Mkwasi Rostam na Vodacom

tiGO for life....

Jamani kwa nini mnaumiza vichwa na kupigizana kelele na watu ambao kwa namna moja au nyingine wanausika na hao watuhumiwa wa ufisadi??

Mimi niwaambie kitu kimoja.. hao wote wanaong'ang'ania kutumia voda ni mafisadi kwa namna moja au nyingine.. Kwa nini nasema hivi...
Hebu ajitokeze mtu mwenye ushahidi hapa Jf kama kuna kampuni yoyote ya simu yenye viwango vilivyo juu kama VODACOM, utume msg utakatwa pesa nyingi upige simu utakatwa pesa nyingi yaani ni kufilisiana kwa kwenda mbele hakuna kingine zaidi ya kuchuma pesa ya mvuja jasho kiulainii alafu mnaenda kudanganya walalahoi kwa udhamini wenu feki ambao hata pesa ya kumsajili kaseja imepita huo udhamini wenu si aibu hiyo??

Naungana na mkuu LUNYUNGU kuwasihi woote mnaotumia VODA ni vyema mkaachana na hiyo kampuni maana ni wanyonyaji wakubwa..... lasivyo tutabakia kusema kama ningejua ningesikiliza ushauri wana wana JF ....

Kumbuka LIFE IS A FULL OF IF
 
Ilianza mwaka 2000 ambapo tayari huyu Bwana alikuwa tayari ameshafilisi viwanda vyetu vya ngozi, tayari alishategeneza himaya yake ya kisiasa ndani ya CCM na kuitumia kuhakikisha kampuni yake ya Caspian inapata kandarasi serikali. Na kampuni hii ndio yenye mahisa humo vodacom. Lakini alikuwa pia na makampuni mengine pembeni yaliyokwiba fedha za mfuko wa Japan. Na pia lile kampuni lake lingine lililojibebea fedha za import support. Halafu akaendeleza mtaji wake miaka ya 2002-2006 kwa kutumia mafedha mengine ya BOT. Huyu ndiye Kagoda ninayemfahamu! Sasa ni bilionere, hata mkimchanganya vodacom, mkono wake upo kila mahali. Upo TICS, msuse kuingiza makontena. Upo habari corporation, msuse kusoma rai na mtanzania. Upo Mwananchi, nako pia msuse. Lakini upo pia ndani ya CCM, hisa zake huko ni nyingi zaidi. Mkitaka kumkomoa basi mjitoe kwenye Chama Cha Mafisadi(CCM),atabaki tu na vile vitega uchumi vyake vilivyopo Oman, Iran, Maritius etc. Hivi ile tenda ya kujenga kiwanja cha ndege alishakamilisha?

Asha
Sawa, hata hivyo, lengo kubwa kuliko yote sio kumkomoa mtu hapa bali ni kutokomeza ufisadi kwa njia tunazoweza kutumia ikiwemo hii ya kususia.

Hili la kususia nimeliona ni muafaka sana kwamba tutaweza kumshawishi hata mwananchi aliyeko kijijini akashiriki kwenye hili na yeye kutambua kwamba kumbe anayo silaha ya kupambana na wahujumu wa nchi ya mababu zake (maana sidhani sasa tunapozungumza nchi hii ni yetu tena).

Hali kadhalika yeye kuona matokeo ya kususia huku - right then. Njia hii naiona ina ufanisi zaidi ukilinganisha na jitihada za kumuelimisha mwananchi kuhusu uwezo wake au nguvu aliyonayo kwenye kupiga kura!

We want our voices to be heard! Hata kama RA ataendelea kuwa tajiri, that is irrelevant to me, there is one thing I want to put a STOP to it na si kingine bali ni UFISADI.

Je ungetaka kumshawishi babako ashiriki maandamano japo kuna police na wana live bullets ungali ukifahamu kwamba njia mbadala zipo? Kwanini basi tushindwe kuwashirikisha wananchi vijijini bila kuwatumbukiza kwenye risks kubwa wakati we have the means? Ni wengi wanatambua dhuluma wanayofanyiwa isipokuwa tu hawajui namna wanavyoweza kushiriki kuikomboa nchi hii toka kwenye mikono ya akina RA.

Tutizame outcome ya hili moja kwanza. Ukihamia Celtel (suppose nako kuna MIFISADI) hakika watatia maji wakiona VODA ananyolewa.

Nakubaliana nanyi kwamba hili lina IMPACT kubwa sana.




.
 
Nimesoma maoni ya wengi na bado naitisha mgomo.Mimi nililenga kisiasa kumbe hata gharama zao ni kubwa nalo limeongezea hili .So tuendelee kupiga makelele ya mwizi hadi kieleweke .

Nina wapa pole wageni 2 ambao wamelazimika kuingia kumjibia RAna Vodacom yao .Uchumi wa Nchi una faida gani kwa Baba na Mama yangu kijijini kwetu ?Hakuna kabisa .Kama siwezi kujitahidi kuwaoa pesa ya kula basi hawawezi maisha na wazee sana .Faida wanaziona mafisadi na si mimi na watu wa kijiji kwetu .
Nawaone huruma kwamba mnakuja wakati mambo ni moto sasa .Tutazidi kuelezana hadi kieleweke tu hapa .Hatuwezi kuungana na CCM kwa kushindwa kuwawajibisha wezi no .Lazima kutafuta silaha ya kupambana nao tu .

Mawazo ya kifisadi haya toka shy na ndugu hawa wapya ambao naamini wametumwa kuja ku spin ni sawa na akili ya Chenge kwenda kumwaga unga kwenye viti vya wabunge anao wachukia Dodoma.

As for Shy .Uongo mwingine hauna maana hata mara moja .Mimi nawe tumewahi kuongea wakati ule wa issue Muhimbili na tokea nilijue you were a senior snitch .Sina mawasiliano nawe hata siku moja na hili linathibitisha madai ya wengi hapa natabia zako .Mimi kuwa Kongo ?Nafanya nini ? Nilete kwako computer ? Yaani kwa akili yako unadhani mtu mjanja kama naweza kuja kwako kuleta computer etu utengeneze ? Kama akili yako kwa hapa ni kama unyoa bado kweli mimi nikae chini nikutafute wewe ? Chekesha umma mimi simo,

Narudia wito wa kuanza na Rostam na Vodacom kwanza .Hili ndilo muhimu kwa sisi hapa .Tuonyeshe kuwa serious kila tukiongea na si maneno .Time now to ditch Vodacom pamoja na kwamba ndugu zetu wana ajira huko .
 
Inaweza Kuwa Kweli Alivipata Kwa Ufisadi.lakini Kashfa Zote Za Ufisadi Zimetoka Mwaka 2004/2005 Wakati Yayari Vodacom Ilikuwepo.sasa Hapo Ilianzishwaje Na Hizo Pesa????au Inakuwa Hadithi Ya Mwana Kondoo Ya Kuwa Kama Siyo Wewe Basi Ni Babu Yako Na Lazima Ni Kule?
KAKA HAWA JAMAA MASIKIO YAO HAYASIKII NA MACHO YAO HAYAONI TENA,ATA UKIWAFINDISHA HAPA KAMWE HAWATAELEWA.WANAOTA TU HAPA HAKUNA MWENYE UJANJA WA KUWAZUIA VODA KUPETA
 
Ilianza mwaka 2000 ambapo tayari huyu Bwana alikuwa tayari ameshafilisi viwanda vyetu vya ngozi, tayari alishategeneza himaya yake ya kisiasa ndani ya CCM na kuitumia kuhakikisha kampuni yake ya Caspian inapata kandarasi serikali. Na kampuni hii ndio yenye mahisa humo vodacom. Lakini alikuwa pia na makampuni mengine pembeni yaliyokwiba fedha za mfuko wa Japan. Na pia lile kampuni lake lingine lililojibebea fedha za import support. Halafu akaendeleza mtaji wake miaka ya 2002-2006 kwa kutumia mafedha mengine ya BOT. Huyu ndiye Kagoda ninayemfahamu! Sasa ni bilionere, hata mkimchanganya vodacom, mkono wake upo kila mahali. Upo TICS, msuse kuingiza makontena. Upo habari corporation, msuse kusoma rai na mtanzania. Upo Mwananchi, nako pia msuse. Lakini upo pia ndani ya CCM, hisa zake huko ni nyingi zaidi. Mkitaka kumkomoa basi mjitoe kwenye Chama Cha Mafisadi(CCM),atabaki tu na vile vitega uchumi vyake vilivyopo Oman, Iran, Maritius etc. Hivi ile tenda ya kujenga kiwanja cha ndege alishakamilisha?

Asha
VIWANDA GANI VYA NGOZI AMBAVYO RA ALIVIFILISI????HAYA NI MAJUNGU MAKUBWA.UNAPOSEMA ALIPEWA KANDARASI ZA SERIKALI LAZIMA UZITAJE NA SIO KUGENERALIZE...MIMI NAKUBALIANA NA HUYO NCHIMBI KUWA WAKATI VODA INAANZISHWA HAKUNA UFISADI WOWOTE AMBAO UNATAJWA WA EPE WALA RICHMOND SASA KUSEMA KUWA VODA INATOKANA NA HIVYO NI MAJUNGU MAKUBWA SANA SANA.HATA KAMPUNI YA KAGODA KAMA KWELI NI YAKE HAIKUCHUKUA FEDHA MIAKA HIO YA 1999 MPAKA 2000 VODA IWE TAYARI KUANZISHWA.WIVU WA KIKE TU UMEKUJAA
 
Nimesoma maoni ya wengi na bado naitisha mgomo.Mimi nililenga kisiasa kumbe hata gharama zao ni kubwa nalo limeongezea hili .So tuendelee kupiga makelele ya mwizi hadi kieleweke .

Nina wapa pole wageni 2 ambao wamelazimika kuingia kumjibia RAna Vodacom yao .Uchumi wa Nchi una faida gani kwa Baba na Mama yangu kijijini kwetu ?Hakuna kabisa .Kama siwezi kujitahidi kuwaoa pesa ya kula basi hawawezi maisha na wazee sana .Faida wanaziona mafisadi na si mimi na watu wa kijiji kwetu .
Nawaone huruma kwamba mnakuja wakati mambo ni moto sasa .Tutazidi kuelezana hadi kieleweke tu hapa .Hatuwezi kuungana na CCM kwa kushindwa kuwawajibisha wezi no .Lazima kutafuta silaha ya kupambana nao tu .

Mawazo ya kifisadi haya toka shy na ndugu hawa wapya ambao naamini wametumwa kuja ku spin ni sawa na akili ya Chenge kwenda kumwaga unga kwenye viti vya wabunge anao wachukia Dodoma.

As for Shy .Uongo mwingine hauna maana hata mara moja .Mimi nawe tumewahi kuongea wakati ule wa issue Muhimbili na tokea nilijue you were a senior snitch .Sina mawasiliano nawe hata siku moja na hili linathibitisha madai ya wengi hapa natabia zako .Mimi kuwa Kongo ?Nafanya nini ? Nilete kwako computer ? Yaani kwa akili yako unadhani mtu mjanja kama naweza kuja kwako kuleta computer etu utengeneze ? Kama akili yako kwa hapa ni kama unyoa bado kweli mimi nikae chini nikutafute wewe ? Chekesha umma mimi simo,

Narudia wito wa kuanza na Rostam na Vodacom kwanza .Hili ndilo muhimu kwa sisi hapa .Tuonyeshe kuwa serious kila tukiongea na si maneno .Time now to ditch Vodacom pamoja na kwamba ndugu zetu wana ajira huko .

Naona Mkuu umewasha moto kweli kweli inatakiwa kama watu wako makini wachukue hatua haraka mpaka Vodacom wahakikishe wanamtimua FISADI.
 
Namshukuru Mungu hizi pesa zilichukuliwa na mtu mwenye akili kama RA kwakuwa ingekuwa ni sisi waswahili ungekuta tayari tumeongeza wake tu hapa....kwanza kama ni kweli alichukua ni sawa na naita ni wizi endelevu kwa kuwa ameiba pesa ambayo imekaa tu bot,amewekeza na amewapatia watanzania ajira,watanzania zaidi ya elfu moja wamepata ajira voda.mwananchi na zaidi ya wananchi elfu tatu wana ajira caspian..Mungu akuzidishie ndugu yangu Rostam Rasul Abdul Aziz....
 
Kenya waligomea hata vyakula kwenye supermarket when they felt kwamba pesa zao zilienda kwa Kibaki na zikatumika kuwanyima haki yao .Tanzania Rostam Aziz kila kukicha ana wezi mpya lakini iko kimya na support anapewa .Sisis tuna lalamika lakini bado tunatumia huduma za simu za Vodacoma ambazo yeye ni mmoja wa share holders .Kama tuna uchungu kweli na huyu ambaye analindwa na CCM na serikali yake , tuhamie sote kwenye tigo ama zantel ama Celtel .Hii itakuwa njia nyingine ya sisi kuonyesha kwamba tumechoka kuibiwa na kuzidi kukamuliwa kila mara .Mimi nimesha hama na huhu unakaribia mwaka tangia nimejua kwamba Rostam anatumaliza bado na vodacom yumo .Mie natumia Zantel sasa na Celtel .Je wewe unangoja nini ?Tuambiane tuachana nao hawa .Wanatuona wajinga katika maamuzi yao je waendelee kutuona wajinga hata katika pesa zetu wenyewe za kutumia katika simu ?
LUNYUNGU hebu tupatie vielelezo ili tukuunge mkono maana zisiwe habari za mitaani au labda una chuki binafsi na huyo Rostam
 
LUNYUNGU hebu tupatie vielelezo ili tukuunge mkono maana zisiwe habari za mitaani au labda una chuki binafsi na huyo Rostam

Ipole
Unataka vielelezo gani ? Unataa ushahidi juu ya RA kuwa na share vodacom ? Au ni kitu gani huelewi mkuu ?
 
VIWANDA GANI VYA NGOZI AMBAVYO RA ALIVIFILISI????HAYA NI MAJUNGU MAKUBWA.UNAPOSEMA ALIPEWA KANDARASI ZA SERIKALI LAZIMA UZITAJE NA SIO KUGENERALIZE...MIMI NAKUBALIANA NA HUYO NCHIMBI KUWA WAKATI VODA INAANZISHWA HAKUNA UFISADI WOWOTE AMBAO UNATAJWA WA EPE WALA RICHMOND SASA KUSEMA KUWA VODA INATOKANA NA HIVYO NI MAJUNGU MAKUBWA SANA SANA.HATA KAMPUNI YA KAGODA KAMA KWELI NI YAKE HAIKUCHUKUA FEDHA MIAKA HIO YA 1999 MPAKA 2000 VODA IWE TAYARI KUANZISHWA.WIVU WA KIKE TU UMEKUJAA

Ama kweli akili ni nywele .Kama RA anaweza kulala mbele na mapesa ya EPA , huko nyuma tutamwamini vipi kwamba alitumia pesa zake kunuua hisa Vodacom? Hapa issue ni kwamba ni Fisadi leo na kama ana kitu alikuwa nacho kabla hajajulikana kwamba ni Fisadi na leo kajulikana lazima alipe price .Hii ndiyo maana ya sisi kuitisha mgomo na kumwaga somo watu waachane na Vodacom
 
Ipole
Unataka vielelezo gani ? Unataa ushahidi juu ya RA kuwa na share vodacom ? Au ni kitu gani huelewi mkuu ?
MIMI NATAKA VYA KUWA WAKATI VODA INAANZISHWA NI PESA GANI ZILIIBIWA NA UFISADI NA WAPI?NA ANA SHARE KIASI GANMI ILI KUJUA KAMA KWELI NA ZA HUO UFISADI WAKO UNAOSEMA
 
Ama kweli akili ni nywele .Kama RA anaweza kulala mbele na mapesa ya EPA , huko nyuma tutamwamini vipi kwamba alitumia pesa zake kunuua hisa Vodacom? Hapa issue ni kwamba ni Fisadi leo na kama ana kitu alikuwa nacho kabla hajajulikana kwamba ni Fisadi na leo kajulikana lazima alipe price .Hii ndiyo maana ya sisi kuitisha mgomo na kumwaga somo watu waachane na Vodacom[/QUOTEHIZO NI CHUKI KAKA KAMA ALIKOPA UNAJUAJE??AU ALIANZISHA KWA UWEZO WA FAMILIA AU ALIUNGANA NA WENZAKE WAKAMSAIDIA.UNACHANGANYA MAMBO KAKA,MWISHO UTASEMA ATA HOSPITAL ALIOZALIWA NAYO TUISUSIE KWA KUWA NDIPO ALIZALIWA GENIOUSE RA.
 
Watanzana tufike mahali tuchukie tuonyeshe kwa vitendo .Rostam na genge lake hawagusiki hili liko wazi ,nasi tuna imba na wao wanasema tutasema mwisho tutakaa kimya .Now it is time tuache na lile ambalo liko wazi kama hili .Kwamba Rostama na Lowasa wana connection na Vodacom basi tuanze nao .Tutaendelea naupelelezi wetu kama kuna supermarket ama hata kisimi cha mafuta kina mkono wa fisadi we avoid them .Ndiyo njia pekee .JF onyeshini njia sasa .Tumekuwa tuna sema sana .Mafanikio yapo lakini we need to hard on them .Hakuna utani.Mimk nafurahi kutangaza kwamba jana hadui leo asubuhi nimewaondoa watu 15 toka Vodacom .Niliwanunulia wachache like jana na leo nimenunua 3 za Tigo.

Jamani naomba tusimame imara kwa hili tumechoka kila kona tunanyonywa tu sasa angalau tunaweza kugomea bidhaa zao .

Nakubali wazo lako moja kwa moja. Ila nakataa kuwa RA na wenzie hawagusiki!! Mbona mimi nauona mwisho wao!!! Cha msingi kila mtu afanye awezalo kuwaangusha!

Mapambano yanaendelea
 
Ususiaji wa bidhaa za kifisadi ni jambo common sana duniani kote si kenya tu! Hata wazungu (wanaharakati) wakisikia kuna blood diamonds na bidhaa kama hizi wanazisusia! Afterall hawa voda ni ghali
 
Masaka hadi muda nina shawishika kuelewa kwamba kichwani u mtupu na kumejaa takataka .Kama huoni makosa ya Rostam kaa pemben tuache sisi tunao yaona tupigane mana CCM wala Serikali ya CCM hawawezi kumgusa kwa kuwa alikodisha helikopta na CCM kushinda Uchaguzi kiteto .
Mh Lunyungu umenichekesha kweli angalau na wewe umeliona hilo....nikisema mimi huwa napuuziwa lkni maadamu na wewe umeliona hilo labda mambo yatabadilika kadiri siku zinavyokwenda kwa maana wewe ni moja wa maheviweiti humu....dawa ni moja tuu kuwafungia na kutubakiza wachache ili tuongelee mambo ya maana... sasa maadamu na wewe upo pmja nami basi tumia nguvu yako ili tuweze kufanikisha hilo na kuweza kuwafungia watu kama hawa........
 
Mh Lunyungu umenichekesha kweli angalau na wewe umeliona hilo....nikisema mimi huwa napuuziwa lkni maadamu na wewe umeliona hilo labda mambo yatabadilika kadiri siku zinavyokwenda kwa maana wewe ni moja wa maheviweiti humu....dawa ni moja tuu kuwafungia na kutubakiza wachache ili tuongelee mambo ya maana... sasa maadamu na wewe upo pmja nami basi tumia nguvu yako ili tuweze kufanikisha hilo na kuweza kuwafungia watu kama hawa........



Kijakazi kumfungia ataanza kulia lia kwamba Lunyungu na kampeni dhidi yangu .Huwa dawa yake ni kumpa ukweli atashikwa na hasira na ataanza matusi then anafungiwa.Yuko kazini anajivua nguo hadi akili na utu wake .Ndiyo madhara haya ya kula pesa za watu na kutumwa kufanya lolote kuwaondoa katika mstari .Mpuuzeni huyu ni mtupu kichwani hadi moyoni .Hana soni na hata tofauti na mafisadi .

Naomba tuendelee kupeana habari kokote na kuhakikisha Vodacome wana elewa kwamba tumechoka kuwa vichwa vya wendawazimu na sasa kuachana nao .Hili ndilo muhimu unaona wana post 2 leo kajiandikisha na anaanza kuparamia hoja .Wandugu JF kusoma ni rahisi kuandika unahitaji akili ya ziada .
 
Hao watu wakikamatwa...Hiyo mali badala ya kuisusia inataifishwa!
Mbona mnazunguka mbuyu?
 
Mushi mada hii haia mahusiano na kumkamata mtu Hawawezi kumkata RA na sisi wanyonge sasa dawa yetu ni kugomea biadhaa za mafisadi .Iwe zao moja kwa moja ama wana mkono ndani yake .This is the only way forward .
 
Mkuu huyu Rostam dawa yake sio kususia huduma ya vodacom dawa yake ni kuuanika ufisadi wake hadharani na njia alizotumia ili mali zake zitaifishwe. Hiyo voda najua ameajiri mitoto mingi ya mafisadi lakini tukumbuke hata walalahoi tupo tunaojipatia kaugali kwa siku.
 
Hii hoja ni muhimu sana, na ninauhakiwa wataalam wa uchumi wa Voda kama wako serious angalau wameshtuka kidogo na kisha itakuwa angalau AOB katika moja ya vikao vyao, napenda kuwakumbusha VODA kuwa Mwanzo wa hesabu ni moja na wasipuuzie hii mada, mwisho ni kweli kuwa Kama uongozi wetu wa nchi hauchukui hatua kwa watu kama RA hii ni njia mwafaka kabisa ya kuwashughulika mafisadi. Naunga mkono hoja hii kwa kuwa naamini uongozi wa Voda hautakubali kuona shirika lao linachafuliwa kwa kumkumbatia Rostam, watamtupilia mbali.

Angalia mahesabu yao kwa siku kwa kukisia tu.

VODA WANA WATEJA 5,000,000. KILA MMOJA AKITUMIA SH.1000.00 TU KWA SIKU WANAPATA SH 5,000,000,000.00. Yaani billion 5 kwa siku moja .Sasa kwa mwezi piga mwenyewe. Linganisha na bajeti ya Tanzania kwa mwaka. Tafakari ..........

Tukigoma ni poa. Nagoma kuanzia leo. NOw I have a reason to quit. Kumbe ni mafisadi again? Walinunua share kwa hela walizoiba EPA, Richie n.k .To hell...BYE VODA.
 
Back
Top Bottom