Msimamo wa nchi za Afrika juu ya suala la Urusi na Ukraine ni jambo dogo sana linalopaswa kuongozwa na kanuni, sio maslahi ya nchi zetu

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Nawashangaa sana viongozi wetu. Eti wengi wanasema hawataki kuchagua upande kati ya Urusi na Ukraine, hata kwenye mambo ya kura wanajitoa. Huu ni uoga na unafiki usiokubalika kwa viongozi wa nchi za Afrika.

Ndio maana nimesema siku zote Nyerere alikuwa mtu mwenye busara sana, alisimamia principles, sio urafiki au maslahi ya Tanzania

NInaamini kwa dhati katika hili Nyerere angemlaani Putin katika suala la hii vita. Alishasema, kwamba hii mipaka ya nchi zetu, japokuwa mara nyingine hatuipendi, lakini hatutalazimisha ibadilishwe. Kuwekwa kwake kwa sasa ni jambo la kihistoria na acha ibaki hivyo kwa ajili ya amani na ujirani mwema, japo labda hatuipendi.

Kwa hivyo basi, katika suala la vita kati ya Urusi na Ukraine, madai ya Putin kwamba Ukraine inawaonea watu wenye asili ya Urusi ndani ya Ukraine kwa hiyo wanavamia Ukraine kuwakomboa watu wenye asili ya Urusi, ni ujinga uliopita kikomo na usiopaswa kukubalika na kiongozi yeyeote mwenye akili timamu. Ni sawa na sisi Tanzania, leo hii tuwaambie Wakenya kwamba maeneo ya Kajiado wanayoishi Masai wa Kenya yako nyuma kimaendeleo kwa hiyo tutaingia Kenya kuchukua maeneo haya kwa kuwa Wamasai wa huko ni sehemu ya Wamasai wa Tanzania na wanapaswa kufikiriwa na kuendelezwa kama sehemu nyingine za Kenya, halafu tuivamie Kenya kijeshi. Unaona ujinga huo?

Sasa hapo ndipo Africa Union ilipaswa isimamie bila woga na kujali maslahi. Kina Malema kule South Africa wanasema tutam-support Putin na Warusi katika huu mgogoro kwa kuwa Urusi ilituunga mkono kwenye freedom strugle. Stupid stinking thinking! Kumbuka Nyerere alichosema pia, hatukuwaunga mkono ANC kwa sababu ni weusi kama sisi, bali kwa sababu walikuwa wanabaguliwa na hatupendi ubaguzi wa rangi kwa kuwa unakiuka haki za binadamu.

Sasa Nyerere alimaanisha nini? Kwamba itakuwa ujinga sana kwa Raisi wa Tanzania, siku ANC, chama cha weusi wengi kule South Africa, wakianza kunyanyasa wazungu na kuwabagua, Tanzania kuendelea kuwaunga mkono kwa sababu tu ANC ni chama cha weusi wenzetu. Ikiwa wazungu hao Afrika Kusini leo hii wakibaguliwa na haki zao za kibinadamu kukiukwa na ANC na watu weusi wa South Afrika, na wazungu hao wakaanzisha mapambano ya kujikomboa, itabidi Tanzania tuwa-support na kuwapa kambi zote hapa nchini zilizokuwa za ANC kuwa kambi zao za kupigania uaswa nchini Afrika Kusini.

Kumbuka pia, kwa nini Nyerere aliunga mkono Biafra kule Nigeria, japo tulikuwa marafiki wa serikali ya Nigeria? Kwa nini Nyerere alivunja uhusiano na Uingereza, Israel na Ujerumani wakati fulani licha ya misaada mikubwa tuliyokuwa tunapata toka kwao? NI suala la principles, sio maslahi ya nchi au urafiki. Haya ndio mambo yalifanya Nyerere aheshimike sana duniani. Rational and fairness principles.

Leo hii jirani yako anakupa lift kwenda kazini, siku akishutumiwa kuwafanyia unajisi watoto, utamtetea au kukaa kimya kwa sababu amekuwa akikupa msaada? Labda wewe kama una tatizo la mtindio wa ubongo.

Sasa hawa viongozi wetu hapa Afrika, kama wangejua jinsi ya kusimamia principles badala ya maslahi, hili suala la Urusi na Ukraine is a no brainer - wangetoa tamko la kumlaani Putin. Huwezi kusema mbona Marekani walivamia sijui Iraq, Libya nk. Utakuwa unatukumbusha tu jinsi usivyo na msimamo kwa sababu wakati Marekani wakivamia Iraq na Libya ulipaswa kulaani kwa nguvu zote pia. Na two wrongs do not make a right. So African leaders, stop your nonsensical approach to the Russia-Ukraine debacle. You are just proving what Trump is always accusing us of - something about shit hole countries!

Angalia hapa unafiki wa nchi yetu Tanzania:
KURA ZA UMOJA WA MATAIFA KUPINGA UVAMIZI WA URUSI KWA UKRAINE
1665769252207.png
 
Naunga mkono hoja hii, kipindi cha president Nyerere (rip),Africa yote ilikua inasubiria tamko kutoka Dar es Salaam ili nao watoe msimamo wao, eti leo tumekua laughing stock hata Rwanda 🇷🇼 inatutingisha,Mr.Malema ni mnafiki na mwongo mkubwa, anapayuka na end of the day anasomesha binti yake kwenye white dominates school na yeye mwenyewe anaishi kwenye hizi security complex za white people's, why asiishi kwenye township yake pale seshogo?,anajua within a week atakula chuma!
 
Nawashangaa sana viongozi wetu. Eti wengi wanasema hawataki kuchagua upande kati ya Urusi na Ukraine, hata kwenye mambo ya kura wanajitoa. Huu ni uoga na unafiki usiokubalika kwa viongozi wa nchi za Afrika.

Ndio maana nimesema siku zote Nyerere alikuwa mtu mwenye busara sana, alisimamia principles, sio urafiki au maslahi ya Tanzania

NInaamini kwa dhati katika hili Nyerere angemlaani Putin katika suala la hii vita. Alishasema, kwamba hii mipaka ya nchi zetu, japokuwa mara nyingine hatuipendi, lakini hatutalazimisha ibadilishwe. Kuwekwa kwake kwa sasa ni jambo la kihistoria na acha ibaki hivyo kwa ajili ya amani na ujirani mwema, japo labda hatuipendi.

Kwa hivyo basi, katika suala la vita kati ya Urusi na Ukraine, madai ya Putin kwamba Ukraine inawaonea watu wenye asili ya Urusi ndani ya Ukraine kwa hiyo wanavamia Ukraine kuwakomboa watu wenye asili ya Urusi, ni ujinga uliopita kikomo na usiopaswa kukubalika na kiongozi yeyeote mwenye akili timamu. Ni sawa na sisi Tanzania, leo hii tuwaambie Wakenya kwamba maeneo ya Kajiado wanayoishi Masai wa Kenya yako nyuma kimaendeleo kwa hiyo tutaingia Kenya kuchukua maeneo haya kwa kuwa Wamasai wa huko ni sehemu ya Wamasai wa Tanzania na wanapaswa kufikiriwa na kuendelezwa kama sehemu nyingine za Kenya, halafu tuivamie Kenya kijeshi. Unaona ujinga huo?

Sasa hapo ndipo Africa Union ilipaswa isimamie bila woga na kujali maslahi. Kina Malema kule South Africa wanasema tutam-support Putin na Warusi katika huu mgogoro kwa kuwa Urusi ilituunga mkono kwenye freedom strugle. Stupid stinking thinking! Kumbuka Nyerere alichosema pia, hatukuwaunga mkono ANC kwa sababu ni weusi kama sisi, bali kwa sababu walikuwa wanabaguliwa na hatupendi ubaguzi wa rangi kwa kuwa unakiuka haki za binadamu.

Sasa Nyerere alimaanisha nini? Kwamba itakuwa ujinga sana kwa Raisi wa Tanzania, siku ANC, chama cha weusi wengi kule South Africa, wakianza kunyanyasa wazungu na kuwabagua, Tanzania kuendelea kuwaunga mkono kwa sababu tu ANC ni chama cha weusi wenzetu. Ikiwa wazungu hao Afrika Kusini leo hii wakibaguliwa na haki zao za kibinadamu kukiukwa na ANC na watu weusi wa South Afrika, na wazungu hao wakaanzisha mapambano ya kujikomboa, itabidi Tanzania tuwa-support na kuwapa kambi zote hapa nchini zilizokuwa za ANC kuwa kambi zao za kupigania uaswa nchini Afrika Kusini.

Kumbuka pia, kwa nini Nyerere aliunga mkono Biafra kule Nigeria, japo tulikuwa marafiki wa serikali ya Nigeria? Kwa nini Nyerere alivunja uhusiano na Uingereza, Israel na Ujerumani wakati fulani licha ya misaada mikubwa tuliyokuwa tunapata toka kwao? NI suala la principles, sio maslahi ya nchi au urafiki. Haya ndio mambo yalifanya Nyerere aheshimike sana duniani. Rational and fairness principles.

Leo hii jirani yako anakupa lift kwenda kazini, siku akishutumiwa kuwafanyia unajisi watoto, utamtetea au kukaa kimya kwa sababu amekuwa akikupa msaada? Labda wewe kama una tatizo la mtindio wa ubongo.

Sasa hawa viongozi wetu hapa Afrika, kama wangejua jinsi ya kusimamia principles badala ya maslahi, hili suala la Urusi na Ukraine is a no brainer matter - wangetoa tamko la kumlaani Putin. Huwezi kusema mbona Marekani walivamia sijui Iraq, Libya nk. Utakuwa unatukumbusha tu jinsi usivyo na msimamo kwa sababu wakati Marekani wakivamia Iraq na Libya ulipaswa kulaani kwa nguvu zote pia. Na two wrongs do not make a right. So African leaders, stop your nonsensical approach to the Russia-Ukraine debacle. You are just proving what Trump is always accusing us of - something about shit hole countries!
Uliyoyasema ni 100% true. Kwa sasa Africa imekosa uongpzi thabiti.

Mandela aliwahi kutamka kuwa kama ubaguzi wa makaburu dhidi ya weusi ulikuwa mbaya, basi hata ubaguzi wa mtu mweusi dhidi ya makaburu hauwezi kuwazuri. Aliyasema hayo baada ya yeye Mandela kuwa Rais, na kuona kuwa kulikuwa na baadhi ya viongozi wenzake waliokuwa wakiona kuwa wakati ule ulikuwa ni wakati wa kulipiza kisasi dhidi ya makaburu.

Ile hoja ya Malema ni ya kijinga kabisa. Ni sawa na kusema, leo hii jirani aje anisaidie kumfukuza mwizi, kesho huyo jirani akaanza kuua ndugu zangu, halafu mimi niseme kuwa mauaji yale aliyoyafanya jirani dhidi ya ndugu zangu siyo kosa kwa sababu eti yule jirani aliwahi kunisaidia kumfukuza mwizi siku nilipovamiwa.

Anachokifanya Putin ni uhayawani kabisa. Mpaka sasa maelfu ya watu, wengi wao wasio na makosa, including watoto wadogo, wanauawa na makombora ya Putin, halafu eti tunasema hatupo upande wowote! Ni ujinga wa hali ya juu.

Kama kweli utawala wa Ukraine unawabagua wananchi wake, wenye asili ya Urusi, kulikuwa na njia za busara zaidi za kuwasaidia wanaodhulumiwa. Lakini hizo zote ni hadithi za Putin katika kuhalalisha uvamizi. Amekuwa anatafuta kila njia kupanua mipaka ya Russia kwa kumega maeneo ya mataifa ambayo zamani yalikuwa kwenye mwungano wa USSR na sasa yamejiunga na EEC. Amekuwa anavipatia silaha na fedha vikundi vinavyopinga serikali zao katika mataifa hayo. Mataifa hayo yakichukua hatua dhidi ya hivyo vikundi, anasema eti vinabaguliwa na kutendewa unyama.

Putin, kwa sasa, ni laana ya Duniani. Na yule mtu ni kichaa. Anavyosema anaweza kutumia silaha za nuclear, yule anaweza kufanya.

Zamani nilikuwa namwona Putin kati ya super intelligents wa Dunia, lakini nilipokuwa Brazil, siku moja nilikutana na Warusi 8 among elites of Russia, walichonieleza kuhusiana na Putin nilishangaa sana, na nikaamini yale maneno ya wahenga kuwa kitanda usichokilalia huwezi kujua kunguni wake. Putin ni dikteta na anaiongoza Russia kwa mkono wa chuma.
 
Nawashangaa sana viongozi wetu. Eti wengi wanasema hawataki kuchagua upande kati ya Urusi na Ukraine, hata kwenye mambo ya kura wanajitoa. Huu ni uoga na unafiki usiokubalika kwa viongozi wa nchi za Afrika.

Ndio maana nimesema siku zote Nyerere alikuwa mtu mwenye busara sana, alisimamia principles, sio urafiki au maslahi ya Tanzania

NInaamini kwa dhati katika hili Nyerere angemlaani Putin katika suala la hii vita. Alishasema, kwamba hii mipaka ya nchi zetu, japokuwa mara nyingine hatuipendi, lakini hatutalazimisha ibadilishwe. Kuwekwa kwake kwa sasa ni jambo la kihistoria na acha ibaki hivyo kwa ajili ya amani na ujirani mwema, japo labda hatuipendi.

Kwa hivyo basi, katika suala la vita kati ya Urusi na Ukraine, madai ya Putin kwamba Ukraine inawaonea watu wenye asili ya Urusi ndani ya Ukraine kwa hiyo wanavamia Ukraine kuwakomboa watu wenye asili ya Urusi, ni ujinga uliopita kikomo na usiopaswa kukubalika na kiongozi yeyeote mwenye akili timamu. Ni sawa na sisi Tanzania, leo hii tuwaambie Wakenya kwamba maeneo ya Kajiado wanayoishi Masai wa Kenya yako nyuma kimaendeleo kwa hiyo tutaingia Kenya kuchukua maeneo haya kwa kuwa Wamasai wa huko ni sehemu ya Wamasai wa Tanzania na wanapaswa kufikiriwa na kuendelezwa kama sehemu nyingine za Kenya, halafu tuivamie Kenya kijeshi. Unaona ujinga huo?

Sasa hapo ndipo Africa Union ilipaswa isimamie bila woga na kujali maslahi. Kina Malema kule South Africa wanasema tutam-support Putin na Warusi katika huu mgogoro kwa kuwa Urusi ilituunga mkono kwenye freedom strugle. Stupid stinking thinking! Kumbuka Nyerere alichosema pia, hatukuwaunga mkono ANC kwa sababu ni weusi kama sisi, bali kwa sababu walikuwa wanabaguliwa na hatupendi ubaguzi wa rangi kwa kuwa unakiuka haki za binadamu.

Sasa Nyerere alimaanisha nini? Kwamba itakuwa ujinga sana kwa Raisi wa Tanzania, siku ANC, chama cha weusi wengi kule South Africa, wakianza kunyanyasa wazungu na kuwabagua, Tanzania kuendelea kuwaunga mkono kwa sababu tu ANC ni chama cha weusi wenzetu. Ikiwa wazungu hao Afrika Kusini leo hii wakibaguliwa na haki zao za kibinadamu kukiukwa na ANC na watu weusi wa South Afrika, na wazungu hao wakaanzisha mapambano ya kujikomboa, itabidi Tanzania tuwa-support na kuwapa kambi zote hapa nchini zilizokuwa za ANC kuwa kambi zao za kupigania uaswa nchini Afrika Kusini.

Kumbuka pia, kwa nini Nyerere aliunga mkono Biafra kule Nigeria, japo tulikuwa marafiki wa serikali ya Nigeria? Kwa nini Nyerere alivunja uhusiano na Uingereza, Israel na Ujerumani wakati fulani licha ya misaada mikubwa tuliyokuwa tunapata toka kwao? NI suala la principles, sio maslahi ya nchi au urafiki. Haya ndio mambo yalifanya Nyerere aheshimike sana duniani. Rational and fairness principles.

Leo hii jirani yako anakupa lift kwenda kazini, siku akishutumiwa kuwafanyia unajisi watoto, utamtetea au kukaa kimya kwa sababu amekuwa akikupa msaada? Labda wewe kama una tatizo la mtindio wa ubongo.

Sasa hawa viongozi wetu hapa Afrika, kama wangejua jinsi ya kusimamia principles badala ya maslahi, hili suala la Urusi na Ukraine is a no brainer matter - wangetoa tamko la kumlaani Putin. Huwezi kusema mbona Marekani walivamia sijui Iraq, Libya nk. Utakuwa unatukumbusha tu jinsi usivyo na msimamo kwa sababu wakati Marekani wakivamia Iraq na Libya ulipaswa kulaani kwa nguvu zote pia. Na two wrongs do not make a right. So African leaders, stop your nonsensical approach to the Russia-Ukraine debacle. You are just proving what Trump is always accusing us of - something about shit hole countries!
Putin ni kiongozi mbaya sana katika dunia hii ya utawandazi na information age; ana mawazo ya kizamani sana yaliyopitwa na wakati. Lakini ngoja waje warusi wa Manzese wakujibu.

Ni kosa kubwa sana kwa nchi kuwa na kiongozi mmoja kwa muda mrefu sana ambaye madaraka yake hayana kikomo. Akifanya maamuzi ya hovyo yanakuwa ni maamuzi ya nchi yote na hakuna wa kuyakemea.
 
Uliyoyasema ni 100% true. Kwa sasa Africa imekosa uongpzi thabiti.

Zamani nilikuwa namwona Putin kati ya super intelligents wa Dunia, lakini nilipokuwa Brazil, siku moja nilikutana na Warusi 8 among elites of Russia, walichonieleza kuhusiana na Putin nilishangaa sana, na nikaamini yale maneno ya wahenga kuwa kitanda usichokilalia huwezi kujua kunguni wake. Putin ni dikteta na anaiongoza Russia kwa mkono wa chuma.
Thank you! Kumbe tupo watu ambao tunaishi kwa principles na ukweli japo hatuonekani. Kuna wakati nashindwa kabisa kuwaelewa hawa watu wanaojiita viongozi wangu. Viongozi wangu wa kuniongoza kwenye nini hasa, huu upuuzi unaofanyika?
 
Putin ni kiongozi mbaya sana katika dunia hii ya utawandazi na information age; ana mawazo ya kizamani sana yaliyopitwa na wakati. Lakini ngoja waje warusi wa Manzese wakujibu.

Ni kosa kubwa sana kwa nchi kuwa na kiongozi mmoja kwa muda mrefu sana ambaye madaraka yake hayana kikomo. Akifanya maamuzi ya hovyo yanakuwa ni maamuzi ya nchi yote na hakuna wa kuyakemea.
Yaani inafaa kuwa na njia fulani ya kumwondoa huyu mtu badala ya dunia nzima kuumia kwa ajili ya mawazo yake ya enzi za kina Hitler na Musolini! Eti anatamani Urusi ya zamani yenye nguvu. Move with times man, hata Uingereza inatamani enzi zake ikiwa dola inayotawala karibu dunia nzima, lakini hatuoni wakienda kuvamia makoloni yao ya zamani
 
Nawashangaa sana viongozi wetu. Eti wengi wanasema hawataki kuchagua upande kati ya Urusi na Ukraine, hata kwenye mambo ya kura wanajitoa. Huu ni uoga na unafiki usiokubalika kwa viongozi wa nchi za Afrika.

Ndio maana nimesema siku zote Nyerere alikuwa mtu mwenye busara sana, alisimamia principles, sio urafiki au maslahi ya Tanzania

NInaamini kwa dhati katika hili Nyerere angemlaani Putin katika suala la hii vita. Alishasema, kwamba hii mipaka ya nchi zetu, japokuwa mara nyingine hatuipendi, lakini hatutalazimisha ibadilishwe. Kuwekwa kwake kwa sasa ni jambo la kihistoria na acha ibaki hivyo kwa ajili ya amani na ujirani mwema, japo labda hatuipendi.

Kwa hivyo basi, katika suala la vita kati ya Urusi na Ukraine, madai ya Putin kwamba Ukraine inawaonea watu wenye asili ya Urusi ndani ya Ukraine kwa hiyo wanavamia Ukraine kuwakomboa watu wenye asili ya Urusi, ni ujinga uliopita kikomo na usiopaswa kukubalika na kiongozi yeyeote mwenye akili timamu. Ni sawa na sisi Tanzania, leo hii tuwaambie Wakenya kwamba maeneo ya Kajiado wanayoishi Masai wa Kenya yako nyuma kimaendeleo kwa hiyo tutaingia Kenya kuchukua maeneo haya kwa kuwa Wamasai wa huko ni sehemu ya Wamasai wa Tanzania na wanapaswa kufikiriwa na kuendelezwa kama sehemu nyingine za Kenya, halafu tuivamie Kenya kijeshi. Unaona ujinga huo?

Sasa hapo ndipo Africa Union ilipaswa isimamie bila woga na kujali maslahi. Kina Malema kule South Africa wanasema tutam-support Putin na Warusi katika huu mgogoro kwa kuwa Urusi ilituunga mkono kwenye freedom strugle. Stupid stinking thinking! Kumbuka Nyerere alichosema pia, hatukuwaunga mkono ANC kwa sababu ni weusi kama sisi, bali kwa sababu walikuwa wanabaguliwa na hatupendi ubaguzi wa rangi kwa kuwa unakiuka haki za binadamu.

Sasa Nyerere alimaanisha nini? Kwamba itakuwa ujinga sana kwa Raisi wa Tanzania, siku ANC, chama cha weusi wengi kule South Africa, wakianza kunyanyasa wazungu na kuwabagua, Tanzania kuendelea kuwaunga mkono kwa sababu tu ANC ni chama cha weusi wenzetu. Ikiwa wazungu hao Afrika Kusini leo hii wakibaguliwa na haki zao za kibinadamu kukiukwa na ANC na watu weusi wa South Afrika, na wazungu hao wakaanzisha mapambano ya kujikomboa, itabidi Tanzania tuwa-support na kuwapa kambi zote hapa nchini zilizokuwa za ANC kuwa kambi zao za kupigania uaswa nchini Afrika Kusini.

Kumbuka pia, kwa nini Nyerere aliunga mkono Biafra kule Nigeria, japo tulikuwa marafiki wa serikali ya Nigeria? Kwa nini Nyerere alivunja uhusiano na Uingereza, Israel na Ujerumani wakati fulani licha ya misaada mikubwa tuliyokuwa tunapata toka kwao? NI suala la principles, sio maslahi ya nchi au urafiki. Haya ndio mambo yalifanya Nyerere aheshimike sana duniani. Rational and fairness principles.

Leo hii jirani yako anakupa lift kwenda kazini, siku akishutumiwa kuwafanyia unajisi watoto, utamtetea au kukaa kimya kwa sababu amekuwa akikupa msaada? Labda wewe kama una tatizo la mtindio wa ubongo.

Sasa hawa viongozi wetu hapa Afrika, kama wangejua jinsi ya kusimamia principles badala ya maslahi, hili suala la Urusi na Ukraine is a no brainer matter - wangetoa tamko la kumlaani Putin. Huwezi kusema mbona Marekani walivamia sijui Iraq, Libya nk. Utakuwa unatukumbusha tu jinsi usivyo na msimamo kwa sababu wakati Marekani wakivamia Iraq na Libya ulipaswa kulaani kwa nguvu zote pia. Na two wrongs do not make a right. So African leaders, stop your nonsensical approach to the Russia-Ukraine debacle. You are just proving what Trump is always accusing us of - something about shit hole countries!
Refu limejaa ujinga mtupu
 
Baada ya AU kulaani itanufaika na nini?!
Labda ngano na alizeti za Ukraine na Russia.
Otherwise kama ulivyosema kitanda usicholalia huwezi kujua ukali wa kunguni wake.
Binafsi naamini hao wanaopigana ndio wanaujua utamu na ukali wa hao kunguni, USA hakuamka tu asubuhi akaenda Libya the same as Russia huko Ukraine.
Nyerere toka zamani ni mtu asiyefungamana ma upande wowote pale UN. Principles zipo kwa ajili ya “jambo” ambalo ni maslahi otherwise hakuna maana nyingine ya principle kwenye diplomatic relations
Mawazo yangu.
 
Baada ya AU kulaani itanufaika na nini?!
Labda ngano na alizeti za Ukraine na Russia.
Mkuu, tunarudi pale pale ninapopakemea - tutanufaika na nini?! Yaani kukemea ufashisti na kusemea amani ili kuzuia watu wasifanye ufashisti sio jambo kuu, bali tutanufaika na nini? Tulipowasaidia South Afrika, Msumbiji, Zimbabwe nk, tulinufaika na nini? Tulipolaani mauaji ya Soweto na kuifanya 16/6/1976 siku maalum ya kukumbukwa hata shule hakuna masomo bali maandamano, tulinufaika na nini? Uko tayari kuwa mtumwa wa mtu ili mradi unanufaika na jambo fulani? Watoto wa kizazi hiki, nyie coach potatoes wa NIntendo na PlayStation mna shida sana. Ndio maana mnalazimishwa kuwa mashoga, na mnakubali ili tu mnufaike na kitu.
 
Mkuu, tunarudi pale pale ninapopakemea - tutanufaika na nini?! Yaani kukemea ufashisti na kusemea amani ili kuzuia watu wasifanye ufashisti sio jambo kuu, bali tutanufaika na nini? Tulipowasaidia South Afrika, Msumbiji, Zimbabwe nk, tulinufaika na nini? Tulipolaani mauaji ya Soweto na kuifanya 16/6/1976 siku maalum ya kukumbukwa hata shule hakuna masomo bali maandamano, tulinufaika na nini? Uko tayari kuwa mtumwa wa mtu ili mradi unanufaika na jambo fulani? Watoto wa kizazi hiki, nyie coach potatoes wa NIntendo na PlayStation mna shida sana. Ndio maana mnalazimishwa kuwa mashoga, na mnakubali ili tu mnufaike na kitu.
Umeenda na hoja bahati mbaya mwishoni umemalizia na vioja.
Nasikitika kukwambia si kila anayeku-challenge mawazo yako ni “watoto wa kizazi hiki” kwa sababu hujui umri wangu na ni tabia ya kama usemavyo ya kifashisti kupenda kutosikia yale ambayo hatajawa programmed kwenye mindset yako.
Hizo zama za kukemea na mambo kama hayo yawekwe kwenye national museums. Sasa hivi unakemea na kemeo lako liwe na manufaa kwako ndivyo dunia ilipo

Leo vijana wetu wanakufa DRC kwa ajili ya peace mission ila deep down wananufaika na nini na damu yao inalipikaje?!
 
Kama Putin ana tatizo na ukosefu wa haki za binadamu kwa wananchi wa Ukraine walio na asili ya Urusi, anapaswa kulipeleka hili jambo Security Council ili hatua zichukuliwe dhidi yao na ICC, kama tulivyofanya nchi nyingine, na vikwazo viwe kwa viongozi wa Ukraine badala ya Urusi. Sio kutumia hiyo kama sababu ya kuvamia na kutaifisha sehemu ya nchi nyingine. Huo ni uendawazimu na viongozi wa Afrika wanapaswa kuliona hilo na kulisema
 
Umeenda na hoja bahati mbaya mwishoni umemalizia na vioja.
Nasikitika kukwambia si kila anayeku-challenge mawazo yako ni “watoto wa kizazi hiki” kwa sababu hujui umri wangu na ni tabia ya kama usemavyo ya kifashisti kupenda kutosikia yale ambayo hatajawa programmed kwenye mindset yako.
Hizo zama za kukemea na mambo kama hayo yawekwe kwenye national museums. Sasa hivi unakemea na kemeo lako liwe na manufaa kwako ndivyo dunia ilipo

Leo vijana wetu wanakufa DRC kwa ajili ya peace mission ila deep down wananufaika na nini na damu yao inalipikaje?!
Mkuu, kuna kitu kinaitwa profiling a person from what he says or does. Umesikia hilo? Basi mie hapo nili-kuprofile nikaona picha ya mtu wa miaka ya 2000s kwa kuzaliwa, kina Y2K
 
Naunga mkono hoja hii, kipindi cha president Nyerere (rip),Africa yote ilikua inasubiria tamko kutoka Dar es Salaam ili nao watoe msimamo wao, eti leo tumekua laughing stock hata Rwanda 🇷🇼 inatutingisha,Mr.Malema ni mnafiki na mwongo mkubwa, anapayuka na end of the day anasomesha binti yake kwenye white dominates school na yeye mwenyewe anaishi kwenye hizi security complex za white people's, why asiishi kwenye township yake pale seshogo?,anajua within a week atakula chuma!
Yaani, imebidi nicheke. Mkuu utakuwa Bondeni wewe. Msalimie Malema ukimwona/ Muulize vipi tenda, zipo tuje kuupiga? Tuna majenereta huku hayauziki, nasikia Bondeni kuna mgao wa umeme huku kwetu nafuu!
 
Viongozi wengi wa Africa wana tabia za Putin, sio rahisi walaani udhalimu. Inashangaza Kagame kuulani uvamizi wake na inasikitisha kuona Africa haina msimamo thabiti dhidi ya uovu kama huu wa Putin.
Nawashangaa sana viongozi wetu. Eti wengi wanasema hawataki kuchagua upande kati ya Urusi na Ukraine, hata kwenye mambo ya kura wanajitoa. Huu ni uoga na unafiki usiokubalika kwa viongozi wa nchi za Afrika.

Ndio maana nimesema siku zote Nyerere alikuwa mtu mwenye busara sana, alisimamia principles, sio urafiki au maslahi ya Tanzania

NInaamini kwa dhati katika hili Nyerere angemlaani Putin katika suala la hii vita. Alishasema, kwamba hii mipaka ya nchi zetu, japokuwa mara nyingine hatuipendi, lakini hatutalazimisha ibadilishwe. Kuwekwa kwake kwa sasa ni jambo la kihistoria na acha ibaki hivyo kwa ajili ya amani na ujirani mwema, japo labda hatuipendi.

Kwa hivyo basi, katika suala la vita kati ya Urusi na Ukraine, madai ya Putin kwamba Ukraine inawaonea watu wenye asili ya Urusi ndani ya Ukraine kwa hiyo wanavamia Ukraine kuwakomboa watu wenye asili ya Urusi, ni ujinga uliopita kikomo na usiopaswa kukubalika na kiongozi yeyeote mwenye akili timamu. Ni sawa na sisi Tanzania, leo hii tuwaambie Wakenya kwamba maeneo ya Kajiado wanayoishi Masai wa Kenya yako nyuma kimaendeleo kwa hiyo tutaingia Kenya kuchukua maeneo haya kwa kuwa Wamasai wa huko ni sehemu ya Wamasai wa Tanzania na wanapaswa kufikiriwa na kuendelezwa kama sehemu nyingine za Kenya, halafu tuivamie Kenya kijeshi. Unaona ujinga huo?

Sasa hapo ndipo Africa Union ilipaswa isimamie bila woga na kujali maslahi. Kina Malema kule South Africa wanasema tutam-support Putin na Warusi katika huu mgogoro kwa kuwa Urusi ilituunga mkono kwenye freedom strugle. Stupid stinking thinking! Kumbuka Nyerere alichosema pia, hatukuwaunga mkono ANC kwa sababu ni weusi kama sisi, bali kwa sababu walikuwa wanabaguliwa na hatupendi ubaguzi wa rangi kwa kuwa unakiuka haki za binadamu.

Sasa Nyerere alimaanisha nini? Kwamba itakuwa ujinga sana kwa Raisi wa Tanzania, siku ANC, chama cha weusi wengi kule South Africa, wakianza kunyanyasa wazungu na kuwabagua, Tanzania kuendelea kuwaunga mkono kwa sababu tu ANC ni chama cha weusi wenzetu. Ikiwa wazungu hao Afrika Kusini leo hii wakibaguliwa na haki zao za kibinadamu kukiukwa na ANC na watu weusi wa South Afrika, na wazungu hao wakaanzisha mapambano ya kujikomboa, itabidi Tanzania tuwa-support na kuwapa kambi zote hapa nchini zilizokuwa za ANC kuwa kambi zao za kupigania uaswa nchini Afrika Kusini.

Kumbuka pia, kwa nini Nyerere aliunga mkono Biafra kule Nigeria, japo tulikuwa marafiki wa serikali ya Nigeria? Kwa nini Nyerere alivunja uhusiano na Uingereza, Israel na Ujerumani wakati fulani licha ya misaada mikubwa tuliyokuwa tunapata toka kwao? NI suala la principles, sio maslahi ya nchi au urafiki. Haya ndio mambo yalifanya Nyerere aheshimike sana duniani. Rational and fairness principles.

Leo hii jirani yako anakupa lift kwenda kazini, siku akishutumiwa kuwafanyia unajisi watoto, utamtetea au kukaa kimya kwa sababu amekuwa akikupa msaada? Labda wewe kama una tatizo la mtindio wa ubongo.

Sasa hawa viongozi wetu hapa Afrika, kama wangejua jinsi ya kusimamia principles badala ya maslahi, hili suala la Urusi na Ukraine is a no brainer matter - wangetoa tamko la kumlaani Putin. Huwezi kusema mbona Marekani walivamia sijui Iraq, Libya nk. Utakuwa unatukumbusha tu jinsi usivyo na msimamo kwa sababu wakati Marekani wakivamia Iraq na Libya ulipaswa kulaani kwa nguvu zote pia. Na two wrongs do not make a right. So African leaders, stop your nonsensical approach to the Russia-Ukraine debacle. You are just proving what Trump is always accusing us of - something about shit hole countries!
 
Viongozi wengi wa Africa wana tabia za Putin, sio rahisi walaani udhalimu. Inashangaza Kagame kuulani uvamizi wake na inasikitisha kuona Africa haina msimamo thabiti dhidi ya uovu kama huu wa Putin.
Kagame yuko makini sana, ndio maana alikubali uraia pacha wkati sisi bado tunadunga embe:D:D:D
 
Yaani, imebidi nicheke. Mkuu utakuwa Bondeni wewe. Msalimie Malema ukimwona/ Muulize vipi tenda, zipo tuje kuupiga? Tuna majenereta huku hayauziki, nasikia Bondeni kuna mgao wa umeme huku kwetu nafuu!
Hapana mkuu mimi nipo lingusenguse, Ruvuma ila ninasoma sana latest information za bara letu la Africa, yes Malema ni mwizi na mwanasiasa mbabaishaji tu,President H&H of Zambia ndio shining star ya sasa ,1ZWK =145TSHS,Ghana cedi yao inazidi kuporomoka against usd, it's only productivity, reform na max export tunayatakiwa kuyafanya nchi yetu ili nasi tununue diesel kwa 15BWP,just imagine unaenda Oil com na kutumia 15TSH kupata 1L of Diesel!sio 3300.00tshs
 
Hapana mkuu mimi nipo lingusenguse, Ruvuma ila ninasoma sana latest information za bara letu la Africa, yes Malema ni mwizi na mwanasiasa mbabaishaji tu,President H&H of Zambia ndio shining star ya sasa ,1ZWK =145TSHS,Ghana cedi yao inazidi kuporomoka against usd, it's only productivity, reform na max export tunayatakiwa kuyafanya nchi yetu ili nasi tununue diesel kwa 15BWP,just imagine unaenda Oil com na kutumia 15TSH kupata 1L of Diesel!sio 3300.00tshs
Unajua kinachosikitisha sana ni nini? Unaweza kusikia Malema kachaguliwa kuwa Raisi wa Bondeni. Unaona signature yangu hapo chini? Ndio maana siku nyingi sana nimesema hili wazi; Changamoto kubwa sana inayoyakabili mataifa masikini duniani na kufanya washindwe kuendelea ni nyingi ya akili ndogo kupewa mamlaka makubwa, kwa njia ya kura au kuteuliwa.
 
Back
Top Bottom