Askari wa barabarani mbeya, morogoro ni wazembe kupita kiasi tunaotumia hii barabara huwa tunaona huwezi kuona au kukuta basi lipo speed kali Iringa. Kila siku trafic wanauza sura na kubishana na wamiliki wa mabasi kwenye tv mara vizibiti mwendo mara kamera.. Poleni sana wafiwa na majeruhi.
Ndugu,ni kama umesoma mawazo yangu. Siku chache zilizopita nimesafiri kwenda Mbeya kwa basi.Kwa sasa mabasi yote yaendayo Mbeya,Malawi au Zambia yanakimbia sana mikoa ya pwani,Morogoro na Mbeya. Mkoa wa Iringa wote huwa wanatembea hata ukiwa na baiskeli unawapita. Na madereva huwa wanapigiana simu kuelezana polisi gani(kwa majina)wamekaa sehemu gani. Nadhani pia abiria waanze kuwapiga na kuwachoma moto madereva waendao kasi kama tufanyavyo kwa wezi mitaani. Itasaidia.
Ndugu,mimi ni dereva tena wa siku nyingi tu,nimeshapinduka na gari mara nne. Mara 2 nilikuwa peke yangu kwenye gari,mara 1 nilikuwa na mwenzangu lakini mimi nilikuwa naendesha na mara 1 nilikuwa nimepanda basi la abiria. Kuna tofauti kati ya CHANZO CHA AJALI na CHANZO CHA MAAFA MAKUBWA YALIYOPATIKANA BAADA YA AJALI KUTOKEA. Tairi inaweza kupasuka wakati wowote ukiwa unaendesha gari au hata kama gari imesimama. Pipe ya brake inaweza kupasuka au kuchomoka kwenye maungio yake wakati wowote dereva akiwa barabarani. Lakini kitakachoamua watu wafe kiasi gani na majeruhi wawe wangapi ukiacha na kudra za mungu ni speed ambayo dereva alikuwa akitembea. Soma research zote zinazoelezea ajali za barabarani utaona kuwa chanzo namba MOJA cha maafa makubwa ya barabarani ni SPEED,namba 2 ni UBOVU/HITILAFU ZA VYOMBO VYA USAFIRI na namba 3 ni UBOVU WA MIUNDOMBINU(in our case BARABARA)
Kuna haja ya kuongeza tochi za ma-polisi barabarani; na basi yote yafungwe Spidi-gavana kwa lazima ilo lisiwe ombi.
Poleni sana wafiwa na mungu awasaidie majeruhi wapone haraka, mimi mara zote huwa siamini mwendo kasi ni chanzo cha ajali nyingi zinazotokea hapa nchini, kampuni ya sumri ni kati ya kampuni bora kabisa ya usafirishaji nchini nategemea watashiriki kikamilifu katika kusaidia wafiwa na majeruhi wote
Ndugu,mimi ni dereva tena wa siku nyingi tu,nimeshapinduka na gari mara nne. Mara 2 nilikuwa peke yangu kwenye gari,mara 1 nilikuwa na mwenzangu lakini mimi nilikuwa naendesha na mara 1 nilikuwa nimepanda basi la abiria. Kuna tofauti kati ya CHANZO CHA AJALI na CHANZO CHA MAAFA MAKUBWA YALIYOPATIKANA BAADA YA AJALI KUTOKEA. Tairi inaweza kupasuka wakati wowote ukiwa unaendesha gari au hata kama gari imesimama. Pipe ya brake inaweza kupasuka au kuchomoka kwenye maungio yake wakati wowote dereva akiwa barabarani. Lakini kitakachoamua watu wafe kiasi gani na majeruhi wawe wangapi ukiacha na kudra za mungu ni speed ambayo dereva alikuwa akitembea. Soma research zote zinazoelezea ajali za barabarani utaona kuwa chanzo namba MOJA cha maafa makubwa ya barabarani ni SPEED,namba 2 ni UBOVU/HITILAFU ZA VYOMBO VYA USAFIRI na namba 3 ni UBOVU WA MIUNDOMBINU(in our case BARABARA)
kila kona ajaliajaliajali inasikitisha vibaya sana lakini hatuna jinsi! Mungu ndiye mwamuzi!jumlisha na mabasi ya kichina mabovumabovu,jamanimuda wenyewe mbaya kweli,saa 4 usiku!tatizo la sumry na hood na sumry ni 'ligi' za kijinga jinga,wanaenda mwendokasi kama wapo kwenye rally.ajali haiepukiki,ila angalau kampuni ya hood wamejiwekea utaratibu kila wakifika moro,lazima gari iingizwe garage kufanyiwa uchunguzi na matengenezo mbali mbali kama matairi,breki n.k!
Poleni sana wafiwa na mungu awasaidie majeruhi wapone haraka, mimi mara zote huwa siamini mwendo kasi ni chanzo cha ajali nyingi zinazotokea hapa nchini, kampuni ya sumri ni kati ya kampuni bora kabisa ya usafirishaji nchini nategemea watashiriki kikamilifu katika kusaidia wafiwa na majeruhi wote
Basi la kampuni ya Sumry likitokea Arusha kuelekea Mbeya, limepata ajali maeneo ya Igawa, kilometa 140 kutoka mji wa Mbeya. Basi hilo likiwa mwendo mkali, tairi la mbele lilipasuka na kupelekea kupinduka kwake. Watu 13 wamepoteza maisha yao papo hapo na wengine kujeruhiwa vibaya.
Habari zaidi zinasema waliokufa wameshafikia 15
Kuna haja ya kuongeza tochi za ma-polisi barabarani; na basi yote yafungwe Spidi-gavana kwa lazima ilo lisiwe ombi.