Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Nawashangaa sana viongozi wetu. Eti wengi wanasema hawataki kuchagua upande kati ya Urusi na Ukraine, hata kwenye mambo ya kura wanajitoa. Huu ni uoga na unafiki usiokubalika kwa viongozi wa nchi za Afrika.
Ndio maana nimesema siku zote Nyerere alikuwa mtu mwenye busara sana, alisimamia principles, sio urafiki au maslahi ya Tanzania
NInaamini kwa dhati katika hili Nyerere angemlaani Putin katika suala la hii vita. Alishasema, kwamba hii mipaka ya nchi zetu, japokuwa mara nyingine hatuipendi, lakini hatutalazimisha ibadilishwe. Kuwekwa kwake kwa sasa ni jambo la kihistoria na acha ibaki hivyo kwa ajili ya amani na ujirani mwema, japo labda hatuipendi.
Kwa hivyo basi, katika suala la vita kati ya Urusi na Ukraine, madai ya Putin kwamba Ukraine inawaonea watu wenye asili ya Urusi ndani ya Ukraine kwa hiyo wanavamia Ukraine kuwakomboa watu wenye asili ya Urusi, ni ujinga uliopita kikomo na usiopaswa kukubalika na kiongozi yeyeote mwenye akili timamu. Ni sawa na sisi Tanzania, leo hii tuwaambie Wakenya kwamba maeneo ya Kajiado wanayoishi Masai wa Kenya yako nyuma kimaendeleo kwa hiyo tutaingia Kenya kuchukua maeneo haya kwa kuwa Wamasai wa huko ni sehemu ya Wamasai wa Tanzania na wanapaswa kufikiriwa na kuendelezwa kama sehemu nyingine za Kenya, halafu tuivamie Kenya kijeshi. Unaona ujinga huo?
Sasa hapo ndipo Africa Union ilipaswa isimamie bila woga na kujali maslahi. Kina Malema kule South Africa wanasema tutam-support Putin na Warusi katika huu mgogoro kwa kuwa Urusi ilituunga mkono kwenye freedom strugle. Stupid stinking thinking! Kumbuka Nyerere alichosema pia, hatukuwaunga mkono ANC kwa sababu ni weusi kama sisi, bali kwa sababu walikuwa wanabaguliwa na hatupendi ubaguzi wa rangi kwa kuwa unakiuka haki za binadamu.
Sasa Nyerere alimaanisha nini? Kwamba itakuwa ujinga sana kwa Raisi wa Tanzania, siku ANC, chama cha weusi wengi kule South Africa, wakianza kunyanyasa wazungu na kuwabagua, Tanzania kuendelea kuwaunga mkono kwa sababu tu ANC ni chama cha weusi wenzetu. Ikiwa wazungu hao Afrika Kusini leo hii wakibaguliwa na haki zao za kibinadamu kukiukwa na ANC na watu weusi wa South Afrika, na wazungu hao wakaanzisha mapambano ya kujikomboa, itabidi Tanzania tuwa-support na kuwapa kambi zote hapa nchini zilizokuwa za ANC kuwa kambi zao za kupigania uaswa nchini Afrika Kusini.
Kumbuka pia, kwa nini Nyerere aliunga mkono Biafra kule Nigeria, japo tulikuwa marafiki wa serikali ya Nigeria? Kwa nini Nyerere alivunja uhusiano na Uingereza, Israel na Ujerumani wakati fulani licha ya misaada mikubwa tuliyokuwa tunapata toka kwao? NI suala la principles, sio maslahi ya nchi au urafiki. Haya ndio mambo yalifanya Nyerere aheshimike sana duniani. Rational and fairness principles.
Leo hii jirani yako anakupa lift kwenda kazini, siku akishutumiwa kuwafanyia unajisi watoto, utamtetea au kukaa kimya kwa sababu amekuwa akikupa msaada? Labda wewe kama una tatizo la mtindio wa ubongo.
Sasa hawa viongozi wetu hapa Afrika, kama wangejua jinsi ya kusimamia principles badala ya maslahi, hili suala la Urusi na Ukraine is a no brainer - wangetoa tamko la kumlaani Putin. Huwezi kusema mbona Marekani walivamia sijui Iraq, Libya nk. Utakuwa unatukumbusha tu jinsi usivyo na msimamo kwa sababu wakati Marekani wakivamia Iraq na Libya ulipaswa kulaani kwa nguvu zote pia. Na two wrongs do not make a right. So African leaders, stop your nonsensical approach to the Russia-Ukraine debacle. You are just proving what Trump is always accusing us of - something about shit hole countries!
Angalia hapa unafiki wa nchi yetu Tanzania:
KURA ZA UMOJA WA MATAIFA KUPINGA UVAMIZI WA URUSI KWA UKRAINE
Ndio maana nimesema siku zote Nyerere alikuwa mtu mwenye busara sana, alisimamia principles, sio urafiki au maslahi ya Tanzania
NInaamini kwa dhati katika hili Nyerere angemlaani Putin katika suala la hii vita. Alishasema, kwamba hii mipaka ya nchi zetu, japokuwa mara nyingine hatuipendi, lakini hatutalazimisha ibadilishwe. Kuwekwa kwake kwa sasa ni jambo la kihistoria na acha ibaki hivyo kwa ajili ya amani na ujirani mwema, japo labda hatuipendi.
Kwa hivyo basi, katika suala la vita kati ya Urusi na Ukraine, madai ya Putin kwamba Ukraine inawaonea watu wenye asili ya Urusi ndani ya Ukraine kwa hiyo wanavamia Ukraine kuwakomboa watu wenye asili ya Urusi, ni ujinga uliopita kikomo na usiopaswa kukubalika na kiongozi yeyeote mwenye akili timamu. Ni sawa na sisi Tanzania, leo hii tuwaambie Wakenya kwamba maeneo ya Kajiado wanayoishi Masai wa Kenya yako nyuma kimaendeleo kwa hiyo tutaingia Kenya kuchukua maeneo haya kwa kuwa Wamasai wa huko ni sehemu ya Wamasai wa Tanzania na wanapaswa kufikiriwa na kuendelezwa kama sehemu nyingine za Kenya, halafu tuivamie Kenya kijeshi. Unaona ujinga huo?
Sasa hapo ndipo Africa Union ilipaswa isimamie bila woga na kujali maslahi. Kina Malema kule South Africa wanasema tutam-support Putin na Warusi katika huu mgogoro kwa kuwa Urusi ilituunga mkono kwenye freedom strugle. Stupid stinking thinking! Kumbuka Nyerere alichosema pia, hatukuwaunga mkono ANC kwa sababu ni weusi kama sisi, bali kwa sababu walikuwa wanabaguliwa na hatupendi ubaguzi wa rangi kwa kuwa unakiuka haki za binadamu.
Sasa Nyerere alimaanisha nini? Kwamba itakuwa ujinga sana kwa Raisi wa Tanzania, siku ANC, chama cha weusi wengi kule South Africa, wakianza kunyanyasa wazungu na kuwabagua, Tanzania kuendelea kuwaunga mkono kwa sababu tu ANC ni chama cha weusi wenzetu. Ikiwa wazungu hao Afrika Kusini leo hii wakibaguliwa na haki zao za kibinadamu kukiukwa na ANC na watu weusi wa South Afrika, na wazungu hao wakaanzisha mapambano ya kujikomboa, itabidi Tanzania tuwa-support na kuwapa kambi zote hapa nchini zilizokuwa za ANC kuwa kambi zao za kupigania uaswa nchini Afrika Kusini.
Kumbuka pia, kwa nini Nyerere aliunga mkono Biafra kule Nigeria, japo tulikuwa marafiki wa serikali ya Nigeria? Kwa nini Nyerere alivunja uhusiano na Uingereza, Israel na Ujerumani wakati fulani licha ya misaada mikubwa tuliyokuwa tunapata toka kwao? NI suala la principles, sio maslahi ya nchi au urafiki. Haya ndio mambo yalifanya Nyerere aheshimike sana duniani. Rational and fairness principles.
Leo hii jirani yako anakupa lift kwenda kazini, siku akishutumiwa kuwafanyia unajisi watoto, utamtetea au kukaa kimya kwa sababu amekuwa akikupa msaada? Labda wewe kama una tatizo la mtindio wa ubongo.
Sasa hawa viongozi wetu hapa Afrika, kama wangejua jinsi ya kusimamia principles badala ya maslahi, hili suala la Urusi na Ukraine is a no brainer - wangetoa tamko la kumlaani Putin. Huwezi kusema mbona Marekani walivamia sijui Iraq, Libya nk. Utakuwa unatukumbusha tu jinsi usivyo na msimamo kwa sababu wakati Marekani wakivamia Iraq na Libya ulipaswa kulaani kwa nguvu zote pia. Na two wrongs do not make a right. So African leaders, stop your nonsensical approach to the Russia-Ukraine debacle. You are just proving what Trump is always accusing us of - something about shit hole countries!
Angalia hapa unafiki wa nchi yetu Tanzania:
KURA ZA UMOJA WA MATAIFA KUPINGA UVAMIZI WA URUSI KWA UKRAINE