Msaada - Gari yangu inakula sana mafuta

Msaada - Gari yangu inakula sana mafuta

Kumbe sikutaja aina ya transmission, ni auto mkuu. Wengi wanaotumia auto hutumia miguu yote, wakushoto breki na kulia mafuta. Wengi wanaotumia mguu mmoja wakati wakuendesha auto hujikuta kosa moja goli, wengi wanafanya hivyio ili kuepuka kupata ajali ya kugonga gari la mbele yako hasa kwenye foleni. Unaweza kufikiri unakanyaga breki kumbe mguu hujaamisha vizuri kutoka kwenye mafuta.
Kutumia miguu miwili AUTO? labda udereva wa vichochoroni, Auto Mguu mmoja wa kulia unatosha, sababu kubwa ukitumia mguu wa kushoto kwenye Break hautakuwa umekaa vizuri au kama miguu yako inamatege is okey.
 
Itakuwa forester subaRu kwakweli wenye hizi gari wapeni heshima tena kwa dar na foleni inameza lita kwa 3km.wakienda sheli mafuta yao akiweka ya bei ndogo ni laki unappoagiza gari uwe unauliza fundi haswaa kwny upatikanaji wa spea na ulaji mafuta.


Arusha hizi SUBARU FORESTER ziko nyingi sana, nadhani hawa jamaa watakua ni watu wa ''mawe'' (Merelani) au ni kule kuigana halafu baada ya hapo mtu anakufa na tai shingoni. Eti utasikia zinakimbia sana, sijui mtu utasafiri mara ngapi hizo safari ndefu za kuhitaji ukimbie?
 
hata hizi auto mara nyingi kule upande wa kushoto kuna kadubwana fulani wamekaweka kanakuwa kanasupport mguu kama vile gari za manual ila hiyo ya mguu wa kushoto kukanyaga brake na kulia kukanyaga mafuta ndo nausikia leo.. yawezekana mkuu hukupitia veta nini...

Mhh huyu jamaa anayeendesha auto kwa miguu miwili sijui kajifunzia wao
pi udereva!!
 
Arusha hizi SUBARU FORESTER ziko nyingi sana, nadhani hawa jamaa watakua ni watu wa ''mawe'' (Merelani) au ni kule kuigana halafu baada ya hapo mtu anakufa na tai shingoni. Eti utasikia zinakimbia sana, sijui mtu utasafiri mara ngapi hizo safari ndefu za kuhitaji ukimbie?
Mkuu kuna dada mmoja hapa ofisini kwetu alimuona mwenzake amechukua Toyota Klugger naye akajitosa akaagiza Subaru Forester, ameitumia toka kwake Kimara mpaka Posta hata mwaka haujaisha ameipaki hapa ofisini amekopa akachukua Vitz sasa hizi anakula kiyoyozi wakati ule wa Subaru alikuwa anaogopa hata kuwasha kiyoyozi.

Nimesikia nyepesi nyepesi anatafuta mteja wa Subaru.
 
Mkuu kuna dada mmoja hapa ofisini kwetu alimuona mwenzake amechukua Toyota Klugger naye akajitosa akaagiza Subaru Forester, ameitumia toka kwake Kimara mpaka Posta hata mwaka haujaisha ameipaki hapa ofisini amekopa akachukua Vitz sasa hizi anakula kiyoyozi wakati ule wa Subaru alikuwa anaogopa hata kuwasha kiyoyozi.

Nimesikia nyepesi nyepesi anatafuta mteja wa Subaru.

anauza shing ngapi mkuu?
 
Cheki plug kwa petrol na pump/nozzle kwa diesel, piaweka air cleaner mpya genuine....otherwise gari chakula chake kikuu mafuta....lazima ile ili itembee ... au fuata ushauri wa bujibuji...isilimishe....

Gari langu linatoa moshi, na petrol linatumia km 8 kwa lita, ni spacio old model, linatumia petrol, msaada jamani
 
Km 8 kwa lita ni wastan wa gari kimatumizi ulitaka liende km 200 kwa lita Hahaha iko sawa hyo gari mkuu
 
Kuna jamaa anauza vifaa vya kupunguzia mafuta kwa zaid asilimia 25 just unaweka sehemu ya kuchomea sigara ni km laki 2 kwa kimoja ndo watu tunavyotumia hpa mjini mkuu wewe maona bdo ipo mbali nitafute nokupe mawasiliano ya muuzaji
 
Mkuu, toa information kamili ili upate msaada. Wataalam wapo.

1. Gari gani
2. Ya mwaka gani
3. Size ya Engine
4. Diesel, Petrol au Mafuta ya Korosho
5. Automatic of Manual Transimmission

Ukianzia hapo msaada utapatikana mkuu.

Hahahahahahahahahhahahaaaaaaaaaaaaaaa..... Hapo kwenye Red. JF burudani sana.
 
Mi bado ntakukatalia kuhusu hoja zako hasa unaposema mguu wake wa kushoto una nguvu. ...mimi mwenyewe natumia kila kitu kushoto toka utoto wangu lkn linapokuja suala La kudrive wala huitaji nguvu nyiiiingi kukanyaga pedal. ...gari yenyewe hata ukiwa kwenye foleni hata usipokanyaga mafuta bado utakuwa inasogea sasa kuna haja gani ya kutumia miguu miwili?

Nashangaa mnabishana weee kuhusu uendashaji wa auto. Mi mwenyewe nakanyaga brake kwa mguu wa kushoto napoendesha auto na nabadili napoendesha manual. Hivi mmeshajiuliza kwa nini pedal ya brake ya auto ni pana kuliko ya manual? Ni kwa sababu iwe rahisi kutumika kwa mguu wowote.
 
Ungetusaidia kutuwekea namba ya simu ya muuzaji wa hicho kifaa cha kupunguza gari kula mafuta ungetusaidia sana mkuu. Ama kwa spacio kula 8km/Ltr siyo mbaya sana. Mara nyungi spacio old model engine yake ni 4A hivyo ni km11-9km hivi kama gari halina tatizo. Kama mdau alivyochangia cheki nozzle, filter na Petrol flter. Pia fundi apime kule kwenye engine kama boya linalounga kutoka kwenye engine na bomba la kutolea moshi. Watu wengi hubadilisha tu oil filter na kusahau kubadili petrol filter wkat wa service. Petrol filter ikiwa chafu mafuta yanapita kwa uwiano usio sahihi hivyo gari linakula mafuta. Na kama mfumo wa umeme hauko active yaan boya linalounga injini na ekizos(exhaust) nyaya unaweza kuona ni mpya ukipima umeme haupiti. Hilo likifanyika kaka gari itakuwa safi. Gari yangu RAV4 ilikuwa inakula mafuta ajabu, baada ya marekebisho ya vitu nilivyosema sasa inaenda angalau 8-9km/ltr.
 
Wewe unaendeshaje hiyo Auto? Jaribu kumshauri mke wako aache kutumia mguu wa kushoto kukanyaga brake, hii imetokana na kuanzia kuendesha gari ya Auto, you never know kuna siku atakuja kwenye manual transmission hapo ndo kitakua kimbembe. Angeanza na gari ya manual hicho kitu usingekiona. Lakini mzee na wewe huoni huo ukakasi ukiwa naye anapokanyaga brake kwa mguu wa kushoto??? Usichukulie kwamba amekua ktk hali hiyo kwa 10 years bila shida, rekebisha hilo ni TATIZO.

Acha hizo. Hiyo ni kawaida. Mi mwenyewe nasukuma zote mannual na automatic na nikiingia auto kushoto breki kulia mafuta. It plays so well. Haya mambo ua hamisha hamisha mi siyawezi
 
Back
Top Bottom