John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo ametoa msamaha kwa vijana 853 kati ya 854 (mmoja alifariki) waliofukuzwa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Aprili 2021 kwa makosa ya kinidhamu.
Jenerali Mabeyo ameagiza vijana hao warejeshwe katika kambi za JKT tayari kuanza mafunzo.
"Vijana wa JKT 853 waliosamehewa wapokelewe ifikapo March 12, 2022 na watakapokelewa katika Kambi moja tu, kambi namba 841 ya JKT ipo Mafinga Iringa.
"Katika msafara wa mamba na kenge watajipenyeza, niwaombe Vijana ambao hawahusiki na msamaha huu wasijipenyeze, Vijana hawa 853 orodha yao yote imeandaliwa na tumefanya utafiti mpaka kwenye ngazi zao za Familia, hata makundi yao ya damu kwa kila mmoja limeorodheshwa kwa hiyo udanganyifu hautojitokeza utapimwa kwa jina picha na damu yako," amesema Luteni Kanali Gaudentius Gervas Ilonda, Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano (JWTZ).
Pia, soma:
1). JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi
Jenerali Mabeyo ameagiza vijana hao warejeshwe katika kambi za JKT tayari kuanza mafunzo.
"Vijana wa JKT 853 waliosamehewa wapokelewe ifikapo March 12, 2022 na watakapokelewa katika Kambi moja tu, kambi namba 841 ya JKT ipo Mafinga Iringa.
"Katika msafara wa mamba na kenge watajipenyeza, niwaombe Vijana ambao hawahusiki na msamaha huu wasijipenyeze, Vijana hawa 853 orodha yao yote imeandaliwa na tumefanya utafiti mpaka kwenye ngazi zao za Familia, hata makundi yao ya damu kwa kila mmoja limeorodheshwa kwa hiyo udanganyifu hautojitokeza utapimwa kwa jina picha na damu yako," amesema Luteni Kanali Gaudentius Gervas Ilonda, Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano (JWTZ).
Pia, soma:
1). JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi