupiga mishe. Biashara gani inaweza kumuingizia milioni 1.5 hadi 2 kwa wiki kwa mtaji wa milioni 10?. Karibuni
Ulikuwa unamaanisha kwa wiki au kwa mwaka?
Yaani uwekeze 10milion leo, baada ya wiki uvune 2milion. Kweli?
Hiyo biashara haipo popote duniani, na haijawahi kuwepo.
 
Ipo inshu ni connection, tafuta connection mzee kuna michongo ya faida ndefu tu kwa mtaji wa kawaida.
Ulikuwa unamaanisha kwa wiki au kwa mwaka?
Yaani uwekeze 10milion leo, baada ya wiki uvune 2milion. Kweli?
Hiyo biashara haipo popote duniani, na haijawahi kuwepo.
 
Asijukatishe mtu tamaa ww sio wao .ila hiyo labda ujikite biashara za it.na ww uwe na kichwa na mjasiri .kwa mil 10 kama pia unaujuzi maalum imetulia.ila chonde usiguse madini

Daah Sasa Mbona Kina Marley Dollars na Chief Godlove wanapiga VIBUNDA kwenye madini?
 
Daah Sasa Mbona Kina Marley Dollars na Chief Godlove wanapiga VIBUNDA kwenye madini?
Sikusema hakuna hela ila kama nilivokwambia uwe na ujuzi maalumu
Ukitaka uingie madini leo ni mchakato mrefu kufikia kufanikiwa kiasi .ikiingia kwenye madini kwa kutamani mafanikio ya watu wa madini umeenda na maji.ila kama unautulivu fanya haya
1.chagua madin unayotaka utoboe nayo
2.nenda hudhuria kozi za kujifunza madini.pale kunduchi wanatoa ni miezi mitatu kozi
3.soma sana material za mtandaoni za kujifunza kuyajua na kuyathaminisha
4.kisha kaanze kushinda sokoni bila kufanya biashara walau miezi sita .
5.anza biashara kwa kiasi kidogo mtaji usizidi mil 2 .wewe jikite kwenye kujifunza sio kutajirika.ukizungusha miezi 3.sasa umejua biashara tukutane triple A kwa papa king tule bia
 
Dili ya direct tairi chakavu kwa mtaji wa nusu ya hiyo hela. Masoko yapo machaka ya kupata mzigo yapo
Dili nyingine ya moja kwa moja oil chafu. Faida yake haina hasara hata siku moja.
Sio Kweli hakuna kisicho na hasara usimjaze imani sana ni mbaya itapotokea kakutana na negative profit
 
Kuna viwanda sasa hivi vinakamua mafuta toka kwenye tairi chakavu huo mchakato unaitwa pyrolysis.

Na mafuta yanayokamuliwa yanaitwa IDO(Industrial Diesel Oli) haya yana soko kubwa sana kwenye viwanda vyote vinavyotumia mfumo wa BOILERS kama chanzo cha NISHATI

Tairi moja chakavu unainunua kati ya 1000 na 2000 nawe unaenda kuuza tani moja (approximately tairi 16 kwa laki moja.. Ukitoa mtaji na usafiri hukosi 50,000 faida kwa kila tani

Tairi kwa wingi zinapatikana kwenye mayard makubwa yenye kampuni za usafri
Viwanda vyenye kuhitaji hiyo malighafi hivi hapa
Mvuti Chanika
Kibada Kigamboni
Madafu Kibaha
Bagamoyo
Tegeta Dar

Naamini nimetoa maelezo ya kutosha sana
TATIANA
aliyetegwa
Nimeipenda biashara ambayo umeisema juu ya oil chafu hivyo ninaomba uweze kunisaidia location ya viwanda Ili nami nifanye investigation juu ya hili.

Pili naomba kuuliza ,kwenye viwanda inapelekwa oili ikiwa tayali au ninachotakiwa kupeleka ni izo taili tuu na kuuzia kiwanda? Asante Sana Kwa madini yako ,Mungu akubariki ,Kwa sisi vijana ambao bado tunajitafuta unatusaidia sana
 
Siku hizi wafugaji wa nguruwe wanakata mikia, waambie wqsikate ili uuze supu ya mikia nguruwe
 
Back
Top Bottom