Mrejesho wangu nikiwa kama mtumiaji wa tigo post paid Internet, The juice i get is worth the squeeze from my wallet

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,033
Nipo natumia huduma hii tangu mwaka jana na msukumo wa kuja huku ilikuwa ni baada ya mitandao kupandisha bei za mabando, nadhani wote mnakumbuka mabando yalikuwa bei chee ila kuna wabongo hawakutosheka wakaanza kuyabipu makampuni ya simu kwamba vifurushi visiwe vina expire, Mb ni chache, n.k. ishu ikafika hadi wizarani ikawa ajenda kubwa, mitandao ikapiga na ndio ukawa mwanzo wa vifurushi kuuzwa bei kali, hakika huwezi jua thamani ya ulichonacho hadi kipotee!!

Ok back to the topic, Nipo na hawa tigo since last year na huu ndio mrejesho wangu.

Kupunguza gharama za internet - Kila mwez naungwa GB 80 kwa shilingi elf 60, hii ni sawa na shilingi 750 kwa kila GB, kwangu ni deal safi kabisa sijui kabisa mambo ya kuzima data,

kumekuwa na mabadiliko ya bei kwa wateja wapya lakini sisi wateja wa zamani hatuguswi na mabadiliko, kwa sasa wateja wapya bei zao hizi hapa, nao hawataguswa na mabadiliko yakija kufanyika.

1685639704118.png


Upigaji / Wizi - Kuna ule upigaji unakuta umejiunga gb 1 ila ukitumia MB 300 tu unaambiwa bando limeisha au unatumiwa sms kwamba umetumia 75%, Huku sijaona hicho kitu, Natumia router inayohesabu nimetumia gb ngapi, na nikiangalia salio kwenye mtandao kweli naona kuna uwiano. Mfano kwa hapa Kwenye router umetumija GB 2 na MB 207, kwenye salio la tigo inaonyesha zimebaki GB 77 na MB 793, kwa kifurushi changu cha GB 80 pana uwiano.

1685639956292.png


1685640913290.png




Speed - Mwanzoni speed nilikuwa napata changamoto nikitumia internet nyumbani nje kidogo ya mji tofauti na nikiwa ofisni sehemu za centre, yani nikifika home nlikuwa napata speed ndogo sana tena ikifika usiku ndio naweza kuzima kabisa, kipindi hiki nilikuwa natumia line yao kwenye simu yangu ya Samsung iliyokuwa na laini 2, Ndipo nilipokutana na kijana wetu wa IT ninapofanyia kazi akanishauri ninunue pocket router sababu ni kifaa maalum kwajili ya kukusanya mawimbi ya Net, Hio router ni 75,000 lakini niliingia group la facebook la mkoa nilipo nikapata iliyotumika kwa 20,000, niliongezea elf 10 ya mwanasheria kutuandalia mkataba wa kuuziana (mkataba unilinde endapo router ni ya wizi).

niliambiwa niiweke dirishani ila kwa speed ilipanda kidogo, kijana wa IT alikuja kunitafutia sehem yenye network zaidi, alichofanya alianza kudownload faili la Gb kwenye simu yake huku anatembea na router na kuipitisha maeneo kadhaa ya mle ndani, haoa alikuwa anacheki maeneo yenye speed kubwa, alipoiweka juu ya mlango speed ikafika MB 2 kwa sekunde, ndio sehemu nayotegesha router kila niwapo nyumbani.

TF.jpg


Malipo - Kila Tarehe 1 inapofika bando linaingia , Napewa siku 9 za kukamilisha malipo kuanzia tarehe 1 hadi tarehe 9.

1685639571199.png


Mobility - Niliwahi fikiria kufunga nyumbani fibre ya nguzo za ttcl elf 50 kwa mwezi unlimited, tatizo likawa ni mobility (utumiaji wa sehemu zaidi ya moja) ndipo paliponishinda, pia umeme ukikatika haitumiki, nguzo zikidondoka hakuna huduma, n.k. ni tofauti na post paid nabeba ki router changu sehemu yoyote napoenda hata nikiwa na drive.
 
Boss mm nataka hichi cha voda au airtel napataje??
Sisi enzi hizo ilikuwa unasaini tu mkataba unaungwa ila siku hizi tigo postpaid, airtel sme na voda supakasi wanahitaji uwe na leseni ya biashara .

Mbadala wa hapo ukubali kutoa 10 ya maji kwa vishoka, wamejaa tele fb, twitter na hata humu wapo ukifatilia post za vifurushi. unawapa namba yako wanamaliza kazi wao,

Kwa airtel ninayo line ina vifushi vya sme ila nimeweka kwa dharura tu, mabando yao haya hapa. uzuri wao si lazima ulipie kila mwezi.

1685648054944.png


Kwa voda sijawai kufikiria, Bei yao imechangamka, bando la chini kabisa ni 120,000 kila mwezi lakini ni bila kikomo.
 
Mbadala wa hapo ukubali kutoa 10 ya maji kwa vishoka, wamejaa tele fb, twitter na hata humu wapo ukifatilia post za vifurushi. unawapa namba yako wanamaliza kazi wao
Hivi Airtel SME wanahitaji TIN number yoyote au ni lazima iwe ya biashara?
Kuna chochote unalipa kama ukiamua kwenda airtel shop?
 
Kwa hakika postpaid haina mbambamba, hata habari za mabando kupanda hazinipi tena pressure.

Binafsi kwenye mawasiliano nawatumia voda, ila wangekuwa na hizi huduma nisingehangaika kutumia mtandao wa ziada
sky soldier uko kama mimi😚mawasiliano Voda internet Tigo na wako vizuri hawaibi GB kabisa

Viva Tigo Post Paid👏(Tigo Business)
 
sky soldier uko kama mimi😚mawasiliano Voda internet Tigo na wako vizuri hawaibi GB kabisa

Viva Tigo Post Paid👏(Tigo Business)
Toka zamani nilikuwa nalazimika kutumia simu yenye laini 2, laini ya voda kwajili ya mawasiliano, laini ya pili kwajili ya internet.

Ila kwa sasa tangu nimenunua haka kadude pocket wifi router sina mpango tena wa kununua simu ya laini 2. yani haka kadude iwe ni ofisini, nyumbani, kwenye gari, n.k. lazima kawepo na uzuri ni kwamba hata kama sehemu haina network basi unakatega hata juu ya mlango.

Kwa sasa hata simu yangu inakaa sana chaji nimegundua wifi inatumia chaji kidogo
 
Natumia tigo postpaid pia. Saiv wamepandisha bei lakini naendelea kupeta na ofa ya mwanzoni.
Ndio uzuri wa ile ofa za mwanzoni, tunaendelea kulipia bei zile zile

kwa sasa hivi bei wamepandisha kwenye vifurushi vya data ila kwenye vifurushi vya combo wamepunguza mda wa maongezi wameongeza Gb

Postpaid kwa wateja waliojisajiliwa mwanzoni

1685710167916.png



Postpaid ya sasa

1685710090161.png
 
Sisi enzi hizo ilikuwa unasaini tu mkataba unaungwa ila siku hizi tigo postpaid, airtel sme na voda supakasi wanahitaji uwe na leseni ya biashara .

Mbadala wa hapo ukubali kutoa 10 ya maji kwa vishoka, wamejaa tele fb, twitter na hata humu wapo ukifatilia post za vifurushi. unawapa namba yako wanamaliza kazi wao,

Kwa airtel ninayo line ina vifushi vya sme ila nimeweka kwa dharura tu, mabando yao haya hapa. uzuri wao si lazima ulipie kila mwezi.

View attachment 2642965

Kwa voda sijawai kufikiria, Bei yao imechangamka, bando la chini kabisa ni 120,000 kila mwezi lakini ni bila kikomo.
Tigo kama huna leseni nicheki nikupe maelekezo utapata huduma 0717700921 hata kama huna hela yakulipia naweza kukulipia hadi uanze kupata huduma ndipo unirudishie hela yangu! Mm naunganisha kwa upand wa tigo
 
Tigo kama huna leseni nicheki nikupe maelekezo utapata huduma 0717700921 hata kama huna hela yakulipia naweza kukulipia hadi uanze kupata huduma ndipo unirudishie hela yangu! Mm naunganisha kwa upand wa tigo
Hongera

Sisi wengine tulijiungia Ofisini tunaendelea kuenjoy tu😊

Kama utakua Muaminifu wengi watakutafuta na kuleta shuhuda hapa
Hermanx
 
WAKUU HIZO BANDO ZA POSTPAID TIGO NAUNGANISHA, MIMI MJE HATAKAMA HUNA VIGEZO WW NJOO TUU HUNA LESENI TIN NAMBA NA NIDA, HUDUMA UTAPATA NA HUNITUMII HELA HATA MIA!! 0717700921
 
Back
Top Bottom