je mzee MS wewe kama nguli katika machapisho nadhani utakuwa umefahamu ni kwa kiasi gani utakuwa umeipa taharuki jamii kwa habari yako kuhusu huyo tapeli
sasa je unawasaidiaje wale uliowapa mtikisiko wa kiakili kwa kuiamani habari yako
pia utalisafishaje jeshi la polisi machoni mwa raia wema waliochukizwa na jeshi la polisi kwa habari ya huyo tapeli
Datz,
Hii habari mimi si wa kwanza kuandika.
Gazeti la An-nuur ndilo lilikuwa gazeti la mwanzo kuandika
habari za
Jamal Yassin na akawa anapita misikitini kueleza
ule uongo wake.
Ikasadifu kuwa akaja kusali Ijumaa msikitini petu na mie siku
hiyo nipo ndipo nilipomsikia.
Hakika nilifadhaishwa sana na stori yake na alipoletwa nyumbani
kwangu na
Sheikh Ali Mbaruk ndipo nikamfanyia mahojiano.
Alikuwa pia na barua kutoka kwa Mufti wa BAKWATA
Abubakar
Zubeir ikimtambulisha kwa Waislam.
Sasa hiyo taharuki sikuileta mimi bali na yeye mwenyewe wakati
akipita misikitini kueleza huo ''mkasa,'' wake.
Ila mimi nilipojua kuwa huyu
Jamal ni tapeli ndipo nilipowaeleza
watu ubaya wa huyu kijana.
Tuje katika hili suala la polisi.
Hiki ni kitendawili kikubwa kwangu.
Haiyumkiniki kuwa polisi walikuwa hawajui uongo huu wa
Jamal.
Kwa nini hadi leo hawajamtia mbaroni kumhoji?