Mrejesho: Nyumba yangu kuuzwa

Mrejesho: Nyumba yangu kuuzwa

Kama unachoeleza ni ukweli, ningekuwa mimi ningeaanza kufanya uchunguzi kujua kama ni kweli hizo hela alimkopea mdogo wake au hisijekuwa anakudanyanga hela alikopa mwenyewe na akatumia kwa maswala anayofahamu mwenyewe.

Pia ningekuwa mimi, hela iliyobaki ningeweka benki yote na kuona kama kweli angebeba mzingo aliyosababisha mwenyewe yaani kodi ya nyumba na nk..

Nasema hivyo kwa sababu kama aliweza kumthamini ndugu yake na kwenda kumkopea mkopo kwa njia za kitapeli ninapata wasi wasi kama ukweli ana mapenzi ya kweli kwako na kama ana thamini juhudi zako katika kuendesha maisha yenu. Hivyo ili kujiridhisha kama kweli huyu mtu ana mspenzi ya kweli kwako au anaonyesha majuto kwa alichokifanya basi ningefanya kama nilivyokishauri hapo juu..

Zaidi ya hayo nakutakia khera na heri kumbuka kitu cha muhimu ni uzima kwani vitu utafutwa..na kama uliweza kutafuta mpaka ukajenga basi sina na wasiwasi na wewe utaweza tena..Ila husikubali kuashindwa..
 
Mkuu usimpinge kana kwamba unajua yote. Mi nilikutana na case kama hiyo nikiwa banker arusha na mkopaji ananyumba mwanza ambayo aliiweka dhamana na wife's consent ikasainiwa na mfanyakazi mwenzake badala ya mke wake. Zipo case nyingi sana za hivi sema bahati tu mkopo mtu anamaliza. Kama mnakosoa kosoeni kwa kuuliza ila sio kubisha...game zinawenyewe hizi kuanzia kwa wafanyakazi wa benki hadi wakopaji
Sasa wewe unaongea vitu gani? Afadhali ungekuja kistaarabu, sasa hapa wewe mwenyewe unasema wife's consent imesainiwa na mtu mwingine huoni kuwa mhusika aki-raise hio issue nyumba haiuzwi?! Ok tusema case yake ndio kama hio yako kwahio hawezi kuzuia nyumba kuuzwa kwa kigezo kuwa hio wife's consent hajasaini yeye?!
 
Pole madam, shida tumeumbiwa binadamu. Mimi niliwahi kukopa milioni kumi nikaongeze na za kwangu kununua dala dala ya milioni 22 ila baada ya kumkabidhi dereva, ndani ya siku tatu gari ikawa scrapper... Pesa yangu ikapotea bureee, ila since then I moved on nikasahau hilo jambo na deni la watu nikalipa nikaendelea na maisha mengine. So usiwaze sana...
 
Nimeuza kabla ya tarehe maana ingekua aibu kubwa mtaani, kinacho niumiza zaidi nyumba yenye thamani ya mill50, nimeuza kwa sh.mill.27
Aisee,,pole sana,,,na deni lilikuwa mil.10. Ela inayobakia katafute kiwanja cha milioni saba ,,mwaga tofari elfu tatu na mia tano,, weka foundation then jipange na tofari kadhaa zitabakia zakupandishia nyumba hadi kwenye lenta na kozi mbili za juu kwa baadae/ kama upo Dar nakushauri sehemu nzuri ambayo ingekufaa na kumejengeka na watu wengi wa mjini now wanakimbilia huko,, maeneo ya kule mapinga dada,,utapata kiwanja safi chenye njia na chenye kufika gari, me nimejenga huko nimepangisha nakula kodi
 
pole madamuu anza upya usiwaze kufeli nayo ni njia ya mafanikio
 
Ninachokijua nyumba ili ikubalike kuwa dhamana kama ni wanandoa lazima msaini wote, kama imeuzwa basi hukupata ushauri mzuri ungeweka zuio la mahakama na ungeshinda isingeuzwa. Nimefanya kazi benki kwa miaka mitano nakuambia kitu ambacho nina uhakika, na hiyo issue ukienda benki huyo afisa mikopo anaweza mpaka kufukuzwa kazi, tatizo watu wengi tunapata matatizo kwa sababu hatujui tufanye nini.
Narudia nyumba haiwekwi dhamana mpaka mama amesign zile fomu za dhamana, na benki wanasisitiza zisainiwe benki kwa ajili ya ushahidi wa cctv ila maafisa mikopo hawaifuati kwa sababu wanajua watu wengi hawaijui. Huwa inafukuzisha maafisa ikileta shida.
 
Sasa wewe unaongea vitu gani? Afadhali ungekuja kistaarabu, sasa hapa wewe mwenyewe unasema wife's consent imesainiwa na mtu mwingine huoni kuwa mhusika aki-raise hio issue nyumba haiuzwi?! Ok tusema case yake ndio kama hio yako kwahio hawezi kuzuia nyumba kuuzwa kwa kigezo kuwa hio wife's consent hajasaini yeye?!
Hata mm sijui huyu mkuu anaongea nn kiukweli labda kwa vile banker ndo mana, ila kwa issue kama hiyo sheria ipo wazi kama huyo dada hajahusika kwa namna yoyote kubariki huo mkopo, kwa wakili yoyote hiyo ni kesi rahisi mno mno lazima angeshinda tu hata iwaje, ila kama story yake ni kweli, pia hata kama dalali angeuza bado huyo dada angekuwa na nafasi ya kuchukua tens mali yake
 
Ninavyo fahamu ukiweka mkopo nyumba lazima uweke title (warka wa nyumba). Afisa mikopo hawezi towa mkopo kama jina la warka ni wa mtu mwengine. Je mumeo alikupa karatasi kuweka sign bila ya wewe kujua ni karatasi ya nini? Nenda mahakamani ukaweke ziwio la kuuzwa nyumba yako. Na kuifungulia kesi benki iliotoa mkopo kinyume na sheria, lakini tambua kesi ikienda mume segerea inamuhusu.
 
Uliwezaje kuuza hiyo nyumba wakati dhamana ya nyumba iko bank.Unless mtu akalipe mkopo upewe hati zako labda hivyo.Halafu ilikuwaje bank ikubali mdhamini amdhamini mtu kwa hati isiyo na jina lake bila bidhaa ya mmiliki?sijaipata vizuri hii issue unless sio bank Ni kwa mtu binnafsi ambapo bado ungeshinda kisheria kea kutangaza kuwa hati za nyumba zimepotea.Sijaelewa kea kweli
 
Sasa wewe unaongea vitu gani? Afadhali ungekuja kistaarabu, sasa hapa wewe mwenyewe unasema wife's consent imesainiwa na mtu mwingine huoni kuwa mhusika aki-raise hio issue nyumba haiuzwi?! Ok tusema case yake ndio kama hio yako kwahio hawezi kuzuia nyumba kuuzwa kwa kigezo kuwa hio wife's consent hajasaini yeye?!
Sasa naye huyu mtu wa bank Ni mwongo,picha alitumia ya Nani ku sign hiyo consent .Wewe ukaweke viambatanisho vya mtu mwingine asign my mwingine nashinda kesi wewe.Bora umempa za uso
 
Uliwezaje kuuza hiyo nyumba wakati dhamana ya nyumba iko bank.Unless mtu akalipe mkopo upewe hati zako labda hivyo.Halafu ilikuwaje bank ikubali mdhamini amdhamini mtu kwa hati isiyo na jina lake bila bidhaa ya mmiliki?sijaipata vizuri hii issue unless sio bank Ni kwa mtu binnafsi ambapo bado ungeshinda kisheria kea kutangaza kuwa hati za nyumba zimepotea.Sijaelewa kea kweli
Ha ha ha ha....aisee hili nalo ni swali linalohitaji jibu!
Chriss Jericho
 
Sasa naye huyu mtu wa bank Ni mwongo,picha alitumia ya Nani ku sign hiyo consent .Wewe ukaweke viambatanisho vya mtu mwingine asign my mwingine nashinda kesi wewe.Bora umempa za uso
Unajua kuna watu hata kitu kiko wazi atakuja na habari za mimi lawyer,mimi banker anafikiri sisi wengine kwasababu hatuhesabu hela hatujui hata aeiou za benki.
 
Hati ya nyumba na kiwanja vimeandikwa jina la nani? Kama ni jina lako hawezi kuchukulia mkopo bila ya hidhini yako.
 
Sasa wewe unaongea vitu gani? Afadhali ungekuja kistaarabu, sasa hapa wewe mwenyewe unasema wife's consent imesainiwa na mtu mwingine huoni kuwa mhusika aki-raise hio issue nyumba haiuzwi?! Ok tusema case yake ndio kama hio yako kwahio hawezi kuzuia nyumba kuuzwa kwa kigezo kuwa hio wife's consent hajasaini yeye?!
Kistaarabu vipi mkuu mbona nimeandika kawaida ispokua mnamu-attack mleta mada kama anadanganya wakati hivi vitu vipo na kesi za hivi ni nyingi mpaka watu wanauana na kurogana. Boss wangu mmoja pale mbeya mpaka akakimbia ofisi akakimbilia benki nyingine sababu kuna nyumba maeneo ya Sai ilikua na kasheshe kama hiyo na kesi ipo pale mahakama kuu mpaka leo zaidi ya miaka mitano.. Kimsingi kesi zipo nyingi sana na wakati mwingine hata ikiwa genuine wife consent bado anaweza kuja kuruka kwamba si yeye alisaini hasa maji yakiwa ya shingo wanaweza kufanya conspiracy na mmewe kugeuka kwamba saini ya mke ilisainiwa. Kwa hiyo in both cases unaweza poteza nyumba tu maana watu wamekua wajanjawajanja hadi mahakama zinahongwa na huwezi shindana na bank hasa ukiwa kwenye matatizo tena lawyers wakaanza kukupiga hela zingine. Nadhani unakumbuka yule mama wa sinza alieamua kupanda juu ya paa nyumba isipigwe mnada ndio vitu kama vile japo yule mama alisema hakutoa consent bado wakatangaza mnada ikabidi apande juu ya paa kupata media attention...tena na wao nadhani ni kesi kama hii mmewe alimdhamini mtu kwa kutumia nyumba yao..bora mdada wa watu kajiuzia kwa hasara abaki na chochote.
 
Ninachokijua nyumba ili ikubalike kuwa dhamana kama ni wanandoa lazima msaini wote, kama imeuzwa basi hukupata ushauri mzuri ungeweka zuio la mahakama na ungeshinda isingeuzwa. Nimefanya kazi benki kwa miaka mitano nakuambia kitu ambacho nina uhakika, na hiyo issue ukienda benki huyo afisa mikopo anaweza mpaka kufukuzwa kazi, tatizo watu wengi tunapata matatizo kwa sababu hatujui tufanye nini.
Narudia nyumba haiwekwi dhamana mpaka mama amesign zile fomu za dhamana, na benki wanasisitiza zisainiwe benki kwa ajili ya ushahidi wa cctv ila maafisa mikopo hawaifuati kwa sababu wanajua watu wengi hawaijui. Huwa inafukuzisha maafisa ikileta shida.
Mkuu mimi pia ni banker na nakuhakikishia hata kama mke alisaini mwenyewe bado baadaye wengine wanaruka kwamba si yeye alisaini bali saini yake ilifojiwa..mwisho itakuja kuuzwa tu japo kesi itachelewesha
 
Patrickn naona unaandika gazeti wakati issue iko straight muhusika kasema yake. FYI huyu dada alikuja kuomba ushauri nyumba inauzwa kwasababu mumewe kaweka dhamana bila yeye kujua.
Leo kaja anasema amefanikiwa kuiuza yeye mwenyewe. Sasa ni hivi
1.Alishauriwa kama hakuhusishwa akaweke zuio.
Leo anakuja kutuambia hata dhamana alikuwa hajatoa na nyumba ni yake yeye.
2. Waliiuza vipi wenyewe wakati benki huwa wanakuwa na hati za nyumba?

Kumuuliza ndio kumshambulia?
 
Back
Top Bottom