Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Naunga mkono 100% kwa vile ni kweli

ni kweli na kwa case ya Sumry nafikiri cause number 1 na 2 zinaplay a big role. Model na build ya basi zao ni unstable sana,anayehisi tofauti afanye practical research. Manouver ndogo tu basi linayumba kweli na drivers wao wako quite on the careless side. Nafikir kwao cash comes first...
 
Ndugu yangu labda hujui tu,lakini kwa taarifa yako kampuni hii ya Sumry ndio inaongoza kwa ajali kwa wastani ajali moja kila week.Nilikuwa mbeya last week pale stand ya Mbeya abiria wa mabasi ya Sumry wanaitwa Mbuzi wa Kafara...Nilishangaa na kuogopa sana.

ni kweli huyo hajui tu. Kinachochanganya wanoisifiya sumry ni vimaji soda na vibiskuti wanavyopatiwa njiani but in actually kwenye overall ubora wako chini. Hapa consider vitu kama equipment failure, accident rate per passengers transported, rate za driver related errors bado parefu...
 
Katika mahojiano na waandishi wa habari abiria walidai kuwa dereva walimwona mara kwa mara akitumia mmojawapo ya madawa ya kulevya na kwa kushirikiana yeye na makonda wake walikuwa wakipiga simu mara kwa mara kuuliza mahali walipo matraffic, hii ni hatari sana.
 
Poleni sana watanzania wote, lakini tujuilize, hii ajali imetokana na kupasuka kwa taili la mbele, tusilaumu kuwa gari ilikuwa speed sana, kwani hivi unadhani gari ikitembe KM 80 kwa saa toka Arusha kwenda mbeya itafika lini? na ni wa husika ndio walitoa hoizo leseni......,
 
kama mtanzania mwenye uchungu saana na maisha ya watanzania wenzangu ambao wanateketea na wengine kuwa vilema wa maisha yao yote ,hivi viongozi wetu kweli wameshindwa kabisa kuondoa hizi ajali????hakuna kweli namna ya kupunguza ajili??? maana kutokana na takwimu ambazo ninazo kwa miezi mitatu hivi kuna watu zaidi ya mia hivi wamepoteza maisha na hii takwimu nilizonazo mimi .....JAMANI WANA JF TUWASAIDIE HAWA WA MAGAMBA USHAURI
 
Swala la ajali ni zao la rushwa na matokeo ya kufanya kazi kwa mazoea.

Ikiwa wasimamizi wa sheria watabadilika ajali zitapungua sana,

Ukiangalia mfumo mzima wa unaosababisha hizi ajali unachangiwa hasa na;

1.Rushwa iliyokithiri katika upatikanaji wa leseni na wasimamizi wa sheria za barabarani

2.Shule za udereva sizizokuwa na viwango.

3.Wanaovunja sheria za barabarani kutokuchukuliwa hatua za uwajibikaji zadi ya kutoa rushwa na faini ndogo.

4.Magari mengi ni mabovu, pia na barabara.

5. Kampuni zenye magari yanayosababisha ajali kutokuchukuliwa hatua kali za kisheria.

6. Kutokujali thamani ya maisha kwa madereva, usalama barabarani na pia raia.

7. Uchovu wa madereva, na pia wengi hawalali usingizi wa kutosha.

8. Pia maslahi ya madereva ni mabovu

La mwisho usitegemee serekali kutatua tatizo hili zaidi ya matamko ya ki#$%^ge kwani nchi imewashinda katika kila sekta hili ni zao moja wapo ya failure. wao ajali hizi haziwahusu na ndio maana wanakimbilia magari ya kifahari kuziepuka.
 
Ili kuweza kujisaidia hii ishu;
1. Leadership needs to acknowledge that there is a problem (and not mapenzi ya Mungu).
2. Need to learn from what and how other developing countries are trying to combat this issue (it is a matter of concern for the UN and WHO also).
3. There should not be loopholes in obtaining a driving license. People should earn it and only then will they really appreciate the importance of safe driving.
4. There is alot of automatic cars in TZ, that makes it very easy for people to get on the road without really learning the road traffic rules.
5. People need to be educated (TV and Radio). I recently gave a lift to a teacher (imagine, a Teacher passing on knowledge to your kids, sisters, brothers) and on my advice to use the belt, she said "huku huwa hatufanyi hivyo"...I insisted, and had to help her on how to use it (she was carrying a baby too..., nilimpa lift kwa shingo upande).

If someone out there has time, they can work on an NGO/organisation that focusses on educating the population on road traffic awareness, am sure you will get support and funds not only internally but also externally (and dont tell me why I cant do it, am busy with other stuff but I can share my thoughts and direction if needed).

So Tambarare hii ishu siyo ya viongozi tu, inatuhusu sisi wote.
 
  1. KItty galore ndo maana umepewa nafasi uchangie jicho la kiroho ndo lipi hilo?? kwa maana miesiamini kuwa zote hizo ni ajali kwani ajali ni ile isiyo epukika lakini hizo ni uzembe mkubwa saana
 
  1. KItty galore ndo maana umepewa nafasi uchangie jicho la kiroho ndo lipi hilo?? kwa maana miesiamini kuwa zote hizo ni ajali kwani ajali ni ile isiyo epukika lakini hizo ni uzembe mkubwa saana
mungu saidia taifa lako linateketea
 
Nzoka mie nilibahatika kukaa ughaibuni ambako mtu ana displine na driving.....na sheria yao wanasema driving is like
previlage ambayo wanaweza kupa na kukunyang'anya pia sasa kwa nini serikali kupitia wizara husika wakafanya hili ili kupunguza hivyo vifo na majeruhi kabla mambo mengine hayaja fuatwa??
 
  1. KItty galore ndo maana umepewa nafasi uchangie jicho la kiroho ndo lipi hilo?? kwa maana miesiamini kuwa zote hizo ni ajali kwani ajali ni ile isiyo epukika lakini hizo ni uzembe mkubwa saana

Nimesema kwa jicho la kiroho kwa sababu, dunia hii ya sasa tunayoishi ina vituko na maajabu mengi. Kumekuwa na matukio ya ajali zisizoeleweka, chanzo ukisikia ni kupasuka kwa tairi ya mbele, ndio ajali nyingi za sasa zilivyo,na ni njia zile zile za kila siku. Barabara ya Moshi Arusha ilikuwa mbaya sana, wakazi wa maeneo hayo waliliangalia hili swala kwa jicho la kiroho, walichukua hatua ya kufanya maombi na mambo mengine kama hayo, je umewahi kusikia ajali za mfululizo tena maeneo hayo? japo zipo lakini sio maeneo yale yale kama ilivyokuwa Kikafu, Karanga na Nduruma.
Nadhani umenielewa
 
Kuna mambo yaliyo nje ya uongozi...mathalan ajali ni janga la kila mahali na halijalishi kwamba u kiongozi raia ama mtu wa kada yoyote...nadhani suluhisho ni sisi wenyewe kujifunza kutokana na mengi yaliyotukia nyuma...Dereva hawezi kuzidisha mwendo bila sababu ya msingi then abiria walinyamazie wakalalamikie viongozi!...Haya ya watu wasiokua na sifa ya udereva kuendesha vyombo vya moto ni tatizo sugu ambalo km mamlaka zinazohusika zikijiweka sawa walao itasaidia somo hili la kupunguza ajali zinazoepukika!
 
Ndugu,mimi ni dereva tena wa siku nyingi tu,nimeshapinduka na gari mara nne. Mara 2 nilikuwa peke yangu kwenye gari,mara 1 nilikuwa na mwenzangu lakini mimi nilikuwa naendesha na mara 1 nilikuwa nimepanda basi la abiria. Kuna tofauti kati ya CHANZO CHA AJALI na CHANZO CHA MAAFA MAKUBWA YALIYOPATIKANA BAADA YA AJALI KUTOKEA. Tairi inaweza kupasuka wakati wowote ukiwa unaendesha gari au hata kama gari imesimama. Pipe ya brake inaweza kupasuka au kuchomoka kwenye maungio yake wakati wowote dereva akiwa barabarani. Lakini kitakachoamua watu wafe kiasi gani na majeruhi wawe wangapi ukiacha na kudra za mungu ni speed ambayo dereva alikuwa akitembea. Soma research zote zinazoelezea ajali za barabarani utaona kuwa chanzo namba MOJA cha maafa makubwa ya barabarani ni SPEED,namba 2 ni UBOVU/HITILAFU ZA VYOMBO VYA USAFIRI na namba 3 ni UBOVU WA MIUNDOMBINU(in our case BARABARA)

Mkuu umechambua kiukweli kabisa. Tatizo watu wanapenda kukwepa ukweli kuwa speed ndo chanzo kikuu cha ajali. Bado tupo mbali kwenye kuziheshimu sheria za barabara,hizi ajali hazitushtui kabisa. Mi ningeshauri mabadiliko ya hii sheria ya barabara,watu wafungwe tu na adhabu ya faini iwe kwa makosa machache tu sio kila kitu faini.
 
Speed limit za hizo barabara za kwenda kutoka mkoa mmoja hadi mkoa mwingine ni ngapi?

Look at me now...naulizia mambo ya speed limit bongo! I must be out of my mind.
wouldn't say out of your mind, out of touch, rather. Speed limit zipo karibu kila mahala along the major highways. Na kuna traffic officers all along, from Dar to Mwanza, for example, njiani nii wazee kwa kwenda mbele, na nimeshakuwa pulled over any number of times. Na speed limit sio moja Tanzania nzima, inategemea na eneo.

Kama unaruka na Precession Air mwanzo mwisho obviously u wouldn't be privvy to these things. Na ni moja ya drawbacks za wataalam wa JF, wengi, kama si majority, ni out of touch.
 
wouldn't say out of your mind, out of touch, rather. Speed limit zipo karibu kila mahala along the major highways. Na kuna traffic officers all along, from Dar to Mwanza, for example, njiani nii wazee kwa kwenda mbele, na nimeshakuwa pulled over any number of times. Na speed limit sio moja Tanzania nzima, inategemea na eneo.

Kama unaruka na Precession Air mwanzo mwisho obviously u wouldn't be privvy to these things. Na ni moja ya drawbacks za wataalam wa JF, wengi, kama si majority, ni out of touch.

Ziko wapi hizo speed limit wewe? Labda uniambie kwenye karatasi lakini ukiniambia vibao labda huwaga vinakuwepo kwa msimu. Au kama vipo basi hata dhumuni lake halieleweki maana mimi huwaga naona vibao pembeni mwa barabara vinavyoonyesha namba fulani, kwa mfano 30, lakini havisemi hiyo 30 ni kitu gani.

Hahaa eti umeshakuwa pulled over. Yeah right...hata mimi nimeshakuwa pulled over mara kibao. Wanachofanya ni kuku flag usimamishe gari uliweke pembeni halafu wanakuja mnajadiliana. Hata kama ulikuwa unaendesha above the speed limit (which to many is unknown) wao hao unaowaita wazee hawana jinsi ya kujua ulikuwa una speed kiasi gani. I have never seen a traffic officer with a radar gun scanning oncoming cars anywhere in Tanzania. Have you?

Na kusema mimi ni out of touch, you are dead wrong. Mara kibao napanda Mombasa kutoka Ibadakuli kwenda Kolandoto na Kahama na njiani sijawahi hata siku moja kuona vibao vya speed limit. Usihukumu watu usiowajua ukadhani wote wamelowea majuu na kushindwa kurudi kwao.
 
watanzania wenzangu poleni tena kwa kuondokewa na wapendwa wetu takribani kumi na nne waliokuwa wanasafiri na basi la sumry kutoka arusha kwendam mbeya usiku wa juzi. kama vile tumezoea vifo hivi bado hatujifunzi kuwa ajali hizi zina mkono wa binadamu na wala siyo makusudi ya Mwenyezi Mungu.

leo nimesoma magazeti yakinukuu salam za rambi rambi alizopelekewa mkuu wa mkoa wa mbeya na rais wetu bwana JK. jk amesikitishwa sana na ajali hizo na tena amewaomba wafiwa wawe watulivu. tofauti na ajali nyingine za nyuma ambazo huwa anawaonya madereva kuwa makini hii hakufanya hivo. pengine wengine mtawaza kuwa rais wetu amechoshwa na ajali za kila mara, lakini ukweli jk anaujua yeye mwenyewe, na huu ndo ukweli;
  • mnamo wiki chache zilizopita, jeshi la polisi lilionya kuwa sumry waache kuendesha magari mabovu njiani ambayo magurudumu yake yameisha, lakini onyo hilo halikutekelezwa.
  • abiria waliopona katika ajali ile, wanaeleza jinsi dereva alivyokuwa anaendesha kwa mwendo kasi huku akibujia mirungi, na kila walipomwonya hakuwasikia, sikio la kufa halisikia dawa
  • kila kituo cha polisi walikopiata, basi lilikuwa linakamatwa na polisi lakini dereva na kondakta R.i.p walikuwa wakiitwa nyuma ya basi na kumalizana na polisi.
  • ingawa miaka ya nyuma safari za mabasi zilikuwa zinaishia saa nne usiku, sheria hii iliondolewa na jshi la poisi kwa amri za mamlaka ya juu, hasa kutokana na mabasi ya sumrny na hood kumilikiwa na wanasiasa mafisadi wa nchi hii.
kwa hiyo jk kama tulivhomzoea, rais pekee katika sayari hii, mwenye majeshi, mahakama., na executive powers ambaye anagwaya kwa mafisadi wanaonyelelea nafasi yake, ambao sasa wako mlangoni kusambaratisha chama chake na kumfanya gorbachev wa afrika mashariki hawezi kuona haya kwa sababu:

mabasi ya summry yanamilikiwa na mama zakhia mehji, huyu ndo yule mama aliyeshirikiana na fisadi namba wani marehemu bilali wakakomba akaunti zote za EPA, sasa wanawafunga akina maranda wakati rafikia zake akina rostam na kagoda bado anasita kuwaleta pale kisutu

kampuni hiyo ya sumry ilikuwa inaingiza magari nchini na kuyasajili kama pikipiki kukwepa ushuru, mama meghji nafahamu sana hili, walikamata machache pale mbeya, laikini wale maofisa wa TRA waliokamata yale magari wanajua kilichowatokea.
askari waliokataza haya magari yasitembee, hawana uwezo wa kufua dafu mbele ya jk kupitia kwa mama meghji mweka hazina mpya wa ccm, ambaye ni mmiliki wa sumry asiyetaka kununua matairii ya mabsi yake bali kuchuna nauli ya watanzania, waendelee kufa wakati yeye akinyanyua mkono na kusema ccm juu!! ju!!! zaidi.


ni wazi kuwa hawa wote ni mafisadi, NI WAKATI MUAFAKA WA KUANDAA NA KUSHIRIKI SIKU YA HASIRA DSM! NA SIKU YA HASIRA TANZANIA, TUNA KILA SABABU. TUTOE HASIRA ZETU KWA PAMOJA NA KWA PAMOJA TUSHINDA UDHALIMU HUU.
 
Madereva wa haya mabasi kiwauliza kwa nin i hawaheshimu trafiki wanakwambia mabosi wao walishamalizana na wakubwa na kuwa hata wakiua hawalali ndani
 
Madereva wa haya mabasi kiwauliza kwa nin i hawaheshimu trafiki wanakwambia mabosi wao walishamalizana na wakubwa na kuwa hata wakiua hawalali ndani

Nilidhani tunapewa huduma ya usafiri, kumbe na kifo pia kinakuwa kimeandaliwa kwa sababu mabos wameshamalizana na wakubwa. Inatia simanzi sana.
 
Back
Top Bottom