Mods tunaomba hadhi ya Chit Chat forum irudishwe!!

Status
Not open for further replies.
... Pole wana CC kwa kuvamiwa..., mkiona hivyo' elewakuwa watu wanalipenda Jukwaa lenu na kuwaonea wivu, ndiyo maana wanakuja huku kuleta fujo. Yawezekana hao wameshindwa huko kwenye majukwaa mengine, ndiyo maana wanakimbilia kwenu. Bilashaka wameelewa hawata wasumbua tena.
 

tatizo sio kwenye red bali nyinyi wenyewe; mnaanzisha thread hovyohovyo(ashakum si matusi);

yani kwa kifupi kila mwana chit chat anapenda kuanzisha pasipo hata na ulazima.
 
Ni kweli kuwa kuna members kwa kukusudia wanapost chuki na kero hadi wengine wanakosa subira. Mfano hai kuna thread humu watu wameporomosheana mitusi mpaka aibu.

Ahsante charminglady kwa kuliona na kulisemea hili kwani kuna membes wengine dahh!!

yani toka watu waanze kutuletea fujo wengine hata kusalimiana tunshindwa maana imekuwa ni fujo mtindo mmoja.......nakusabahi swahiba hata katikati ya hii kadhia
 
Last edited by a moderator:
Heshima ya jukwaa haiwezi kamwe kuletwa kwa matusi na kejeli dhidi ya wale walio na mtazamo tofauti na mwingine anavyo fikiri!
 
dah ki ukweli inakera sana hali hii mi ninvyoona hakuna haja ya mods hapa kwani mods anahukumu kama member anakosa au karipotiwa. HADHI YA CC tuirudishe sisi wenyewe kwani wabaya tumeshawajua tutumie njia ya PM kujulishana nini cha kufanya hapo kama kampeni za miss cc zilivyokuwa zikiendeshwa.
 


Nakubaliana na wewe wivu unawasumbua huku stress free full kucheka
 

Mkuu hii ndo sababu haswaaaa!!!!
 
Heshima ya jukwaa haiwezi kamwe kuletwa kwa matusi na kejeli dhidi ya wale walio na mtazamo tofauti na mwingine anavyo fikiri!

Hivi mnalazimishwa kuingia humu?????? Kama sio viherehere vyenu na vimbelembele vinavyowawasha kuja huku ni nini????

Nendeni kwenye majukwaa yenu ya maana. Sisi tusio na kazi tuacheni mumu humu.......
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…