Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Zaidi ya kupoteza mali, kuna mtu alipoteza maisha?
Pole kwa mwenye mali, labda BIMA watamrejeshea.
Lakini mwaka huu is the worst kwa ajali nadhani.
Au reporting ndo imeongezeka?
 
Poleni, ila sijapata chanzo halisi cha ajali, tuwe na kawaida ya kukagua magari yetu.
 
Hii sukari ndani a kontena ilikuwa imechanganyika na petroli au ni kawaida ya sukari kuwaka moto kiasi hicho? Utafiti ufanyike, inawezekena ajali nyingi za moto zinasababishwa na sukari!!
 
Polen saana kwa msiba wote tulioguswa.Hii si ndo ajali ya Mhe.Salome?Wasiwasi wangu wasije wakaendelea kuhusisha majanga haya na yaliyotokea bungeni na hasa kama alichangia kwenye hoja ya kumtoa mheshimiwa Z nje.RIP
 
Sijui hata tukimbilie wapi? Ee Mwenyezi Mungu tunaomba utunusuru na hizi ajali
 
Naona mlango wa Container uko wazi na ndani kuna moto mkali.
Magunia ya sukari yawakayo moto yako wapi?

Na walifungua milango ya kontena ili iweje?
 
Huo moto ulikuwa balaa, nafikiri Mjengwa alipiga hizi picha anaweza kueleza kwa undani kidogo kilichotokea hapo. Kutokana na shughuli naona ametingwa kidogo lakini akiona haya maswali atayafanyia kazi jinsi alivyoona.
 
Jamani mimi naona kuna kila dalili kwamba hii ajali ni ya "kupanga" ....... jamaa "wamekomba" sukari, halafu wakapiga kibiriti kintena.
 
Utaratibu wa njia tatu umesababisha vifo 11

MBUNGE JIMBO LA SAME MASHARIKI

na Irene Mark na Rahel Chizoza, Dodoma

MBUNGE wa Same Mashariki, Anne Malecela (CCM), ameitaka serikali kuweka wazi idadi ya vifo vilivyotokana na ajali zinazobabishwa na utaratibu wa njia tatu jijini Dar es Salaam.

Aidha, mbunge huyo alisema hakubaliani na utaratibu huo uliowekwa na serikali kwa lengo la kupunguza msongamano wa magari na foleni katikati ya jiji hilo na kwamba haujasaidia kupunguza tatizo.

Naibu Waziri wa Usalama wa Raia, Mohamed Abood, katika majibu yake, alisema baada ya kuanza kwa utaratibu wa njia tatu, foleni za magari zimepungua katika jiji hilo.

Aidha, alibainisha kuwa kati ya Mei na Oktoba 29, mwaka huu, jumla ya ajali 107 zilizosababisha vifo vya watu 11 zilitokea baada ya kuanza kwa utaratibu wa njia tatu kutokana na mwendo kasi na uzembe wa madereva kutofuata sheria za barabarani.

Abood alisema utaratibu wa njia tatu hasa nyakati za asubuhi na jioni, umezoeleka jijini Dar es Salaam na kumtaka mbunge huyo kuondoa hofu, huku akiwaomba madereva na watumiaji wengine wa barabara zinazohusika na utaratibu huo kuwa makini.

Alisema jumla ya sh bilioni 10 zimetengwa na serikali kwa ajili ya kuboresha utaratibu huo kwa muda wakati wakitizama namna ya kuondoa tatizo la msongamano na foleni za magari.

Hata hivyo, majibu hayo hayakumridhisha mbunge huyo na kueleza kuwa utaratibu wa njia tatu haujazoeleka wala kusaidia kupunguza foleni badala yake umeongeza idadi ya ajali na vifo huku akiitaka serikali kubuni mbinu mpya.

Mwanzo mwa mwaka huu, Waziri Mkuu Edward Lowassa, aliagiza uwepo utaratibu wa njia tatu katika baadhi ya barabara jijini Dar es Salaam, ili kupunguza msongamano na foleni, hasa wakati wa asubuhi na jioni.

Barabara zinazohusika na utaratibu huo ni Morogoro na Ali Hassan Mwinyi.
 
Ajali 107 na watu 11 wamepoteza maisha yao ktk muda usiofika miezi sita!..
Yaani adha inazoeleka kiasi kwamba agizo la Waziri mkuu linajengewa sheria za barabarani...
Nina hakika kabisa kama ilivyokuwa agizo la Mitumba kama vazi la dharura, leo miaka 20 imekuwa kawaida kabisa na tena imejenga hekalu east Afrika nzima tunasifika. magonjwa yanayotokana na mavazi hayo hata kama watu wanakufa hayana nafasi kabisa.
Ama kweli ndege inapaa/ Itapaa.
 
Ajali 107 na watu 11 wamepoteza maisha yao ktk muda usiofika miezi sita!..
Yaani adha inazoeleka kiasi kwamba agizo la Waziri mkuu linajengewa sheria za barabarani...
Nina hakika kabisa kama ilivyokuwa agizo la Mitumba kama vazi la dharura, leo miaka 20 imekuwa kawaida kabisa na tena imejenga hekalu east Afrika nzima tunasifika. magonjwa yanayotokana na mavazi hayo hata kama watu wanakufa hayana nafasi kabisa.
Ama kweli ndege inapaa/ Itapaa.

Tatizo ni kuwa baadhi ya viongozi wetu huwa wanakurupuka sana kutoa maamuzi bila kufuata taratibu za kitaalamu. Na bado, tutashuhudia mengine menngi tu.
 
Ndio matatizo ya kukurupuka haya, watu wanakufa tunaambiwa foleni zimepungua wat a sh.t

Bora tuchelewe lakini tufike, huu utaratibu wa njia tatu ni mgumu kweli binafsi nimekoswakoswa zaidi ya mara mbili kugongwa, kibaya zaidi hakuna alama za kutosha za tahadhari hasa kwa madereva wanaotoka ktk fider roads, mamvi nae anachemka mno yaani noma tupu...
 
Huyu EL anataka kuwaletea mvua ya Thailand unafikiri kichwa chake kiko sawa? Dar ina watu na magari mangapi? Hili swala ni rahisi sana akitumia wataalam wazawa ambao wamesomeshwa kwa pesa za serikali kulifanyia kazi. HEBU AWAULIZE?
 
Tangu mwanzo alipotangaza utaratibu huo nilikuwa na mashaka, huu ni uamuzi wa kitaalamu au wa kisiasa? Kuna wataalamu wa fani hiyo waliotoa ushauri huo? Walifanya wapi utafiti na ripoti iko wapi? Maana unapotaka kubadilisha utaratibu lazima kuwe na utafiti uliofanyika na kuonesha kwamba intervention inayofaa ni kadha wa kadha, na ukilinganisha utaratibu A na B, basi A ni bora zaidi kwa asilimia kadhaa, hapo ndipo uamuzi huchukuliwa. Uamuzi huo uliegemea kwenye ushahidi gani wa kiutafiti? Yani tunafanyiana masikhara tu!
 
one day nilishuhudia ajali moja mbaya saaanaa machoni pangu pale mrorogoro road...nikalaani hiyo njia tatu thing...na aliyetoa wazo hilo na akasupportiwa..yeye ana wasi wasi gani??hata akienda chooni njia yazuiwa kwanza...yafungwa..mashushu kumi wamwagwe ndipo apite..so sio yeye wala familia yake yajua uchungu huo..unless mmoja wapo ya family member ikimpata au waziri ndipo kilio chetu kitasikika..better late than never jamanii
 
Mtikila hapa kapata kesi ya kumshitaki Lowasa. Yaani maisha ya watu yanapotea hivi hivi kwa sababu ya amri za kisiasa?
Hivi viongozi wetu huawa hawana washauri jamani? maana najua watalamu tunao wengi tuu. yaani watu waache kukarabati infrustructure watu wafe wao wanasema tusiwe na wasiwasi? Huku ni kuonyesha jinsi maisha ya mwananchi yasivyothaminiwa na viongozi wetu.
 
Back
Top Bottom