Mkutano wa Mwakyembe na Hoja za Mgongano wa Maslahi

mi nashangaa watu wanaompigia kura mtu ambaye hana hata uchungu na maisha yao. hivi RA wanampa kura za nini? hivi watu wa huko igunga wakoje? napenda siku moja niwaone.

kuhusu dowans, RA anajua hasara itakayopatikana asipouza ile mitambo, hivyo anang'ang'aniza kwa nguvu zake zote, akitumia magazeti na mitandao yake yote, ili alimradi apate kitu isiwe hasara kubwa kakwe. anatapatapa. Watanzania tusimpe nafasi, akitapatapa asijeinuka, tumbane palepale chini hasi atoe kamasi. moto wa mafisadi umeshawashwa. hata watu wakifa, upo mioyoni mwa watz wengi. kama hamuamini subirini kipindi cha uchaguzi mwakani mtaona,patawaka moto.
 
Ukweli ni kuwa RA ni FISADI, period. Yes ni hard working, kwenye UFISADI.

Dr ni , well, mwana CCM ila yes na yeye amesema maneno ya KIKABURU, kwa hiyo na yeye ni KABURU na inabidi awithdraw hizo statement zake kama anataka kuchukuliwa kama serious leader.

Hizi siasa za KIKABURU za "uzawa", yes zitapata support kubwa kwani tunacheza na numbers, lakini hazisaidii nchi hata siku moja. Ukaburu mbaya kule Afrika Kusini na ni Mbaya hata leo kwa Tanzania yetu. Tukemee haya kwa nguvu zote, tusijidanganye hata siku moja!

Mimi nimesikiliza mahojiano ya Dr. Mwakyembe na waandishi wa habari kama ilivyowekwa hapa JF (Shukran Invisible kwa hilo). Katika mahojiano yote, sijasikia kauli yoyote ambayo Dr. Mwakyembe alisema inayomfanya awe kaburu.

Alichosema Dr. Mwakyembe (ambacho wala hakina mjadala, kwa kuwa ni kweli) ni kwamba mara nyingi taasisi zetu hapa nchini, hujali zaidi watu wa nje na kuwapa kipaumbele kuliko waTanzania wa kawaida. Alitoa mfano wa jinsi Bank zetu zinavyotoa mikopo kwa urahisi zaidi kwa wazungu, wahindi, waarabu n.k. na kuwapa shida sana waTanzania wengine wa kawaida kupata mikopo hiyo. Kwa mtazamo wangu ni kwamba, kauli kama hizi si za kibaguzi. Ubaguzi unatokana na kauli za kutaka watu wa rangi/jinsia/kabila/imani/itikadi au vinginevyo kupewa kipaumbele zaidi ya wengine. Dr. Mwakyembe angekuwa mbaguzi kama angesema ni vyema waTanzania wapewe kipaumbele zaidi ya watu wengine wasio na asili ya Tanzania (hakusema hivyo, bali alionyesha masikitiko yake kutokana na ubaguzi unaoonekana kuwepo dhidi ya waTanzania). Ubaguzi hauwezi kuwepo kwa kutoa malalamiko ya ubaguzi unaofanywa. Ubaguzi unakuwepo kwa kuanzisha ubaguzi usiokuwepo dhidi ya tabaka fulani.

Sidhani kama kuna mtu hapa anaeweza kukanusha ukweli kuwa imefikia kwamba kampuni za watu binafsi (waTanzania wa kawaida) kuamua kuajiri au kuuza share zao kwa watu wa nje ili tu waweze kupata sauti na attention inayohitajika katika maombi na mambo mengine wanayotaka kuyafanya ili kukuza biashara zao. Vingenevyo, biashara zao haziwezi kufika popote.

Hii ni kasumba iliyojengeka ndani ya fikra za waafrika wengi. Kasumba kuwa Mwafrika hawezi bila kusaidiwa na mtu mwingine wa nje ya Afrika kwa kuwa hajui au hana utaalamu au uaminifu unaotosha kupewa kipaumbele anachohitaji kuendesha shughuli zake.
 
mi nashangaa watu wanaompigia kura mtu ambaye hana hata uchungu na maisha yao. hivi RA wanampa kura za nini? hivi watu wa huko igunga wakoje? napenda siku moja niwaone.

kuhusu dowans, RA anajua hasara itakayopatikana asipouza ile mitambo, hivyo anang'ang'aniza kwa nguvu zake zote, akitumia magazeti na mitandao yake yote, ili alimradi apate kitu isiwe hasara kubwa kakwe. anatapatapa. Watanzania tusimpe nafasi, akitapatapa asijeinuka, tumbane palepale chini hasi atoe kamasi. moto wa mafisadi umeshawashwa. hata watu wakifa, upo mioyoni mwa watz wengi. kama hamuamini subirini kipindi cha uchaguzi mwakani mtaona,patawaka moto.

kuna ushahidi kuwa ile mitambo yake? au?
 
Spika inabidi aelewe kuwa wabunge wana haki zote za kiraia, na kama wanataka kuongelea mambo yao nje ya bunge wanaweza.

Spika hana wajibu wala mamlaka ya kuwashurutisha wabunge jinsi ya kuongea nje ya bunge, almuradi hawavunji kanuni za bunge.Nafahamu kuwa hawavunji.

Kama kuna watu wanaoweza kuwashurutisha wabunge hawa jinsi gani ya kuongea basi ni chama chao, CCM. CCM wameshafanya hivyo.

Chombo chochote kinachoingilia jinsi gani wabunge hawa wajieleze kinavunja misingi muhimu ya demokrasia, ikiwamo uhuru wa kujieleza.

Kwa kuongezea tu, suala linalojadiliwa halijafikishwa Bungeni. Speaker anaweza kuchukua hatua kama suala limeshajadiliwa na Bunge na uamuzi kupitishwa na Bunge. Ni baada ya hapo tu, ndipo Kamati ya maadili inaweza kujadili mgongano huu kwa kuzingatia maamuzi yaliyokwisha pitishwa.
 
Kuna habari kwamba Mtikila na leo atazungumza na waandishi wa habari kuzungumzia kuwasema wengine na huenda akawasema wale wanaopingana na Rostam kwa maana leo huenda akamsaidia Rostam. Huyo ndiye Mtikila, hebu tusubiri
 
kuna ushahidi kuwa ile mitambo yake? au?
Hata kama si yake ila ana connection au maslahi na ile mitambo!hujiulizi kwa nini magazeti yake yanatetea sana pia campuni hii ya Dowans kutumia aniani yake ya CAsPIAN. Richmond/downs!haihitaji kuwa Isaac Newton kujua kuwa RA ana uhusiano na Dowans
 
Hata kama si yake ila ana connection au maslahi na ile mitambo!hujiulizi kwa nini magazeti yake yanatetea sana pia campuni hii ya Dowans kutumia aniani yake ya CAsPIAN. Richmond/downs!haihitaji kuwa Isaac Newton kujua kuwa RA ana uhusiano na Dowans

Jee, Dowans imetenda dhambi gani? ukifatilia habari kwa makini utakuta kuwa Dowans wamepandishwa mkenge na Richmond au hilo hulioni?

Rostam ni mfanya biashara, ikiwa Dowans wametumia address zake za Caspian hilo si tatizo kwani inabidi ufahamu kuwa, muwekezaji aliyeenda shule, kabla ya kuwekeza katika nchi ngeni ni busara kwake kuanza kuwatafuta wenyeji wenye biashara zinazofanana na zake au zenye ukubwa unaofanana ili awe na mwenyeji na ndio maana tunazo chamber of commerce, BET na kadhalika, akiwapata hao wafanya biashara wakamkaribisha hawezi akatumia anuani au namba za simu za hoteli, obviously atatumia namba za mwenyeji wao katika kujisajili, na sidhani kama hili ni kosa. Au RA kujuwana na mwenye Dowans, hilo ni kosa pia?

Tutazame ukweli na tusikurupuke kwa ajili ya chuki binafsi zinazopandikizwa kwenye vichwa vyetu, narudia, RA hayuko juu ya sheria, kama kuna kosa lolote unaloliona anafanya, hata wewe unaruhusiwa kwenda mahakamni kumshitaki, lakini hakikisha unakwenda na ushahidi tosha sio Dowans wametumia namba ya simu ya caspian basi ndio uwe ushahidi, utajuta kwenda mahakamani kwa hilo.

Kuna mtu anaependa kwenda mahakamani kushitaki kama mtikila? serikali yenyewe kisha ishitaki na kuna kesi kisha ishinda serikali, unalijuwa hilo? na unajuwa jinsi RA alivyomuumbuwa mtikila? sasa nambie ikiwa huyu mtu ana-madhambi yote haya, hakuna hata moja la kushitakika? na mtikila hajaliona hilo?

Au ni ''agenda za siri''?
 
Kama Rostam ni mbaguzi, kwa nini Mtikila alienda kukopa kwake? Mtikila aache unafiki
 
Mimi nimesikiliza mahojiano ya Dr. Mwakyembe na waandishi wa habari kama ilivyowekwa hapa JF (Shukran Invisible kwa hilo). Katika mahojiano yote, sijasikia kauli yoyote ambayo Dr. Mwakyembe alisema inayomfanya awe kaburu.

Alichosema Dr. Mwakyembe (ambacho wala hakina mjadala, kwa kuwa ni kweli) ni kwamba mara nyingi taasisi zetu hapa nchini, hujali zaidi watu wa nje na kuwapa kipaumbele kuliko waTanzania wa kawaida. Alitoa mfano wa jinsi Bank zetu zinavyotoa mikopo kwa urahisi zaidi kwa wazungu, wahindi, waarabu n.k. na kuwapa shida sana waTanzania wengine wa kawaida kupata mikopo hiyo. Kwa mtazamo wangu ni kwamba, kauli kama hizi si za kibaguzi. Ubaguzi unatokana na kauli za kutaka watu wa rangi/jinsia/kabila/imani/itikadi au vinginevyo kupewa kipaumbele zaidi ya wengine. Dr. Mwakyembe angekuwa mbaguzi kama angesema ni vyema waTanzania wapewe kipaumbele zaidi ya watu wengine wasio na asili ya Tanzania (hakusema hivyo, bali alionyesha masikitiko yake kutokana na ubaguzi unaoonekana kuwepo dhidi ya waTanzania). Ubaguzi hauwezi kuwepo kwa kutoa malalamiko ya ubaguzi unaofanywa. Ubaguzi unakuwepo kwa kuanzisha ubaguzi usiokuwepo dhidi ya tabaka fulani.

Sidhani kama kuna mtu hapa anaeweza kukanusha ukweli kuwa imefikia kwamba kampuni za watu binafsi (waTanzania wa kawaida) kuamua kuajiri au kuuza share zao kwa watu wa nje ili tu waweze kupata sauti na attention inayohitajika katika maombi na mambo mengine wanayotaka kuyafanya ili kukuza biashara zao. Vingenevyo, biashara zao haziwezi kufika popote.

Hii ni kasumba iliyojengeka ndani ya fikra za waafrika wengi. Kasumba kuwa Mwafrika hawezi bila kusaidiwa na mtu mwingine wa nje ya Afrika kwa kuwa hajui au hana utaalamu au uaminifu unaotosha kupewa kipaumbele anachohitaji kuendesha shughuli zake.

Recta,

Kauli inayosemwa ilikuwa ya kibaguzi ni ile ya "wengine wana passport tatu tatu, sisi ni wazawa/wazalendo hatuna kwa kwenda na tutafia hapa hapa" Sija quote exactly ila ilikuwa karibu na hiyo.

Hivi Dr. Hayajui ya Ballali? Mweusi mwenzetu yule na katuibia na kuishia visiwani huko.

Hayajui ya Chenge, mweusi mwenzetu huyo na visenti vyake kwenye visiwa.

Sidhani kama Dr. ana ushahidi kwamba Rostam ana passports tatu, kilikuwa kijembe cha kisiasa ambacho kinalenga kwenye ubaguzi.
 
hakuna ubaguzi, na hata ungekuwepo kusingekuwa na uwongo, ingekuwa kweli. kwanini watz wa asili ya asia siku zote ndo wanakuwa hivyo? hata kama weusi wenzetu wako hivyo lakini percentage kubwa ni wahindi na waarabu. cha maana ni kubadili tabia na kujitahidi kufanya mema ili waisafishe mioyo ya wtz wawaamini. kuna ukweli kuwa, hawa watu ndio wamekuwa mafisadi wa kutupwa tangu awali, walishajijenga na kuwadondosha yataka moyo, wana network kibao.
 
Kuna habari kwamba Mtikila na leo atazungumza na waandishi wa habari kuzungumzia kuwasema wengine na huenda akawasema wale wanaopingana na Rostam kwa maana leo huenda akamsaidia Rostam. Huyo ndiye Mtikila, hebu tusubiri

Tayari amekwisha kuzungumza na kumtukana matusi ya nguoni Mengi. Huyo ndiye Mtikila
 
Mtikila ni call box, akija Mangugu akaweka coin itasema, akija Panjun akaweka rupia ataimba, akaja Kunguru akaweka noti, atatukana, akaja Mwangananga akaweka fedha ataimba kwaya na kadhalika. Alitumika mwaka 1995, 2000, 2005 na sasa anarudi tena. Enyi Wadanganyika SAA YA UKOMBOZI NI SASA!!!!!!
 
Recta,

Kauli inayosemwa ilikuwa ya kibaguzi ni ile ya "wengine wana passport tatu tatu, sisi ni wazawa/wazalendo hatuna kwa kwenda na tutafia hapa hapa" Sija quote exactly ila ilikuwa karibu na hiyo.

Hivi Dr. Hayajui ya Ballali? Mweusi mwenzetu yule na katuibia na kuishia visiwani huko.

Hayajui ya Chenge, mweusi mwenzetu huyo na visenti vyake kwenye visiwa.

Sidhani kama Dr. ana ushahidi kwamba Rostam ana passports tatu, kilikuwa kijembe cha kisiasa ambacho kinalenga kwenye ubaguzi.

Well said Mtanzania! Kwa muda mrefu watz kuna wanasiasa wakizidiwa hoja wanakimbilia kwenye rangi. Ni uvivu wa hoja, hakuna zaidi, na hapa Mwakyembe alitokota na amempa angle nzuri sana Rostam ya kutokea. Hata ile ya kulialia kwamba Rostam anatumia magazeti yake kumchafua ni hoja dhaifu sana. Yeye alipaswa ku-address issue yake ya mgongano wa kimaslahi ambayo, kwa maoni yangu, ni rahisi kabisa kuipangua.

Mwakyembe anajua kuongea na kupanga hoja. Tatizo lake ni uzembe wa kuchagua maneno na kuingiza vijembe vya kisiasa katikati ya hoja nzito na ya maana. Hata pale alipokuwa anaongelea kuhusu Dowans alikuwa na hoja nzito sana katika kupinga ununuzi wa mitambo hiyo ya kifisadi, lakini aliharibu kabisa alipoanza kuingiza mambo operesheni sangara. Alipofanya hivi wengine akatuudhi, tukamdharau na kudharau maudhui mazima ya hotuba yake! Sasa na katika hili la juzi, alikuwa na hoja nzuri sana katika kujitetetea kuhusu yeye kuwa ni shareholder wa ile kampuni ya umeme, lakini aliharibu kabisa ladha ya hotuba yake alipoanza kuingiza mambo ya uzalendo na kujiona yeye, kwa kuwa ni mweusi na kazaliwa Mbeya, kwamba ni mtanzania wa maana zaidi kuliko wengine, supposingly wale wenye asili ya asia. This was rubbish and it completely killed his good message.

Wanasiasa wetu inabidi waelewa kwamba katika siasa "it is what people hear rather than what you say" that matters. Sasa kwa hili, yes Mwakyembe alikuwa na mengi mazuri aliyoyasema, lakini walichokisikia watu ni hilo la ubaguzi, na sidhani kwamba ndio ujumbe wa maana aliokuwa anataka watu wausikie. Angekuwepo Nyerere, kwa kuingiza mambo ya ubaguzi, ndio na uanasiasa wake ungekuwa umefika kikomo!
 
alikuwa na hoja nzuri sana katika kujitetetea kuhusu yeye kuwa ni shareholder wa ile kampuni ya umeme, lakini aliharibu kabisa ladha ya hotuba yake alipoanza kuingiza mambo ya uzalendo na kujiona yeye, kwa kuwa ni mweusi na kazaliwa Mbeya, kwamba ni mtanzania wa maana zaidi kuliko wengine, supposingly wale wenye asili ya asia. This was rubbish and it completely killed his good message.


Mwalimu Nyerere alisema mwaka 1995 kuwa anachukia ukaburu - na kwa maana aliyoitoa wakati ule ni uzawa. Yaani watu kwa sababu wao ni weusi basi wao ndiyo wana haki ya kuishi Tanzania na wengine hawana haki. UKABURU MTUPU
 
lakini aliharibu kabisa ladha ya hotuba yake alipoanza kuingiza mambo ya uzalendo na kujiona yeye, kwa kuwa ni mweusi na kazaliwa Mbeya, kwamba ni mtanzania wa maana zaidi kuliko wengine, supposingly wale wenye asili ya asia. This was rubbish and it completely killed his good message.


- Maneno mazito sana haya ndugu Kitila, na ndio nimekuwa nikikisema kwamba maadui wa DK, kisiasa walichofanya ni kuwa-plant watu wao pale kwenye press wakiwa na one goal ya kumtoa DK kwenye hoja muhimu na kum-provoke kwa kumshambulia mapema kabisa,

-Either ni kwa bahati mbaya au ndio tabia ya DK akiwa provoked, akaishia ku-fall into his enemies hands, in the end akashindwa kuipangua hoja ndogo sana ambayo jana ilipanguliwa kirahisi sana na Mheshimiwa Shelukindo, kwamba kuna siku DK aliwahi kuji-excuse kwenye kikao cha kamati kutokana na kuelewa huu mgongano wake wa masilahi unaopigiwa kelele, sasa hapa angewarushia swali wabunge wengine bila ya kuwataja majina kwamba je wamewahi na wao kuji-excuse kwenye kamati zao?

- Ujumbe wangu kwa Wa-Tanzania wenzangu ni kwamba tusidharau mwiba kwa sababu huwezi kupigana na adui ambaye hujui mbinu zake, adui tunayepigana naye hapa ni too sophisticated kuliko wengi tunavyoamini na kumuelewa, tunamuongelea kama vile ni mtu mjinga mjinga tu mwenye hela basi!, shutuma nyingi tunazomrushia ni za kisiasa tu badala ya kisheria.

- Sasa ifike mahali tutafute hoja nzito za kisheria meaning legal facts za kumbana kwa sababu the little I know kuhusu huyu adui ni kwamba anaonekana kujua uchafu na hata harufu tu ya uchafu wa kila kiongozi wetu wa taifa, na huuachia to the public only anapotaka ku-advance biashara zake kwa sababu sio siri kwamba hapa the emergency ni kununuliwa kwa mitambo ya Dowans, ndio maana ikatokea ishu ya DK na mgongano wa masilahi.

Wito wangu kwa viongozi wetu wa sisi wanyonge huku upande wa pili, please mjitayarishe na muwe makini, tafuteni ushauri wa nje ya ma-box yenu, wachujeni kwa makini mnaojihusisha nao, tafuteni ukweli wa kisheria against adui kwa sababu huyu adui sio lelemama na amejitayarisha siku nyingi sana kuliko tunavyofikiri, halafu tusimdharau kwa sababu kisiasa ana strong record ya ushindi kwenye kila anachokigusa. Msisahau kwamba siasa bado ni mchezo mchafu sana unaowezwa kuchezwa vizuri zaidi na wanasiasa wachafu kama huyu adui.

Mungu Aibariki Tanzania.

William.
 
Hivi babake Obama alienda lini USA? Watu waliohamia Tanzania 1852 Mtikila anawaona ni wageni?

Mtanzania, nilidhani kama tunavyo jiita ni think tank basi tungecapitalise kwenye issues na kuzipa wait kubwa na kukejeri nonsense katika hoja. Hata Makanisani au misikitini sio kila kitu kinachosemwa na watumishi wa munu tunatakiwa tukichukue kama kilivyo lahasha tunatakiwa tuchuje kile tunachoona ni cha msingi na kinaukweli zaidi. Hapa mi nimeona issue kubwa nne:

1. Swala la ugabuzi wa RA na kesi iliyofunguliwa kuthibitisha hilo;
2. Maamuzi feki ya kamati ya bunge ikiiongozwa na Zitto;
3. Kifo cha chacha wangwe na way forward ya UDP;pamoja na
4. Pretense ya CCM kupambana na mafisadi na future impact zake.

Nadhani hizi ni issue za msingi mengineyo ni vibwanga na vionjo katika kuexpress jambo hasa kwamtu especially mwenye high temper. Hivyo ingefaa tujadili haya na may be kukejeri bla bla nyingine kama ulivyo fanya.
 
Mtikila ni call box, akija Mangugu akaweka coin itasema, akija Panjun akaweka rupia ataimba, akaja Kunguru akaweka noti, atatukana, akaja Mwangananga akaweka fedha ataimba kwaya na kadhalika. Alitumika mwaka 1995, 2000, 2005 na sasa anarudi tena. Enyi Wadanganyika SAA YA UKOMBOZI NI SASA!!!!!!

Unaweza kuwa sahihi kwa sababu unamfahamu vizuri mtikila. Hata hivyo nivema kuona kama hoja iliyopo hapo ni feki au ni ya msingi. Kama hoja aliyoitoa sasa iposambamba na mission zetu tucapitalize hapo japo tunajua the otherside.
 
...shutuma nyingi tunazomrushia ni za kisiasa tu badala ya kisheria.

- Sasa ifike mahali tutafute hoja nzito za kisheria meaning legal facts za kumbana....

Wito wangu kwa viongozi wetu wa sisi wanyonge huku upande wa pili, please mjitayarishe na muwe makini, tafuteni ushauri wa nje ya ma-box yenu, wachujeni kwa makini mnaojihusisha nao, tafuteni ukweli wa kisheria against adui kwa sababu huyu adui sio lelemama....... Msisahau kwamba siasa bado ni mchezo mchafu sana unaowezwa kuchezwa vizuri zaidi na wanasiasa wachafu....

Asante W. J. Malecela.

Hoja ulio njenga hapo juu ndio silaha yetu muhimu kutumia, kama kweli tunataka kujiwezesha kukabiliana na huyu adui.
 
Last edited:
Back
Top Bottom