kibogo
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 9,739
- 4,746
Wakuu kama mnavyojua leo Mwigamba aliahidi kuzungumza na waandishi wa habari.... ... Nitakuwa nawaletea live kutoka eneo la tukio....... Niko hapa Premier Palace Hotel..... Mda wowote kuanzia sasa Mwigamba ataanza kuzungumza.....
Nawakilisha
====================
Mwingamba ndiyoanaingia..
Awali ya yote napenda kuongea na watanzania na wanaoipenda chadema wanaoipenda chadema na wenye imani na chadma wanao amini kuwa chadema ndiyo mkombozi wao, imani yao hiyo ni sahihi kabisa hata mimi ninaimani hiyo na wale wale wanoamini kuwa yaliyotokea juzi kuwa yataisambalatisha chadema wanakosea, chadema ni taasisi ambayo ni mjumuiko wa watu wengi wenye mitazamo tofauti, ndugu wana habari mimi ndiyo samson Mwigamba mwanachama wa chadema nilijiiunga nikiwa usa river 2004 nikifundisha ukidoma sec...machi 2012 nilichaguliwa kuwa kuwa mwenyekiti wa chadema mkoa wa Arusha.Mabadiliko tunayo hitaji yatapatikana kupitia chadema kama wote mjuavyo ni kiongozi pekee niliye andika makala nyingi kuliko kiongozi yoyote pamoja na kutishiwa akiwemo katibu wa bunge na baadae kukamatwa na leo hii nina kesi mahakama ya kisutu, siyo hayo tu baada ya maandamano ya mwaka 2011 mwajiri wangu aliniambia nichague moja kazi au chadema nilichagua chadema bila kujali mshahara wa 1,900,000 niliokuwa nalipwa. nilifanya hivyo kwa mapenzi yangu niliyo nayo chadema na nina amini niko sahihi..
==============
Sasa Mwigamba anaelezea namna ilivyokuwa siku hiyo anasema Lema aliingia kwenye ukumbi akamkuta mwenyekiti akitoa speech lema akiw na IPAD mkononi akaa sehemu yake lakini baada ya muda akasimama na kumwambia mwenyekiti samahani kuna jambo la dharua.. lema akaanza kuelezea alichokiona kwenye mitandao, Selesini akanyosha mkono kumuomba lema asome kilicho bandiko husika. alipo maliza wakatoa pendekezo kuwa laptop ikabidhiwe meza kuu akiwa bado hajawaambia anakadhidhi ama laah lema alifika na kumnyakua ile laptop na kumwita mwenyekiti wa chadema mkoa wa manyara mabae ni mtaalamu wa IT akaiwasha wakagundua inapassword Mwigamba hakuona tatizo kutoa password akatoa wakaanza kulinganisha path na kujiridhisha kuwa ilitoka kwake basi ile laptop ikarudishwa meza kuu
Mwaka 2011, Mwalimu Secondary na mshahara wa Tsh. 1,900,000/= mbona inaonyesha wazi huyu jamaa ni muongo? yaani hata mkuu wa Idara Secondary wakati huo alikuwa hapokei kiasi hicho cha fedha.