Tlaatlaah
JF-Expert Member
- May 18, 2023
- 45,144
- 36,953
pole gentleman,Tafadhalini sana naombeni msaada wa tiba juu ya nguvu za kiume, umri wangu ni miaka 24 , nimetumia dawa za kisuni na kwa waging ila bado naona tatizo linazidi, kusimamisha tu ni kazi hata asubuhi nikiamka haisimami naombeni sana msaada wenu
huenda una infectious kwenye via vya uzazi au njia ya mkojo. Tafadhali muone daktari kwa msaada wa kina zaidi kuhusu hilo.
Lakini pia huenda una muunganiko wa maradhi mengine yanayotibika kama vile vidonda vya tumbo, malaria au typhoid na mambo ambayo yanaweza kudhoofisha uzalishaji wa vichocheo vya mwili na kukukosesha hisia za kingono na kukufanya kuhisi au kujistukia kua una changamoto ya nguvu za kijinsia kumbe ni maradhi tu ya kawaida mwilini.
Ni muhimu sana pia kucheki sukari na wingi wako wa damu mwilini kwasababu mzungukuo sahihi wa damu ndio hufanya mkunyange au mshedede usimame vizuri, na kwahivyo pakiwepo na changamoto kwenye damu panaweza kupelekea ushindwe kusimamisha mkunyange na kusababisha upate mfadhaiko wa kisaikolojia unaoathiri na kudidimiza msisimuko wa kingono kwa kiasi kikubwa sana.
Kujitibu bila dawa ni pamoja na kuacha kabisa kuangalia video za ngono, kujipa likizo ya walau miezi miwili bila ya kupiga nyetro, kushiriki mazoezi mepesi ya viungo mara kwa mara, kula chakula kizuri cha kutosha, kunywa maji na maziwa ya kutosha mara kwa mara, kula matunda ya kutosha mara kwa mara, kutafuna korosho au karanga kiasi mara kwa mara, kupumzika vya kutosha, kupunguza matumizi ya sukari kwa wingi kwenye chai au uji, kupunguza matumizi ya pombe na sigara kupita kiasi n.k
kwa kufanya hivyo,
utapata nafuu ya taratibu lakini ya uhakika na hatimae kupona kabisa changamoto hiyo ya fedheha unayoipitia ukiwa kwenye umri mdogo mno.
Mungu akujalie afya njema gentleman 🐒