Mrejesho: Nyumba yangu kuuzwa

Mrejesho: Nyumba yangu kuuzwa

so sad, lakini sio wanaume wote ila wale yenye akili ndogo mfano wa sisimizi,komaa tu ipo siku utatoka nyumba za kupanga kumbuka Mungu hamtupi mja wake
 
Kuna vitu unatuficha, hasa kwenye ushiriki wako kuweka dhamana nyumba.
 
Madam vero kama alichukua mkopo akaweka dhamana nyumba yako isingeweza kuuzwa. Itauzwa vipi wakati aliechukua mkopo si mmiliki? Hilo haliwezekani bila dhamana yako.
Kuna haja ya kufanya analysis za kisheria nakuja kuanzisha uzi maalumu wa mambo haya ili kutoa elimu kwa jamii ili kuweka mambo sawa.
Mimi nilishawahi kopa benki moja mwaka juzi na ghafla biashara ikaanza kuyumba, marejesho yakashindikana kabisa na jamaa wakataka kuuza dhamana zangu nilizoweka, bahati nzuri nikakutana na mwanasheria mmoja anakanmbia nimpe mkataba wa benki ausome then atajua la kufanya.
Baada ya hapo akagundua mkopo ulikuwa wa kibiashara na biashara imefirisika so alichonishauri kwa haraka ni kumtafuta muhasibu anifanyie mahesabu Kisha nipeleke TRA na ku-declare biashara yangu imefilisika na imefungwa nikawakabidhi TIN number yako.
Tukarudi mahakamani na zile nyaraka za ushahidi wa kufilisika, mahakama wakatoa hukumu yao nyumba yangu ikabaki kwangu na benki wakamilikishwa vitu vilivyokuwa vinamilikiwa chini ya biashara wavipige mnada kufidia deni.
Kilichowaangusha benki ni mkataba wa mkopo wa biashara tu...ifike mahari tukabidhi wataalamu majukumu yao ili kujiweka salama.
 
Mnavyozizungumzia benki mnafikiri hatuzijui. Ndio maana mnakuja na hoja nyepesi eti mimi banker blah blah. Eti benki haipendi kuuza nyumba yako wangekupa basi riba 1%. Wanakupa riba 22% au zaidi kwa makaratasi ya biadhara za kupikwa huku wanajua deni hilo hutalipa au halilipiki. Tunazijuahizi benki vizuri sana.
Mkuu bank unazijua kwa nje nasisi tunaojua kwa ndani tunajaribu kukupa mwanga bado unaona tunakuja humu kujinadi kwamba tunafanya kazi bank kitu ambacho ni kidogo sana kufanya kazi bank. Cha msingi tambua kuna regulators wengi kwenye hii industry ndio maana riba ziko juu hivyo unavyoona na ndio maana serikali kupitia bank kuu hawafanyi kitu juu ya riba. Mfano mdogo tu bank employees walikua wanakopeshwa kwa 7 percent lakini TRA wakaja juu na riba ikaongezwa bila bank kupenda ikafika hadi 12pc. Kwa hiyo jamaa kusema bank hazipendi kuuza nyumba maana yake ni kwamba wanapenda mkopo ulipike ndio maana wanaweza hata kufanya loan restructuring ili kukupunguzia kiasi cha marejesho. Ukiona mtu nyumba imeuzwa ujue kapewa njia zote za kulipa na muda wa kutosha ila imeshindikana kabisa maana kupiga nyumba mnada inagharama sana na inachafua hata jina la bank katika jamii...Kama bank zingekua zinapenda kuuza nyumba nakuhakikishia kwa hiki kipindi cha JPM nyumba nyingi sana zingeuzwa hasa mahoteli maana hali ni mbaya lakini wanatoa demand notice then wanakaa mezani na kuweka mikakati mambo yaende. Kwanini usijiulize NPA as per BOT ni 5 percent lakini karibu bank zote zina NPA above 10 percent lakini BOT wapo tu na wao ndio regulator?
 
Msioe wapaka pafyumu kali na suti za US mkaamini ndio wanaume bora.

Mnakataa watu sahihi
 
Nimeuza kabla ya tarehe maana ingekua aibu kubwa mtaani, kinacho niumiza zaidi nyumba yenye thamani ya mill50, nimeuza kwa sh.mill.27
Pole sana ingekuwa ndiyo mwanaume kalileta hapa ungesikia fukuza wanawake akili zao wanazijua wenyewe, ila mie tungepambana ningewambia mbebeni tu ila nawewe inakuwaje waje kuuzwa wakati sio nyumba yake? Hao ndiyo wanaitwa vichwa vya familia ?
 
Ndugu zangu ndoa ni taasisi tumewekwa vikao na ndugu wa pande zote mbili, mume anadai amekosa sina budi kumsamehe na kuanza upya kusorve tatizo. Tulikosa MTU wa kutukopesa pesa hiyo nikaona bora niuze mwenywe maana wala jamaa wakija kupiga mnada wanaweza kuuza hata mill15 nikapata hasara zaidi
Kwahiyo wakija wanaambulia patupu na huyo aliye kopewa yupo wapi?
 
Aman iwe kwenu wakuu,

Kutoka Moyoni mwangu, nawashukuru wana jamvi kwa ushauri mzuri. Japo wapo wapo walio nidhihaki nawao pia nawashukuru pia.

Jamani wanaume mnatutesa wake zenu IPO HV wakuu, mume wangu alimchukulia nduguye mkopo wa mill.20 bank akaweka dhamana ya nyumba yetu.

Nyumba ambayo nimejenga kwa jasho langu miaka mitano najenga yeye kaja kunioa juz juz kanikuta nimejiimarisha nyumba yangu imeisha bado kuweka vioo na gypsum tu. Nimetumuia gharama kubwa na mikopo juu ili tu niwe na kwangu.

Akaja kuweka dhamana ya nyumba bila kunishirikisha yaani bado mwezi mmoja ndo napata habar kuwa nyumba yetu inapigwa mnada.

Na usitoshe kwasasa sina kazi ni maza House nimefukuzwa kazi kwa uzembe kazini, na riba imeongezeka plus na dalali jumla nimelipa million10

Amenipa presha nimeuza nyumba yangu, nimelipa deni sasa HV nipo kwenye upangaji napambana na wenye nyumba zao.

Imeniuma SNA wanaume MNA roho gani, yaan hata hamu nae sina natamani niachike ila dini hairuhusu.

HV tukiwasaliti, mtatuona Malaya kweli. Ndoa ngumu ndugu zangu acheni tu.

Unakubali wewe ni mzembe na ni mzembe mpaka kazini!!! Uzembe wakutokutunza stakabadhi zako, documents muhimu under lock, note that do not trust any body even your Pastor and in addition to that do not trust even yourself kwani unaweza kukumbwa na ibilisi unafanya maajabu na baadaye unajutia, Trust only God.
 
Aman iwe kwenu wakuu,

Kutoka Moyoni mwangu, nawashukuru wana jamvi kwa ushauri mzuri. Japo wapo wapo walio nidhihaki nawao pia nawashukuru pia.

Jamani wanaume mnatutesa wake zenu IPO HV wakuu, mume wangu alimchukulia nduguye mkopo wa mill.20 bank akaweka dhamana ya nyumba yetu.

Nyumba ambayo nimejenga kwa jasho langu miaka mitano najenga yeye kaja kunioa juz juz kanikuta nimejiimarisha nyumba yangu imeisha bado kuweka vioo na gypsum tu. Nimetumuia gharama kubwa na mikopo juu ili tu niwe na kwangu.

Akaja kuweka dhamana ya nyumba bila kunishirikisha yaani bado mwezi mmoja ndo napata habar kuwa nyumba yetu inapigwa mnada.

Na usitoshe kwasasa sina kazi ni maza House nimefukuzwa kazi kwa uzembe kazini, na riba imeongezeka plus na dalali jumla nimelipa million10

Amenipa presha nimeuza nyumba yangu, nimelipa deni sasa HV nipo kwenye upangaji napambana na wenye nyumba zao.

Imeniuma SNA wanaume MNA roho gani, yaan hata hamu nae sina natamani niachike ila dini hairuhusu.

HV tukiwasaliti, mtatuona Malaya kweli. Ndoa ngumu ndugu zangu acheni tu.
Mimi nipo tofauti hivi kwa maisha gani Mtu uchukue million 20 ukafanye biashara , Tena 10 million unampa ndugu , hivi Kuna biashara ya kuaminiana ukifanya na ndugu kweli, afu pia Kama hip nyumba angeijenga mwanaume sizani Kama hata mkopo angechukua.
 
Huyu dada naona hakutafuta mwanasheria, hakika hiyo nyumba benki wasingweza kuuza, nyumba ya wanandoa huwezi kukopea bila ridhaa ya mwenza, sembuse hiyo ambayo mke aliijenga kabla ya ndoa. Kumbukeni nyumba ya Cheyo Mapesa haikuuzwa kwa pingamizi la mke. Kama kulikuwa na kughushi, basi hiyo ni jinai na si kuuza hiyo nyumba.
Huyo Dada nafikilia alisaini yeye mwenyewe
 
Haiwezekani ukoo mzima wasijue hii sheria. Alipoleta hii kesi hapa alipewa ushauri kama huu. Siku hizi ukikopa benki kama umeoa lazima na mkeo ashirikkishwe hata kama nyumba ni ya mume, sasa hii nyumba ya mke iwekwe dhamani bila mke aka mwenye nyumba kushirikishwa benki gani hio? Au mlichukua hela kwa papaa msafi?!
Huyu Dada walikubaliana yeye na mme wake ,
 
Naomba niwashukuru tena kwa mawazo yenu. Ndoa ni taasisi, tumeshawekwa chini na viongozi wa dini wakaniambia nikubali tu yaishe kuwa mm nilishirikishwa nikawaelewa. Na nimeamua kumove on, sababu imeshatokea na haiwezi jirudia. Na kama msamaha ameshaomba SNA mume wangu na Nimemsamehe.

Nawaza tu mtoto wangu angeishi maisha gani,
Niwatakie kheri ya mwaka mpya, yaliyopita si ndwele tugange mapya
Pole mumeo ninawasiwasi nae pia unafanya biashara ya ndugu kweli
 
Maisha ya mahusiano yapo vise versa not women or men, nikisimama upande wako kuna mwingine Men atakuja na heavy story more than yours alafu naye inabidi nisimame uoande wake.

So hakuna upande ambao una hafueni, kikubwa haya maisha ukiweza kubeba uvumilivu basi uvae usonge nao mpaka uzeeni ukiona huwezi, usisingizie dini, mchungaji au sheikh hao hawakupeleki 'peponi kama ipo' pambana na hali utakayokuwepo.

Kwaheri.
 
Back
Top Bottom