Msimjaribu Zitto, mtaumia!

I believe I am dealt the unfortunate and futile task akin to transmitting electromagnetic signals to a newly found species of non-ruminant Andean llamas, llamus ignoramus.

Poor you.
 
wewe ni zitto z kabwe nakushauri usubiri hadi 2025 utakuwa na hekima zaidi. tumwachie LOWASA kwanza

Hapana mimi si Zitto Kabwe, mimi naona Zitto anatufaa zaidi ya Lowassa ikiwa sheria zitamruhusu kugombea ikifika wakati wa kugombea.
 
Sheria za kibinaadam hutungwa kwa nyakati zake, zamani darsa la kwanza watu wanaanza tayari washa balehe, imeshuka mpaka sasa hata miaka 5 wanaanza std 1.

Zamani ilikuwa inaaminika kila unavyokuwa ndio unakuwa na uwezo zaidi, siku hizi watafiti na wasomi wanaamini kuwa "productivity tends to fall with age" soma hapa: Age and productivity: Over 30 and over the hill | The Economist

Nadhani ni wakati muafaka wakati tunaelekea kwenye kutunga katiba mpya umri wa kugombea Urais nao upunguzwe ili tuwe na highly productive president. Wewe unaonaje.

Sina nia ya kuwachafua chadema, kwani Zitto ni yeye mwenye aliyetangaza nia ya kugombea Urais na mimi namkubali na ikiwa chama chake kitamptisha na niko hai basi nnamuahidi kura yangu.

Lakini chadema "msimjaribu, mtaumia".

Mimi naamini uwepo wa upinzani wowote wenye nguvu (chadema kwa sasa) ndiyo chachu ya maendeleo na usimamizi mzuri wa mali za Watanzania.
Ahahah! haha! haha hapo pekundu mkuu wangu umechapia wala sii kutoka rohoni na ndicho tunachoogopa wadanganyika. Zitto hazuiliwi na mtu yeyote kugombea wala nia yake haiwezi kupotea ikiwa ruksa kikatiba. Chadema kama chama walimshangaa tu Zitto kusema nia ile wakati anajua fika kwamba katiba hairuhusu na pia sii muda wake kujitamngaza.

Ikumbuikwe tu kugombea Urais inatakiwa usiri, tactics na mipango kamambe nyuma ya mgombea kwa kutazama hali na mazingira ya nyakati na sii swala la kukimbia Olimpiki mwenye mbio ndiye atachaguliwa. Kugombea Urais ni kaa mchezo wa mpira mnapolitafuta goli, hivyo sii vizuri kwa mchezaji kucheza faul ktk eneo la penaty, itakuwa umewapa mwanya wapinzani kufunga goli kwa miguu 12 na huwezi kukaba hadi penalty..

Ndio maana nasema Zitto bado anapikwa, utampenda zaidi pindi muda wake utakapo fika fanya subra maana Chadema wapo vijana wengi tu mfano wake japokuwa hawana sauti..Hakuna aliyemkataza kugombea isipokuwa tunamwombe Mungu ampe subira, SIASA ni mchezo wa mpira unaochezwa na watu 11 sio golf au Tennis kila mchezaji anajitegemea kwa uwezo wake.
 
Mkandara,

Hiyo ni sentensi moja kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
 
Mkuu mbona ishu ya zito ni nyepesi sana kama unaona ana umaarufu kuliko CDM basi mshauri awe mgombea binafsi ili umpe kura yako . Na kuhusu nani atagombea urais kwa tkt ya CDM ni vikao halali na wanachama wataamua .
 
Mkuu mbona ishu ya zito ni nyepesi sana kama unaona ana umaarufu kuliko CDM basi mshauri awe mgombea binafsi ili umpe kura yako . Na kuhusu nani atagombea urais kwa tkt ya CDM ni vikao halali na wanachama wataamua .

Hivi hujamsikia Zitto akitangaza nia ya kugombea Urais 2015?
 
Back
Top Bottom