Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Poleni sana wafiwa na mungu awasaidie majeruhi wapone haraka, mimi mara zote huwa siamini mwendo kasi ni chanzo cha ajali nyingi zinazotokea hapa nchini, kampuni ya sumri ni kati ya kampuni bora kabisa ya usafirishaji nchini nategemea watashiriki kikamilifu katika kusaidia wafiwa na majeruhi wote
 
Poleni sana wafiwa na mungu awasaidie majeruhi wapone haraka, mimi mara zote huwa siamini mwendo kasi ni chanzo cha ajali nyingi zinazotokea hapa nchini, kampuni ya sumri ni kati ya kampuni bora kabisa ya usafirishaji nchini nategemea watashiriki kikamilifu katika kusaidia wafiwa na majeruhi wote

Ndugu,mimi ni dereva tena wa siku nyingi tu,nimeshapinduka na gari mara nne. Mara 2 nilikuwa peke yangu kwenye gari,mara 1 nilikuwa na mwenzangu lakini mimi nilikuwa naendesha na mara 1 nilikuwa nimepanda basi la abiria. Kuna tofauti kati ya CHANZO CHA AJALI na CHANZO CHA MAAFA MAKUBWA YALIYOPATIKANA BAADA YA AJALI KUTOKEA. Tairi inaweza kupasuka wakati wowote ukiwa unaendesha gari au hata kama gari imesimama. Pipe ya brake inaweza kupasuka au kuchomoka kwenye maungio yake wakati wowote dereva akiwa barabarani. Lakini kitakachoamua watu wafe kiasi gani na majeruhi wawe wangapi ukiacha na kudra za mungu ni speed ambayo dereva alikuwa akitembea. Soma research zote zinazoelezea ajali za barabarani utaona kuwa chanzo namba MOJA cha maafa makubwa ya barabarani ni SPEED,namba 2 ni UBOVU/HITILAFU ZA VYOMBO VYA USAFIRI na namba 3 ni UBOVU WA MIUNDOMBINU(in our case BARABARA)
 
Jana Usiku wa Saa 4.45 basi la Sumry lililokuwa likitokea Arusha kwenda Mbeya limepata ajali na kuuwa abiria 15 papo hapo,ajali iliktokea eneo la Igawa Mbarali Mbeya!
Sasa jamani mbona swala la Vidhibiti mwendo linakuwa kama 'politiki' wakati maisha ya ndugu zetu yanapotea na tuliobaki tupo hatarini,manake mabasi Yaliyopo ni yaleyele na ndo twategemea kuyapanda kwa safari zetu na tatizo la mwendo kasi ndio chanzo namba moja cha ajali TZ!
AU utatuzi wa jambo hili ni mpaka Urudishwe kwa wananchi na Makamanda ndio kieleweke!
 
Mkuu hii habari hapa si maala pake! Lakin kwa nin ajari zimezidi njia hyo?
 
Taarifa kutoka Mkoani Mbeya ni kuwa bus la Sumry likitokea Aruuha kwenda Mbeya liimepata ajali na watu 15 kufa papo hapo huku majeruhi waliolazwa ni 20.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Advocete Nyombi amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka taili la mbele na mwendo kasi na kupelekea basi hilo kukosa mwelekea na kupinduka.

Dereva wa basi hilo ni kati ya watu waliofariki dunia na kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa 4.45 usiku.
Majina ya waliokufa ktk ajali hiyo na majeruhi utayapata pindi yatakapo tajwa na kutambuliwa .

Chanzo:Blog ya Francis Godwin
 
BREAKINGNEWS BASI LA SUMRY LAUA 15 PAPO HAPO

Habari zinasema kuwa waliokufa ajali ya basi la Sumry ni watu 15 huku majeruhi waliolazwa ni 20 . Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Advocete Nyombi ameuambia mtandao huu kuwa chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka taili la mbele na mwendo kasi na kupelekea basi hilo kukosa mwelekea na kupinduka. Dereva wa basi hilo ni kati ya watu waliofariki dunia na kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa 4.45 usiku. Wakati basi hilo likitokea Arusha kwenda Mbeya .Majina ya waliokufa ktk ajali hiyo na majeruhi utayapata pindi yatakapo tajwa na kutambuliwa

Kwa hisani ya blog ya Francis Godwin
 
Nimeambiwa na mmoja wa kondakta wa Sumry kwamba watu 17 walikufa papo hapo na majeruhi waliobaki wapo kwenye hali mbaya. Maiti wapo Hospital ya Rufaa Mbeya. Chanzo cha ajali ilikuwa ni tairi la mbele kupasuka lakini maafa makubwa yametokana na mwendokasi wa dereva. Gari ilipinduka na kutambaa kwa mgongo matairi yakiwa juu mwendo wa mita kama 500.

Dereva alikata roho papo hapo.Kama gari ingekuwa mwendo mdogo maafa yasingekuwa makubwa kiasi hicho hata kama tairi ilipasuka. Inasikitisha sana roho za watu wasio na hatia kuondolewa kikatili kila siku.

Sijui kama tuna chombo makini cha kusimamia usalama barabarani.
muda wenyewe mbaya kweli,saa 4 usiku!Tatizo la sumry na Hood na sumry ni 'ligi' za kijinga jinga,wanaenda mwendokasi kama wapo kwenye rally.Ajali haiepukiki,ila angalau kampuni ya Hood wamejiwekea utaratibu kila wakifika moro,lazima gari iingizwe garage kufanyiwa uchunguzi na matengenezo mbali mbali kama matairi,breki n.k!
 
Inasikitisha sana. Inasikitisha kwa sababu watu wamepoteza maisha yao lakini pia inasikitisha kwa sababu ni kama vile Watanzania hatujifunzi.

Sijui hizi ajali hadi ziue watu kiasi gani ndo tupate ufunuo kuwa aha kumbe zinatumaliza hivi! Ukiangalia mabasi mengi ya abiria Tanzania ni makuukuu mno. Ingekuwa kwenye nchi zilizoendelea yangekuwa yameshapigwa marufuku kuwa barabarani na kubeba abiria.

Sasa jumlisha huo ukuukuu na mwendo kasi ambao madereva huendesha unachopata ni majanga kama haya. Lakini licha ya ukuukuu wa hayo mabasi kinachosababisha ajali zaidi ni mwendo kasi usio hata na maana. Kwa ujumla watu Tanzania hawana ustaarabu kabisa wa barabarani. Wanaendesha kama vile hawajali maisha yao.

Aaah ngoja niishie hapa maana nisije kuambiwa huo ndo utamaduni wa Mtanzania na mimi najifanya najua sana. Pole zao waliofiwa na walioumia.

Umesema kweli Nyani, na hawa madereva wa magari ya Mbeya wanasifika kwa kuendesha mabasi kwa mwendo wa kasi... hata madereva wa Arusha na Moshi wanawaogopa sana hawa madereva wa Mbeya kwa mwendo.

Tusipotafuta dawa watatumaliza hawa
 
Poleni sana kwa wahanga wa ajari hii ila kuepukana na ajari za kizembe ni pale wanausalama wanahusika watakuwa wawajibakaji na kushilikiana na abiria.
 
Mungu awalaze mahali pema peponi wote waliokufa
na majeruhi tuwaombee wapone haraka
 
Umesema kweli Nyani, na hawa madereva wa magari ya Mbeya wanasifika kwa kuendesha mabasi kwa mwendo wa kasi... hata madereva wa Arusha na Moshi wanawaogopa sana hawa madereva wa Mbeya kwa mwendo.

Tusipotafuta dawa watatumaliza hawa
Haswaa,juzi tu nilipanda basi la happy nation nikielekea mbeya,mpaka naingia stendi kuu sikuamini kama tumefika salama,lazima ile basi ina injini ya scania lori!
 
Kwa alieangalia taarifa ya habari ya juzi Ijumaa TBC 1, basi la Sumry lilijaza abiria kupita kiasi mpaka kufikia hatua ya waliosimama kuwa wengi kuliko waliokaa, abiria wakatoa taarifa polis na kweli gari lilisimamishwa, cha ajabu askar aliangalia tu na kuruhusu gari kuendelea na safar, leo yametokea maafa kwa gari hilo hilo tena, kwa nini hii kampun isifutiwe leseni?????

aya yote tukisema yanaletwa na utawala mbovu wewe na ID kama yako mko mbele kupinga,tufanyeje sasa,acha tu tukose wasimamizi makini na taifa liangamie. We unadai trafiki kashindwa kulikamata je unajua umiliki wa kampuni ile?
 
Ajali imekuwa kama wimbo wa taifa. Wamiliki wa magari wawajibishwe inapotokea ajali za kizembe zinazosababishwa na madereva wao. Mmiliki wa gari anaweza kumbana dereva wake asikimbie.
 
aya yote tukisema yanaletwa na utawala mbovu wewe na ID kama yako mko mbele kupinga,tufanyeje sasa,acha tu tukose wasimamizi makini na taifa liangamie. We unadai trafiki kashindwa kulikamata je unajua umiliki wa kampuni ile?

mbunge
 
BREAKINGNEWS BASI LA SUMRY LAUA 15 PAPO HAPO

Habari zinasema kuwa waliokufa ajali ya basi la Sumry ni watu 15 huku majeruhi waliolazwa ni 20 . Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Advocete Nyombi ameuambia mtandao huu kuwa chanzo cha ajali hiyo ni kupasuka taili la mbele na mwendo kasi na kupelekea basi hilo kukosa mwelekea na kupinduka. Dereva wa basi hilo ni kati ya watu waliofariki dunia na kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa 4.45 usiku. Wakati basi hilo likitokea Arusha kwenda Mbeya .Majina ya waliokufa ktk ajali hiyo na majeruhi utayapata pindi yatakapo tajwa na kutambuliwa

Kwa hisani ya blog ya Francis Godwin

mlachake!!!!!!!taili-tairi--naomba tuwe makini
 
Back
Top Bottom