Kama Mwigamba atajibu maswali haya, tutamwelewa. akijikanyaga tu!!!!. Aende kwa shonza na Juliana hajachelewa bado fungu limetengwa kwa kazi yao ya kishetani!!.
Swali la kwanza:
1. Nini lengo na nia ya andishi lako mtandaoni?.
2. Ukiwa kama kiongozi, unajua hali ambayo CDM inapitia kisiasa kwa sasa?. kama unafahamu unadhani kubadili uongozi kutaleta afya kwa chama au maafa?.
3. Unaweza kuwasemeaje ama unaweza kujitofautishaje na masalia waliofukuzwa ndani ya CDM?.
4. Wewe kama mwanadam, unajua kuwa ipo siku utahukumiwa mbele za Mungu kwa nia yako Ovu au safi.Unajipimaje katika mazingira ya hukumu ya Mungu na nia/lengo la andishi lako na haya unayojinasibu kuwa hukuwa na nia mbaya?
Mbona hii kila mtu mwenye reasoning ya kawaida tu anaweza kujibu haya maswali!
1. Ni baada ya kuona kila malalamiko yanayotolewa kwa njia sahihi (kwenye VIKAO HALALI VYA CHAMA) hayafanyiwi kazi, tena aliyelalamika anaishiwa kutishiwa na GREEN GUARD
2. Hali inajulikana, pamoja na hiyo hali bado haitoshi kuwa excuse ya kushindwa kutimiza ratiba tulizojiwekea sisi wenyewe kwenye VIKAO HALALI VYA CHAMA bila kuwasiliana na wajumbe waliokaa mwanzoni kwenye kuipitisha, je huoni kama hiyo hali inaweza kuwa inasababishwa na sisi Viongozi Wenye Maamuzi kushindwa kutekeleza majukumu yetu? Achilia mbali kuweka target ambazo sio achievable! Sasa kama jibu ni ndiyo, kwa nini hawa viongozi wanaoweka malengo wasiyoweza kufikia halafu baadaye wanabadili ratibu kimya kimya wasipumzishwe?
Vipi kuhusu kipindi kigumu kama kinasababishwa na matumizi mabaya ya fedha? Tunashindwa kuimarisha mashina ya chama kwa sababu hela ziko mifukoni mwa wachache! Kwa nini wasipumzike?
Report ya Mwigamba imegusia juu ya hela ya Sabodo, Ruzuku, michango ya harambee (fund raising), michango ya pale mikutanoni (sadaka) na uuzaji/ununuaji wa vifaa bila kamati ya manunuzi kushirikishwa! Je hawa kwa nini wasipumzike?
3. Masalia ni masalia, chama kama chama tunahitaji kuwa na njia nzuri ya kureport issues bila kujulikana ni nani aliyereport (whistleblowing), sasa kama mtu akireport taarifa zinavujishwa unategemea tulalamike wapi kama sio kwa wananchi/wanachama?
4. Ya Mungu mwachie Mungu, ya Kaisari mwachie Kaisari; kwa nini msijitetee kwa point! Mfano, toeni report za mapato na matumizi (monthly, quarterly na annually), leteni katiba ya 2004, leteni minutes za vikao vya katiba ya 2006, leteni katiba mpya. Elezeni kwa nini operesheni zinastop kinyemela, zinaanzishwa zingine bila vikao HALALI VYA CHAMA.
Baada ya kuleta haya, tujadiri ukweli wa kile mnachokisimamia, je ni kweli mnataka kutukomboa? Au mnataka kututumia?
Asante, uliza maswali mengine.