Msimjaribu Zitto, mtaumia!

Msimjaribu Zitto, mtaumia!

Sio wananchi wote tuna vyama

Kweli kabisa, nakubaliana nawe 100 kwa 100, wako wengi wasio na vyama na wengi wao ni wapiga kura pia na hao ni mfano mzuri wa hii mada, huwa hawachagui chama wanachaguwa wanaeona anafaa kuwa kiongozi mzuri.
 
magamba yanajua kimeshanuka hapo 2015

Leo nimemsikia kiboko yenu kwenye ITV akikumbusha operation Sangara mwaka 2008, mlikuwa mkisema hayo hayo lakini kufika wakati wa kura mkaambulia wabunge 23 kati ya zaidi 200. Safari mkijitahidi sana mnaweza kuongeza viti vingine 23 vikawa 46. Tunawatakia kila la heri. Lakini Urais muusahau kabisa labda agombee Zitto kama bado atakuwepo chadema, hapo kidogo ntashawishika kwa sababu kura yangu atakuwa nayo (kama kuna uhai na majaaliwa) na ntampigia debe kwa wengine.
 
Hapana sijakatiwa pochi na mtu wala sitegemei kama kuna siku itakuwa hivyo.

Zitto ni kijana ambae hakuna ataepinga kuwa ameipaisha sana chadema, lakini kwa masikitiko makubwa naona chadema wanamtenga, sijui kwanini.

Namfatilia sana siasa zake, ingawa na yeye ni kama binaadam mwengine yeyote kwani sote sisi hakuna aliyekamilika, juu ya mapungufu yake lakini ni kijana anaejituma, mchapa kazi na anakwenda na wakati kisiasa. hayumbishwi hovyo na huwa ana misimamo katika hoja zake. Namsikitikia sana kuwepo CHADEMA kwani mwisho wa siku watampiga teke kama vile hajawafanyia kitu. Nyota njema huonekana Alafajiri.

Zitto hata akiwa chadema na akigombea basi kura yangu anayo.
Ningependa sana kuamini lakini kwa maneno ya hapo juu kila nikisoma naona Pochi kubwa tu.. Maana siku hizi CCM wanakata sii mchezo ahaaahahaha!
Zitto kusema kweli kichwa lakini wewe huelewi tu kwamba bado kabisa hajakomaa kisiasa na anapopingwa ni ktk shule ya kumkomaza zaidi kisiasa, naweza kwambia kwamba January mbali na utaalam ni mwanasiasa zaidi na nadhani kwa sababu ameishi nje anajua mchezo wa Siasa ni kama chase. Kama ulivyosema binadamu hatukosi mapungufu na pengine hujatuelewa Chadema ya kwamba kwa kila tunapompinga Zitto ni ktk kumwonyesha njia nzuri ya kisiasa alotakiwa kupita na sii vinginevyo. Wewe kama mwanaCCM unaona sawa tu na sisi ndio hatumpendi kwa sababu hiyo ndio njia yako wewe unayopita, hivyo hapa bado kabisa Zitto hajaweza kutofautisha na kikubwa zaidi kuelewa maana ya neno UPINZANI.

Huku Majuu siasa zake hata kama wewe uko sawa na najua fika sera yako ni bora zaidi bado kama mpinzani nitakupinga na kukuonyesha ya kwamba yangu bado nzuri zaidi kwa kukukosoa sera, utekelezaji wake na mafao yake. Hii ndio siasa kaa sii kukosoana kuna sababu gani ya kuiwepo upinzani wa kisiasa. Lakini kwetu unakuta kina Zitto wanafikiria kwamba CCM is on the right track kama watafanya marekebisho ktk utekelezaji. Hii sio siasa tena ila ni mawazo ya kuendesha corporates. Siasa na kuendesha shirika ni mchezo na uwanja tofauti kabisa kama vile tofauti ya kucheza mpira wa miguu na Cricket.

Siasa sio utekelezaji bali itikadi na sera kwanza. Mnapingana hapo nmaana kama sote tunakubali tatizo nchini lipo ktk utekelezaji basi kuna sababu gani ya kuwa na vyama vingi?..Tukiweza kuelewa hilo na vijana wetu wakielewa nini maana ya tofauti za kiitikadi, kisera na kikubwa zaidi neno UPINZANI basi Zitto na vijana wengine watakuwa wameiva. Zitto ni msomi mzuri tu na anapenda kujiendeleza lakini bado kisiasa anatakiwa kujiendeleza zaidi.. Hapo atakuwa amekamilika.
 
Kuwa chama chochote hakumuondelei mtu umahiri wake wa kazi. Isipokuwa wale ambao hawakufanya lolote la maana kutoka katika vyama walivyokuwepo zamani, mfano Slaa alitemwa CCM katika kura za maoni kwa kuwa walishamuona kuwa hafai uongozi, wakati huohuo chadema licha ya kumpa shutuma nyingi sana Zitto wameshindwa kumpiga chini kwa kuwa ni kijana hodari na amezisoma mbinu na anapambana nazo akiwa humohumo ndani. Slaa yalimshinda hayo ya kupambana akiwa ndani ya CCM, inaonesha kabisa ni mtu aliyekuwa ana uchu wa madaraka na si uongozi.

Ulimaanisha nini uliposema unamsikitikia kuwa CDM?
 
Leo nimemsikia kiboko yenu kwenye ITV akikumbusha operation Sangara mwaka 2008, mlikuwa mkisema hayo hayo lakini kufika wakati wa kura mkaambulia wabunge 23 kati ya zaidi 200. Safari mkijitahidi sana mnaweza kuongeza viti vingine 23 vikawa 46. Tunawatakia kila la heri. Lakini Urais muusahau kabisa labda agombee Zitto kama bado atakuwepo chadema, hapo kidogo ntashawishika kwa sababu kura yangu atakuwa nayo (kama kuna uhai na majaaliwa) na ntampigia debe kwa wengine.

inshallah Mungu atatupa uhai..mimi kiukweli simpingi Zitto na wanaompinga zitto hapa wanapinga tu kwa vile wewe mwana ccm ndio umeileta hii mada hapa wakijua kuwa umelipwa,
la zitto akichaguliwa na chama basi tutakuwa nyuma yake,
kwa hiyo anza kukusanya watu kabisa huko piga kampeni za chini chini wainge madarakani kwani wakiingia hapo 2015,
hata kama Zito hatakuwa rais ila atakuwa kwenye cheo kikubwa na chenye maamuzi.
 
Mkandara,

Nimekusoma na nimekuelewa. Mimi na Zitto labda afanye madudu yasiyo-sameheka. Namkubali sana tena sana.

Mfano mzuri ni pale alipopigania mitambo ya Dowans inunuliwe, wengi wakampinga hususan kupitia humu JF, mwishowe, umeme tukakosa kwa muda mrefu, mitambo tutailipia kwani mahakama zimeshaamuwa, na mitambo bado ipo na ndiyo inatumika kwa sasa na watu wote kimya. Jee, wangemsikiliza Zitto? Hasara tuliyoipata isingekuwepo au ingekuwa ni haba sana. Hilo wapingaji wakubwa walikuwa chadema wakiongozwa na mzee mwanakijiji humu JF. Nashangaa sana kuwa hata yeye kakaa kimya na mitambo inadunda.

Kwa mfano huo, namuona Zitto kuwa anaona mbali zaidi ya wanasiasa wengi na maslahi yake ni nchi kwanza.
 
Ulimaanisha nini uliposema unamsikitikia kuwa CDM?

Namsikitikia kwa kuwa chadema hawamuenzi na kumkubali ipasavyo, hata ukisoma maoni tu ya wanachadema wa humu JF kuhusu Zitto utaona kuwa na uchapa kazi wake wote lakini chadema hawamthamini kwa sana, wanamuona kama yupo yupo tu.
 
Na wewe si tupo pamoja ndio maana ukaziona zote hizo. Au? Humu tutabanana sote, labda mtuambie CCM marufuku, mdanganyane wenyewe kwa wenyewe.
Zombi kanunua modem juzi Hana kazi ya kuifanyia zaidi ya kufungua thread na kuisimamia ili malipo kwa nape yawe makubwa
 
inshallah Mungu atatupa uhai..mimi kiukweli simpingi Zitto na wanaompinga zitto hapa wanapinga tu kwa vile wewe mwana ccm ndio umeileta hii mada hapa wakijua kuwa umelipwa,
la zitto akichaguliwa na chama basi tutakuwa nyuma yake,
kwa hiyo anza kukusanya watu kabisa huko piga kampeni za chini chini wainge madarakani kwani wakiingia hapo 2015,
hata kama Zito hatakuwa rais ila atakuwa kwenye cheo kikubwa na chenye maamuzi.

Bado ni mbali sana na siasa hazitabiriki. Ni vizuri mkaendelea kukijenga chama chenu kwani uwepo wake ni faraja kwa wananchi wa Tanzania kwa kuwa faida ya vyama vingi ni kuwa chama chochote kilichopo madarakani ni lazima kichape kazi kwa bidii la sivyo kitakosa uongozi. Uwepo wa upinzani wenye nguvu ni kichocheo cha maendeleo, hilo halipingiki.
 
Namsikitikia kwa kuwa chadema hawamuenzi na kumkubali ipasavyo, hata ukisoma maoni tu ya wanachadema wa humu JF kuhusu Zitto utaona kuwa na uchapa kazi wake wote lakini chadema hawamthamini kwa sana, wanamuona kama yupo yupo tu.
Mbona nyie hamumuenzi lowassa mmeiba Mihela kibao kawabebea mizigo yenu mpaka ya Rais wenu
 
Mkandara,

Nimekusoma na nimekuelewa. Mimi na Zitto labda afanye madudu yasiyo-sameheka. Namkubali sana tena sana.

Mfano mzuri ni pale alipopigania mitambo ya Dowans inunuliwe, wengi wakampinga hususan kupitia humu JF, mwishowe, umeme tukakosa kwa muda mrefu, mitambo tutailipia kwani mahakama zimeshaamuwa, na mitambo bado ipo na ndiyo inatumika kwa sasa na watu wote kimya. Jee, wangemsikiliza Zitto? Hasara tuliyoipata isingekuwepo au ingekuwa ni haba sana. Hilo wapingaji wakubwa walikuwa chadema wakiongozwa na mzee mwanakijiji humu JF. Nashangaa sana kuwa hata yeye kakaa kimya na mitambo inadunda.

Kwa mfano huo, namuona Zitto kuwa anaona mbali zaidi ya wanasiasa wengi na maslahi yake ni nchi kwanza.
Katika mitambo ya Dowans mkuu wangu sikuwa naye Zitto maadam sababu za chama chake zilikuwa wazi kabisa. Na binafsi yangu siamni kukunua mali ya dhulma, wizi, ama mali ambayo ingekuwa ushahidi mzuri wa kesi nzima ya Richmond dhidi ya EL maana ilikuwa chakavu, utapeli na wakabadilisha sheria ili tuinunue. Wewe kama mpinzani huwezi kukubali sheria ibadilishwe kwa ajili ya kitu kimoja tena chenyeb utata wa mkataba wakati nyuma chama chako kimepigana kwa nguvu zote kuondoa ununuzi wa vifaa chakavu baada ya kujifunza toka ATC, magari na vifaa ktk serikali na mashirika mengine ya Umma.

Pale kulikuwa na mchezo wa kumsafisha EL mapema na kupoteza ushahidi halafu unamlipa mtu yuleyule mbaya wenu kisheria. Hata kama mitambo hiyo imenunuliwa na shirika la Marekani na tumepachikwa kiraka ktk nguo yetu bado haina maana tunakubaliana na hatua iliyochukuliwa. Na kikubwa zaidi matatizo yetu ya Umeme ni zaidi ya uwezo wa Dowans wala hizo megawatts 100 hazikuwa sababu kabisa ya sisi kukosa umeme kwa sababu kama JK angetaka kununua mtambo mpya angeweza na kwa order ya siku moja. Kama unakumbuka toka mgogoro wa Dowans wakisema kuagiza mtambo itachukua miezi tisa kufika nchini haya ilipita miezi 16 kabla ya mitambo hiyo kuanza kazi kwa hiyo CCM na uongozi walilazimisha kitu ambacho hakikutakiwa. Tumeozeshwa mke tusompenda.
 
Katika mitambo ya Dowans mkuu wangu sikuwa naye maadam sababu za chama chake zilikuwa wazi kabisa. Na binafsi yangu siamni kukunua mali ya wizi, mali ambayo ingekuwa ushahidi mzuri wa kesi nzima ya EL maana ilikuwa chakavu na wakabadilisha sheria ili tuinunue. Wewe kama mpinzani huwezi kukubali sheria ibadilishwe kwa ajili ya kitu kimoja wakati nyuma chama chako kimepigana kwa nguvu zote kuondoa ununuzi wa vifaa chakavu baada ya kujifunza ATC na mashirika mwngine ya Umma.

Pale kulikuwa na mchezop wa kumsafisha EL mapema na kupoteza ushahidi halafu unamlipa mtu yuleyule mbaya wenu kisheria. Hata kama mitambo hiyo imenunuliwa na shirika la Marekani na tumepachikwa kiraka ktk nguo yetu bado haina maana tunakubaliana na hatua iliyochukuliwa. Na kikubwa zaidi matatizo yetu ya Umeme ni zaidi ya uwezo wa Dowans wala hizo megawatts 100 hazikuwa sababu kabisa ya sisi kukosa umeme kwa sababu kama JK angetaka kununua mtambo mpya angeweza na kwa order ya siku moja. Kama unakumbuka toka mgogoro wa Dowans wakisema kuagiza mtambo itachukua miezi tisa ilipitwa miezi 16 kabnla ya mitambo hiyo kuanza kazi kwa hiyo CCM na uongozi walilazimisha kitu ambacho hakikutakiwa. Tumeozeshwa mke tusompenda.

Mbona mpaka leo hii inatumika? na kila mtu yuko kimya, fedha ambayo inabidi walipwe na mitambo ilikuwa imezimwa ni nyingi kuliko tungeinunua.
 
Namsikitikia kwa kuwa chadema hawamuenzi na kumkubali ipasavyo, hata ukisoma maoni tu ya wanachadema wa humu JF kuhusu Zitto utaona kuwa na uchapa kazi wake wote lakini chadema hawamthamini kwa sana, wanamuona kama yupo yupo tu.

Inaonekana magamba wanatafuta kujua Zitto amepewa kazi kubwa katika kuhakikisha CDM kinaisambaratisha CCM. Maana kila siku watauliza mbona Zitto haonekani Jangwani? wakijibiwa watauliza katika M4C nako? wakijibiwa atashiriki saa ngapi katika kamati za bunge? Ulishawahi kujiuliza kwanini wafuga kuku wa kisasa kila cycle wanarudi kununua vifaranga na kwa nini wasizalishe wenyewe?
 
Inaonekana magamba wanatafuta kujua Zitto amepewa kazi kubwa katika kuhakikisha CDM kinaisambaratisha CCM. Maana kila siku watauliza mbona Zitto haonekani Jangwani? wakijibiwa watauliza katika M4C nako? wakijibiwa atashiriki saa ngapi katika kamati za bunge? Ulishawahi kujiuliza kwanini wafuga kuku wa kisasa kila cycle wanarudi kununua vifaranga na kwa nini wasizalishe wenyewe?

Zitto for President 2015!
 
Back
Top Bottom