Morogoro ni kama imerogwa

Morogoro ni kama imerogwa

Kwa mtu ambae ana miaka zaidi ya 15 toka alipouona mji wa Morogoro kwa mara ya mwisho , nina uhakika akiuona hivi sasa hataiona tofauti yoyote Ile ya kimaendeleo hususani miundombinu na makazi binafsi ya watu.
mji umechakaa, watu wanatembea mitaani wamefubaa kama mazombie sababu ya vumbi , huo mji umerogwa

Adios!!
CHUKI kwa wageni inawagegeda,matajiri wako DSM,kwahiyo biashara inafanyika Moro pesa inaamkia Dsm
 
Moshi pale kwenye Boma tuna nyumba 3. Moja imepangishwa. Moja iko wazi na moja ndio anakaa Mama Mkubwa. Na yuko mwenyewe na dada wa kazi.

Tuna family tree ndogo.

Alaf Unajenga nyumba kule nani akae. Tushajenga mjini. Kule tutarud kuzikwa.
Kafo mbee
 
Nirudi zangu nikapaendeleze himo, Ila Moshi imepoa sana wallah, Bora kule kwa Rafaeli na kindi
 
Morogoro kila mtu tapeli,eti wanadalia hadi watu wanaotafuta lodge.

Kipindi hicho najitafuta nikajikuta niko Msamvu naelekea Mbeya sina hata mia. Likaja lorry la viazi na boss akaulizia soko, kuna shabiki mmoja nayeye na safari yake ya Dodoma alikwama kama mimi. Akasema fasta twende town. To make the story short tukajikuta madalali wa viazi wa Morogoro ghafla 🤣
 
Huyu yupo kilosa sio Moro kama mleta mada alivyokusudia. Labda aulizwe Abood.
 
Morogoro ni mahali pazuri pa kuishi na kufuga,Kuna plenty ya ardhi kwa ufugaji na ukulima.
Ni rahisi kufika Dar/Dom kupiga mishe na kurudi home kuchil.
Its a nice place to raise kids compare to many places here in Tanzania.
Private Schools ni cheap,watu wao hawana mambo mengi,vyakula ni vingi,na unavipata fresh.
Ni Mji mzuri wa kuanzia maisha kama ilivyo mbeya,rukwa na Mwanza.

Done!
 
Majengo. Dec,2024.

Na pia Old moshi . Maeneo ya Kcmc na Kibosho nilifika.
Ni vile vile mkuu. Maendeleo ni madogo kulinganisha na miji mingine.
Mkuu huko ulipoenda palikuwa tayari pameendelea ndo maana umeona hivo,ukija sehemu kama mjohoroni,sango ukisema uangalie 10 years back na saiv maendeleo ni makubwa aisee ,,,,na kama old moshi mi pia nimeishi huko sana zamn kulikuwa hamna lami saiv lami ipo and other social services kama maji(tofauti na zamani)…..pia mkuu usiangalie majengo majengo tu angalia sekta ya elimu📈,afya📈 nk?

NB: kumbuka miji mingine ni mikubwa compared to moshi,(kwenye sekta ya uwekezaji na viwanda kidogo moshi iko chini)
 
Ni kama Moshi mjini.

Wageni mara nying ndio hufanya mji kuchangamka na kuwa na maendeleo.

Moshi wana thamini sana Ardhi.
Sio rahisi kuuza ardhi na kama wakiuza basi ni bei juu tofauti n bei elekezi.

Hivyo unakuta Hakuna kitu kipya . Ni Moshi ile ile ya miaka 20 nyuma . Pia wanajenga vijijini kwao ambako vijana hakuna maana hakuna fursa ya uchumi.
Braza umeongea kitu ambacho nilikiona kama miaka minne iliyopita. Moshi inakufa aisee
 
Kwa mtu ambae ana miaka zaidi ya 15 toka alipouona mji wa Morogoro kwa mara ya mwisho , nina uhakika akiuona hivi sasa hataiona tofauti yoyote Ile ya kimaendeleo hususani miundombinu na makazi binafsi ya watu.
mji umechakaa, watu wanatembea mitaani wamefubaa kama mazombie sababu ya vumbi , huo mji umerogwa

Adios!!
Hapana bana,Morogoro imechakaa pale katikati,ila ukiwa unatoka nje ya mji wamejitahidi sana upande wa makazi mapya,ingawa sehemu nyingi hazikupangwa vizuri...
 
"Jaman Morogoro yapendeza oooh,
Maji yatiririka Milimani oooh,, "

mji naupenda sana,, Mji umenilea Umenikuza,,
mkataa kwao ni mtumwa 😎
Kuna wanaotumia maji kutika mlimani na wale wa bwawa la mindu
Ila moro kuko poa tu sema bila kuwa alwatan hapo hutoboi

Ova
 
Back
Top Bottom