20 Kali za Judith Mbibo Lameck Wambura

mocoservices

Member
Feb 24, 2023
45
144
20 KALI ZA JUDITH MBIBO LAMECK WAMBURA
LADY JAY DEE, KOMANDO, MAMA SOME FOOD, JIDE, ANACONDA
THE BONGO FLAVOUR FIRST LADY

1. Amechanganya damu kutoka mikoa miwili; Shinyanga na Mara, wilayani Bunda. Na ni dada wa mwanamuziki mwingine aitwaye DABO MTANZANIA.

2. Alianza kama rapa, akageukia utangazaji wa redio, lakini alijitafuta zaidi na kuona anatosha kuwa MWIMBAJI.

3. Ni msabato na kama walivyo wasanii wengi, alianzia kuimba kanisani na hivi karibuni kuna video moja imetembea mtandaoni ikimwonesha akiwa kanisani anaimba na kwaya.

4. TOFAUTI na ilivyokuwa imekaririwa kuwa ili uwe MSANII mkali, lazima uingie Bongo Records na kurekodiwa na P FUNK. Jide, alikuwa kwenye mikono ya Master Jay na ameingia Bongo Recs kufanya chorus ya KADI NA UA ROSE ya Fid Q, NIMEAMINI ya Prof Jay na kufanya "chorus ya mtoto wa P" ajiitaye Rapcha kwenye ngoma iitwayo AMEN. Kwenye hili anaungana na MR BLUE, MR NICE, na SAIDA KALORI, wasanii waliotamba kwa NYAKATI TOFAUTI kwa kipindi kile na kuishika Bongo bila MIDUNDO ya BAMAGA.

5. Jide ni miongoni mwa wasanii wa awali kumiliki studio yake mwenyewe iliyoitwa JAG RECORDS huku mipini ya hapo ikisukwa na mtaalam HERBALIST.
LAWAMA - CHID BENZ FT MATONYA
NISHIKE MKONO - K LYNN FT BLUE
Ni miongoni mwa ngoma zilizosukwa na HERBALIST lakini pia ngoma kadhaa za Ismail wa WASHKAJI au SOUL n FAITH.

6. Alikiri mara kadhaa kuwa asingekuwa mwanamuziki, angekuwa mtu wa mapishi. Kuthibitisha hili akafungua NYUMBANI LOUNGE, AMBAYO Pengine imekuja KUZALISHA mawazo mapya kama SHISHI FOOD.

7. Amewahi kumiliki kiwanda cha maji ya kunywa lakini kikapigwa pini kabla ya uzinduzi rasmi. Na hii ilikuwa way back before TANZANIA YA VIWANDA au GARI LA MASOUD KIPANYA. JIDE IS ALWAYS AHEAD OF TIME.

8. Jide amewahi kuwa na kipindi kinachoangazia maisha yake ya kila siku, JIDE REALITY SHOW, hapa akaungana na CHID BENZ na WEMA SEPETU, ambao wamewahi kufanya vipindi vyao pia kwa NYAKATI TOFAUTI.

9. Jide ni mmiliki wa tuzo za Kili, tuzo TOFAUTI za Afrika Mashariki ikiwemo KISIMA lakini pia ukienda bondeni, Kuna jina lake kwenye zilizokuwa tuzo kubwa sana kwa kipindi kile, KORA AWARDS.

10. Jide anamiliki Kolabo nzito na majina makubwa kwenye muziki;
Muziki ft Samba Mapangala
I am ft Oliva Mtukudzi
Sirimba - Ngoni
Kiboko yao - ft Chameleone
Nimpate wapi - Longombaz
Kwa Bongo hapa, wasanii wote wakubwa wamefanya kazi na Jide, ukimtoa AFANDE SELE, SOLO, MOE na DIAMOND.

11. Jide amesafiri mara kadhaa kwenda nchi tofauti kujifunza lugha za mataifa mengine ikiwemo Kifaransa.

12. Anamiliki albums nyingi lakini album ninayoipenda kuliko zote ni SHUKRANI. Album AMBAYO alisema aliitoa kwa ajili ya kuwashukuru MASHABIKI zake, ambao mimi ni miongoni mwao. Hapa anaungana na Sugu, Mr Ebbo, na Wakazi ambaye yeye, ametoa zaidi mixtapes.

13. Ni miongoni mwa wasanii wa awali kabisa kumiliki bendi, MACHOZI BAND, ambayo ilikuwa inafanya shows zake palepale kwake Nyumbani lounge, hivyo, nyimbo za Jide zikampa hela na kuimbwa live na bendi yake lakini pia akapata pesa kwa kuuza msosi palepale kwake.

14. Ni miongoni mwa wasanii wengi walioingia kwenye mtafaruku mzito na 'klaudzi' mpaka bosi wao akatangaza kuwa siku ile iliyokuwa climax ya ugomvi wao USIPIGWE WIMBO WOWOTE WA BONGO FLEVA. HAPO NIKAAMINI JIDE IS BIGGER THAN BONGO FLEVA. IF IT IS SAFE, I MAY SAY, JIDE IS THE BONGO FLEVA ITSELF.

WAKATI "WANAUME" WALIPIGISHWA MAGOTI, JIDE HAKUSANDA NA BADO YUKO PALE WAKATI ILIAMINIKA UKIGOMBANA NA JAMAA UNAPOTEA MAZIMA.

15. Amekuwa akiandaa maonesho yake mwenyewe na kutomlalamikia mtu kwa kutomwita kwenye maonesho yao. Viingilio huwa ni 20,000 mpaka 100k na bado watu wanaingia.

16. Wakati inaaminika wanawake hawapendani kwenye muziki, Jide ameshafanya Kolabo na Ray C, Mwasiti, Karen, Atemi, lakini pia amewaalika watoto wa kike kibao kwenye shows zake na amewahi kufanya joint show na ZAHRA aliyetamba na kibao chake cha DESTINY.

17. Zililetwa COPIES nyingi kwenye game na zikaonekana kufunika original versions. Nani hakumbuki kuwa BARNABA ni carbon copy ya BUIBUI,
nani hajui kuwa Z ANTO aliletwa kumpoteza MB DOGGY, umewasikiliza vizuri VUMILIA na MWASITI, achana na Hawa akina ZILLA na BILNASS au RUBY na NANDY. Hebu niambie nani amewahi kumbite JIDE na akatoka salama?? Huamini, rudi kaisikilize ZAMANI ya Q CHIEF ft JIDE halafu sikiliza ZAMANI RMX ya BARNABA, LINAH na Q CHILA, uone namna LINAH SANGA alivyoelea kwenye vesi ya JIDE.

18. Jide amefanya mitindo yote kuanzia rap, RnB, Zouk, Mduara, Reggae, Dansi, Qaito mpaka Afro pop.

19. Jide amefanya official covers kali na nyingine zimekuwa kali kuliko hata original versions
Siwema - Marijani Rajab
Muhogo wa jang'ombe - Bi Kidude
Nimekusamehe - Hamza Kalala
Na nyinginezo.

20. Amesimangwa na magazeti na waja wengi kuwa hazai lakini amekuwa akitumia msemo wa SUGU kwenye HAYAKUWA MAPENZI, "WANGAPI WAMEZAA WATOTO NA BADO WAKAWA MATEJA"

KUNA MUDA NAJIONA KAMA MTOTO WA JIDE HIVI NA SIYO KAMA MTOTO WAKE ILA KAMA FIRST BORN WAKE KABISA, HIVYO MSISEME TENA KUWA HANA MTOTO.

MIMI NI SHABIKI NAMBA MOJA WA JIDE, HATA AKIACHA KUIMBA.

MADA GANI HAJAIIMBIA, ALBUM GANI ILIFLOP? WIMBO GANI KAIMBA CHINI YA KIWANGO??

Nimemwona mara mbili tu katika maisha yangu, mara ya kwanza alikuwa kwenye gari yake maeneo ya CCBRT na mara ya pili nimemwona akiwa na GARDNER G HABASH pande za MLIMANI CITY walipoenda kufanya shopping kwa ajili ya show kipindi kile Cha JOTO HASIRA.

UKINIULIZA MTU MMOJA AMBAYE NINATAMANI KUONANA NAYE NA KUPATA WALAU DAKIKA KUMI TU ZA KUONGEA NAYE, DUNIA NZIMA, MY ANSWER IS LADY JAY DEE, THE TRUE AND ONLY DEFINITE DEFINITION OF BONGO FLEVA.

JIDE, I LOVE YOU, MOM!!!

HILI SIYO ANDIKO KAMA MENGINE, HII NI BARUA YANGU YA WAZI KWA JUDITH.

MUZIKI WAKE UMENILEA, ITIKADI ZAKE ZIMENIKOMAZA NA FALSAFA ZAKE ZIMENIFIKISHA NILIPO.

SISUBIRI MPAKA AFE NIKUBALI SHE IS THE BEST.

MWANDISHI WA AINA YAKE.
LUAH.
 
20 KALI ZA JUDITH MBIBO LAMECK WAMBURA
LADY JAY DEE, KOMANDO, MAMA SOME FOOD, JIDE, ANACONDA
THE BONGO FLAVOUR FIRST LADY

1. Amechanganya damu kutoka mikoa miwili; Shinyanga na Mara, wilayani Bunda. Na ni dada wa mwanamuziki mwingine aitwaye DABO MTANZANIA.

2. Alianza kama rapa, akageukia utangazaji wa redio, lakini alijitafuta zaidi na kuona anatosha kuwa MWIMBAJI.

3. Ni msabato na kama walivyo wasanii wengi, alianzia kuimba kanisani na hivi karibuni kuna video moja imetembea mtandaoni ikimwonesha akiwa kanisani anaimba na kwaya.

4. TOFAUTI na ilivyokuwa imekaririwa kuwa ili uwe MSANII mkali, lazima uingie Bongo Records na kurekodiwa na P FUNK. Jide, alikuwa kwenye mikono ya Master Jay na ameingia Bongo Recs kufanya chorus ya KADI NA UA ROSE ya Fid Q, NIMEAMINI ya Prof Jay na kufanya "chorus ya mtoto wa P" ajiitaye Rapcha kwenye ngoma iitwayo AMEN. Kwenye hili anaungana na MR BLUE, MR NICE, na SAIDA KALORI, wasanii waliotamba kwa NYAKATI TOFAUTI kwa kipindi kile na kuishika Bongo bila MIDUNDO ya BAMAGA.

5. Jide ni miongoni mwa wasanii wa awali kumiliki studio yake mwenyewe iliyoitwa JAG RECORDS huku mipini ya hapo ikisukwa na mtaalam HERBALIST.
LAWAMA - CHID BENZ FT MATONYA
NISHIKE MKONO - K LYNN FT BLUE
Ni miongoni mwa ngoma zilizosukwa na HERBALIST lakini pia ngoma kadhaa za Ismail wa WASHKAJI au SOUL n FAITH.

6. Alikiri mara kadhaa kuwa asingekuwa mwanamuziki, angekuwa mtu wa mapishi. Kuthibitisha hili akafungua NYUMBANI LOUNGE, AMBAYO Pengine imekuja KUZALISHA mawazo mapya kama SHISHI FOOD.

7. Amewahi kumiliki kiwanda cha maji ya kunywa lakini kikapigwa pini kabla ya uzinduzi rasmi. Na hii ilikuwa way back before TANZANIA YA VIWANDA au GARI LA MASOUD KIPANYA. JIDE IS ALWAYS AHEAD OF TIME.

8. Jide amewahi kuwa na kipindi kinachoangazia maisha yake ya kila siku, JIDE REALITY SHOW, hapa akaungana na CHID BENZ na WEMA SEPETU, ambao wamewahi kufanya vipindi vyao pia kwa NYAKATI TOFAUTI.

9. Jide ni mmiliki wa tuzo za Kili, tuzo TOFAUTI za Afrika Mashariki ikiwemo KISIMA lakini pia ukienda bondeni, Kuna jina lake kwenye zilizokuwa tuzo kubwa sana kwa kipindi kile, KORA AWARDS.

10. Jide anamiliki Kolabo nzito na majina makubwa kwenye muziki;
Muziki ft Samba Mapangala
I am ft Oliva Mtukudzi
Sirimba - Ngoni
Kiboko yao - ft Chameleone
Nimpate wapi - Longombaz
Kwa Bongo hapa, wasanii wote wakubwa wamefanya kazi na Jide, ukimtoa AFANDE SELE, SOLO, MOE na DIAMOND.

11. Jide amesafiri mara kadhaa kwenda nchi tofauti kujifunza lugha za mataifa mengine ikiwemo Kifaransa.

12. Anamiliki albums nyingi lakini album ninayoipenda kuliko zote ni SHUKRANI. Album AMBAYO alisema aliitoa kwa ajili ya kuwashukuru MASHABIKI zake, ambao mimi ni miongoni mwao. Hapa anaungana na Sugu, Mr Ebbo, na Wakazi ambaye yeye, ametoa zaidi mixtapes.

13. Ni miongoni mwa wasanii wa awali kabisa kumiliki bendi, MACHOZI BAND, ambayo ilikuwa inafanya shows zake palepale kwake Nyumbani lounge, hivyo, nyimbo za Jide zikampa hela na kuimbwa live na bendi yake lakini pia akapata pesa kwa kuuza msosi palepale kwake.

14. Ni miongoni mwa wasanii wengi walioingia kwenye mtafaruku mzito na 'klaudzi' mpaka bosi wao akatangaza kuwa siku ile iliyokuwa climax ya ugomvi wao USIPIGWE WIMBO WOWOTE WA BONGO FLEVA. HAPO NIKAAMINI JIDE IS BIGGER THAN BONGO FLEVA. IF IT IS SAFE, I MAY SAY, JIDE IS THE BONGO FLEVA ITSELF.

WAKATI "WANAUME" WALIPIGISHWA MAGOTI, JIDE HAKUSANDA NA BADO YUKO PALE WAKATI ILIAMINIKA UKIGOMBANA NA JAMAA UNAPOTEA MAZIMA.

15. Amekuwa akiandaa maonesho yake mwenyewe na kutomlalamikia mtu kwa kutomwita kwenye maonesho yao. Viingilio huwa ni 20,000 mpaka 100k na bado watu wanaingia.

16. Wakati inaaminika wanawake hawapendani kwenye muziki, Jide ameshafanya Kolabo na Ray C, Mwasiti, Karen, Atemi, lakini pia amewaalika watoto wa kike kibao kwenye shows zake na amewahi kufanya joint show na ZAHRA aliyetamba na kibao chake cha DESTINY.

17. Zililetwa COPIES nyingi kwenye game na zikaonekana kufunika original versions. Nani hakumbuki kuwa BARNABA ni carbon copy ya BUIBUI,
nani hajui kuwa Z ANTO aliletwa kumpoteza MB DOGGY, umewasikiliza vizuri VUMILIA na MWASITI, achana na Hawa akina ZILLA na BILNASS au RUBY na NANDY. Hebu niambie nani amewahi kumbite JIDE na akatoka salama?? Huamini, rudi kaisikilize ZAMANI ya Q CHIEF ft JIDE halafu sikiliza ZAMANI RMX ya BARNABA, LINAH na Q CHILA, uone namna LINAH SANGA alivyoelea kwenye vesi ya JIDE.

18. Jide amefanya mitindo yote kuanzia rap, RnB, Zouk, Mduara, Reggae, Dansi, Qaito mpaka Afro pop.

19. Jide amefanya official covers kali na nyingine zimekuwa kali kuliko hata original versions
Siwema - Marijani Rajab
Muhogo wa jang'ombe - Bi Kidude
Nimekusamehe - Hamza Kalala
Na nyinginezo.

20. Amesimangwa na magazeti na waja wengi kuwa hazai lakini amekuwa akitumia msemo wa SUGU kwenye HAYAKUWA MAPENZI, "WANGAPI WAMEZAA WATOTO NA BADO WAKAWA MATEJA"

KUNA MUDA NAJIONA KAMA MTOTO WA JIDE HIVI NA SIYO KAMA MTOTO WAKE ILA KAMA FIRST BORN WAKE KABISA, HIVYO MSISEME TENA KUWA HANA MTOTO.

MIMI NI SHABIKI NAMBA MOJA WA JIDE, HATA AKIACHA KUIMBA.

MADA GANI HAJAIIMBIA, ALBUM GANI ILIFLOP? WIMBO GANI KAIMBA CHINI YA KIWANGO??

Nimemwona mara mbili tu katika maisha yangu, mara ya kwanza alikuwa kwenye gari yake maeneo ya CCBRT na mara ya pili nimemwona akiwa na GARDNER G HABASH pande za MLIMANI CITY walipoenda kufanya shopping kwa ajili ya show kipindi kile Cha JOTO HASIRA.

UKINIULIZA MTU MMOJA AMBAYE NINATAMANI KUONANA NAYE NA KUPATA WALAU DAKIKA KUMI TU ZA KUONGEA NAYE, DUNIA NZIMA, MY ANSWER IS LADY JAY DEE, THE TRUE AND ONLY DEFINITE DEFINITION OF BONGO FLEVA.

JIDE, I LOVE YOU, MOM!!!

HILI SIYO ANDIKO KAMA MENGINE, HII NI BARUA YANGU YA WAZI KWA JUDITH.

MUZIKI WAKE UMENILEA, ITIKADI ZAKE ZIMENIKOMAZA NA FALSAFA ZAKE ZIMENIFIKISHA NILIPO.

SISUBIRI MPAKA AFE NIKUBALI SHE IS THE BEST.

MWANDISHI WA AINA YAKE.
LUAH.
Umeandika vema saaana. Na imani amesoma na mtaonana.
 
Hivi chorus ya wimbo huu unaimbwaje mkuu, maana kuna maneno pale huwa siyasikii vzuri.
What I need from you is understanding (understanding)
Nachotaka toka kwako maelewano (maelewano)
Ugomvi kila siku na maneno (oh no) Nimechoka ah! Nataka maelewano

All I need from you is understanding (understanding... standing)
Kwani kila ifikapo mwisho wa wiki (mmh yeah)
Vitimbi, vitimbi, vitimbi na mikiki
Ndio sababu uuh usitoke na mimi
 
Jide pia alimfukuza Gadina dibashi
Jide pia aliwahi tongozwa na Chid Benz, na kupelekea kukerekwa na kitendo kile alichofanya Benzino,,, na akaenda mbali akamuanika kwa mapaparazi,,, pia akafuta ile verce ya ule wimbo wa UKO JUU na akaacha kufanya kazi na Chid Benz,,,, akawa anafanya na Mr Blue na wakatoa wimbo unaitwa NALIA NA MOYO.

Ila kinachonishangaza kwanini baada ya kufariki Ruge ameamua kuukacha muziki,,,au alikuwa anafanya ili Kumkomoa Marehemu Ruge???
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom