Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Miaka 70! sipo tayari kwa hili. Ngoja niendelee kufanya utaratibu wa kumiliki ardhi kisheria maana hizi projects za muda mrefu ni lazima uwashirikishe watu wa ardhi kikamilifu kabla ya kuanza kupanda miti. Tuliangalie kwa umakini hili swala, watu wengi wamepoteza ardhi kwa kutofuata taratibu za umiliki
Well said mkuu, hivi ule utaratibu wa hati za kimila uliishia wapi? nasikia ilikuwa 20,000 tu, au hauwahusu wanunuzi wa ardhi yaani mpaka uwe umerithi?
 
Asante KVM,

Nichangie kwa kuleta nyongeza za hapa na pale ili kujazia mjadala wetu. Maeneo ya kupanda miti yaliyosahaulika ni Kilolo, Mfindi,Mby vijijini, Makonde plateau.

Tumetaja sana pines, cyprus, teak,eucalyptus, tumesahau acrocarpus kwa ukanda wa baridi na Msederela kwa kanda za joto kiasi.

Hatujazungumzia mbegu, mbegu bora za Pines kwa sasa ni Tatizo sugu.Tangu mwaka jana kituo cha Iringa wameshindwa kuzalisha, kwa hiyo pines/cyprus zinaandaliwa kienyeji na vijana huko vijijini.Kwa sasa pines za uhakika zinapatikana Nairobi, ila bei imesimama.

Mwaka jana tulipata taabu sana ya tubes, ila mwaka huu walau zipo pale TFA Iringa, bei iko juu. Ukiwa na usafiri wako, ni bora kununua Dar ukasafirisha. Dar ni Tsh 5000/ kwa kilo na TFA Iringa ni 6500/ kwa kilo.

Ili kupunguza gharama za kitalu, watika miche mapema, miezi mitano kabla ya msimu wa kupanda haujafika.

Kama unataka ardhi kubwa,Makete usiende, ni kazi ngumu kupata eka 50 za pamoja zinazofikiwa na miundo mbinu. Utapanda milimani ambako utashindwa kuvuna. Na maeneo mazuri yaliyobaki bei iko juu. Ludewa/Wino/Lupembe/Mfindi kusini huko bei poa.Kilolo bei inaanza kupanda.

Kwa wale wanaonunua miti na ardhi, wawe waangalifu, vijijini unaweza kuta miti ni mtu mwingine na ardhi ni ya mtu mwingine.

Asante, tuendelee kukata issue.



Kiongozi unaonekana unafahamu mengi juu ya miti hapo aithee, NAOMBA KUJOIN naamini nitafamu mengi nitakapopata mawasiliano yako... Email yangu ni waggmwz@gmail.com
 
well said mkuu, hivi ule utaratibu wa hati za kimila uliishia wapi? nasikia ilikuwa 20,000 tu , au hauwahusu wanunuzi wa ardhi yaani mpaka uwe umerithi?

Utaratibu ule bado upo na kuna maeneo wanaendelea kugawa hata sasa. Sehemu zingine hakuna kinachoendelea kwa sababu ya ulegelege wa serikali za maeneo hayo.
 
OOh!!! Mkuu hilo tu?

Mi nipo huku Iringa. Kuhusu shamba la miti ya mbao hususani pine naweza kukusaidia kwa kukuunganisha na kikundi kimoja kinacho jihusisha na uhamasishaji wa upandaji miti hasa mipaine: Yaani wao watakutafutia shamba, watapanda, na kukumilikisha chinni ya serikali ya kijiji na utakabidhiwa hati ya umiliki wa shamba hilo.

Na jumla ya gharama zote ni SH;250000 Kwa eka moja.Pia kipo kikundi kingine ambacho unaweza kuingia mkataba juu ya utunzaji wa miti yako hasa issue ya moto na mambo mengine ambayo ni hatarishi kwa ustawi na ukuaji wa miti yako. Hii ni serious issue kama upo Interested ninyongee kupitia 0768953122 or via lupyana.kimela@yahoo.com;

Japo mi ni mdau mpya so nimeipenda sana topic ya kimaendeleo zaidi.
 
Nataka kujuzwa soko la mbao kwa Dar likoje? Mbao Moja inanunuliwa kwa sh ngapi? Na soko lake kwa ujumla, nataka kukata kibali kutoa mikoani kuleta Dar, mwenye kujua soko anipe dira.
 
Mkuu mbao aina gani,na za wapi? Mninga, Mvule, Mtondoro, Mwarobaini, Mwembe, Mnazi, Mpodo, Treated au zipi? Funguka upewe data.
 
Kama unataka mninga na jamii yake inabidi ujipange vizuri, unaweza kuwaletea watu mzigo toka porini, sio kazi ya kuingia kichwa kichwa mkuu.

Nimekusoma mkuu but bdo sijapata jibu la swali bei zikoje town?
 
Mkuu hivi Mwarobaini unachukua miaka mingapi hadi kufikia kuvunwa kwa mbao?

Kama eneo lina maji maji unaweza kuvuna mbao baada ya miaka 8 na kuendelea, kama eneo lina udongo mgumu basi hesabu ni baada ya miaka kumi. Taabu ya mwarobaini ni kupata pingili ya urefu wa ubao unaotakiwa.
 
Kama eneo lina maji maji unaweza kuvuna mbao baada ya miaka 8 na kuendelea, kama eneo lina udongo mgumu basi hesabu ni baada ya miaka kumi. Taabu ya mwarobaini ni kupata pingili ya urefu wa ubao unaotakiwa.

Ni kweli mkuu kwa miaka hiyo bora kupanda mikaratusi tu nilifikiri ina shortcut kama miaka mitatu tu hivi.
 
Nmekusoma mkuu bt bdo cjapata jibu la swali bei zkoje town?

Town ya dar ft 8 au 10 ni kt ya Tsh 35,000/ kwa 2x6 na 2x8 zinalala kt ya Tsh 45,000/ ila huku Kilwa Masoko unaweza kupata kwa 15,000/ ft 8 2x6. Soko linabadilika sana.

Uhakika mzuri tembelea maduka ya mbao Mbagala uone range zake mwenyewe.
 
Ni kweli mkuu kwa miaka hiyo bora kupanda mikaratusi tu nilifikiri ina shortcut kama miaka mitatu tu hivi

Eucalyptus ni deal kali bro, unaanza kula kuanzia miaka 6 tu na kuendelea. Naiotesha sana sasa hivi.
 
Back
Top Bottom