Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Sie tunoona madhara yake tuwape njia m-badala, tusiwalaumu; nia yao ilikuwa njema, ila utekelezaji kama haufikii kile walichotegemea kupata warudi kujipanga upya nasi tuwasaidie mawazo mapya

Pinokyo,

Tunahitaji wazalendo kama wewe, hoja nzuri sana!

Lakini siku zote najiuliza swali hili!

Kwa kuwa mwananchi hawana raslimali za kufanya lile wanalotaka serikali ilifanye,,, na kwa kuwa mwananchi wanaweza kutoa mawazo tu kwa mambo ambayo yanahitaji rasilimali na sio kuyafanya wao!
Je kama mwananchi anatoa mawazo kama hivi tutoavyo hapa JF, si mwananchi atakuwa ametenda wajibu wake?


Huko nyuma kwenye thread hii hii, nilishasema nini kilitakiwa kifanyike kabla ya zoezi lenyewe!!! sasa kwa kuwa havijafanyika basi sasa vifanyike...


Hata hivyo sina imani kama waheshimiwa hao wanaona maoni yetu,,, maana idara kama ya polisi ambapo bado mfupi uliopita (sina hakika sasa) walikuwa wakiandikia mifuko ya sementi, je wataweza kuingia humu kwenye mitandao waone maoni yetu.

Ndio tunarudi kulekule kwamba tuwe wabunifu katika kupeleka ujumbe,,, mfano,,, maoni yanayotolewa yanaweza forwardiwa kwa waheshimiwa kamshina wa usalama barabarani... otherwise sisi kama raia tutakuwa hatujatekeleza wajibu wetu kisawasawa.
 
Kilitime (na wewe ni memba wa bonanza hapo Uwanja wa Kinesi?) na AmazingFriend nawasoma...shukran!

Hata hivyo, mtakubaliana nami kuwa moja ya sehemu yenye ajali nyingi kabisa kwa waenda kwa miguu (hata kabla ya kuanzisha "utaratibu wa Lowasa") ni Manzese (kati ya Argentina na Urafiki)? Kwa nini?

Isitoshe barabara zetu karibu zote ni za njia moja (single lane) hivyo watu wanapaswa wawe wamezoea pia kuangalia kulia-na-kushoto kabla ya kuvuka!
 
Kuna tabia fulani mbaya sana kwa upande wa waendeshaji magari na watembea kwa mguu pale Dar.

(a) Waendesha magari wana tabia ya kudhani kuwa magari tu ndiyo yana haki ya kutumia barabara. Ni mara chache sana kuona madareva wakiwa waangalifu kwa wapita njia kama vile kusimama makusudi ili kuruhusu wapita njia.

(b) Pamoja na hatari zitokanazo na kiburi cha madereva (a) hapo juu, wapita njia wengi wanakatisha barabara sehemu yoyote ile. Kwa mfano, ingawa serikali ilijenga daraja pale Manzese, bado watu walikuwa wakikitisha sehemu yoyote ya barabara mpaka serikali ikalazimika kujenga uzio wakati ule, sijui kama uzio huo bado upo.

Matatizo haya ya madereva na wapita njia nadhani ndiyo yanayochangia ajali zaidi ya mpango wenyewe wa Waziri Mkuu.

Njia mojawapo ya kusaidia kupunguza matatizo haya ni kujenga pedestraian crossing nyingi barabarani na kuwawekea madereva alama ya STOP kwenye hizi crossings. Madereva wafundishwe na kusistizwa kuwa ni lazima wasimame kwenye hizi pedestrian crossing hata kama hakuna mpita njia; halafu wapita njia wafundishwe pia kuwa wasikatishe barabara sehemu yoyote isipokuwa tu pale penye pedestrian corssing.

Mafunzo haya yaambatane na adhabu kali. Wapita njia wakikatisha barabara sehemu ambayo haina pedestrian crossing washitakiwe kwa makosa ya kujihatarishia maisha yao, na madereva wasiosimama kwenye pedestrian corssing pia washitakiwe kwa makosa ya kughaili usalama wa wapita njia.
 
Hata hivyo, mtakubaliana nami kuwa moja ya sehemu yenye ajali nyingi kabisa kwa waenda kwa miguu (hata kabla ya kuanzisha "utaratibu wa Lowasa") ni Manzese (kati ya Argentina na Urafiki)? Kwa nini?

Nakubaliana na wewe manzese tulipoteza watu wengi sana, siku hizi imepungua au kuondoka kabisa baada ya serikali kuamua kuwatreat wananchi wasiojiheshimu kama ng'ombe (yaani kulivyowekwa uzio si unajua wananchi wetu)

Isitoshe barabara zetu karibu zote ni za njia moja (single lane) hivyo watu wanapaswa wawe wamezoea pia kuangalia kulia-na-kushoto kabla ya kuvuka!

Si unajua ndio hivi karibuni tumeweza kupeleka watoto shule ya msingi by >97% kwa maana before watu wengi hawakuwahi kusoma kitabu cha ROZA na MUSA wakifuka barabara kwenye somo la "USALAMA BARABARANI"

Nchini tunamadereva hata hawajui nini maana ya alama ya barabarani "Tri-angle yenye alama ya mshangao ndani"
 
tembea uone,nchi za wenzetu wameweka fenci kwenye barar kuzuia watu wasiingie kwenye barbara na kuna sehemu maalumu za watu kuvuka kwa miguu.wanatunia taaau alama za pundamilia,nimeona barabara ya morogogo wameweka sijui ni hapo manzese au ni yote.
 
tembea uone,nchi za wenzetu wameweka fenci kwenye barar kuzuia watu wasiingie kwenye barbara na kuna sehemu maalumu za watu kuvuka kwa miguu.wanatunia taaau alama za pundamilia,nimeona barabara ya morogogo wameweka sijui ni hapo manzese au ni yote.

Katibu tarafa,

ndio mkuu, panaitwa manzese Argentina hadi Tip Top,

Karibu nyumbani; kutakupatia ugali na maharage na kuku wanaohifadhiwa kwa kuwekwa kwenye gongo... watamu muno
 
Kuna tabia fulani mbaya sana kwa upande wa waendeshaji magari na watembea kwa mguu pale Dar.

(a) Waendesha magari wana tabia ya kudhani kuwa magari tu ndiyo yana haki ya kutumia barabara. Ni mara chache sana kuona madareva wakiwa waangalifu kwa wapita njia kama vile kusimama makusudi ili kuruhusu wapita njia.

(b) Pamoja na hatari zitokanazo na kiburi cha madereva (a) hapo juu, wapita njia wengi wanakatisha barabara sehemu yoyote ile. Kwa mfano, ingawa serikali ilijenga daraja pale Manzese, bado watu walikuwa wakikitisha sehemu yoyote ya barabara mpaka serikali ikalazimika kujenga uzio wakati ule, sijui kama uzio huo bado upo.

Matatizo haya ya madereva na wapita njia nadhani ndiyo yanayochangia ajali zaidi ya mpango wenyewe wa Waziri Mkuu.

Njia mojawapo ya kusaidia kupunguza matatizo haya ni kujenga pedestraian crossing nyingi barabarani na kuwawekea madereva alama ya STOP kwenye hizi crossings. Madereva wafundishwe na kusistizwa kuwa ni lazima wasimame kwenye hizi pedestrian crossing hata kama hakuna mpita njia; halafu wapita njia wafundishwe pia kuwa wasikatishe barabara sehemu yoyote isipokuwa tu pale penye pedestrian corssing.

Mafunzo haya yaambatane na adhabu kali. Wapita njia wakikatisha barabara sehemu ambayo haina pedestrian crossing washitakiwe kwa makosa ya kujihatarishia maisha yao, na madereva wasiosimama kwenye pedestrian corssing pia washitakiwe kwa makosa ya kughaili usalama wa wapita njia.

Kichuguu Mawazo,

Mazuri, lakini unajua hata kufundisha/kuelimisha mtu lazima awe ameandaliwa kupokea mafundisho/elimu yako,,,

Madereva wetu ziro, Askari wa Barabara ziro, Wananchi wetu Ziro, a chemical reaction btn those substance above will produce a reactor of killing mass people.

Nifagilie kwa kujua chemistry kuliko wataalamu wa nuclear reactor za Iran!
 
Kichuguu Mawazo,

Mazuri, lakini unajua hata kufundisha/kuelimisha mtu lazima awe ameandaliwa kupokea mafundisho/elimu yako,,,

Madereva wetu ziro, Askari wa Barabara ziro, Wananchi wetu Ziro, a chemical reaction btn those substance above will produce a reactor of killing mass people.

Nifagilie kwa kujua chemistry kuliko wataalamu wa nuclear reactor za Iran!

Mzee Kilitime unanisema mimi au??? (JOKE!!!).
 
You have all overlooked one important factor.Which/whose children go to school walking???Amy or Kayumbo ?
There are traffic laws in the country, if they are changed even for a minute a Govt Notice ( GN ) has to be issued.Was that ever done.
 
Tuwe fair hapa; Lowassa alikutana na jopo lililohusisha wataalam, polisi na wawekezeja katika usafirishaji; ni jopo hilo ndilo lilifikia maamuzi haya, siyo maamuzi ya Lowassa binafsi! hao wahusika wote wanatakiwa kukaa tena kwa upya kuangalia kama hilo zoezi walilopa muda wa majaribio linafaa au halifai, watizame njia m-badala kama inalazimu kufanya hivyo. Sie tunoona madhara yake tuwape njia m-badala, tusiwalaumu; nia yao ilikuwa njema, ila utekelezaji kama haufikii kile walichotegemea kupata warudi kujipanga upya nasi tuwasaidie mawazo mapya

Lowassa bado anamakosa kwani haya mabadiliko ni ya serikali za mitaa na hupitishwa na vikao vya Halmashauri ya Mji/Jiji kama sheria. Ndiyo kazi kubwa ya madiwani (council members).

Kwahiyo, Muheshimiwa Waziri Mkuu kukurupuka na kutangaza haya mabadiliko kwani ni kinyume cha sheria za Halmashauri ya Mji/Jiji.

Hii tabia inatupotezea imani kwa viongozi kama hawa wakati wanapofanya maamuzi yao tunajiuliza what was the motive behind his decision. Anafanya kampeni za 2015 kwa gharama za maisha ya walala hoi?
 
Jamani mweee,
Mbona mtazamo wenu ni wa Upande mmoja tu!..
Hivi kweli mnataka kunambia kuwa magari yanachukua sheria kubwa kiliko mwenda kwa miguu. Na kama ndivyo inakuwaje waendesha magari ndio hupata darasa la kuendesha na kujali alama za barabarani na sio mwenda kwa miguu..hivi kweli ukimwona mtu katikati ya barabara basi wewe gonga tu!
Tanzania taa nyingi za traffic hazifanyi kazi acha hizo za limingoti ambayo ndio kiza kitupu.Hizo alama ndio kabisa watu wanaendesha kwa akili ya kuzaliwa mbali kabisa na kupata somo la Udereva amblo asilimia kubwa hawana, hayo magari mengine hata taa hayana.. leo lawama zote zinamfuata mwenda kwa miguu.
Kumbukeni tu kuwa tatizo la Dar ni heavy traffic, halikuwa vifo vya waenda kwa miguu kulikosababisha sheria hii mpya itumike!.. Kwa hiyo kila kinachopangwa ni lazima kitazame usalama wa waenda kwa miguu ambao siku zote za maisha yao, makuzi yao na kisheria uendashaji magari ni kupita upande mmoja!.
Public safety inatangulia kila kitu ndugu zangu hata kwa huyo mwendesha magari inabidi ziwekwe alama zinazoonyesha wazi matumizi ya barabara hizo!..
Ebu fikiria kitu kimoja, tuachane na hao waenda kwa miguu. Mjomba ndio kwanza umetoka zako huko Morogoro ukaingia mjini mara unaona gari linakuja kasi uso kwa uso upande wako! Kwanza utafikiria kuwa wewe ndiye mwenye sheria! kisha huyu mwendawazimu..bado ukifikiria mara jamaa huyu hapa...
Na kama sikosei upande wa lane ya tatu inayokubaliwa kutumika kama ya tatu ni ile ya fast lane!... nambie hapo wewe umekanyaga 100 mara ghafla lane hiyo sii yako tena ati kumesha kuchwa mjini Dar na hiyo ni lane ya waendao upande mwingine!..
jamani acheni kutumia mitulinga!
 
Ebu fikiria kitu kimoja, tuachane na hao waenda kwa miguu. Mjomba ndio kwanza umetoka zako huko Morogoro ukaingia mjini mara unaona gari linakuja kasi uso kwa uso upande wako! Kwanza utafikiria kuwa wewe ndiye mwenye sheria! kisha huyu mwendawazimu..bado ukifikiria mara jamaa huyu hapa...
Na kama sikosei upande wa lane ya tatu inayokubaliwa kutumika kama ya tatu ni ile ya fast lane!... nambie hapo wewe umekanyaga 100 mara ghafla lane hiyo sii yako tena ati kumesha kuchwa mjini Dar na hiyo ni lane ya waendao upande mwingine!..
jamani acheni kutumia mitulinga![/
QUOTE]

Mkandara,

Uchwara wa askari wetu wa barabarani tu, wasiojua sheria wanazozisimamia; Katika ya mji hairuhusiwi above 60Kmph. Na kwa gari lolote ambalo liko 60kmph, unaweza kuepusha vifo, ingawa majeruhi wanawezapatikana.
 
Siku zote huogopa sana kusafiri na basi. Ajali zetu nyingi zinasababishwa na madereva wasiokuwa na leseni, hawajali kufuata sheria za barabarani, kuendesha kwa kasi kubwa, mabasi yasiyostahili kuwepo barabarani, na traffic wazembe ambao wakishapewa mshiko huangalia pembeni na kuwaacha Watanzania wakipoteza maisha kwa idadi kubwa. Mwenyezi mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi.

~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_~_

Ajali mbaya ya basi yaua watu 27 Mbeya

2007-09-08 19:15:42
Na Radio One Habari


Habari kutoka Mbeya zinasema watu 27 wamefariki dunia na wengine 23 kujeruhiwa vibaya baada ya gari waliokuawakisafiria kutoka Mbeya kuja Dar es salaam kugonga lori liliobeba mawe katika eneo la Igurusi nje kidogo ya mji wa Mbeya.

Basi liliopinduka ni ya kampuni ya SABCO Lenye namba za usajili T443 APF wakati lori likiwa na trela lenye namba za usajili T220 Art lilikuwa linatokea Tanga kuelekea Mbeya.

Katika ajali hiyo gari lingine lenye namba za usajili SM 3349 la idara ya elimu wilaya ya Mbarali iligongwa kwa nyuma na kusababisha majeruhi mmoja.

Miili ya waliokufa pamoja na majeruhi wamekimbizwa katika hospitali ya misheni ya Chimala.

Watu wawili kati ya hao 27 waliokufa, walikuwa watembea kwa miguu na watatu walikuwa katika lori.

Habari kutoka mkoani Morogoro zinasema, watu wanne wamefariki dunia na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa vibaya katika ajali ya barabarani iliyotokea jana usiku katika eneo la Lubungo, tarafa ya Mikese katika barabra kuu ya Dar es salaam - Morogoro.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Bwana Thobias Andengenye amesema ajali hiyo imehusisha magari manne, likwemo basi la abiria la kampuni ya Najmunisa liliokuwa likitokea Mwanza kuja Dar es salam.

Magari mengine yaliyohusika katika ajali hiyo ni Fuso lililokua likisafirisha kutoka Morogoro kuja Dar es salaam na lori la mafuta pamoja na lori la mizigo likiwa na trela, ambalo liligongwa na basi hilo kwa nyuma.

Mejeruhi wa gari hiyo ambao wamelazwa katika hospitali kuu ya serikali ya Morogoro, wamepoteza viungo, hasa miguu na kusababisha wavuje damu kwa wingi.

Mganga Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dakta Meshak Mmasi amethibitisha kupokea majeruhi 32 pamoja na miili ya watu wawili waliofia katika eneo la ajali na kwamba majeruhi wawili walifariki dunia wakati wanapatiwa matibabu.

Dakta Mmasi ameiomba ofisi ya Chama cha Msalaba Mwekundu Kanda ya Mashariki na wananchi wengine, kujitolea damu kwa ajili ya majeruhi hao, kwa kuwa walipokuwa wakipokelewa hospitali ilikuwa na unit tano tu za damu.

Mkoani Dar es salaam watu wawili wamefariki dunia na wengine 22 wamejeruhiwa katika ajali tofauti za barabarani zilizotokea jana usiku.

Kamanda wa polisi wa kimkoa wa Temeke Bwana Emanuel Kandihabi Masido amesema ajali ya kwanza ilitokea katika makutano ya barabara za Nyerere na Mandela.

Katika ajali hiyo gari nambari T627AHC aina ya Isuzu Journey lililokuwa likiendeshwa na dereva aliyetambulika kwa jina la Kassim Ayoub liligongana na gari nambari T552ADL, aina ya Toyota pick lililokuwa likiendeshwa na John Magaga ambaye alikufa papo hapona abiria 12 waliokuwa ndani ya basi hilo walijeruhiwa vibaya.

Ajali nyingine ilitokea katika barabara ya Shekilango wilayani Kinondoni, ambapo Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kinondoni Bwana Jamal Rwambo,amesema ilisababishwa na gari lenye namba za usajili T 600AQY aina ya Toyota Starlet.

Amesema gari hilo lililokuwa likiendeshwa na Oscar Shayo, likitokea Sinza lilimgonga mwenda kwa miguu Nicko Shirima na kufariki papo hapo.

SOURCE: Radio One
 
Inasikitisha sana hii, mabarabara finyu lakini magari bado yana enda kama yako kwenye highway 61 au M1 vile..

Naomba Mwenyezi Mungu aziweke mahali pema pemoni Roho za marehemu. Ameni. Pia naungana na ndugu na familia zote zilizokumbwa na majonzi haya yasiyo kipimo.

SteveD.
 
Ndugu zangu, nimesoma kwa masikitiko makubwa juu ya ajali hii, basi lilohusika ni kati ya mabasi ninayopenda sana kusafiri nayo niwapo nchini.

Ni jana tu nilikuwa najaribu kufanyia utafiti fulani juu ya kupunguza ajali zinazohusisha mabasi ya abiria huko nyumbani.

huku niliko sijawahi kusikia basi limepata ajali na niko huku kwa mwaka mmoja sasa. nikimaliza utafiti wangu, nitajaribu kuwashirikisha ninyi pia ili kuona kwamba tatizo hili linakomeshwa kabisa ili abiria wawe na uhakika wa safari zao.
 
Itakumbukwa kwamba Jana magazeti yetu yameripoti juu ya ajali ya basi kule Mbeya iliyohusisha basi la Sabco na kupoteza maisha ya zaidi ya watu 27. Nilieleza masikitiko yangu katika jamboforum na kuahidi kutoa mchango wangu juu ya kupunguza kama si kutokomeza kabisa ajali zinazohusisha mabasi ya abiria hasa yaendayo mikoani.

Tukirejea nyuma itakumbukwa kwamba hii si ajali ya kwanza kutokea, karibu kila mwezi kuna ajali mbaya hutokea na kuangamiza maisha ya abiria wasio na hatia. Athari za vifo hivi ni kubwa na sote tunazijua si kwa familia husika pekee bali pia kwa Taifa.

Kinachonisukuma kuandika makala hii ni sababu zinazotolewa juu ya ajali husika. siku zote Polisi wa usalama barabarani wameelezea mwendo wa kasi kama sababu za ajali husika. kwa maana nyingine ni kwamba asilimia kubwa ya ajali za barabarani hususani mabasi ya abiria ni udhaifu wa kibinaadamu na si uchakavu wa mabasi yenyewe.

Kutokana na sababu hizo basi, tunapaswa kushughulika na Jambo moja kwa nguvu yaani Udhaifu wa Kibinadam (human error) ili kupunguza ajali za barabarani. Katika utafiti wangu Nchini Morocco ambako nafanya kazi kwa mwaka mmoja sasa, sijawahi kusikia au kuona Ajali za mabasi ya Abiria yanayosafiri katika miji mbalimbali. kwa hiyo ilinilazimu kujiuliza kwa nini hapa haitokei lakini nyumbani ni kila mwezi ili hali mabasi ni yale yale kama ya kwetu na madereva si roboti bali ni binadamu kama wale wa kwetu.

Katika utafiti wangu mambo yafuatayo yamesaidia kupunguza/kuondoa Ajali za mabasi ya abiria Nchini Morocco.

Kwanza:
Kazi ya udereva wa mabasi ya Abiria ni sekta rasmi ya Ajira kama ilivyo kwa sekta zingine kama ualimu, udakitari, uhandisi n.k

Pili:
Sheria za barabarani kwa magari yaendayo kasi ni kali sana.

Tatu:
Barabara zao ni nzuri na alama za barabarani zipo kila mahali panapohitajika na zinafuatwa kwa nidhamu ya hali ya juu sana.

Nne:
Kila basi la abiria lina madreva wawili kwa safari inayozidi kilomita 500

Tano:
Hakuna mashindano ya kufika mapema kwani kila basi limepangiwa muda wake wa kufika kule linakokwenda.

Sita:
mabasi husafiri bila kujali usiku au mchana hivyo kuwa na wigo mpana kwa abiria kuchagua muda gani asafiri kuingana na shughuli anayofanya au anayotarajia kufanya kule aendako.

saba na mwisho:
ni nidhamu ya hali ya juu ya madereva wa mabasi ya abiria ambayo sijaiona huko nyumbani.

Sababu nilizozitaja hapo juu ndiyo hasa zimesaidia kuondoa jinamizi la ajali hapa Morocco.

Kutokana na utafiti huu basi nimeona ni bora pia nikatoa mchango wangu kwa Serikali pamoja na vyombo vinavyohusika na usalama barabarani ili pengine tuondokane na kadhia hii.

Lakini kabla sijatoa mapendekezo yangu, kwanza tujue sababu zinazofanya madereva waendeshe kwa kasi, wenzangu mnisadie katika hili maana sina uwanja mpana sana wa ufahamu juu ya hili lakini inasemekana ni kutokana na msukumo wa wafanyabiashara wanaotaka kuwahi kufika kunakohusika ili wawahi biashara zao na kupunguza muda wa kukaa huko kwa sababu za gharama. sababu zingine zinaweza kuwa ni sifa tu kwamba Basi fulani linakimbia sana n.k

Basi kama sababu ni hiyo niliyoitaja hapo juu, basi pendekezo langu la kwanza ni kuondoa sheria ya mabasi kutosafiri usiku ili kuwepo na mabasi wakati wote bila kujali usiku au mchana. (mnisaidie pia iwapo sheria hii ya kupiga marufuku mabasi kusafiri usiku imesaidia kupunguza ajali) hii itawasaidia wafanyabiashara kwa mfano wanaotaka kufika Dar Asubuhi, wafanye biashara zao mchana na jioni waondoke kurudi makwao.

Pendekezo lingine ni kwamba, kama nilivyoona hapa Morocco, nasi pia tuitambue sekta ya udereva wa mabasi ya abiria kama sekta rasmi na si kazi ya watu wanaotoka vijiweni baada ya kushindwa kuendelea na shule.
(wapewe heshima sawa na madakitari, Waalimu, wahandisi, watangazaji n.k)

Tupitie upya alama zetu za barabarani kama zinakidhi mahitaji ya watumiaji ama la, inasemekana watu wanaiba mabango ya alama za barabarani kwa ajili ya kuuza vyuma chakavu, tubuni chuma mbadala ili alama ziwepo wakati wote.

Mabasi yote yanayosafiri umbali unaozidi kilomita 500 yawe na madereva wawili.

Serikali iangalie upya sheria ya usalama barabarani hasa kwa mabasi ya Abiria ili waajiri ambao ndiyo wamiliki wa mabasi hayo wawe wanawaadabisha madereva wao pindi wanapopatikana na kosa la kuendesha kwa kasi. Maana yangu ni kwamba, adhabu ielekezwe kwa mwenye basi na si dereva kwa hiyo impact yake ni pamoja na wamiliki kuajili madereva wenye nidhamu.

Mwisho, ni mabasi yote kufungwa kifaa maalumu cha kurekodi mwendo (si kudhibiti mwendo) ili Askari wa barabarani wawe wanatoa adhabu halali kwa wale waendao kasi. lakini pia kifaa hiki kina faida nyingi na kwa mtazamo wangu kitafanya madereva wasio na nidhamu kuondolewa kabisa katika sekta ya usafirishaji wa abiria. (Mzee James Kombe kama yuko serious basi anaweza kuwasiliana nami ili nimtayarishie mpango mzima ikiwa ni pamoja na kufunga kifaa hicho kwa majaribio katika gari yoyote ya polisi wa usalama barabarani ili waweze kutathmini ni namna gani kitasaidia kupunguza ajali za barabarani kutokana na mwendo wa kasi).

Tunao uwezo wa kuokoa maisha ya watu kama sote tukiamua kwa dhati kupambana na jambo hili. tukumbuke sisi sote ni watumiaji wa mabasi haya hivyo tunao wajibu wa kusaidia kurekebisha hili.
Kupambana na ajali za mabasi ya abiria kuwe sawa na mapambano ya Ukimwi.
 
ami1km6.jpg



ami2wz1.jpg



ami3qc9.jpg



ami7bp7.jpg




Leo alasiri lori lililobeba kontena iliyojaa magunia ya sukari lilipata ajali na kulipuka moto kilomita 40 kutoka Ruaha Mbuyuni kwenye barabara ya Dar- Tunduma. Nilifika mahala hapo saa tisa alasiri muda mfupi baada ya ajali hiyo kutokea. Barabara ilizibwa kwa saa kadhaa kutokana na ajali hiyo. Kulikuwa na msururu mrefu wa magari katika pande zote za barabara. Pamoja na baadhi yetu kushiriki zoezi la kuuzima moto huo kwa mchanga, lakini hadi nilipoondoka mahala hapo kunako saa kumi jioni bado moto mkubwa ulikuwa ukiendelea kuwaka.

Credit: Mjengwa Blog
 
Hii ni ajali au...?

Naona mlango wa Container uko wazi na ndani kuna moto mkali.
Magunia ya sukari yawakayo moto yako wapi?
 
Back
Top Bottom