Mkutano wa Mwigamba na vyombo vya habari

Mkutano wa Mwigamba na vyombo vya habari

Atasema kuwa aliondolewa makao makuu kwa hila.

Atasema aliombwa kufanya kazi pale lakini mambo yakaenda ndivyo sivyo.

Atasema hakuna uhuru wa kutoa maoni. Atasema kuna ukabila na udini.

Atasema yeye ni msomi hawezi kutumika. Kisha atasema anaipenda Chadema na kambi ya upinzani na ni muumini wa mabadiliko.

Atasema anakusudia kukata rufaa. Atasema anaenda mahakamani.

Hakuna mapya!

Bosi mbona unamwekea maneno mdomoni?

Nikwambie kitu, unakuwa kama baba aliyekorofishana na Housegirl aliyekuwa anatembea naye, sasa mama akianza kuulizia vipi! Baba anaanza huyu mpuuzi sana, anataka aseme eti nilikuwa natembea naye, au nimemtongoza.

Ha ha ha!
 
Pambana Mwigamba pambana tunataka viongozi wapya chadema Mbowe, Zitto na Slaa wakae pembeni maana wanaharibu chama na wanajenga makundi
Usijali usajili wake unakamilika hivi punde atakuwa CCM akaungane na Shoza na Mwampamba...
 
Kama Mwigamba atajibu maswali haya, tutamwelewa. akijikanyaga tu!!!!. Aende kwa shonza na Juliana hajachelewa bado fungu limetengwa kwa kazi yao ya kishetani!!.

Swali la kwanza:
1. Nini lengo na nia ya andishi lako mtandaoni?.
2. Ukiwa kama kiongozi, unajua hali ambayo CDM inapitia kisiasa kwa sasa?. kama unafahamu unadhani kubadili uongozi kutaleta afya kwa chama au maafa?.
3. Unaweza kuwasemeaje ama unaweza kujitofautishaje na masalia waliofukuzwa ndani ya CDM?.
4. Wewe kama mwanadam, unajua kuwa ipo siku utahukumiwa mbele za Mungu kwa nia yako Ovu au safi.Unajipimaje katika mazingira ya hukumu ya Mungu na nia/lengo la andishi lako na haya unayojinasibu kuwa hukuwa na nia mbaya?
 
Hiyo ndo dawa ya wasaliti na wanafiki wa umri wake! Kupigwa tu.Kuna watu wanakatisha tamaa sana kwenye hii safari ya ukombozi,najaribu kutafakari juu ya hawa watu tuliowamini kiasi hiki wanawezaje kufanya mambo ya ajabu kiasi hiki? Mwigamba aliyehubiri saa ya ukombozi kwa ujasiri kupitia kalamu yake ,kuna wakati alikuwa anaandika CCM itakavyo angamia akitumia mifano ya maneno ya vitabu vitakatifu,akadiriki kuonyesha ujasiri hadi kwenye vyombo vya dola kwa kuwashawishi wapiganaji wa vyombo hivyo kugoma! Leo mtu mjasiri mbele ya Davis Adolf Mwamnyange,Said Mwema,Manumba nk. eti anamuogopa Mh Mbowe hadi anadiriki kukana jina lake ? Aibu kiasi gani hii! Kiukweli Samson Mwigamba si tu kwamba ni msaliti ni mtu dhaifu sana asiyestahili kuwa kiongozi wa ngazi yeyote.Labda mimi ndo simuelewi vizuri Mh Mbowe yawezekana nguvu zake zinapimwa kwa mizania ya amiri jeshi mkuu? Labda! Lakini kiukweli safari yetu CDM bado ina vikwazo vingi,rejea watu aina ya Juliana,Mtela,Matata meya wa Mwanza eti hawa ndo chama kingechukua Nchi ndo wangesaidiana na Dr Slaa na Mbowe kuendesha serikali! Ni vigumu wakati mwingine kuzuia mawazo kwamba kama hawa ndo viongozi tulionao bora hata ya kuendelea na CCM japo kuwa fikra hizi sitaki zikae zinajirudia kichwani mwangu.Natamani watu hawa aina ya Mwigamba,Juliana,Mtela nk. wajue ni kiasi gani tuna-feel kwa matendo yao ,lakini utajuaje pengine wanafurahia matokeo haya maana huenda mission yao inakuwa imetimia,ila kama mnafanya kwa bahati mbaya jua mnachotufanyia sio fear hata kidogo.

"M4C Segerea"

Umeandika kwa uchungu sana..
 
Mwigamba aliamini cdm itamlipa zaidi..., mambo yamekuwa tofauti, badala ya kufaidi ruzuku amejikuta akiwa Maskini Mkulima. Hapa mimi napata picha, tatizo la cdm na vyama vingine vya siasa ni mapato. Vijana wanategemea kula chamani hivyo pesa ya chama isipofika mikoani kwa wakati basi matatizo yanaanza. Kama sikosei, hata akina shonza walidai kutokulipwa ilhali heche akilipwa mshahara wa kutosha. Suluhu ya haya yote ni kuhakikisha chama kinawawezesha vijana wake ili waweze kujitegemee, vinginevyo migogoro haitaisha,
Kama wamefata mshiko wahamie ccm,mpaka mtu anakumbuka 1,900,000 ujue njaa ndio ilimleta cdm
 
Huwezi kuwa insider and outsider kwa wakati mmoja mkuu. CHADEMA hawajamtupa Mwigamba, wamemsimamisha uongozi. Kwa falsafa yako hii, ina maana wamemleta huku nje tuliko sisi ambako ndipo alikochagua mwenyewe kuongelea... outsider. Kwa sasa Mwigamba ni kama mimi tu, an outsider, aje huku tunamuhitaji kwenye kuongea...

Mojawapo ya disadvantage kubwa sana ya democracy ni concept ya Wengi wape, hata kama wako 100% wrong. Hapa inafanyika kuaminisha wengi kwamba Mwigamba kakosea na aliyosema ni uongo mkubwa, jamii (Walio wengi) wakishakubali hilo basi tayari ushindi umepatikana, tutamuita Mwigamba msaliti, masalia, muasi na kadhalika.
Ni kweli sasa Mwigamba ni kama mimi na wewe tu, Outsider na yuko huru kuongea lolote tu. Tatizo litaonekana ni upande wake tu katika maisha yake kisiasa, wengi wetu tutasema amecommit political suicide japo mimi nitaita political murder.Tutakachoshindwa kutambua ni ushindi wa giza dhidi ya nuru!
 
Chadema wamenisikitisha sana,,,,kama wanadai saimon mwigamba amekiuka katiba ya cdm,,,kwa nini waamue kujichukulia sheria mkononi na kuumpiga mwigamba.....kwakweli cdm imenikera sana ,,,,,isitoshe wamefanya hivyo mbele ya mwanzilishi wa cdm mh mtei,,,,,

Apigwe tuu maana tumechoka..
 
Mmh serikali haijakosea kurudisha mpango wa jkt ili kuhakikisha kila raia anajua kupigana / kujihami anapokutana na dhoruba kama ya mwigamba manaake sasahivi kila mtu anajifanya jonsina.
Tunasubira kaka
 
Lumumba FC mbona mnazidi kupungua kwenye thread

tuliwaambia Mwigamba hana jipya,

Chadema imeshamwagiwa majitaka ya kila aina kilichobaki ni marudio tu.
 
Atasema kuwa aliondolewa makao makuu kwa hila.

Atasema aliombwa kufanya kazi pale lakini mambo yakaenda ndivyo sivyo.

Atasema hakuna uhuru wa kutoa maoni. Atasema kuna ukabila na udini.

Atasema yeye ni msomi hawezi kutumika. Kisha atasema anaipenda Chadema na kambi ya upinzani na ni muumini wa mabadiliko.

Atasema anakusudia kukata rufaa. Atasema anaenda mahakamani.

Hakuna mapya!

Usimlishe maneno kaka, mwache aongee kwanza (hii ni style ya kudilute kosa),

Unakuwa kama baba aliyegombana na Housegirl aliyekuwa anatembea naye, sasa mama akiuuliza vipi? Baba anadakia akisema, "Huyu mpuuzi sana, eti anataka kusema mi nilikuwa natembea naye".

Ukweli utajulikana tu.
 
Hakikisha Mzee wa Sumu hayupo maana unaweza pofoka soon! Ujiridhishe Kama hayupo Arusha maana yupo kimya ndani ya JF huenda yupo busy akiratibu mpango wa tindikali!

Huo ndio wosia wangu kwako pia ujitahidi sana kutotembea peke yako na usijulikane unalala wapi!

Angalizi tafadhali sana Mzee wa Sumu mwache Mwigamba tunakusihi sana ndugu yetu bado baba yetu tunampenda!

Sawa kabisa Mwigulu atakuwa amekusikia..
 
Mleta mada angalia Saa yako! sredi imegeuka kuwa Kijiwe cha Kahawa fuly Porojo!!
 
looking at it from different angle, tunaishi katika nyakati na jamii ambapo ukweli haupendwi na unaogopwa kuliko uongo. Mwigamba anaendelea kuwa positive kwa alichokifanya akiamini alichokisema alikusudia kilete positive impact kwa chama na jamii nzima. Ni kweli angeweza kuyasema ndani ya kikao as insider, lakini ya ndani hayatakiwi kutoka nje na aliona inatakiwa impact kutoka nje to make it happen ndio sababu aliamua kuongea as an outsider.
Ni muhimu kwa chadema na wanachadema kutambua kuwa ikiwa chama kinahitaji kuingia madarakani then tegemeo ni wananchi wasio wanachama wa chadema. Wanachama watasaidia tu kukipigia debe chama lakini kura za wanachama tu ni nyongeza ndogo sana. Kama wanachama wanaamua tu kumhukumu na kumtupa mwigamba basi impact yake ni kubwa mno kwa wananchi (wapiga kura) na watu wengine makini. Mwigamba kufanya kosa sio ishu, ishu ni kwanini kaamua kufanya kosa hilo???

hivi kweli kwa position ya samson mwigamba kama mwenyekiti cdm mkoa wa arusha anaamua kufanya hivyo,,,,hii inadhihirisha kabisa ndani ya cdm kuna fukuto na hakuna haki yakujieleza coz angetumia mikutano ya cmama kufikisha mawazo yake,,,wengine wanahisi ni msaliti lakini kuna siri kubwa sana ndani ya cdm,,,,watakataa mdomoni ila moyoni watakubali tu
 
Mwigamba umenisikitisha sana kwa usaliti huu.
 
hivi kweli kwa position ya samson mwigamba kama mwenyekiti cdm mkoa wa arusha anaamua kufanya hivyo,,,,hii inadhihirisha kabisa ndani ya cdm kuna fukuto na hakuna haki yakujieleza coz angetumia mikutano ya cmama kufikisha mawazo yake,,,wengine wanahisi ni msaliti lakini kuna siri kubwa sana ndani ya cdm,,,,watakataa mdomoni ila moyoni watakubali tu

kuliko ile ya magamba ya kutaka kumpora rais uenyekiti wa chama?
hebu tupe dondoo za siri hiyo mkubwa!!
unaonekana kujua mengi ya cdm kuliko yale ya ugambani unakoishi kwa b7.
 
Kama wamefata mshiko wahamie ccm,mpaka mtu anakumbuka 1,900,000 ujue njaa ndio ilimleta cdm

bado chadema haijapata watu ambao ni loyal kwa chama...

Pia cdm lazima wajue kuwa viongozi wake ambao hawana ajira ama vyanzo mahususi vya vipato wanalia njaa. CCM wanaombea hiyo njaa iwe kali zaidi ili wapate kuwatumia kuibomoa cdm. Viongozi waandamizi wa cdm pia wanatumia njaa ya viongozi wa chini na kati ili kupata uungwaji mkono katika harakati zao za kisiasa. Tukihitaji cdm imara tuanahitaji viongozi wasiotegemea ruzuku za chama kuendesha maisha yao.
 
Back
Top Bottom