Moshi yakataliwa kuwa jiji

Moshi yakataliwa kuwa jiji

Watu wanapiga kelele kuhusu majiji fulani kutokuwa na hadhi na mengine kunyimwa sifa. Sio suala la kuona mji una ghorofa ngapi ili upewe hadhi ya kuwa jiji. Tanzania tuna kanuni zetu za kuufanya mji kuwa jiji - mbili kuu ni idadi ya watu na pato. Lakini zipo nyingine. Kama hatupendi mji fulani kutofanywa jiji au mji fulani kufanywa jiji inapaswa tuzirudie sifa tulizojiwekea wenyewe na kuzirekebisha.

Bahati mbaya sana ukiacha Mwanza na Arusha, majiji mengine yalipopata hadhi ya kuwa jiji hayakupata pesa za kutengeneza miundo mbinu. Mwanza ilipewa pesa nyingi sana za kujenga miundo mbinu. Kipindi kile ilipata hadhi peke yake baada ya Dar es Salaam.

Nje ya mada, wewe binafsi umefanya nini hapo ulipo hadi uone mji wako ni mzuri au mbaya. Usije ukawa kuchwa nzima wasifia au wachukia kazi za mikono ya wenzako. Kazi yako imeung'arisha mji uliopo?
Hapo umesema ukweli nimefuatilia vigezo vya kuwa jiji manispaa au mji sijaona kigezo cha barabara na magorofa kwani hiki hufuata baada ya serikali kupandisha hadhi ndipo hutengeza barabara zenye hadhi ya mji wako na kujenga ofisi zenye hadhi ya mji wako mfano watu wanacheka kahama hakuna barabara lakini baada ya miaka 5 wataishangaa kahama maana sasa inatengewa bajeti kubwa hata dodoma ya leo sio ya miaka 4 iliyopita ila tu watu wamoshi wajutahidi kulipa Kodi ni aibu kukusanya bilion 4 sawa na halmashauri ya geita vijijini halafu muombe jiji
 
Mh hangaya alipokuwa moshi leo ameikataa moshi kupandishwa kuwa mji akisema haina sifa

My take kaamua kubalance na chato

Minne inatosha

Ni mfumo mbaya tu mimi naishi USA hapa hakuna cha mji au jiji vyote vina Meya na shughuli za maendeleo hata kama ni watu 10,000. Haya mambo ya kusubiri wanasiasa ndiyo waamue kisiasa mji ni upi, mkoa ni upi sio mzuri
 
Kwani uamuzi wa manispaa kugeuzwa kuwa jiji ni wa Rais peke yake? Na hao wanaoomba hawajui kuwa kuna sifa na viwango vinavyotakiwa kufikiwa kabla ya kuwa jiji?

Amandla...
Wanataka wapewe kwa upendeleo kama dodoma halafu vigezo ndivyo vifuate
 
Hifadhi ya Kilimanjaro (Kinapa) inaingiza mapato makubwa sana hapa Tz kuliko hifadhi za wanyama, huweza kusema Moshi sio mji wa kiuchumi.
Hayo mapato inakusanya manispaa ya Moshi? Watu wengine mnaandika vitu hatari vimejaa uongo
 
Hifadhi ya Kilimanjaro (Kinapa) inaingiza mapato makubwa sana hapa Tz kuliko hifadhi za wanyama, huweza kusema Moshi sio mji wa kiuchumi.
Je kinapa ipo ndan ya manispaa ya Moshi?
 
Hivi ninyi ndugu zangu wachagga sometimes uwa mnawaza nini!!!! Kamoshi kapewe jiji!!! Kwa lipi haswaa? Kuna singida, Shinyanga/khm, geita, kagera n.k na hakuna tetesi ya kuitwa jiji sembuse huko kijijini moshi ndiyo ipewe jiji!!!! Be serious mzee.
Unajua vigezo vya jiji
 
Back
Top Bottom