Msimjaribu Zitto, mtaumia!

Msimjaribu Zitto, mtaumia!

Lowassa kiboko yao wanamsema pembeni akiingia wanafyata mikia Kama mbwa koko kuanzia huyo nape anayemlipa zombi
 
Kuna kila njama zinazofanywa kwa makusudi kabisa, kupunguzia kasi Zitto Kabwe katika jukwaa la kisiasa. Njama hizo zinatokea kwa vigogo fulani wa CHADEMA, wanaomuona kuwa Zitto ni mwiba mkali.

Historia ya karibuni ilionesha kuwa Zitto alisakamwa sana alipotaka kugombea uenyekiti na baada ya kuzipangua hoja zote za kumuumiza kisiasa ndani ya CHADEMA akaambulia kupoozwa kwa kusukumiwa cheo cha unaibu Katibu Mkuu, cheo ambacho hakina manufaa yoyote kwa CHADEMA wala kwa Zitto. Ili kuponesha maumivu na kutibu majeraha ya kisiasa, Zitto akakikubali cheo hicho, lakini ukweli ni kwamba hakifanyii kazi yoyote.

Uthibitisho mwingine wa kumshusha kisiasa Zitto ni pale ambapo hajahudhuria vikao vya CHADEMA na Kikwete huko Ikulu, kuna mambo ya msingi ambayo Zitto amekuwa akitofautiana na viongozi wengine wa CHADEMA na hayo ndio yanamfanya ajaribiwe kushushwa hadi na kutokuwekwa kwenye maamuzi mengi ya chama na yeye hustukia tu maamuzi yameshafanywa. Na anapotoa misimamo yake huwa ina tofauti na ya chama chake, mifano ipo mingi.

Tunawaasa vigogo wa CHADEMA kuwa hata ndugu zetu wa Kigoma walipopiga kura za Ubunge zilikuwa ni kura za Zitto na si za CHADEMA, hilo walielewe. Kama ilivyo kwa kura za Shibuda, zilikuwa ni za Shibuda lakini si za CHADEMA hilo linajidhihiri kwa kuwa kura za Urais za Kigoma 90% zilikuwa za Kikwete hata kwenye jimbo la Zitto.

Aliposhindwa Mbowe uchaguzi mkuu wa 2005, 2010 akawekwa Slaa, tunataka Zitto agombee 2015 tumpe kura zetu, kumbuka, hatuwapi kura CHADEMA tutampa Zitto Kabwe, bila yeye sahauni kura za wengi.

Kati ya vitu asivyopendezwa navyo Zitto ni namna ya chaguzi za wabunge wa upendeleo zinavyoendeshwa kimabavu ndani ya CHADEMA.

Tunawatahadharisha CHADEMA wasimjaribu Zitto, wataumia kisiasa.
Wewe ni zitto nini!!! Nadhani unajihami mapema baada ya kugundua kuwa jitihada zako za kuutafuta urais zinaweza kugonga mwamba mbele ya wapiganaji wengine ndani ya cdm. Kama wewe ndiwe kabwe basi usijidanganye na ndoto zako za kuwa RAIS wa nchi labda kama ni kuwa RAHISI. Inawezekana huto tusafari twako twa kukutana na viongozi maarufu duniani ni mbinu mojawapo utakayoitumia wakati wa kuchukua fomu lakini mbele ya cdm hilo si lolote si chochote. Utaangukia pua tu.
 
Lowassa kiboko yao wanamsema pembeni akiingia wanafyata mikia Kama mbwa koko kuanzia huyo nape anayemlipa zombi

Naona umeishiwa na hoja. Punguza munkar, kapate kikombe cha kahawa, labda hoja zitakujia.
 
Anagombea na lowassa kiboko yenu Mzee wa mamvi toka kaskazini chezea yeye

Lowassa akigombea na Zitto kura yangu ni kwa Zitto, akigombea na mwingine yeyote kura yangu ni kwa Lowassa.
 
Zombi=zomba umeingia mitini lowassa Mzee wa makanisa Hana mpinzani ndani ya ccm lazima wote mfyate Mkia mpaka Rais wenu
 
Zombi=zomba upo wapi? Naona huko ccm mnamtamani sana zito kiongozi wetu shupavu CDM. Viongozi wenu ni lowassa mwamba kaskazini jaribuni kumgusa muone moto Pambaf
 
Aliposhindwa Mbowe uchaguzi mkuu wa 2005, 2010 akawekwa Slaa, tunataka Zitto agombee 2015 tumpe kura zetu, kumbuka, hatuwapi kura CHADEMA tutampa Zitto Kabwe, bila yeye sahauni kura za wengi.

zomba mshauri Zitto achukue fomu kama anataka kugombea na sababu zote ulizozitoa siyo sifaya kuwa mgombea Uraisi kwa sababu wengi wanazo........................we are looking for someone uniquely wise and free of official graft and Zitto's habds are full of filthy gunk.............................sijui nikumbushie barrick alikata ngapi pale..............sijui Tanesco kwenye Dowans alikatiwa ngapi...............the list is endless.................hakuna atakayempa bwana mdogo ugali na ikifikia huko bora wanamagamba waendelee tu kutesa........theyr are the devils we know............at least...........
 
Last edited by a moderator:
Aliposhindwa Mbowe uchaguzi mkuu wa 2005, 2010 akawekwa Slaa, tunataka Zitto agombee 2015 tumpe kura zetu, kumbuka, hatuwapi kura CHADEMA tutampa Zitto Kabwe, bila yeye sahauni kura za wengi.

Kati ya vitu asivyopendezwa navyo Zitto ni namna ya chaguzi za wabunge wa upendeleo zinavyoendeshwa kimabavu ndani ya CHADEMA.

Tunawatahadharisha CHADEMA wasimjaribu Zitto, wataumia kisiasa.

Wewe zomba wewe unataka kumwaga damu! Urais ndani ya CDM kwa sasa ni taboo kuusema. CDM wana kauli yao kuwa hata ukiweka jiwe dhidi ya CCM basi CDM itashinda! Hivyo kila mtu anadhani akiwekwa na CDM kwenye kugombea urais atashinda. Kila mtu anautolea macho urais huko CDM.
 
Last edited by a moderator:
mkuu zomba kama unadhani zitto atasapoti unachoongelea ni vizuri zaidi ukamshawishi aanzhishe chama chake.awe mwenyekiti then 2015 agombee uraisi.naona shida yako na wachache wengine ni zitto kuwa mwenyekiti wa chadema.unadhani ni zitto tu ndani ya cdm mwenye uwezo wa kuwa mwenyekiti?kama watu wengine wapenzi w a tundulissu au mnyika au slaa nk wangetaka kila wanaomshabikia kuwa mwenyekiti chadema ingeishia wapi?kama ni supporter wa zitto ni vizuri kusapoti nafasi yake aliyeko sasa na sio kuingilia maamuzi ya chama ya kupanga uingozi.unaona jinsi viongozi wengine wanavyozunguka nchi nzima kuimarisha chama na kukijenga lakini huoni umuhimu wao.unachotaka ni zitto awe mwenyekiti na uimarishaji wa chama wafanye wengine.una laana wewe.be blessed!

Well well said mkuu!
 
Back
Top Bottom