Basi hizo tabia za wamanyema wa mtambani uziache, post zako sometimes zinawa-radicalize waumini na kuwa jihad fanatics
Bowlibo,
Sina sababu ya kuwakwepa Wamanyema wa Mtambani au kwengineko kule.
Wamanyema wamefanya makubwa katika historia ya ukombozi wa Tanganyika.
Mwaka wa 1933 wakati African Association ilipokuwa chini wa uongozi wa
Kleist
Sykes kama katibu na
Mzee bin Sudi (Mmanyema) kama rais ndipo walipounda
Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Hii Al Jamitul Islamiyya ndiyo iliyotoa viongozi wa kwanza katika TANU 1955 kama
Idd Faiz Mafongo (Mmanyema) aliyekuwa mweka hazina wa TANU na ndiye
aliyeaminiwa kukusanya fedha za safari ya
Mwalimu Nyerere UNO 1955.
Hii Al Jamiatul Islamiyya ndiyo iliyomtoa
Idd Tosiri (Mmanyema) ambae yeye na
Idd Faiz Mafongo ndiyo waliompeleka
Mwalimu Nyerere kwa
Sheikh Mohamed
Ramia (Mmanyema) Bagamoyo kumjulisha.
Ndugu wawili
Abdallah na
Maulid Kivuruga (Wamanyema) ndiyo waliokuwa waasisi wa
TANU Tabora, 1955 pamoja na
Bilal Rehani Waikela (Mmanyema).
Hawa biti Maftah, Dharura biti Abdulrahman na akina mama wengi mstari wa mbele
kupambana na ukoloni walikuwa wanawake wa Kimanyema.
Saadan Abdul Kandoro mmoja wa waasisi wa TANU 1954 ni Mmanyema.
Katika historia ya uhuru wa Tanganyika Wamanyema wamejaa wengi.
Jiulize kwa nini iwe Wamanyema.
Sasa tuje suala la ''radicalisation.''
Ningependa unifahamishe nini ubaya wa watu kuwa ''radical.''
Hilo la ''fanaticism'' ukweli ni kuwa inategemea umesimama upande upi.