Msaada: Kutafuta maisha nje ya Tanzania

Msaada: Kutafuta maisha nje ya Tanzania

Mie nimehangaika weeeeee,but nimeshindwa kupata nafasi ya Ulaya,kuna uzi wangu upo humu natafuta msaada wa kutumbukia Dubai nikawe ata machinga tu.
 
Kama unatamani sana kwenda kuishi Ulaya
1. Fanya kazi ya u porter mlima Kilimanjaro ujenge ukaribu na wateja. Ukipata anaekupenda ng'ng'ania.

2. Ingia match.com
Kumbe huo mtandao wa Match.com kumbe kuna mambo ya kulipia kwa pesa,kweli hakuna cha bure dunia hii
 
Me niliondoka Tz last month. Nilikuja likizo nikakaa miez 5. Kiukweli kama isingekuwa ile ticket ya return nahisi mpaka leo ningekuwa Tz natafuta nauli ya kuondokea. Jua linawaka mpaka mifukoni. Vyuma vimekaza jamani ila tusisahau kuwa ukiona Mambo yanazidi kuwa magumu basi ujue neema inakaribia.

USHAURI WANGU KWAKO: Piga vibarua ujikusanyie pesa yako kwaajili ya safari yako. nenda Pale pepsi vingunguti vibarua vipo kibao una uwezo wa kupata Hadi 50000 kwa wiki,ukipiga miez yako 4 utakuwa umesogea hatua kadhaa mbele.
 
Duh sawa mkuu.ungenipa hata hilo shamba au kunifanyia connection ya kazi nahisi ni busara zaidi

Nafikiri kuna kazi umekuja kuitafuta humu JF maana inaonekana kila kitu wewe hujui au huna na unahitaji msaada..

Kijana usihofu mda si mrefu tutakuja kukusaidia, utalala,kula na kuendesha magari mazuri mjini buree kabisa na wala hutohitaji kwenda tena huko ughaibuni utaishi vizuri tu kijana usihofu..
 
kijana safari sio mchezo mchezo kama unavyofikiri tena kwa wewe ambaye hata passport huna na namna ya kuipata tena hujui na wala hata hujajaribu hata kufika Tunduma uende south ambayo ndio naweza kusema ni moja ya safari rahisi ambayo unaweza kujikuta unafika bila maumivu..

Fika Uganda toboa mpaka south sudan, nyoosha kama unaelekea North Sudan halafu unatobolea Sinai Egypt. Hapo Egypt utachagua mwenyewe uzamie ukatize suez to Europe au uendelee road to road mpaka syria - turkey to Europe..
Safari sio kunywa chai na mkate, unatakiwa ujikaze kijana usije ukafike Europe na Bikra haipo..
 
Hatua ya kwanza tafuta hela na kitabu/pasipoti then chagua nchi then andaa mwenyeji
 
Back
Top Bottom