Mkutano wa CHADEMA viwanja vya NMC Arusha

Mkutano wa CHADEMA viwanja vya NMC Arusha

Nyinyi fanyeni mchezo na hii Amani tu. Mtu akikosea lazima muwe wakweli, jiandaeni kumtetea mahakamani.


Amani hatadumu kwenye njaa, watu wanaweza kujivunia amani, lakini si kuvumilia njaa. Tanzania hakuna amani, NI KA UTULIVU TU AMBAKO KANAWEZA KUTOWEKA MUDA WOWOTE, NA KWA HAYA YANAYOTOKEA NA TUNAYOYAONA, KA UTULIVU HAKA HAKANA MUDA MREFU, TUKIFIKA 2015 BILA LOLOTE KUBWA KUTOKEA, BAHATI SANA. PLS, quote my words......
viva CDM
 
"ndugu wana Arusha kuanzia Leo natangaza Kuwa Tanzania kuna Jamhuri huru ya watu wa MERU. Mimi ndiyo Rais wa watu wa MERU na Lema ndiyo waziri mkuu. Tunamwambia kikwete Kuwa tuna andaa utaratibu wa kumpiga marufuku Kuja Arusha, tutaziba njia zote asije huku." Joshua Nassari , MB Arumeru Mashariki

Kama kweli hauna agenda ya siri ungetakiwa kueleza kila kitu kuhusu statement hizi. Kwanza kabisa uhaini hauwezi kufanywa kwa matamko ya jukwaani, uhaini unafanywa kwa vitendo. Pili Kamanda Mbowe aliliweka wazi hili on spot hivyo hakuna hoja hapa. Kuna watu wengi humu JF wanaitana mkuu, je mkuu wa nini?. Nadhani sasa tujifunze kuelewa lugha za vijana na sidhani kama Nassari ni msemaji wa sera za CDM.

Halafu mtu kujiita rais wa jamhuri isiyokuwepo si uhaini. Kama wangejitangaza kama wao ni rais na waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania hilo lingekuwa suala jingine. Lakini pia halitoshi tu kujiita hivyo kwani Tanzania ni nchi yenye katiba. CDM hawana jeshi, CDM hawana serikali hivyo matamshi kama haya sidhani kama yanaweza kuitwa ni kujiharibia. Ni lugha za hamasa tu. Japo watu wazima kama Mbowe wameyatolea ufafanuzi. Ukiaanza kufuatilia kila kauli ya mwachama wa kila chama utawehuka, fuatilia matendo yao.
 
Saizi ndio nimejua kwa nini Chadema walisusia sherehe za muungano kumbe ni mkakati maalum wa kujitenga...Nassari katuweka wazi picha halisi ya Chadema tunaiona sasa.

Mkuu ningeshangaa sana kama ungekosekana hapa, bado Rejao make hapa mnaweza kukesha kabisa, naamini una GB za kutosha kabisa kukesha kwenye hii thread,
 
Anatoa majibu ya kijinga nawe kwa ujinga wako unashangilia!!

Majibu kama hayo na kuhalalisha uvunjaji wa katiba ya nchi ndio kumetufikisha hapa tulipo!!

Nyie endeleeni na ujinga wenu kwani mahaba yenu kwa chama chenu yamewapofusha!!

Siwezi kumkimbiza mwehu...
 
Kwenye bold.
Huwezi kujitetea mahakamani kwa kusema toka enzi za Nyerere hakimu akakubaliana na wewe, neno 'toka enzi' si sheria kuhalalisha makosa mengine.

Bold ya pili, kuna makosa mengine yako wazi kiasi hayahitaji wanasheria 'amevunja katiba' PERIOD, nikiona mwizi anaiba sina haja ya kusubiri mwanasheria ili niseme.

Mkuu Feedback,
Sitaki kubishana na wewe maana hilo halikuwa lengo la ujumbe wangu. Niliona kuna kitu ambacho baadhi wachangiaji hawaelewi na nikaona umuhimu wa kuelemisha.
Kuna watu wametukana na kuna watu wamekebehi. Siwezi hata siku moja kupoteza usingizi kwa hilo.

Tanzania ina wasomi mahiri wengi tu akina Shivji, waulizeni na watawaambieni.

Hata zamani kulikuwa na watu wengi tu walikuwa wanakosoa serikali ilipokuwa inakiuka katiba. Kumbuka rais Nyerere alipomteua Mgonja kuwa mkuu wa mkoa wakati huo mgonjwa ubunge wake ulikuwa umetenguliwa na mahakama na akafungiwa kugombea ubunge kwa miaka mitano/kumi (sikumbuki vizuri). Kwa katiba ya wakati huo wakuu wa mikoa walikuwa pia wanakuwa wabunge.

Tumewapeni na mifano ya mawaziri kutoka Zanzibar lakini watu wanakimbilia kutukana. Unajua mwerevu hujifunza na mjinga hubisha mpaka ujinga unapomwumbua. Nyerere alikuwa na watu makini wengi wa kumshauri na alipokosea alikuwa anarekebisha mara moja. Hili sio katika mambo ambayo Nyerere alifanya makosa.

Ifike mahali kama utaratibu huu hatuupendi basi tuuondoe kwenye katiba mpya na sio kubisha tu kwasababu ya kubisha. Binafsi naona watanganyika tuna kila sababu ya kuupinga utaratibu huu. Kupanua wigo wa majadiliano ni kwamba hata UK wana utaratibu kama huu kisheria na wananchi wa England wanaupinga lakini bado unaendelea. Sisi tuna nafasi ya katiba mpya kufikia 2014 basi tuubadili.

Watu walilamika na Nyerere akakubali kwamba amefanya makosa na akatengua ukuu wa mkoa wa Mgonja.

Kwenye hili hakuna mahali popote kwenye katiba ya Tanzania panaposema Wazanzibari watakuwa mawaziri kwenye wizara zile tu ambazo zinahusu mambo ya muungano.
 
Nyinyi fanyeni mchezo na hii Amani tu. Mtu akikosea lazima muwe wakweli, jiandaeni kumtetea mahakamani.

Mkuu ebu acha ushabiki. Kufanya mchezo na amani ni kuanzisha vurugu na kuhatarisha maisha ya wananchi. Nafikiri wanaofanya mchezo na amani ni wale waliochinja mwenyekiti wa CDM. Nina hakika kama aliyechinjwa angekuwa ni CCM basi ingekuwa ni leading story kama vile wale waliomwagiana tindikali Igunga kwa kudhulumiana fedha za kubandika mabango ya Kafumu.

Chadema sidhani kama wanaweza kuleta vurugu kwa kwauli za hamasa majukwaani. Ila nitawapinga kwa nguvu zote kama wataamlisha watu waingie barabara kufanya vurugu bila ya kuwa provoked. Hakuna issue hapa mkuu. Take your dinner and sleep well. Leo Chelsea kashinda FA Cup!
 
Mimi ni mtu wa Kusini...CCM imetusaliti na CDM siiamini japo kwa punje ya uwele!! Huwa najiuliza, ikiwa CDM inatutupa mkono wakati wa kuitafuta keki ya taifa, je watatukumbuka wakati imeshapatikana!!!? napata shaka hasa nikikumbuka jinsi ambavyo Dr. Slaa alienda kusini kuomba kura! In few hourz, akapiga kampeni kwenye mikoa miwili....lakini bado wanatushawishi kwamba waliibiwa kura! Kama kuna mtu ninayemuona mjinga kuishabikia CDM basi ni mtu wa kusini unless kama ana nasaba na kaskazini!! Mtanzania mwingine yeyote labda anaweza kuishabikia CDM lakini sio mtu wa kusini!

Kutokana na mwenendo huu wa CDM ndio maana naiangalia kauli ya Dogo Janja kwa jicho la pili...!!
I'm missing something here, umesema wewe ni mtu wa Kusini unalalamika CDM kutofika huko, wakati huo huo unasema huiamini CDM na vilevile unasema mtu yeyote wa Kusini atakayeishabikia CDM ni mjinga.

Kwa nini basi unataka CDM wao waende huko? huoni hao watakaoshabikia watakuwa wajinga kama unavyosema.
 
Nilikuwa sijawahi kumsikiliza Heche leo nimekubali ni Kamanda!!
 
..Nassari ni **** ndo kaingia mjengoni anajipeleka kwa jasusi lema,jimbo litamshinda,nawashauri chadema jengeni chama chenu achaneni na hao wanaotaka toka ccm kama wanataka waanzishe chama chao kingine watawaaribia

we shoa huwe kutuchagulia wanachama shugulika na chama chako achana na chadema
 
"Wingi wa makamasi si ukubwa wa pua".
 
Huu mkutano kama ulifanyika Arusha, ujuwe 95-5!

Wakawaleta kutoka Moshi na dayosisi zote za karibu!

Kwi kwi kwi kwi teh teh teh.
 
Wadau,

Katika hali ya kushangaza, ama kuchanganyikiwa mwanachama maarufu wa CDM a.k.a "Dogo janja"

Ametamka hadharani katika viwanja vya nmc kuwa kama CCM ikiboa wataigawanya nchi kama Sudan.

Wakuu sijajua sababu ya kutoa maneno haya na nina wasiwasi sana na agenda hizi za siri, ukiunganisha na post ya

pasco ya ukaskazini ambayo sikuweza kuijibu kwa kuwa nilikuwa kifungoni naona kuna siri nzito imefichika.

Nawakilisha

Sasa watamwita ''DOMO GANJA''
 
Mkuu imenisikitisha sana hii, kumbe jamaa wana agenda ya kugawa kanchi ketu? ndio maana wanang'ang'ania utawala wa
majimbo.

Siri imefichuka, siri imefichukaa .........
A%20S-devil1.gif

Jamaa zako wa Jumuiya ya Uamsho wa dini kule visiwani Zanzibar wanaokusanya saini zenu ili kuvunja Muungano huwaoni? Saini yako haimo kwenye harakati za kutaka nchi mpya?
Huku tuwamoja hata kwenye
majimbo.
 
Tafadhalini saana, mwenye kipande cha sauti ya DOGO JINGA kuhusiana na kuigawa Tz aiweke jamvini.
Natanguliza shukrani.
 
Kumbe "mgodi" ndio triple M? ahsante kwa kutujuza, tutafanyia uchunguzi!

dogo soma acha kudandia mambo...kipi cha kufanyia utafiti, bado mavi yako kuyafanyia utafiti..
 
Tafadhalini saana, mwenye kipande cha sauti ya DOGO JINGA kuhusiana na kuigawa Tz aiweke jamvini.
Natanguliza shukrani.
Hangaikeni na mawaziri wezi wa mali ya umma ili wapelekwe mahakamani, kuliko kusumbuka kutafuta sauti zisizo na faida kwa taifa.
 
Back
Top Bottom