sady kimwana
Member
- Feb 6, 2024
- 28
- 103
Msanii aliyetamba na ngoma ya Imekaa vibaya na Tumbo joto , Abdul Miraj maarufu kama Kali P amesema hataki tena kusikia masuala ya Muziki .
Kali P amesema ameamua Kumrudia Muumba wake na sasa hive ana takribani miaka 12 ameingia katika dini na ameachana na maswala ya Muziki.
"katika dini yetu ya Uislamu muziki ni haramu ndio maana mimi nikajitoa kwa sababu ya kumuogopa Mungu, Kama Ujumbe kuna njia watu kuwafikishia ila sio Mziki, siku ambayo niliacha mziki nafsi yangu ilisema sipendi tena Mziki. Kipindi nafanya Muziki nilikuwa na miaka 22, nyimbo zangu zikipigwa najisikia vibaya sana na sina habari nazo tena, atakayeimba atakuwa anajichochea moto mwenyewe" Alisema Kali P
kali P kwa sasa anafahamika kama Sheikh Abdul Miraj na anapatikana maeneo ya Kitunda.