Mkutano wa Mwigamba na vyombo vya habari

Mkutano wa Mwigamba na vyombo vya habari

Nimesikitishwa sana na haya yaliyotokea arusha naanza kupata mashaka kama ukombozi wa kweli tuliokuwa tunautafuta kupitia CDM utapatikana. Ninasema hivyo kwa kuwa kilichotokea arusha ni ishara mbaya kwa chama ambacho kimekuwa kipenzi cha watu wengi na sasa inaonekana dhahiri kuna vita ya madaraka imeanza ndani ya CDM. Pia hakuna kuaminiana tena huyu jamaa inadaiwa alipigwa kwa sababu ya kudaiwa kuwa anatumiwa na Zitto kukihujumu chama kwa mantiki hiyo wanachadema hawana imani na zitto ambaye ni mmoja wa viongozi wakuu wa chama na amekuwa ktk chama kwa muda mrefu. Nina dhani kwa mtazamo wangu CDM ingefocus kwenye kujenga chama wakati huu tunapokaribia uchaguzi mkuu wa 2015 na si kujikita kwenye malumbano ya kuwa fulani anahujumu chama kama ushahidi upo huyo anayehujumu chama aondolewe na chama kisonge mbele. Huku tuendako si kunzuri naanza kuiona CDM ikijijengea taswira mbaya machoni pa wananchi ambao tuliamini kuwa CDM ndiyo mkombozi wetu. Tunaanza kupata taswira ya tofauti kuwa si chama cha ukombozi tena wa tanzania bali ni kichaka cha kutafuta madaraka kwa maslahi binafsi kama ilivyo CCM.

Wenzako wapo field tangu asubuhi wanajenga chama mkuu. Wewe tu ndo una hofu. Usiogope uko chama kubwa. CDM ingekuwa inapuuzia watu kama hawa ungekuta kilishakuwa NCCR/TLP/CUF siku nyingi. Uzuri wa CDM wanamkunja samaki akiwa bado kifaranga, wanamsweka kwenye ndoo, safari inaendelea...
 
Sasa Mwigamba anaelezea namna ilivyokuwa siku hiyo anasema Lema aliingia kwenye ukumbi akamkuta mwenyekiti akitoa speech lema akiw na IPAD mkononi akaa sehemu yake lakini baada ya muda akasimama na kumwambia mwenyekiti samahani kuna jambo la dharua.. lema akaanza kuelezea alichokiona kwenye mitandao, Selesini akanyosha mkono kumuomba lema asome kilicho bandiko husika. alipo maliza wakatoa pendekezo kuwa laptop ikabidhiwe meza kuu akiwa bado hajawaambia anakadhidhi ama laah lema alifika na kumnyakua ile laptop na kumwita mwenyekiti wa chadema mkoa wa manyara mabae ni mtaalamu wa IT akaiwasha wakagundua inapassword Mwigamba hakuona tatizo kutoa password akatoa wakaanza kulinganisha path na kujiridhisha kuwa ilitoka kwake basi ile laptop ikarudishwa meza kuu

Ameshakuwa historia. Awasalimie sana kina Shitalamba...
 
Lakini kwanini kila anaeikosoa chadema anakuwa ni msaliti? Mnataka wanachama tuwe mazoba? Nilikiamini Sana chadema ila imani imenipungua sana

usife moyo. Jitahidi kuujua utaratibu na kuutumikia. Watu wengi sana(akiwemo Mwigamba) wanashindwa kuutumikia utaratibu/kanuni walizojiwekea. Mahali popote uataratibu ukifuatwa kila mtu anakuwa huru, usiogope Chadema ni imara na itaimarika zaidi kutokana na haya yanayotokea. Mwigamba anakuwa shujaa---(a) kwa kuharibu future yake ya kisiasa (b) kwa kufanya tukio litakaloiimarisha zaidi Chadema kwani lazima kuna mambo yatashughulikiwa.
 
Kama maneno hayo ndo ya Mwigamba, hana tofauti na akina Shonza. Ameshakula vipande vya fedha kama Yuda Iskariote, kwa kujifanya eti anampenda YESU kwa kumbusu. Hakuna jipya chini ya jua. Anakoelekea ni kuumbuka zaidi
 
Wenzako wapo field tangu asubuhi wanajenga chama mkuu. Wewe tu ndo una hofu. Usiogope uko chama kubwa. CDM ingekuwa inapuuzia watu kama hawa ungekuta kilishakuwa NCCR/TLP/CUF siku nyingi. Uzuri wa CDM wanamkunja samaki akiwa bado kifaranga, wanamsweka kwenye ndoo, safari inaendelea...
Pamoja ni chama kubwa kama unavyodai lakini kuna madai ya msingi wanachama wanataka yatimizwe kama uchaguzi, uwazi, taarifa za fedha, kuodosha ubaguzi nk. kama yatafanyika hayo ndiyo uhai wa chama la sivyo kesho na keshokutwa atazuka Mwigamba mwingine kwa sababu hoja iko palepale.

 
Mojawapo ya disadvantage kubwa sana ya democracy ni concept ya Wengi wape, hata kama wako 100% wrong. Hapa inafanyika kuaminisha wengi kwamba Mwigamba kakosea na aliyosema ni uongo mkubwa, jamii (Walio wengi) wakishakubali hilo basi tayari ushindi umepatikana, tutamuita Mwigamba msaliti, masalia, muasi na kadhalika.
Ni kweli sasa Mwigamba ni kama mimi na wewe tu, Outsider na yuko huru kuongea lolote tu. Tatizo litaonekana ni upande wake tu katika maisha yake kisiasa, wengi wetu tutasema amecommit political suicide japo mimi nitaita political murder.Tutakachoshindwa kutambua ni ushindi wa giza dhidi ya nuru!

Nimefuatilia maelezo yako kwa kina sana mkuu wa kazi ni kweli kuwa wengi wetu hatuko makini na hatujui vyema kama sio kujisahau . Kunapokuwa na chama lazima kuwepo na uongozi. Maamuzi ya chama ni maamuzi ya vikao, vikao vipo katika ngazi mbalimbali- ambapo ngazi zote maamuzi ya mwisho ni mkutano mkuu wa wanachama.

Kwenye vikao vya viongozi wa chama ndipo mahala ambapo mitazamo inatofautiana kwa lengo la kujenga na mijadala inatakiwa iwe mizito sana kwani kinachotakiwa ni kuchambua mambo katika nyanja zote kulingana na ajenda. Mwisho wa mijadala ya vikao vya ndani kinachotakiwa na wajumbe kukubaliana na kuwa kitu kimoja kwenye maamuzi ambayo yamejadiliwa kwa kina-maamuzi hayo yanapelekwa kwenye mkutano mkuu kwa hatua zaidi kwani mkutano mkuu unamamlaka ya kukataa ama kukubaliana na yaliyoletwa na viongozi wao. Sasa ni jambo la kushangaza kama mijadala ya ndani kabla haijatolewa maamuzi unaipeleka nje, hii ni demokrasia ya wapi mnayoizungumzia ? Hapa ndipo panakasoro- kwamba wanaotoa mambo ya ndani kabla hayachakatwa vyema wanamalengo gani ? Hawa ndio wanaoitwa mamluki ,wametumwa ,wachochezi na wenye malengo mabaya na chama na watanzania kwa ujumla.

Hawa watu wa aina hii ni hatari kwa mustakabali wa taifa wasikubalike kwa chama chochote iwe CDM,CCM,CUF ana NCCR nk. Watu kama hawa watatoa siri za nchi kwa mataifa mengine kabla ya mambo kuchakatwa vyema. Mtu huyu akiwa waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa atatoa siri za nchi kisa anapishana mitazamo na Raisi nje ya vikao halali .

Njia sahihi za kutatua matatizo kwa usahihi kwenye vyama vyetu ni kusoma na kuelewa katiba na taratibu ili unafuata taratibu halafu ukahukumiwa wananchi wanakuwa bega kwa bega na wewe. Mfano upo wazi; Zitto alipofukuzwa Bungeni wananchi walikuwa bega kwa bega na Zitto kwani kilichotokea walikiona na hakukukua na uvunjaji wa taratibu kwa lile alilolifanya Zitto.
 
Better be that, unajua Mwigamba ni good boy ila tu anaonekana kuwa ni mtu wa misimamo fulani hivi ambayo hukwaza baadhi ya watu, the good thing kwa watu wa namna hiyo hawakubali kutumika kama sources bali husimamia show zao wenyewe!

Sometimes watu wanadhani demokrasia bora ni kumsikiliza kila mtu kwa kila anachosema. Binafsi naamini CDM ingewaendekeza kina Shitalamba, Kafulila, Mkosamali, Madiwani wa Arusha nk leo ingekuwa vipande vipande. Kama una mawazo yatakayowachanganya wananchi, hata yawe mazuri namna gani, hayaruhusiwi yaingilie momentum ya chama. Tukianza kupiga maktaim na hoja za kumng'oa Mbowe sasa hivi tutabaki hapa hapa, alafu tukija kushtuka CCM wameshatuacha tena km 100...
 
Chadema inakufa soon

Ninachowapenda LB7 mna akili kuliko hata Wasira. Maana yeye alijichanganya akatoa time frame. Eti inasambaratika ndani ya mwaka mmoja. Leo mwaka umeisha, but akisikia neno CDM anakurupuka bila kuvaa pichu kwenda "DAKIKA 45" ITV...
 
Hawa ndo wasomi wa nchi yetu,kwa akili ya kawaida mwigamba anadhani ana nguvu ya kuivuruga cdm,kitendo anachofanya kitaipa umaarufu zaidi cdm na kuna mambo yatashughulikiwa ili kukifanya chama kiimarike zaidi. Hv mtu ambae hana uwezo hata wa kushinda udiwani,atatuvuruga vp!? Hata huyo baba yake ZZK,dawa yake inachemka. Cdm msiilinganishe na nccr ya mrema na waasira wale wote haziwatoshi.
 
Tuache ushabiki, mwigamba ameifanyia mengi chadema, na kama kuna kazi yakujitolea amefanya nyingi tu, kna haja ya kamati kuu kulitafakari hili swala kwamba iweje mtu kama mwigamba afikie hatua hiyo kwa sababu kama ingelikuwa ni pesa mwigamba asingeacha kazi UN kwa ajili ya chadema a kwa mtu yeyote anayemjua mwigamba atakubaliana na mimi lazima chama kiangalie vizuri vvinginevyo watu kama hawa watakuwa wengi ndani ya chama.
 
Pamoja ni chama kubwa kama unavyodai lakini kuna madai ya msingi wanachama wanataka yatimizwe kama uchaguzi, uwazi, taarifa za fedha, kuodosha ubaguzi nk. kama yatafanyika hayo ndiyo uhai wa chama la sivyo kesho na keshokutwa atazuka Mwigamba mwingine kwa sababu hoja iko palepale.


Huko nyuma walishazuka Mwigamba wangapi but CDM inazidi kukua?... Mawazo ya Mwigamba ni sawa na mpo kwenye mashindano ya magari kutoka Dar hadi Moro, mmefika Chalinze, CCM mmeshamuacha Mlandizi huko halafu Mwigamba anasema "simamisheni gari, hii JEEP sio nzuri, twendeni turudi Dar najua kuna jamaa ana Vogue yake nzuri sana atatuazima tukamalizie nayo mashindano"!!!
 
Sometimes watu wanadhani demokrasia bora ni kumsikiliza kila mtu kwa kila anachosema. Binafsi naamini CDM ingewaendekeza kina Shitalamba, Kafulila, Mkosamali, Madiwani wa Arusha nk leo ingekuwa vipande vipande. Kama una mawazo yatakayowachanganya wananchi, hata yawe mazuri namna gani, hayaruhusiwi yaingilie momentum ya chama. Tukianza kupiga maktaim na hoja za kumng'oa Mbowe sasa hivi tutabaki hapa hapa, alafu tukija kushtuka CCM wameshatuacha tena km 100...
Haijawa vipande vipande lakini chama kiko mapande mawili ndiyo maana karibu wote walionyanyasika ni wa kanda ya ziwa baadhi ni hao uliowataja hapo juu pamoja na Shibuda, Zitto, Kabouru, Wangwe, Mwigamba nk. lakini wa Moshi-Arusha wanakula kuku.
 
Amegundua au Ameshauriwa na magamba kuongea hivyo!
Kama angeikandya cdm watu walishajua kwamba katumwa na magamba, asingefaidika yeye wala magamba.
Anajaribu kutumia mbinu hii ili arudishiwe cheo chake, harafu abadilishe mtindo wa uharibifu wake!
Magamba yameona yameshtukiwa ndio wamemshauri hivyo.
So be careful na mtu kama huyu!
 
Wakuu kama mnavyojua leo Mwigamba aliahidi kuzungumza na waandishi wa habari.... ... Nitakuwa nawaletea live kutoka eneo la tukio....... Niko hapa Premier Palace Hotel..... Mda wowote kuanzia sasa Mwigamba ataanza kuzungumza.....

Nawakilisha
====================
Mwingamba ndiyoanaingia..
Awali ya yote napenda kuongea na watanzania na wanaoipenda chadema wanaoipenda chadema na wenye imani na chadma wanao amini kuwa chadema ndiyo mkombozi wao, imani yao hiyo ni sahihi kabisa hata mimi ninaimani hiyo na wale wale wanoamini kuwa yaliyotokea juzi kuwa yataisambalatisha chadema wanakosea, chadema ni taasisi ambayo ni mjumuiko wa watu wengi wenye mitazamo tofauti, ndugu wana habari mimi ndiyo samson Mwigamba mwanachama wa chadema nilijiiunga nikiwa usa river 2004 nikifundisha ukidoma sec...machi 2012 nilichaguliwa kuwa kuwa mwenyekiti wa chadema mkoa wa Arusha.Mabadiliko tunayo hitaji yatapatikana kupitia chadema kama wote mjuavyo ni kiongozi pekee niliye andika makala nyingi kuliko kiongozi yoyote pamoja na kutishiwa akiwemo katibu wa bunge na baadae kukamatwa na leo hii nina kesi mahakama ya kisutu, siyo hayo tu baada ya maandamano ya mwaka 2011 mwajiri wangu aliniambia nichague moja kazi au chadema nilichagua chadema bila kujali mshahara wa 1,900,000 niliokuwa nalipwa. nilifanya hivyo kwa mapenzi yangu niliyo nayo chadema na nina amini niko sahihi..
==============
Sasa Mwigamba anaelezea namna ilivyokuwa siku hiyo anasema Lema aliingia kwenye ukumbi akamkuta mwenyekiti akitoa speech lema akiw na IPAD mkononi akaa sehemu yake lakini baada ya muda akasimama na kumwambia mwenyekiti samahani kuna jambo la dharua.. lema akaanza kuelezea alichokiona kwenye mitandao, Selesini akanyosha mkono kumuomba lema asome kilicho bandiko husika. alipo maliza wakatoa pendekezo kuwa laptop ikabidhiwe meza kuu akiwa bado hajawaambia anakadhidhi ama laah lema alifika na kumnyakua ile laptop na kumwita mwenyekiti wa chadema mkoa wa manyara mabae ni mtaalamu wa IT akaiwasha wakagundua inapassword Mwigamba hakuona tatizo kutoa password akatoa wakaanza kulinganisha path na kujiridhisha kuwa ilitoka kwake basi ile laptop ikarudishwa meza kuu

LEMA kitu kinachoitwa ustaarabu kimemshinda kabisa! anatamba kwa kuwa CHADEMA ni ya wamachame wenzake!
 
Ninachowapenda LB7 mna akili kuliko hata Wasira. Maana yeye alijichanganya akatoa time frame. Eti inasambaratika ndani ya mwaka mmoja. Leo mwaka umeisha, but akisikia neno CDM anakurupuka bila kuvaa pichu kwenda "DAKIKA 45" ITV...

Na wewe Tuko, umeamua kujitoa ufahamu!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom