Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Haya mabasi ya SUMMRY inabidi kuyasusa kabisa kama serikali imeshindwa kuyadhibiti, wale ambao mshawah kuyapanda kutoka arusha mtakuwa mashahidi kuwa ni mabovu japo kwa ndani yanaonekana mapya.
Mbona sijawahi kusikia ajali ya HOOD kuuwa abiria wake? labda sikumbuki mtu anieleze hapa... HOOD wameanza safari ndefu za arusha mbeya kwa miaka mingi sasa na haijawah kutokea ajali akauwa abiria, hili linanifanya nihoji kuhusu hawa SUMMRY ambao mwaka hauishi utasikia wameua abiria... ni uzembe? au ni nini?
 
Ziko wapi hizo speed limit wewe? ... naona vibao pembeni mwa barabara vinavyoonyesha namba fulani, kwa mfano 30, lakini havisemi hiyo 30 ni kitu gani.

...wazee hawana jinsi ya kujua ulikuwa una speed kiasi gani. I have never seen a traffic officer with a radar gun scanning oncoming cars anywhere in Tanzania. Have you?
Sio lazima kibao kisema "hii namba ni kikomo cha mwendokasi - kilomita 50 kwa saa!" Sijui umetembea wapi na wapi zaidi ya "Mombasa kutoka Ibadakuli kwenda Kolandoto na Kahama", lakini nchi nyingi kama Ujerumani, Australia, Finland, USA, vibao vyao vya mwendokasi ni kama hivi:

120px-Trucks_speed_55_sign.svg.png

Marekani
z274.gif

Australia

z278.gif

Ujerumani
z279.gif


info_15.gif

Finland

Vibao vyote hivyo havisemi "speed limiti ndio hii." Sasa usikandye kitu tu kwa sababu kiko Bongo kumbe ni vitu vina exist kimataifa. Na kama hujui kwamba polisi Bongo wanatumia radar speed detection basi unakuwa commentator wasiwasi, kwa lugha ya kiungwana, wa masuala ya udhibiti wa mwendokasi kwa sababu uko out of touch.
 
Mkuu haya magari sio ya mama Meghji ya yanamilikiwa na Sumry the Tycoon mwenyewe ukitaka kumjua nenda Sumbawanga labda kidogo kukusaidia katika magari hayo kuna magari yaliyopenyezwa ya Riz1.
 
Mkuu haya magari sio ya mama Meghji ya yanamilikiwa na Sumry the Tycoon mwenyewe ukitaka kumjua nenda Sumbawanga labda kidogo kukusaidia katika magari hayo kuna magari yaliyopenyezwa ya Riz1.
Mbona wafanyakazi wake wanasema anaubia na wakubwa hata akishitakiwa kesi zake zinzishia hukohuko juu, na askari wa barabarani wengi wanatolewa kwa ajili ya kukamata magari yao.Ndiyo maana madereva wake ni wababe na hawana heshima hata kidogo.
 
Madereva wa haya mabasi kiwauliza kwa nin i hawaheshimu trafiki wanakwambia mabosi wao walishamalizana na wakubwa na kuwa hata wakiua hawalali ndani
Hayo ndiyo majibu yao,lakini hicho kiburi chao kina mwisho mpaka walidiriki kuandika katika mabasi yao summsry dora,wakiwa na maana kwamba dora iko mikononi mwao.
 
Hapa tunaongelea ajali na jinsi ya kuzizua na uzembe wa watawala wetu katika kutatua matatizo au tuna orodhesha wamiliki wa vyombo vya usafiri na wabia wao!?

Mali ya wizi zinaisha kwa wizi, scandnavia Bus service ipo wapi?! au imeamia Kenya?
 
Nilidhani tunapewa huduma ya usafiri, kumbe na kifo pia kinakuwa kimeandaliwa kwa sababu mabos wameshamalizana na wakubwa. Inatia simanzi sana.


Kuna siku nilipanda basi la rangi nyekundu tupu kwenda Mbeya weee sikupata usingizi njia nzima, nilikoma sikuyarudia kuyapanda yale tena hadi leo!
 
Basi la Abood limeanguka usiku huu ktk sehemu ijulikanayo kama MlimaNyoka karibu sana na mji wa Mbeya: inasemekana hakuna aliyekufa ila abiria 32 wamejruiwa vibaya, lilikuwa linatoka Dar kuelekea Mbeya.
Source: Festus Sikagonamo via ITV saa4 usiku..
 
Hakuna vifo ila majeruhi zaidi ya 32 akiwemo dereva wa bus hilo
 
Wadau taarifa ya dharura ITV ni kuwa bus la Abood limeanguka ktk eneo la mlimanyoka takribani km 15 kutoka Mbeya mjini. Zaidi ya watu 30 wamejeruhiwa vibaya sana. Nimeipata kwa ufupi tu, bus lilikuwa likitokea Dar. Ee Mungu inusuru TZ.
 
Hizi ajali ni sababu ya uzembe wa madereva, uchakavu wa vyombo vya usafiri, na tabia sugu ya trafiki ya kuendekeza rushwa.
Uswahilini wanamsingizia Rama mla watu kuwa eti ndiye chanzo cha ajali zote hapa nchini
 
Nakiri ajali zimekuwa nyingi sana sasa, lakini basi hili la Abood sijui ni mara ngapi limepata ajali ndani ya miezi 12 iliyopita. muda umefika sasa kwamba kila kampuni ya mabasi iwekewe record ya ajali inapotekea ajali zinajirudia rudia kama hawa wakina abood basi kampuni ifutiwe leseni. haya makampuni yamepewa leseni za kufikisha watu salama huko wanakoenda na sio kuuwa.
 
Nakiri ajali zimekuwa nyingi sana sasa, lakini basi hili la Abood sijui ni mara ngapi limepata ajali ndani ya miezi 12 iliyopita. muda umefika sasa kwamba kila kampuni ya mabasi iwekewe record ya ajali inapotekea ajali zinajirudia rudia kama hawa wakina abood basi kampuni ifutiwe leseni. haya makampuni yamepewa leseni za kufikisha watu salama huko wanakoenda na sio kuuwa.

Uko sahii kiongozi: ajari zimedi kwakweli.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mapenzi ya Mungu

hapa mkuu ni uzembe tu...Mungu alituumba tuishi maisha mema,marefu na yenye baraka ila kwa kukosa maharifa na uvivu wetu wa kufikiri ndo maana haya yanatokea alafu tunasema eti ni mapenzi ya Mungu,Mungu yupi huyo?????
 
Back
Top Bottom